Brigedia Chan-ocha
JF-Expert Member
- Mar 7, 2014
- 1,353
- 2,842
Chief kalumana inasemekana amakamatwa na polisi akiwa eneo la kuapishwa mawakala na mawakala wa chadema hawajaapishwa hadi sasa.
=====
Jeshi la polisi mkoani Kagera limelazimika kutumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakiongozwa na mgombea ubunge jimbo la Bukoba Mjini, Chief Karumuna baada ya kugomewa kuapishwa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Bukoba mjini Mourice Limbe.
Mgombea huyo aligoma kutoka katika eneo la uwanja wa Kaitaba mara baada ya zoezi la kuwaapisha mawakala wa vyama vya siasa kukamilika akitaka wagombea nao waapishwe kauli iliyopingwa na msimamizi wa uchaguzi akisema wao wataapishwa kwa pamoja siku ya kesho.
=====
Jeshi la polisi mkoani Kagera limelazimika kutumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakiongozwa na mgombea ubunge jimbo la Bukoba Mjini, Chief Karumuna baada ya kugomewa kuapishwa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Bukoba mjini Mourice Limbe.
Mgombea huyo aligoma kutoka katika eneo la uwanja wa Kaitaba mara baada ya zoezi la kuwaapisha mawakala wa vyama vya siasa kukamilika akitaka wagombea nao waapishwe kauli iliyopingwa na msimamizi wa uchaguzi akisema wao wataapishwa kwa pamoja siku ya kesho.