Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,638
MTUNZI: ALLY MBETU
0713646500
Toka nimefika kwa mshikaji wangu Sammy ambaye tulisoma shule moja, baada ya kuandamwa na matatizo yaliyosababishwa na watoto wa kike kiasi kuwa nuksi kila nilipokwenda. Baada ya kuponea tundu la shindano nilipotaka kuchomwa moto kwa ajili ya mke wa mtu na kuamua kwenda kwa rafiki yangu Sammy kupumzika, ambaye naye nilimkuta moto chini kwa mademu. Sikutaka tena kushughulika na masuala ya wanawake nami nilikuwa mlokole flani.
Lakini nilipofika kwa rafiki yangu Sammy nilikuta msichana mmoja akiwasumbua sana. Lazima nimpe sifa zake nimekutana na wanawake wengi lakini Enjo au binti mlokole alikuwa tishio kwa uzuri. Enjo pamoja na umbile tata alikuwa na sifa mmoja ya ucheshi, alionekana kushika sana dini kufikia hatua ya kuitwa binti mlokole.
Toka nimefika pale sikuwahi kumuona na mwanaume zaidi ya kila aliyemtokea kugonga mwamba akiwemo mshikaji wangu Sammy ambaye naye alikuwa na sifa ya kuvunja moyo mgumu wa kila kwanamke lakini pale alidunda.
Binti huyu pamoja na kuwa na umbile tata bado hakuwa na dharau alimchangamkia kila mmoja na wengi kuwaamini ni maharage ya Mbeya. Kila mtu aliyemtamkia neno ya mapenzi alimjibu "Ashindwe na alegee kwa jina la Yesu".
Kama nilivyosema mwanzo safari yangu ya mapenzi ilijaa balaa ya kukosa kuuawa hivyo nami nilikuwa mmoja wa vijogoo vilivyomtamani lakini sikutaka kuwa mmoja ya watu ambao walitupia ndoano ya kuishia kutoka patupu kwani haikuwa sifa yangu kwani toka nizaliwe sikuwahi kudunda kwa demu. Japokuwa nilikuwa na uhakika wa kumg’oa lakini niliamua kukaa kimya kuwaacha vijana wapimane naye ubavu japo ilionekana kabisa wamechemka.
Kwa vile nilipotoka nilijua mwenyewe na kuuapia moyo wangu kutojihusisha na wanawake niliwatazama tu. Tukiwa nimekaa kijiweni na washikaji zangu jirani na nyumba ya kina Enjo, mara lilisimama gari na mzee Masawe baba yake Enjo na kuteremka wanawe akiwemo Anjo msichana aliyewatesa wanaume wengi pale mtaani.
Baada ya Enjo na wadogo zake kuteremka walielekea ndani kwao kwa vile gari lililowaleta lilikuwa likiendelea na safari. Alitembea kwa mwendo wa taratibu kuingia ndani ya geti huku akiwaacha wadogo zake watangulie mbele. Kwa kweli Mungu alifanya makusudi kwa msichana yule ambaye hakuna aliyeamini kwa urembo wake ule kama kweli hana mpenzi pale mtaani.
“Enjo anautesa mtima wangu,” mshkaji wangu Sammy alisema huku akitikisa kichwa.
“Mzee we si mtaalamu wa totozi umechemka vipi?” nilimuuliza mshikaji wangu kwa kumtania kama sijui kitu.
“Kaka wee acha usimuione vile anachekacheka mgumu ajabu.”
“Mmh! Yule demu anatuyeyusha nasikia kuna mtu anamchukua,” jamaa mwingine aliingiza neno.
“Haiwezekani,” Sammy alibisha.
“Kakaaa yule demu nasikia kuna mtu anatoka naye,” jamaa alisisitiza.
“Hakuna, yule semu inaonekana hamjui mwanaume,” Sammy bado alimtetea Enjo.
“Kama unabisha muulize demu wako Sinta anajua kila kitu, kuna jamaa mmoja huwa anatoka naye lakini kwa siri sana.”
“Sasa mi nimeshindwa wapi?” Sammy alijishangaa mwenyewe kusikia Enjo anatoka na mtu lakini yeye kachemka.
