Nebuchadinezzer
JF-Expert Member
- Oct 1, 2018
- 1,403
- 2,549
Pesa ina umuhimu mkubwa sana katika kuleta mahusiano mazuri ila pesa pekee yake kamwe haiwezi dumisha mahusiano.
Jirani yangu mzee Joseph ana pesa za kutosha. Anamiliki miradi mingi sana. Kuna kipindi alikosana na mkewe mama watoto wake. Sikujua chanzo cha ugomvi ni kipi ila nilichokuja kujua ndoa yao imevunjika na mwanamke akaanza kuishi anapopajua na akawa ameshapata mwanaume mwingine. Hali ya mzee Joseph ilianza kuzorota na haikuchukua miezi minne mzee wa watu aliaga dunia.
Wapo watu mashuhuri wengi tumeshuhudia wote namna gani afya zao zilivyozorota mara baada ya kuachwa na wake zao au waume zao bila kutegemea na badae afya zao zilizolota na hawakuchukua muda wakaungana na wafu.
Usicheze na mapenzi, mapenzi yanaua. Kamwe usidhanie kuwa uliyenae hawezi kukuacha eti Kwa sababu wewe ni tajiri, ni mtu mashuhuri, umeshakuzalia watoto...usijidanganye unaweza achwa na stress zikakuua.
Jamani tuchezeeni pesa, mapenzi tuyaheshimu.
"Tumia komoni sensi"
ASANTENI
Jirani yangu mzee Joseph ana pesa za kutosha. Anamiliki miradi mingi sana. Kuna kipindi alikosana na mkewe mama watoto wake. Sikujua chanzo cha ugomvi ni kipi ila nilichokuja kujua ndoa yao imevunjika na mwanamke akaanza kuishi anapopajua na akawa ameshapata mwanaume mwingine. Hali ya mzee Joseph ilianza kuzorota na haikuchukua miezi minne mzee wa watu aliaga dunia.
Wapo watu mashuhuri wengi tumeshuhudia wote namna gani afya zao zilivyozorota mara baada ya kuachwa na wake zao au waume zao bila kutegemea na badae afya zao zilizolota na hawakuchukua muda wakaungana na wafu.
Usicheze na mapenzi, mapenzi yanaua. Kamwe usidhanie kuwa uliyenae hawezi kukuacha eti Kwa sababu wewe ni tajiri, ni mtu mashuhuri, umeshakuzalia watoto...usijidanganye unaweza achwa na stress zikakuua.
Jamani tuchezeeni pesa, mapenzi tuyaheshimu.
"Tumia komoni sensi"
ASANTENI
