China yatoa waraka wa kwanza unaolenga kuchochea ufufukaji wa kina katika maeneo ya vijijini

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG211262777201.jpg

China imetoa waraka muhimu wa kisiasa unaojulikana kama “Waraka Na. 1 wa serikali kuu” wa mwaka 2023, ambapo nchi hii imesisitiza lengo lake la kusukuma kwa pande zote ufufukaji wa vijijini kwa kuunganisha juhudi za Chama cha Kikomunisti cha China na jamii nzima, na pia kuongeza kasi ya kutimiza maendeleo ya kisasa vijijini.

Waraka huo pia umetambulisha majukumu tisa ya kutimiza malengo hayo ikiwemo kuhakikisha upatikanaji wa zana za kilimo na uzalishaji na kuimarisha ujenzi wa miundombinu ya vijijini, ikiwa ni mwendeleo za majukumu ya mwaka jana lakini pia yakiwakilisha vipaumbele vipya.

Kwa mujibu wa waraka huo, kipaumbele kikubwa cha kazi zote za Chama ni kutatua matatizo ya kilimo, maeneo ya vijijini na wakulima na kutoa nafasi kubwa katika juhudi za Chama na jamii nzima katika kuboresha kwa kina ufufukaji wa maeneo ya vijijini na kuongeza kasi ya kilimo cha kisasa na maendeleo katika maeneo ya vijijini.

Waraka huo pia umesisitiza kuwa, kutokana na kasi ya mabadiliko ya dunia katika ngazi ambayo haijawahi kushuhudiwa katika historia, maendeleo ya China yameingia katika kipindi cha maingiliano ya fursa za kimkakati, matishio na changamoto, na kutokana na kuongezeka kwa sintofahamu na masuala mengine yasiyotabiriwa, ni muhimu sana kudumisha msingi wa “kilimo, maeneo ya vijijini na wakulima” na kutoruhusu makosa yoyote.

Mtafiti katika Akademia ya Sayansi ya Jamii ya China Li Guoxiang anasema, msisitizo wa waraka huo katika umuhimu wa kufanya kilimo kuwa cha kisasa na maeneo ya vijijini unaendana na mpango makini wa maendeleo uliotolewa katika ripoti ya Mkutano Mkuu wa 20 wa CPC, ambao unaeleza kuwa “kazi kubwa na yenye changamoto kubwa zaidi ambayo China inakabiliwa nayo katika kujenga jamii ya kisasa ya kijamaa ya China katika pande zote bado iko katika maeneo ya vijijini.”

Bw. Li anasema, sera nyingi zilizopewa kipaumbele katika waraka wa kwanza wa mwaka huu ni mwendelezo wa zile za mwaka jana, ikitoa taswira ya kivitendo na kihalisi ambayo itarahisisha utendaji kazi katika maeneo husika.

Waraka wa mwaka huu umeorodhesha maeneo tisa muhimu ya kazi ambayo China itayatekeleza kwa mwaka 2023 ili kuchochea ufufukaji wa maeneo ya vijijini. Jukumu la kwanza ni kuhakikisha usalama wa nafaka na upatikanaji wa bidhaa muhimu za kilimo na uzalishaji wa uhakika, ikiwa ni mwendelezo wa msisitizo wa serikali katika usalama wa chakula kuendana na mkakati wa muda mrefu.

Wito wa China wa kuimarisha usalama wa chakula pia umekuja katika wakati ambao mivutano ya siasa za kijiografia imeongezeka duniani, huku mgogoro kati ya Russia na Ukraine ukiendelea, na vitendo vya kujilinda vya upande mmoja vinavyoongozwa na Marekani vikionyesha dalili ndogo ya kumalizika.

Takwimu zilizotolewa na Idara ya Takwimu ya China zinaonyesha kuwa, mwaka 2022, China ilizalisha tani milioni 687 za nafaka, ikiwa ni ongezeko la tani milioni 3.68 ikilinganishwa na mwaka 2021.

Waraka huo pia umesisitiza majukumu kadhaa ili kuchochea ufufukaji wa vijiji, ikiwemo kuimarisha ujenzi wa miundombinu ya kilimo na kuunganisha uungaji mkono ya zana, sayansi na teknolojia katika kilimo, jambo ambalo liligusiwa katika waraka wa mwaka jana, lakini halikuwekewa msisitizo.

Waraka huo pia unasema China itaunga mkono ujenz wa maabara za kitaifa, vituo vya uvumbuzi wa uzalishaji, na majukwaa mengine katika sekta ya kilimo, na pia kuboresha mchakato wa uungaji mkono wa utafiti wa msingi wa sayansi na teknolojia katika kilimo.

Utekelezaji wa majukumu tisa yaliyoainishwa katika waraka wa kwanza wa serikali wa mwaka 2023 utaiwezesha China kuwa na usalama wa chakula, na pia kuleta maendeleo katika sekta ya kilimo na kuchochea ufufukaji katika maeneo ya vijijini.
 
Back
Top Bottom