“Labda amenyaka sifa yako ya kubadili mademu kama nguo,” mshkaji mwingine alichangia.
“Ainyake wapi?”
“Rose si shoga yake lazima alimwambia kuwa kiwembe baada ya kutembea na Rose si ndo utakatoka na Sinta lazima alimuuliza tu.”
“Bado sikubali, kama kweli anatoka na mtu lazima na mimi kwa hali na mali nitamvua nguo ya ndani,” Sammy alijigamba.
Muda wote nilikuwa kimya nikiwasikiliza wakali wa kitaa ambao walikuwa wakimtaka msichana hachomoi lakini kwa Enjo walionekana kukata tamaa.
***
Kwangu mimi nilionekana mwoga wa mademu toka nifika kwa Sammy hakuwahi kunisikia nikizungumzia mademu. Chumba cha Sammy kilikuwa na sifa ya kuingiza kila siku wanawake zaidi ya watatu tofauti. Lakini kwangu ilikuwa tofauti toka nilipofika kwake hakuwahi kuniona natongoza wala kuzungumzia habari za wanawake mpaka siku moja aliniuliza.
“Anda mshikaji wangu una matatizo gani?”
“Ya vipi mzee?”
“Toka uje hapa sijakuona unatongoza demu au jogoo awiki?”
“Anawika kama kawaida.”
“Mbona sijawahi kukuona na demu.”
“Ndugu yangu nipo likizo ndefu, sasa hivi wanawake nawaogopa kama ukoma.”
“Unawaogopa kwa nini?”
“Kaka huko nilipotoka mpaka nafika hapa nimetokea tundu la sindano kufa kifo kibaya, ndo maana wanawake sitaki.”
“Anda acha kuzunga kipi kimekutokea?”
“Sammy nimekuja kwako kupumzika nimekosa kuuawa zaidi ya mara tatu kwa Ajili ya wanawake hao, ndo maana wanawake nawaogopa sana.”
“Walikufanya nini?”
“Nitakuelezea, mi nilikuwa zaidi yako hakuna msichana aliyenishinda, hata huyu anayekusumbueni kwangu mbona cha mtoto.”
“Sasa hizo dharau.”
“Sammy, mimi nina tofauti kubwa na ninyi, nikimtaka yule apindui.”
“Unajikosha tu mshkaji wangu unaonekana mwoga kama kunguru kwa watoto wa kike.”
“Sammy hunijui mi ni kikaango cha moto kwa watoto wa kike?”
“Ni kwa hao lakini si kwa Enjo, yule msichana mgumu bwana.”
“Ni kwenu si kwangu sijawahi na sitawahi kumshindwa.”
“Kama kweli we kidume mchukue Enjo.”
“Utanipa nini?”
“Chochote utakachotaka.”
“Basi niachie hiyo kazi, ipo siku utamkuta Enjo humu ndani katika kanga moja.”
“Labda utumie kizizi.”
“Kaka vita mbinu, najua kupigana vita vyote bila kuangalia eneo, kwa Enjo hesabu amekwisha.”
“Haya nieleze ilikuwaje mpaka ukaponea tundu la sindano?” Sammy alitaka kujua mikasa ilinifikisha pale.
Sikuwa na budi kumueleza tokea nilipokoswa na risasi na baba wa rafiki yangu baada ya kumpa ujauzito binti yake ambaye alitaka nimfundishe twisheni na kuingia kichwakichwa nami sikulaza damu kwani mtoto alikuwa akiliapa.
Mchezo wetu tulicheza kwa siri ambao ulimfanya mtoto wa kike kushiba, baada ya kubanwa sana na wazazi wake alinitaja kuwa mimi ndiye muharibifu. Baba yake kwa hasira alinisaka ba bastora kwa kumuharibia mwanaye. Binti alinijulisha mi nikadhania uongo.
Siku moja nikiwa kijiweni mzee alisimamisha gari na kuteremka na bastora mkononi ili anifumue ubongo. Bahati nilikimbia nyuma aliapa lazima atanyogwa kwa ajili yangu. Nikaona imeisha kuwa msala nikatokemea zangu mkoa kwa Brother.
Huko nilipata baada ya muda mfupi nilihama kwa brother na kupanga chumba changu huko nako ndipo kulikonifanya niwachukie wanawake na kuamua kukaa mbali nao. Nakumbuka nilikimbia vimevaa pensi na singland chini ndala, nguo nilinunulia mbele ya safari, baada ya kukoswa kugeuzwa ndafu kwa ajili ya mke wa mtu.
Najua una hamu kujua ilikuwaje tega sikio:
Baada ya kufika kwa kaka na nilikaa muda na kupata kazi, baada ya kuanza kazi iliyonipelekea kupanga nyumba. Nyumba niliyopanga ilikuwa na wapangaji zaidi ya wanne na wote walikuwa na wake, masela tulikuwa wawili. Tatizo likawa lile ile la mke wa mpangaji mwenzangu alikuwa akinifanyia vituko kila nilipokuwa peke yangu.
Kutokana na matatizo niliyokumbana nayo nilijua ule tena ulikuwa mkosi mwingine. Ili kujiepusha kila nilipotoka alfajiri nikienda kazini nilirudi usiku. Niliporudina mara nyingi nilijitahidi kuwa karibu ya mumewe kama kinga. Kumbe kitendo kile kilimuuma sana mke wa jirani yangu. Siku moja nikiwa naingia ndani baada ya mumewe kutangulia kuingia ndani aliniambia.
"Unajifanya mjanja ipo siku," sikumjibu nilicheka tu na kuingia ndani.
Nilishindwa kumwelewa yule mwanamke alikuwa akitafutia nini wakati alikuwa akifahamu mimi na mumewe ni marafiki. Sikumjibu niliendelea na mtindo wangu ule ule wa kuwa karibu na mumewe ili asinitie majaribuni. Nilikuwa nimechoka na kuhamahama kwa ajili ya wanawake.
Kwa mtindo ule niliweza kumdhibiti kila hila zake alizoifanya ikiwemo kukaa mikao ya hasara akiwa mbele yangu. Nilitahidi kumkwepa kitu kilichomuudhi sana. Kumbe kila siku alikuwa akinipigia mahesabu makali kuhakikisha siku moja nauonja mwili wake.
Je nini kitaendelea?
0713646500
Toka nimefika kwa mshikaji wangu Sammy ambaye tulisoma shule moja, baada ya kuandamwa na matatizo yaliyosababishwa na watoto wa kike kiasi kuwa nuksi kila nilipokwenda. Baada ya kuponea tundu la shindano nilipotaka kuchomwa moto kwa ajili ya mke wa mtu na kuamua kwenda kwa rafiki yangu Sammy kupumzika, ambaye naye nilimkuta moto chini kwa mademu. Sikutaka tena kushughulika na masuala ya wanawake nami nilikuwa mlokole flani.
Lakini nilipofika kwa rafiki yangu Sammy nilikuta msichana mmoja akiwasumbua sana. Lazima nimpe sifa zake nimekutana na wanawake wengi lakini Enjo au binti mlokole alikuwa tishio kwa uzuri. Enjo pamoja na umbile tata alikuwa na sifa mmoja ya ucheshi, alionekana kushika sana dini kufikia hatua ya kuitwa binti mlokole.
Toka nimefika pale sikuwahi kumuona na mwanaume zaidi ya kila aliyemtokea kugonga mwamba akiwemo mshikaji wangu Sammy ambaye naye alikuwa na sifa ya kuvunja moyo mgumu wa kila kwanamke lakini pale alidunda.
Binti huyu pamoja na kuwa na umbile tata bado hakuwa na dharau alimchangamkia kila mmoja na wengi kuwaamini ni maharage ya Mbeya. Kila mtu aliyemtamkia neno ya mapenzi alimjibu "Ashindwe na alegee kwa jina la Yesu".
Kama nilivyosema mwanzo safari yangu ya mapenzi ilijaa balaa ya kukosa kuuawa hivyo nami nilikuwa mmoja wa vijogoo vilivyomtamani lakini sikutaka kuwa mmoja ya watu ambao walitupia ndoano ya kuishia kutoka patupu kwani haikuwa sifa yangu kwani toka nizaliwe sikuwahi kudunda kwa demu. Japokuwa nilikuwa na uhakika wa kumg’oa lakini niliamua kukaa kimya kuwaacha vijana wapimane naye ubavu japo ilionekana kabisa wamechemka.
