Chips nyama 8000 Singida Hotelini

Chips nyama 8000 Singida Hotelini

Naona watu wengi wanamsiliba mtoa mada kwa maneno ya fedheha lakini lets be realistic. Hilo suala sio sawa. Hata kama mtu ana options za kuka sijui biakuti na soda, kuna watu kwa mfano wagonjwa wa kisukari, je na hao pia wafanyeje? Ndio tuweke utani lakini while we are at it tuliangalie hili pia maana hii ni platform kubwa. Hakuna justification ya wqo kuuza chakula 8000 na zaidi kwa kitu ambacho thamani haifiki hata 3000.
Sasa mtu mwenye kisukari ndiyo hatakiwi kabisa kula kula hovyo njiani, bora atoke home na Chakula chake..
 
Picha tafwadhali
Unashindwajwe kununua nusu kuku home na kufunga kwa foil wakuu??
FB_IMG_1662987028483.jpg
 
Sio kila safari mtu anatokea nyumbani.

Safari zingine unatokea mkoani kikazi (mfano Musoma/Rukwa), unarudi zako Dar es Salaam.

Unatoka Musoma/Rukwa saa kumi usiku, unafika Dar 11 alfajiri au kesho yake kabisa
Nunua biskuti na juice ya Azam mixer, apple , chungwa/ndizi...
 
Tumia akili.

Sio kila safari mtu anatokea nyumbani.

Safari zingine unatokea mkoani kikazi (mfano Musoma/Rukwa), unarudi zako Dar es Salaam.

Unatoka Musoma/Rukwa saa kumi usiku, unafika Dar 11 alfajiri au kesho yake kabisa
Kwani huko mikoani hakuna hotels? Mfano Kigoma pale kuna fast food restaurants unaweza nunua Usiku na wakakufungia vizuri tuu..
 
Ukiwa unaenda dom, ukifika pale Moro napo mambo ni hayo hayo ...

Yaan wasafiri sasa ndio Chambo waku pigwa pesaa kufanyiwa ulanguzi yaan. Wali wa 2000 ukiwa safarini utaununua kwa 5000 ujinga sanaaa huu alafu pale mahala mabasi yapo simama hapako vizuri kuanzia usafi na mazingira ya uaandaji wa vyakula ni pachafu mnooo
Pale Moro ukipanda ABC UPPER CLASS BUS wana hotel yao pale Kingoluwira instwa Carte Hotel, yaani vyakula ni bei mbaya sanaaa..
 
Mkuu naomba nikunukuu
"Kaanga vipande vya ndizi mzuzu na vioande vya nyama kiasi funga kwenye foil panda bus.
Ukifika njiani unakula mdogomdogo"

Pengine ulikuwa unaanisha nini kusema kula mdogo mdogo njiani wakati wa safari manake point ya kulia ni moja tu?
Unaruhusiwa kula ndani ya Bus huku safari ikiendelea na ma Bus mengi yana dust bin Mbona?? Hata kwenye hizo hotel zao utasikia tunasimama dakika 10 tujisaidie, na tuchukue chakula na kurudi kwenye Bus..
 
Pale Moro ukipanda ABC UPPER CLASS BUS wana hotel yao pale Kingoluwira instwa Carte Hotel, yaani vyakula ni bei mbaya sanaaa..
Napajua pale sasa ni kheri ya pale mazingira ni mazuri na ni pa safi sanaaa..uje upande shabib ili waka jutupe hapo ninapo sema utajionea mazingira ni machafuuuu wali maharagwe unauziwa 5000 can you imagine ? Bahati mbaya siku piga picha
 
Unazani ni rahisi hivyo safari ya masaa kumi unakula tu vitu vya baridi tu mimi kwangu wala huwa sijutii kununua chakula hicho hotelini kwa bei kubwa kutokana na mazingira kikubwa watu tujifunze kujipanga tunavyosafiri ata kama utabeba chakula chako safari ikiwa ndefu tumbo huwa linagoma kuendelea kupokea chakula cha baridi
Chips za hivi usafi sifuri kabisa... Ila mazoea bwana yaani kweli mtu anashindwa kutoka home na skonzi/slesi 2 za mkate, mayai ya kuchemsha 2, chungwa/ndizi na juice/soda kweli?? Tena safari yenyewe Dar to Dodoma
 
Unazani ni rahisi hivyo safari ya masaa kumi unakula tu vitu vya baridi tu mimi kwangu wala huwa sijutii kununua chakula hicho hotelini kwa bei kubwa kutokana na mazingira kikubwa watu tujifunze kujipanga tunavyosafiri ata kama utabeba chakula chako safari ikiwa ndefu tumbo huwa linagoma kuendelea kupokea chakula cha baridi
Sijui una maanisha nini kwa chakula cha baridi, nowadays kuna vi container vizuri tuu vidogo ambavyo vipande vya kuku 2 au nyama finyango 5 zilizoko kwenye foil unaziweka ndani ya kikontaina na muda wa kula bado vinakuwa fresh kabisa. Tatizo hatuna hayo mazoea sisi, niliwahi kufanya kazi na mzungu mmoja kwenye NGO fulani for 3 years sikuwahi kumuona kantini au akiagiza chakula sijui chips au nini. Kwenye begi lake la laptop ana maji yake, coffee mug, na kikontena kidogo cha chakula from home. Cha ajabu ni kwamba huyo mzungu salary yake ni kubwa mnooo kutushinda siye woootee mpaka mkurugenzi mkuu but siye ndiyo tunaongoza kuagiza chips kuku, biriani, makange etc... Na tukiishiwa huwa tunaenda kumkopa yeye pesa, basi huwa anacheka sana jinsi ambavyo hatuna bajeti na nidhamu ya pesa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom