VAN HEIST
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 1,434
- 617
SEHEMU YA 01
Akiwa amefikisha umri wa kubalehe, Beka anayetokea Tanga mjini hakuwa bize na masuala ya mabinti kama vijana wa umri wake ambao walikuwa wanakwenda puta kuvifukuzia vidosho.
Mbaya zaidi vijana hao watukutu walikuwa wakiwatokea mpaka dada zao, walichokihitaji ni kumaliza tamaa za miili yao. " Mama Beka , kuna jambo linanitatiza ni vizuri tulizungumze," baba Beka almaarufu kwa jina la Mzee Kibandiko alimwambia mkewe. " Na wewe umeanza , yaani kitendo cha siku mbili hizi kukwambia mgongo unanisumbua unaona shida!" mama Beka alimwambia mumewe . " Hahahaha!" baba Beka alicheka. " Sasa unacheka nini?" mama huyo alihoji.
Kufuatia mkewe kuuliza sababu ya kucheka, Mzee Kibandiko aliyepewa jina hilo kutokana na kupenda kuvaa kibalaghashia kwa staili ya kukiegesha kichwani alimwambia hakuwa na maana aliyoitafsiri. " Sasa unamaanisha nini kama siyo kugeuza maneno baada ya kuona nimekubana ?" mkewe alimwuliza . Mzee Kibandiko alicheka na kumweleza kwamba jambo alilotaka kumuuliza ni kuhusiana na kijana wao Beka . " Umeanza, mtoto kafanyaje ?" mama huyo alihoji . " Siyo kafanyaje , we unamuona yupo sawa na wenzake ?" Mzee Kibandiko alimwuliza mkewe. " Kwani ana tofauti gani, hajafanyiwa suna au hasomi shule nzuri ?" mama huyo alimkomalia mumewe kwa maswali.
Mumewe ambaye kicheko chake kilikuwa karibu , alicheka na kumwambia mkewe kwamba alichotaka kumwambia siyo suala la Beka kufanyiwa suna au kusoma shule nzuri isipokuwa ni zaidi ya hayo . " Eh ! Makubwa ! Madogo yana nafuu!" mama huyo alimwambia mumewe . " Tena tusipokuwa makini yatakuwa makubwa haswa !" Mzee Kibandiko alimwambia mkewe.
Mama huyo alipoona mumewe hafunguki kuhusu alichotaka kumweleza alimwambia hakuwa na lolote zaidi ya kulilia chakula cha usiku ambacho zilipita siku tatu bila kukitafuna. Mzee Kibandiko alicheka lakini kabla hajamwambia hisia alizokuwanazo juu ya kijana wao , mlango wa sebuleni ulifunguliwa Beka aliyetoka shuleni akaingia. " Shikamoo baba, shikamoo mama?" aliwaamkia wazazi wake . " Marhaba mwanangu za shule?" mama mtu alimwuliza mwanaye. " Nzuri mama, " Beka aliitikia. " Vipi we mswahili za huko shuleni kwenu ?" baba yake alimsabahi . " Nzuri tu , pole kwa kazi !" Beka aliyekuwa kidato cha kwanza alimpa pole baba yake kisha akaelekea chumbani kubadili nguo.
Beka aliyekuwa handsome boy alipobadili nguo alitoka na kwenda sebuleni na kunyoosha sehemu ya chakula . Kabla hajafanya chochote, mama yake alimwambia kwenye poti kulikuwa na wali isipokuwa mboga, akamwambia asuburi akaipashe moto . Mama huyo aliinuka akaenda jikoni akawasha jiko la Mchina akawa anapasha moto mboga, wakati huo Beka alikuwa akisoma kipande cha Gazeti la Ijumaa Wikienda ambacho mama yake alifungiwa bidhaa alipotoka sokoni.
Huyu Kulwa Mwaibale na hizi stori zake za mapenzi sijui huwa anazitoa wapi ? Mfano hii ya Chikoko wa Mtwara inafurahisha sana ! Beka alijisemea moyoni wakati akisoma kipande hicho cha gazeti kilichokuwa na chombezo la Chikoko wa Mtwara lilomuhusu kijana aliyekuwa akipenda sana masuala ya mademu badala ya masomo . Wakati akiendelea kusoma , mama yake alirejea akiwa na mboga aliyoipasha moto na kumuwekea kisha mama huyo alikwenda kuketi alipokuwa mumewe. " Sasa mama Beka mimi naona nilichotaka kukueleza tutakiongea baadaye muda huu ngoja niende kwa baba Tunu kuna jambo nataka kuongea naye, " mzee huyo alimwambia mkewe. Mimi nilijua huna lolote zaidi ya kutaka naiii , lakini ngoja nisubiri utakaporudi nisikie unachotaka kuniambia, " mama huyo alimwambia mumewe.
Mzee Kibandiko ambaye kucheka ilikuwa kawaida yake alicheka na kumwambia amsubiri kisha aliomba ampikie tambi. " Na wewe na hizo tambi , hazipiti siku tatu lazima ule tambi, hamia basi huko Unguja ukazile mpaka uchoke!" mkewe alimtania.
Mzee huyo alipoondoka mkewe huku nyuma akajaribu kuchekecha akili kujua mwanaye alikuwa na tatizo gani lakini hakugundua . " Sijui atakuwa kafanyaje lakini kama anamtuhumu kwa mambo mabaya nitamtetea Beka wangu, kwanza hana makundi yeye muda wote ni kujisomea na kunisaidia kazi za nyumbani , akitoka ni kwenda kucheza mpira tu !" mama huyo aliwaza... itaendelea
Source: Global Publishers
Akiwa amefikisha umri wa kubalehe, Beka anayetokea Tanga mjini hakuwa bize na masuala ya mabinti kama vijana wa umri wake ambao walikuwa wanakwenda puta kuvifukuzia vidosho.
Mbaya zaidi vijana hao watukutu walikuwa wakiwatokea mpaka dada zao, walichokihitaji ni kumaliza tamaa za miili yao. " Mama Beka , kuna jambo linanitatiza ni vizuri tulizungumze," baba Beka almaarufu kwa jina la Mzee Kibandiko alimwambia mkewe. " Na wewe umeanza , yaani kitendo cha siku mbili hizi kukwambia mgongo unanisumbua unaona shida!" mama Beka alimwambia mumewe . " Hahahaha!" baba Beka alicheka. " Sasa unacheka nini?" mama huyo alihoji.
Kufuatia mkewe kuuliza sababu ya kucheka, Mzee Kibandiko aliyepewa jina hilo kutokana na kupenda kuvaa kibalaghashia kwa staili ya kukiegesha kichwani alimwambia hakuwa na maana aliyoitafsiri. " Sasa unamaanisha nini kama siyo kugeuza maneno baada ya kuona nimekubana ?" mkewe alimwuliza . Mzee Kibandiko alicheka na kumweleza kwamba jambo alilotaka kumuuliza ni kuhusiana na kijana wao Beka . " Umeanza, mtoto kafanyaje ?" mama huyo alihoji . " Siyo kafanyaje , we unamuona yupo sawa na wenzake ?" Mzee Kibandiko alimwuliza mkewe. " Kwani ana tofauti gani, hajafanyiwa suna au hasomi shule nzuri ?" mama huyo alimkomalia mumewe kwa maswali.
Mumewe ambaye kicheko chake kilikuwa karibu , alicheka na kumwambia mkewe kwamba alichotaka kumwambia siyo suala la Beka kufanyiwa suna au kusoma shule nzuri isipokuwa ni zaidi ya hayo . " Eh ! Makubwa ! Madogo yana nafuu!" mama huyo alimwambia mumewe . " Tena tusipokuwa makini yatakuwa makubwa haswa !" Mzee Kibandiko alimwambia mkewe.
Mama huyo alipoona mumewe hafunguki kuhusu alichotaka kumweleza alimwambia hakuwa na lolote zaidi ya kulilia chakula cha usiku ambacho zilipita siku tatu bila kukitafuna. Mzee Kibandiko alicheka lakini kabla hajamwambia hisia alizokuwanazo juu ya kijana wao , mlango wa sebuleni ulifunguliwa Beka aliyetoka shuleni akaingia. " Shikamoo baba, shikamoo mama?" aliwaamkia wazazi wake . " Marhaba mwanangu za shule?" mama mtu alimwuliza mwanaye. " Nzuri mama, " Beka aliitikia. " Vipi we mswahili za huko shuleni kwenu ?" baba yake alimsabahi . " Nzuri tu , pole kwa kazi !" Beka aliyekuwa kidato cha kwanza alimpa pole baba yake kisha akaelekea chumbani kubadili nguo.
Beka aliyekuwa handsome boy alipobadili nguo alitoka na kwenda sebuleni na kunyoosha sehemu ya chakula . Kabla hajafanya chochote, mama yake alimwambia kwenye poti kulikuwa na wali isipokuwa mboga, akamwambia asuburi akaipashe moto . Mama huyo aliinuka akaenda jikoni akawasha jiko la Mchina akawa anapasha moto mboga, wakati huo Beka alikuwa akisoma kipande cha Gazeti la Ijumaa Wikienda ambacho mama yake alifungiwa bidhaa alipotoka sokoni.
Huyu Kulwa Mwaibale na hizi stori zake za mapenzi sijui huwa anazitoa wapi ? Mfano hii ya Chikoko wa Mtwara inafurahisha sana ! Beka alijisemea moyoni wakati akisoma kipande hicho cha gazeti kilichokuwa na chombezo la Chikoko wa Mtwara lilomuhusu kijana aliyekuwa akipenda sana masuala ya mademu badala ya masomo . Wakati akiendelea kusoma , mama yake alirejea akiwa na mboga aliyoipasha moto na kumuwekea kisha mama huyo alikwenda kuketi alipokuwa mumewe. " Sasa mama Beka mimi naona nilichotaka kukueleza tutakiongea baadaye muda huu ngoja niende kwa baba Tunu kuna jambo nataka kuongea naye, " mzee huyo alimwambia mkewe. Mimi nilijua huna lolote zaidi ya kutaka naiii , lakini ngoja nisubiri utakaporudi nisikie unachotaka kuniambia, " mama huyo alimwambia mumewe.
Mzee Kibandiko ambaye kucheka ilikuwa kawaida yake alicheka na kumwambia amsubiri kisha aliomba ampikie tambi. " Na wewe na hizo tambi , hazipiti siku tatu lazima ule tambi, hamia basi huko Unguja ukazile mpaka uchoke!" mkewe alimtania.
Mzee huyo alipoondoka mkewe huku nyuma akajaribu kuchekecha akili kujua mwanaye alikuwa na tatizo gani lakini hakugundua . " Sijui atakuwa kafanyaje lakini kama anamtuhumu kwa mambo mabaya nitamtetea Beka wangu, kwanza hana makundi yeye muda wote ni kujisomea na kunisaidia kazi za nyumbani , akitoka ni kwenda kucheza mpira tu !" mama huyo aliwaza... itaendelea
Source: Global Publishers