Kwa vile nilipotoka nilijua mwenyewe na kuuapia moyo wangu kutojihusisha na wanawake niliwatazama tu. Tukiwa nimekaa kijiweni na washikaji zangu jirani na nyumba ya kina Enjo, mara lilisimama gari na mzee Masawe baba yake Enjo na kuteremka wanawe akiwemo Anjo msichana aliyewatesa wanaume wengi pale mtaani.
Baada ya Enjo na wadogo zake kuteremka walielekea ndani kwao kwa vile gari lililowaleta lilikuwa likiendelea na safari. Alitembea kwa mwendo wa taratibu kuingia ndani ya geti huku akiwaacha wadogo zake watangulie mbele. Kwa kweli Mungu alifanya makusudi kwa msichana yule ambaye hakuna aliyeamini kwa urembo wake ule kama kweli hana mpenzi pale mtaani.
“Enjo anautesa mtima wangu,” mshkaji wangu Sammy alisema huku akitikisa kichwa.
“Mzee we si mtaalamu wa totozi umechemka vipi?” nilimuuliza mshikaji wangu kwa kumtania kama sijui kitu.
“Kaka wee acha usimuione vile anachekacheka mgumu ajabu.”
“Mmh! Yule demu anatuyeyusha nasikia kuna mtu anamchukua,” jamaa mwingine aliingiza neno.
“Haiwezekani,” Sammy alibisha.
“Kakaaa yule demu nasikia kuna mtu anatoka naye,” jamaa alisisitiza.
“Hakuna, yule semu inaonekana hamjui mwanaume,” Sammy bado alimtetea Enjo.
“Kama unabisha muulize demu wako Sinta anajua kila kitu, kuna jamaa mmoja huwa anatoka naye lakini kwa siri sana.”
“Sasa mi nimeshindwa wapi?” Sammy alijishangaa mwenyewe kusikia Enjo anatoka na mtu lakini yeye kachemka.
“Labda amenyaka sifa yako ya kubadili mademu kama nguo,” mshkaji mwingine alichangia.
“Ainyake wapi?”
“Rose si shoga yake lazima alimwambia kuwa kiwembe baada ya kutembea na Rose si ndo utakatoka na Sinta lazima alimuuliza tu.”
“Bado sikubali, kama kweli anatoka na mtu lazima na mimi kwa hali na mali nitamvua nguo ya ndani,” Sammy alijigamba.
Muda wote nilikuwa kimya nikiwasikiliza wakali wa kitaa ambao walikuwa wakimtaka msichana hachomoi lakini kwa Enjo walionekana kukata tamaa.
***
Kwangu mimi nilionekana mwoga wa mademu toka nifika kwa Sammy hakuwahi kunisikia nikizungumzia mademu. Chumba cha Sammy kilikuwa na sifa ya kuingiza kila siku wanawake zaidi ya watatu tofauti. Lakini kwangu ilikuwa tofauti toka nilipofika kwake hakuwahi kuniona natongoza wala kuzungumzia habari za wanawake mpaka siku moja aliniuliza.
“Anda mshikaji wangu una matatizo gani?”
“Ya vipi mzee?”
“Toka uje hapa sijakuona unatongoza demu au jogoo awiki?”
“Anawika kama kawaida.”
“Mbona sijawahi kukuona na demu.”
“Ndugu yangu nipo likizo ndefu, sasa hivi wanawake nawaogopa kama ukoma.”
“Unawaogopa kwa nini?”
“Kaka huko nilipotoka mpaka nafika hapa nimetokea tundu la sindano kufa kifo kibaya, ndo maana wanawake sitaki.”
“Anda acha kuzunga kipi kimekutokea?”
“Sammy nimekuja kwako kupumzika nimekosa kuuawa zaidi ya mara tatu kwa Ajili ya wanawake hao, ndo maana wanawake nawaogopa sana.”
“Walikufanya nini?”
“Nitakuelezea, mi nilikuwa zaidi yako hakuna msichana aliyenishinda, hata huyu anayekusumbueni kwangu mbona cha mtoto.”
