Chips nyama 8000 Singida Hotelini

Chips nyama 8000 Singida Hotelini

Wacha kulalamika wewe ndo hali halisi ya uchumi, ukilishwa nguchiro au mzoga wewe wewe utakuwa wa kwanza kukenua humu!
 
Turudi miaka ya nyuma; inatubidi tuchome nyama nyumbani ndio tusafiri nazo
 
Salam,

Nilipita hapo leo nikazama nikauliza bei ya hizo chips, kuna vifuko vya kaki vilivyokatwa nusu wamewekemo chips kidogo ba nyama finyango hazifiki 7.

Nilichoona kwa bei zile wasafiri wanapigwa sana. Utanunua tu kwa kuwa hakuna option. Hii nchi hakuna wanaodhibiti bei za vitu?
kuna tume ya ushindani. ukipeleka malalamiko huko wataitika
 
Salam,

Nilipita hapo leo nikazama nikauliza bei ya hizo chips, kuna vifuko vya kaki vilivyokatwa nusu wamewekemo chips kidogo ba nyama finyango hazifiki 7.

Nilichoona kwa bei zile wasafiri wanapigwa sana. Utanunua tu kwa kuwa hakuna option. Hii nchi hakuna wanaodhibiti bei za vitu?
lakini pia ukumbuke kwenye soko huru, demand inaamua bei kwenye bidhaa zisizodhibitiwa. hata kama ungekuwa wewe una kamgahawa pale nata nzega, mabasi kama kumi yakakwama kwa sababu yoyote ile, nakwambia kikombe cha chai ya siturungi utauza buku. miaka fulani ya nyuma barabara bado zile za wahenga, tulikwama pale kateshi kwenye kamlima kale kalikuwa na utelezi sana,ilikuwa usiku kimvua kinanyesha ni kijijini, tuluziwa chai yenye chumvi sio sukari, chapati nadhani zilikuwa za unga wa mhogo bei siikumbuki ila ilikuwa maradufu. waache tuwapige pesa wasomali hao na wewe hapo ujifunze kitu. halafu investment yao naona ni too risky ukikosana na madereva tu imekula kwake, au latra wakatoa utaratibu mwingine, wamewake. kwa hiyo wanakimbizana kurudisha pesa zao
 
Mwalimu wangu aliniambia
"Sio kila kitu kimewekwa/tengenezwa kwaajili yako"
Hata hivo naona,zile bei ni za kukomoana,finyango 4 ndogo vichips vya kusambazwa,Free market economy quality of the service matter.5000 ndio halali,nchi haiwezekani ikaenda kiholela.itafikia pahala 10,000 na hushibi.ila uzuri mmoja hawakulazimishi
 
Nilipita pale Four Ways ndo mara ya kwanza sijui bei zao, naenda kuulizia msosi bei nilizotajiwa nilikimbia . Ndio maana nikiwa safarini nakuwa na biscuits sanasana Digestive na karanga au korosho...imetoka hiyo mpaka nifike ninakoenda
 
Nilipita pale Four Ways ndo mara ya kwanza sijui bei zao, naenda kuulizia msosi bei nilizotajiwa nilikimbia . Ndio maana nikiwa safarini nakuwa na biscuits sanasana Digestive na karanga au korosho...imetoka hiyo mpaka nifike ninakoenda
To some extent inaweza kuwa justified,

Kuna kipindi nilikutana na jamaa anasafirisha inputs za mahoteli kutoka moshi na Arusha kwa ajili ya kuandaa vyakula mombo, kutokana na hayo mahoteli kuwa allocated interior, hivyo ku-add kwenye gharama ya bidhaa.
 
WaTz tunaendekeza sana kulakula njiani tukiwa safarini.
Kaanga vipande vya ndizi mzuzu na vioande vya nyama kiasi funga kwenye foil panda bus.
Ukifika njiani unakula mdogomdogo.

Vinginevyo mwendo wa bites tu na juice mbona safi tu.

Huwezi kufa kwa kushindwa kula siku moja tu ya safari.
Bites na juice au soda ni salama zaidi.
 
Wateja wenyewe ni wasafiri tu lazima bei iwe kubwa
Kwa mfano ukifungua hapo na wewe ukauza bei poa kama hotel za mjini utatoboa?
Hauwezi kwa sababu bus likiondoka hakuna wateja tena
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom