Mahakama ya Bukoba imemwachia huru aliyekuwa mgombea Ubunge Bukoba Mjini (CHADEMA), Chief Kalumuna na wenzake 6

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,521
217,786
Tulionya Mapema sana kwamba Shetani hajawahi kumshinda Mungu katika lolote , na nadhani hata nyinyi wenyewe ni mashahidi, wote waliojipa uungu Mtu na kujimwambafai wanazidi kupukutika huku wengine wakiwa njiani.

Video hii inaonyesha umati wa watu wa Bukoba wakishangilia baada ya aliyekuwa Mgombea ubunge wa Chadema Kalumuna kushinda kesi ya uongo aliyobambikiwa.

=====

Mahakama ya wilaya Bukoba imemwachia huru aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Bukoba mjini kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Chif Karumuna na wafuasi wengine 6 wa chama hicho waliokuwa wanakabiliwa na mashitaka 8 likiwemo la kushambulia na kudhuru mwili wa askari polisi SSP Babu Sanare baada ya mahakama kutilia shaka hoja za ushahidi upande wa jamhuri.

Wafuasi hao wa CHADEMA walishitakiwa baada ya kutokea vurugu katika uwanja wa Kaitaba kulipokuwa kunafanyika zoezi la kuwaapisha wakala,wagombea udiwani na ubunge.




 
Tulionya Mapema sana kwamba Shetani hajawahi kumshinda Mungu , Video hii inaonyesha umati wa watu wa Bukoba wakishangilia baada ya aliyekuwa Mgombea ubunge wa Chadema Kalumuna kushinda kesi ya uongo aliyobambikiwa

View attachment 1772248
Mahakama kuu ina unafuu kidogo, ngoma ipo mahakama ya rufaa ni uozo mtupu, atarudishiwa ubunge wake na mahakama ya rufaa kule imejaa vilaza tupu
 
Kama mbunge katenguliwa na mahakama kiti chake huondolewa siku hiyo hiyo akikata rufaa akishinda anarudishiwia kiti
Mfano wa wabunge waliotenguliwa na mahakama:
1. Padri Simon Chiwanga Dodoma mjini uchaguzi wa 80-85
2. Makongolo Nyerere uchuguzi wa 200-2005
wengine, Wasira, Kihiyo

Nitashangaa kama Byabato wa Bukoba mjini ataendelea kukalia kiti.
 
BAVICHA_&_CHASO_(@bavicha.tz)_posted_on_Instagram_•_May_3,_2021_at_1:24pm_UTC%22_.jpg
 
Back
Top Bottom