“Sasa hizo dharau.”
“Sammy, mimi nina tofauti kubwa na ninyi, nikimtaka yule apindui.”
“Unajikosha tu mshkaji wangu unaonekana mwoga kama kunguru kwa watoto wa kike.”
“Sammy hunijui mi ni kikaango cha moto kwa watoto wa kike?”
“Ni kwa hao lakini si kwa Enjo, yule msichana mgumu bwana.”
“Ni kwenu si kwangu sijawahi na sitawahi kumshindwa.”
“Kama kweli we kidume mchukue Enjo.”
“Utanipa nini?”
“Chochote utakachotaka.”
“Basi niachie hiyo kazi, ipo siku utamkuta Enjo humu ndani katika kanga moja.”
“Labda utumie kizizi.”
“Kaka vita mbinu, najua kupigana vita vyote bila kuangalia eneo, kwa Enjo hesabu amekwisha.”
“Haya nieleze ilikuwaje mpaka ukaponea tundu la sindano?” Sammy alitaka kujua mikasa ilinifikisha pale.
Sikuwa na budi kumueleza tokea nilipokoswa na risasi na baba wa rafiki yangu baada ya kumpa ujauzito binti yake ambaye alitaka nimfundishe twisheni na kuingia kichwakichwa nami sikulaza damu kwani mtoto alikuwa akiliapa.
Mchezo wetu tulicheza kwa siri ambao ulimfanya mtoto wa kike kushiba, baada ya kubanwa sana na wazazi wake alinitaja kuwa mimi ndiye muharibifu. Baba yake kwa hasira alinisaka ba bastora kwa kumuharibia mwanaye. Binti alinijulisha mi nikadhania uongo.
Siku moja nikiwa kijiweni mzee alisimamisha gari na kuteremka na bastora mkononi ili anifumue ubongo. Bahati nilikimbia nyuma aliapa lazima atanyogwa kwa ajili yangu. Nikaona imeisha kuwa msala nikatokemea zangu mkoa kwa Brother.
Huko nilipata baada ya muda mfupi nilihama kwa brother na kupanga chumba changu huko nako ndipo kulikonifanya niwachukie wanawake na kuamua kukaa mbali nao. Nakumbuka nilikimbia vimevaa pensi na singland chini ndala, nguo nilinunulia mbele ya safari, baada ya kukoswa kugeuzwa ndafu kwa ajili ya mke wa mtu.
Najua una hamu kujua ilikuwaje tega sikio:
Baada ya kufika kwa kaka na nilikaa muda na kupata kazi, baada ya kuanza kazi iliyonipelekea kupanga nyumba. Nyumba niliyopanga ilikuwa na wapangaji zaidi ya wanne na wote walikuwa na wake, masela tulikuwa wawili. Tatizo likawa lile ile la mke wa mpangaji mwenzangu alikuwa akinifanyia vituko kila nilipokuwa peke yangu.
Kutokana na matatizo niliyokumbana nayo nilijua ule tena ulikuwa mkosi mwingine. Ili kujiepusha kila nilipotoka alfajiri nikienda kazini nilirudi usiku. Niliporudina mara nyingi nilijitahidi kuwa karibu ya mumewe kama kinga. Kumbe kitendo kile kilimuuma sana mke wa jirani yangu. Siku moja nikiwa naingia ndani baada ya mumewe kutangulia kuingia ndani aliniambia.
"Unajifanya mjanja ipo siku," sikumjibu nilicheka tu na kuingia ndani.
Nilishindwa kumwelewa yule mwanamke alikuwa akitafutia nini wakati alikuwa akifahamu mimi na mumewe ni marafiki. Sikumjibu niliendelea na mtindo wangu ule ule wa kuwa karibu na mumewe ili asinitie majaribuni. Nilikuwa nimechoka na kuhamahama kwa ajili ya wanawake.
Kwa mtindo ule niliweza kumdhibiti kila hila zake alizoifanya ikiwemo kukaa mikao ya hasara akiwa mbele yangu. Nilitahidi kumkwepa kitu kilichomuudhi sana. Kumbe kila siku alikuwa akinipigia mahesabu makali kuhakikisha siku moja nauonja mwili wake.
Je nini kitaendelea?