Chips nyama 8000 Singida Hotelini

lakini pia ukumbuke kwenye soko huru, demand inaamua bei kwenye bidhaa zisizodhibitiwa. hata kama ungekuwa wewe una kamgahawa pale nata nzega, mabasi kama kumi yakakwama kwa sababu yoyote ile, nakwambia kikombe cha chai ya siturungi utauza buku. miaka fulani ya nyuma barabara bado zile za wahenga, tulikwama pale kateshi kwenye kamlima kale kalikuwa na utelezi sana,ilikuwa usiku kimvua kinanyesha ni kijijini, tuluziwa chai yenye chumvi sio sukari, chapati nadhani zilikuwa za unga wa mhogo bei siikumbuki ila ilikuwa maradufu. waache tuwapige pesa wasomali hao na wewe hapo ujifunze kitu. halafu investment yao naona ni too risky ukikosana na madereva tu imekula kwake, au latra wakatoa utaratibu mwingine, wamewake. kwa hiyo wanakimbizana kurudisha pesa zao
Shida siyo soko huru abiria hana option huu ni uonevu uliopitiliza na uwizi wa nguvu. Wasimame maeneo ya mjini kupata chakula.
 
Nilipita pale Four Ways ndo mara ya kwanza sijui bei zao, naenda kuulizia msosi bei nilizotajiwa nilikimbia . Ndio maana nikiwa safarini nakuwa na biscuits sanasana Digestive na karanga au korosho...imetoka hiyo mpaka nifike ninakoenda
Sema ukila korosho usizidishe kula
Nafikiri umenielewa

Ova
 
Wateja wenyewe ni wasafiri tu lazima bei iwe kubwa
Kwa mfano ukifungua hapo na wewe ukauza bei poa kama hotel za mjini utatoboa?
Hauwezi kwa sababu bus likiondoka hakuna wateja tena
Wewe ni mjinga?

Basi likiondoka linakuja lingine. Na lingine tena. Bado watu wenye usafiri binafsi.
 
Pengine haupo updated,
Mabasi mengi nw days hawaruhusu watu kula kwenye basi sababu ya uchafu.

Unaposema watu wanaendekeza kula njiani sidhan sana upo sahihi, hilo ni swala la personal choices kama vile wewe unapoamua kupika nyumbani na kusafiri nacho- Ni choices zinazokuwa executed in different modalities.
Yaan nisafiri na chakula changu unizuie kula kwenye gari?
 
PIKA CHAKO NYUMBANI WE UNAJUA UNAMATATIZO ALAFU UNATAKA ULE HOTELINI WALE KUMBUKA WATEJA WAO NI WASAFIRI TU MDA WA MAGARI UKIISHA NDO HAWAUZI TENA SASA MTU AMEWEKEZA HELA NYINGI AJE AKUUZIE KAMA KWA MAMANTILIE
Kwanin wasipaki stand abiria akajichagulia sehemu ya kula?acha undilo
 
Salam,

Nilipita hapo leo nikazama nikauliza bei ya hizo chips, kuna vifuko vya kaki vilivyokatwa nusu wamewekemo chips kidogo ba nyama finyango hazifiki 7.

Nilichoona kwa bei zile wasafiri wanapigwa sana. Utanunua tu kwa kuwa hakuna option. Hii nchi hakuna wanaodhibiti bei za vitu?
Bei nafuu kabisaa hyo😀
 
Njia ya kaskazini ni hatari sana kwa bei
Haya ni mambo ya kijitakia, wakati mwingine naona no bora tuendelee kupigwa tu kwani tunastahili. Zamani magari yote yalikuwa yanasimama stendi, sehemu yenye hoteli na migahawa mingi, na bei za kila aina, wasafiri wanachjagua wale wapi. Ushindani kwenye hizo hoteli ulikuwa unafanya wenye hoteli kupika vyakula vizuri na kuuza bei rafiki. Mara ''wajanja'' wachache wakaanza kujenga hoteli katikakati ya mapori na kufanya deal na wenye mabasi ili yasimame pale. Ukienda pale hakuna ushindani, msosi ni kidogo na wanapanga bei wanayotaka. Na mbaya zaidi mnapewa dakika kumi tu ili muwe na haraka ya kununua na vichwa vyenu visiweze ku-mind bei ya vyakula. Tukiunga wote na kudai magari yarudie kupaki stendi za umma kama zamani mambo yatabadilika.
 
Salam,

Nilipita hapo leo nikazama nikauliza bei ya hizo chips, kuna vifuko vya kaki vilivyokatwa nusu wamewekemo chips kidogo ba nyama finyango hazifiki 7.

Nilichoona kwa bei zile wasafiri wanapigwa sana. Utanunua tu kwa kuwa hakuna option. Hii nchi hakuna wanaodhibiti bei za vitu?
Mnawacheka wasukuma kubeba viazi kwenye masufuria safarini halafu unakuja kulialia huku wakati kila mtu humu jf ni Tajiri.
 
Salam,

Nilipita hapo leo nikazama nikauliza bei ya hizo chips, kuna vifuko vya kaki vilivyokatwa nusu wamewekemo chips kidogo ba nyama finyango hazifiki 7.

Nilichoona kwa bei zile wasafiri wanapigwa sana. Utanunua tu kwa kuwa hakuna option. Hii nchi hakuna wanaodhibiti bei za vitu?
Ukiwa unaenda dom, ukifika pale Moro napo mambo ni hayo hayo ...

Yaan wasafiri sasa ndio Chambo waku pigwa pesaa kufanyiwa ulanguzi yaan. Wali wa 2000 ukiwa safarini utaununua kwa 5000 ujinga sanaaa huu alafu pale mahala mabasi yapo simama hapako vizuri kuanzia usafi na mazingira ya uaandaji wa vyakula ni pachafu mnooo
 
Mi nikitaka kusafiri ninafungasha chakula na vinywaji vya kutosha.

Sinunui maji wala soda njiani.

Niliwahi kuuziwa soda ya buku kwa buku mbili. Tangu hapo nimeacha kununua vyakula 😊
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom