Chips nyama 8000 Singida Hotelini

Chips nyama 8000 Singida Hotelini

Ili kunogesha safari zaidi unaandaa mayai yako ya kuchemsha yakutosha, hotpot kubwa la makande yakisindikizwa na chupa kubwa la juice ya parachichi mixer ndizi.
Hapo safari yako itakuwa murua hasa ukiwa kwenye zile bus za luxury full Ac.
Mmmh mayayiii tena.... air conditioner iwepo aisee
 
Haya ni mambo ya kijitakia, wakati mwingine naona no bora tuendelee kupigwa tu kwani tunastahili. Zamani magari yote yalikuwa yanasimama stendi, sehemu yenye hoteli na migahawa mingi, na bei za kila aina, wasafiri wanachjagua wale wapi. Ushindani kwenye hizo hoteli ulikuwa unafanya wenye hoteli kupika vyakula vizuri na kuuza bei rafiki. Mara ''wajanja'' wachache wakaanza kujenga hoteli katikakati ya mapori na kufanya deal na wenye mabasi ili yasimame pale. Ukienda pale hakuna ushindani, msosi ni kidogo na wanapanga bei wanayotaka. Na mbaya zaidi mnapewa dakika kumi tu ili muwe na haraka ya kununua na vichwa vyenu visiweze ku-mind bei ya vyakula. Tukiunga wote na kudai magari yarudie kupaki stendi za umma kama zamani mambo yatabadilika.
Uko sahihi..kuna bus kama Kilimanjaro na Dar expess na Bm hotel wanayotumia hakika ni wizi mtupu, vyakula vibovu na kidogo sana
 
Pengine haupo updated,
Mabasi mengi nw days hawaruhusu watu kula kwenye basi sababu ya uchafu.

Unaposema watu wanaendekeza kula njiani sidhan sana upo sahihi, hilo ni swala la personal choices kama vile wewe unapoamua kupika nyumbani na kusafiri nacho- Ni choices zinazokuwa executed in different modalities.
Mimi sijasema ulie kwenye gari.

Ukishasema ni personal choice basi huna budi kupambana na gharama zake pasipo malalamiko maana its personal.
Ni wewe umechagua, na kupanga ni kuchagua.
Ndio maana nasema unaweza kuchagua kutokula au kula bites na safari ikaisha vizuri tu.

Lakini ukichagua kula chips kuku njiani au chips nyama choma basi ujue kupambana na gharama zake.
 
Mimi sijasema ulie kwenye gari.

Ukishasema ni personal choice basi huna budi kupambana na gharama zake pasipo malalamiko maana its personal.
Ni wewe umechagua, na kupanga ni kuchagua.
Ndio maana nasema unaweza kuchagua kutokula au kula bites na safari ikaisha vizuri tu.

Lakini ukichagua kula chips kuku njiani au chips nyama choma basi ujue kupambana na gharama zake.
Mkuu naomba nikunukuu
"Kaanga vipande vya ndizi mzuzu na vioande vya nyama kiasi funga kwenye foil panda bus.
Ukifika njiani unakula mdogomdogo"

Pengine ulikuwa unaanisha nini kusema kula mdogo mdogo njiani wakati wa safari manake point ya kulia ni moja tu?
 
Safari ya masaa nane siyo lazima kula njiani. Kwani ukipiga msosi wako wa nguvu asubuhi ukabeba na maji lita 1 kuna shida?
 
Shida siyo soko huru abiria hana option huu ni uonevu uliopitiliza na uwizi wa nguvu. Wasimame maeneo ya mjini kupata chakula.
tatizo liko hapo sasa, yaani cc abiria tuapenda kufika haraka hasa safari ndefu, unadhani bus lilipakiwa pale msamvu stendi mkapewa dkk10 kutafuta chakula!!!!, loooh utashangaa kama sio abiria wengi kuachwa labda likae saa nzima kusubiri abiria warudi. lakini mimi najiuliza tunashindwaje kujinyima uvumilie au usile mpk ufike au kunywa juice/soda na andazi au skonzi usijilazimishe kununua chakula cha bei kubwa halafu mwisho wa siku unalalamika, au beba kaugali kako na dagaa unapoanza safari ili wakipaki kula we fungua kaugali kako hautatumia hata mia hapo!!!!. au nunua plate ya matunda baaaasi tosha kabisa, ukikubali kulipa elfu8 halafu unaanza kulalamika kama vile hapakuwa na alternative, napigwa bumbuwazi
 
Mkuu naomba nikunukuu
"Kaanga vipande vya ndizi mzuzu na vioande vya nyama kiasi funga kwenye foil panda bus.
Ukifika njiani unakula mdogomdogo"

Pengine ulikuwa unaanisha nini kusema kula mdogo mdogo njiani wakati wa safari manake point ya kulia ni moja tu?
Kula mdogomdogo sikumaanisha kudonoadonoa garini, nilimaanisha wakati wa kula unakuwa hina pressure kwenda kupanga foleni kununua msosi huku ukikimbizana na dakika chache wanazotoa kwa ajili ya kula.
Wakati wengine wanakimbizana wewe utakuwa unajipigia msosi wako mdogomdogo.
 
Kula mdogomdogo sikumaanisha kudonoadonoa garini, nilimaanisha wakati wa kula unakuwa hina pressure kwenda kupanga foleni kununua msosi huku ukikimbizana na dakika chache wanazotoa kwa ajili ya kula.
Wakati wengine wanakimbizana wewe utakuwa unajipigia msosi wako mdogomdogo.
Ooooh, Thanks.
 
Niliwahi kukaa na jamaa flani tukitokea Arusha kuelekea Dar, huyo jamaa ile tunakaribia hapo highway akatoa mkate brown na peanut butter, akapaka mkate wake na kuendelea mdogo mdogo.

Mimi nilishuka nikanunua chips kwa kuku robo shs 8,000/- na bado sikutosheka, jamaa alinikaribisha nikajifanya kupotezea (asante) ila nilijifunza kitu from that day!.

Ile tabia niliwahi ona watasha wakifanya so nikakumbuka mbali.
 
Subiri gari ikiingia singida stendi huwa inasimama kwa muda kidogo kuna watu wanaletega Chipsi pale take away sh 2000 unaweza ukanunua chap
Chips za hivi usafi sifuri kabisa... Ila mazoea bwana yaani kweli mtu anashindwa kutoka home na skonzi/slesi 2 za mkate, mayai ya kuchemsha 2, chungwa/ndizi na juice/soda kweli?? Tena safari yenyewe Dar to Dodoma
 
WaTz tunaendekeza sana kulakula njiani tukiwa safarini.
Kaanga vipande vya ndizi mzuzu na vioande vya nyama kiasi funga kwenye foil panda bus.
Ukifika njiani unakula mdogomdogo.

Vinginevyo mwendo wa bites tu na juice mbona safi tu.

Huwezi kufa kwa kushindwa kula siku moja tu ya safari.
Exactly
 
Ndizi zikipoa zinakua ngumu
Unakaanga zile ndizi ambazo zimeanza kuiva kwa mbali, ndiyo nzuri. Ukikaanga mbichi lazima ziwe ngumu. Pia weka kwa foil then kwenye kikontena kidogo..
 
Ili kunogesha safari zaidi unaandaa mayai yako ya kuchemsha yakutosha, hotpot kubwa la makande yakisindikizwa na chupa kubwa la juice ya parachichi mixer ndizi.
Hapo safari yako itakuwa murua hasa ukiwa kwenye zile bus za luxury full Ac.
Kudadadeki
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom