Chikawe awakemea Mwakyembe na Sitta: Waache kuzungumzia DOWANS

Chikawe hana madaraka wala uwezo wa kulazimisha nidhamu kwa waziri yeyote. Kama yeye aliona kuwa wenzake wamekosea kwanini na yeye asimwambie Waziri Mkuu au Rais yeye mwenyewe? Sasa kesho kina Mwakyembe nao wakimjibu kwa magazeti ataona wamemvunjia heshima au wamevunja kanuni?
 

hujui ulisemalo, kwa hiyo wakae kimya? Rudi kwenu India we Rostam na ni bora utumie identity yako ili hujibu tuhuma dhidi yako!
 

Unajua wakati mwingine uszungumzie tu mkataba ulivunjwa bali ututajie kama mkataba ulikuwa halali au la na kama kweli Tanzania tulifanya makosa katika kuvunja mkataba uliokuwa halali na kama tunastahili kulipa fidia hiyo. Fikiria Dowans ilirithishwa mkataba na Richmond iliyokuwa kampuni feki, kampuni feki itarithishaje mkataba? Kuhusu Dowans SA Costarica tumeambiwa kuwa hiyo kampuni haipo kwenye orodha ya makampuni kule Costarica na wao ndio wenye asilimia 54 ya hisa katika Dowans Tanzania. Tuambie kama kuna utata katika hilo kuna haja gani ya kulipa fidia?

Wewe unadhani mkataba ni mkataba tu hata kama si halali?
 
mi nadhan wapo sawa cz hwz kuta2a matatz ukiwa mbal nayo "fimbo ya mbali haiui nyoka",acha waendelee kubaki na positions zao hk wakiendelea kupamban na ufisad wa ndg zao kwa ukarb zyd "juen kweli,nayo kwel itawaweka huru"
 
Chikawe kuwakemea mawaziri wenzake anatumia mamlaka yake vibaya (ultra vires).
 
Tatizo JK hakuwapa uwaziri hawa SITTA na MWAKYEMBE kwa roho moja ...aliwapa kwa lengo la kuwaziba mdomo tu ...na wao wanajuwa ...ndio maana hawataacha kuongea pale ambapo wanahisi maoni yao kupuuzwa barazani.

midomo mingine haizibiki hata kwa super glue! Wanalo babu
 

Sisi ndotuliowaajili simafisadi unataka wateteeakinanani? zaidiyamwajiliwake
 
Mimi nadhani tafsiri ya uwajibikaji wa pamoja inakosewa. Sidhani maana yake nsio hiyo ya kufanya uppuuzi wote ni siri ya Baraza la mawaziri. Kwanza mnasema siri ni siri zipi hizo wakati ni mambo yanayoihusu nchi na watanzani kwa ujumla wake? Ni usiri gani huo wa maamuzi mnao usema kuwa baraza la mawaziri lazima ufuate? Hayo mambo ya sirisiri ndiyo yameifikisha nchi hapa ilipo. Sidhani kama mawaziri wanaotoa maoni yao hadharani wanakuwa wamekosea. Kwani kuna ubaya gani wananchi wakijua kuwa Mawaziri wanatofautiana ktk baadhi ya mambo na maamuzi? Huo si ndio uongozi bora? Kwanini Mzee Mwinyi wakati ule akiwa mambo ya ndani alijiudhuru baada ya mauaji, na kwa nini Baraza zima lisijiudhuru kwani ni uwajibikaji wa pamoja?

Mimi nadhani hawa mawaziri wapo sahihi kabisa, hata kama wametoa maoni yao hadharani, huo ndio msimamo wao hata ktk baraza la mawaziri, hawatabadirika. Unajua watanzania tuymejisahau sana na hawa viongozi wanadhani kuwa wakisha kuwa viongozi wanauwezo wa kujiamulia tu mambo kwa vile ni mawaziri. Juzi mzee Msuya kasema, uongozi ni kujitoa kafara kuwahudumia wananchi, na ukiamua kuwa kiongozi ni lazima ujitoa muhanga huo, ndio maana anasema hata watoto wake ameamua kuwaeleza wajipime kwanza kama wanataka kuwa viongozi. Sasa hiyo ndiyo tafsiri sahihi ya uongozi na sio usiri usiri uliokidhiri. Kama yataendelea hayo ya usiri na mawaziri wetu hawatabadilika, ya Tunisia yanawezekana.
 
Kombani, Werema na Membe wakikurupuka na baadaye kusema ni mawazo yao binafsi hatujamsikia Chikawe kuwakemea au hakuwa na masilahi nayo asitufanye wote wajinga, kwenye suala la Dowans ndiyo kakumbuka kwa sababu ana maslahi nalo, nawashauri Sitta na Mwakyembe nao waseme yalikuwa ni mawazo binafsi si ya baraza la mawaziri full stop.
 
:A S thumbs_up:
 

Ijapokuwa kweli Sitta na Mwakyembe walikiuka taratibu, ni muhimu watanzania wakafahamu kuwa wajibu wa kwanza wa kiongozi kama waziri ni kulinda na kuendeleza maslahi ya taifa na wananchi wake. Huu utaratibu wa waziri kuwa na ruhusa ya kushauriana na wachache na kutolea maamuzi mambo bila baraza zima la mawaziri kukaa unatoa mwanya kwa waziri ku-conspire na wenzake wachache akiwemo raisi kuuza nchi. Kama mambo ni hivi ipo siku tutakuta raisi au waziri akishirikiana mafisadi wawili watatu ametuuza watz wote. Katika hali hiyo, ni lazima waziri mwenye uchungu na nchi yake akiuke utaratibu wa collective responsibility akemee mambo kunusuru nchi. Ndiyo Sitta na Mwakyembe wamekosea utaratibu, lakini yaangaliwe pia mazingira ya kukosea kwao jamani.

Ikumbukwe kuwa taratibu huwekwa kwa ajili ya watu, sio watu kwa ajili ya taratibu. Tatizo la baadhi ya viongozi ni kwamba wao huenzi taratibu badala ya watu. Wako tayari kulinda taratibu hata kama ni kwa gharama ya taifa zima! Shame. Wakati Lowassa alipolazimika kujiuzulu, nilishangaa kuwasikia wanasiasa wakongwe kama Kingunge wakilalamika eti utaratibu umekiukwa kwa kutokumuuliza Kwanza Lowassa ili ajitetee, huku akipuuza kabisa hoja mama iliyokuwa mezani ya kuhujumiwa uchumi wa nchi na Richmond. Yaani kwa Kingunge na wenzake hujuma kwa nchi aliyosababisha Lowassa halikuwa tatizo ila kutokulindiwa heshima kwa kupewa kwanza nafasi ya kujieleza ndio waliloliona ni issue!!! Hii ndiyo hali ya ccm ya kulindana iliyotufikisha hapa tulipo leo.

Cha ajabu watu hawa hawa hawasikiki kamwe zinapokiukwa taratibu kwa lengo la kujinufaisha. Ziko taratibu nyingi tu zilizokiukwa katika kusaini mikataba mibovu ambazo hawa watu hawazisemi. Kwao taratibu zinazowauma zikikiukwa ni zila zinazowaumbua tu. Unless Tz, learn a new culture of transparency and accountability we will not make it as a nation. Arise Tanzania, unaliwa mchana mchana.
 

we ckilz,unaota?haya taja ushujaa wa membe hapa,ume2mwa ee
 
Sitta na Mwakyembe wanajaribu kuficha aibu. Najua hawachomoki katika hili. They were supposed to foresee the repucation of breaching the Dowans contract. Were are paying Dowans b'se of Bunge fail to foresee!!

It's shame to have those kind of people!
Ni aibu gani hiyo wanayoificha tuambie seems you are speaking the opposite nani kati ya kina Sitta na mnaotetea Dowans wanaojaribu kuficha aibu, jaribuni kumwogopa Mungu hata siku moja, nyie ndio mlioleta madudu how comes wanaopinga hayo madudu wawe ndio waficha siri tena.
 
Chikawe kuwakemea mawaziri wenzake anatumia mamlaka yake vibaya (ultra vires).

Wenzangu, haya mambo yoote yanayoendelea ni maandalizi ya 2015. Kila aliyepo kwenye nafasi sasa anaangalia mbele na anaangalia pia ajiunge na mtandao gani kujihakikishia nafasi in 2015. Alianza mwana sheria mkuu, akawakataza wadanganyika kuwa suala la dowans limefungwa, na hakuna mjadala. As if yeye ni Muumba, akawaambia Wadanganyika, keep your mouth shut, we are going to pay Dowans, whether you like it or not. Huyo ni mwanasheria mkuu wa nchi, katili na kichwa ngumu

Akaja huyu Ngeleja, ninavyomfahamu Ngeleja, yeye hana maamuzi, kaletewa tu minute mezani kuwa lipa. Kwanza nashangaa, suala la kulipa si la Ngeleja, ni suala la hazina. Ngeleja hana bajeti hiyo, na kama ni kulipa, alitakiwa aseme Waziri mwenye dhamana ya hazina au mkuu wa Tanesco, sio Waziri. But ni jinsi anavoona upepo wa 2015 kuwa ajiunge na mtandao upi, kila mtu anangalia upepo.

Kama hilo halikutosha, akaja wakili anaitwa Fungamtama, akatisha sana kuwa nchi itayumba Dowans wasipolipwa. In my life sikuwahi kuona wakili wa kujitegemea akifanya hivyo, huyu naye kasukumwa na ulafi na uchu wa fedha. Akamshambulia waziri Sita na kusema ana chuki binafsi. Loh, nikashangaa, Sita ana chuki binafsi na wale watu wa nje waliotajwa na Ngeleja kuwa ndio wamiliki wa Dowans. Sita ana haja gani ya kuwa na chuki binafsi na wamalysia? Wenye akili wakajua mmiliki halali wa Dowans ni nani, na si shaka huyo mmiliki Sita anamjua na ndio maana ana bifu naye

Sasa kaja naye Chikawe, ambaye sijui kama anajua maana ya utawala bora, manake alivyofafanua kuhusu Sitta na Mwakyembe, si maana halisi ya utawala bora. Utawala bora ni ule unashirikisha jamii katika maamuzi mazito ya nchi, mfano kuilipa Dowans. Ngeleja na kikundi kidogo cha wanasheria hawawezi kufanya matumizi ya fedha za walipa kodi ya shs hizo bila walipa kodi kuelezwa na kukubaliana na jambo hilo. Wawakilishi wa wananchi ni wabunge, ipelekwe legislation bungeni kuomba kibali cha kuilipa Dowans-- hup ndio utawala bora.
Chikawe, with due respect Nadhani unatakiwa uende Ngurdoto ujifunze maana ya utawala bora. Kubariki mikataba hewa, si utawala bora, kufanya matumizi bila ridhaa ya walipa kodi kama kuwalipa dowans, si utawala bora. Sita kutoa maoni yake, hakuna muingiliano na utawala bora, Sita kusema bila kumshauri boss wake hakuna uhusiano na utawala bora, hiyo inaweza kuwa ni insubordianation. Chikawe, please unabore, kwa sababu kama waziri wa utawala bora hajua maana ya utawala bora, anazungumzia insurbodination kuwa ni kukosa utawala bora, hafai
 
Hiyo ndiyo serikali ya JK, kila mmoja na lwake, anakuja huyu anasema hili, mwenzake anamrushia upupu ili aweze kumpiku kumbe ni urojo tu na akili mgando kama kawaida yao.

Chikawe atambue kuwa Sitta na Mwakyembe wametoa faraja kwa umma kuwa angalau wanapata uchungu kwa wizi wa mchana unaohalalishwa na Ngeleja kumlipa mwajiri wake wa zamani RA.

Chikawe ni kipofu na 'nyani asiyeona kundule' maana asiwalaumu wanaowaeleza umma ukweli eti wanakiuka utawala bora. ni porojo na kufilisika.

Yeye atupe ukweli toka ktk wizara yake kuhusu mali za vigogo ambao kwa mamia wamegoma kutaja utajiri wao na yeye hana kauli au lolote la kueleza umma. je huo ndio utawala bora?
asimtishe yeyote! hapo alipo naye kawekwa ili kuficha ufidhuli wa wakuu wake akiwepo JK na RA na mfano halisi ni kama hili la DOWANS. Apotelee mbali asizidishe uchungu na hasira kwa umma unaodhulumika kila uchao.
 


Mimi naona hawa wanatunishiana misuli.

Ningetamani kumsikia Sitta na Mwakiembe wakimnjibu Chikawe. Na kama wanaona kauli ya chikawe inapingana na mawazo yao, basi wajiuzulu ili waungane na wanachi na wanasheria wengine wapinge haya malipo mahakamani.
 
Chikawe hana akili hata chembe na sijui Kikwete aliwatoa wapi wa aina hii?? ni bora tu kikwete akawaingiza akina maralia sugu, mtu wa pwani nk watanzania tukajua moja, kuliko kuingiza mbunge sjui wa wapi ambaye anawaibisha waliomchagua!!! Hakika kama nchi hii ingelikuwa ni kenya kwa katiba mpya, wananchi wange petition na kumvua ubunge wake!!!
 
Wanachokifanya Sitta na Mwakyembe ni kama mtu mzima anapoona mtoto mdogo ametumbukia kwenye ndoo ya maji na wakachukua hatua ya kumtoa kumuokoa na baadaye kumtafuta mama yake (ni logic than sheria) kwa sababu ukimtafuta mama yake ili aje amuokoe huenda akawa ameshakufa. Uzalendo wa Mwakyembe na Sitta umewafanya kuona taratibu za kupeleka isshu kwenye baraza la mawaziri ni upotezaji wamuda ambao wizi wa Dowans huenda ukawa umeshafanyika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…