hii jokes au ndo kutesena tu sijui ana
Tumia cauchy euler equation formular utapata jibu kiulaini.
Kuna mtu kanitumia hili swali kwenye Simu yangu!!?
Nguo inauzwa Shilingi 10,000 lakini wewe huna pesa, Unaamua kwenda Kukopa kwa dada yako Shilingi 5,000 na ukakopa tena shilingi 5,000 kwa kaka yako na ukafanikiwa kuzipata shilingi 10,000 zinazohitajiwa kununulia Nguo. Dukani ukaomba upunguziwe bei ya nguo muuzaji akakubali kukuuzia kwa shilingi 9,700 na akakurudishia shilingi 300 kama chenji yako. Uliporudi nyumbani ukaamua kupunguza deni unalodaiwa na ndugu zako.
Ukatoa shilingi 100 ukampa dada yako na shilingi 100 ukampa kaka yako na wewe ukabakia na shilingi 100 kutoka katika ile chenji ya shilingi 300 uliyorudishiwa. Hivyo ukawa deni unalodaiwa na Kaka yako zimebaki shilingi 4,900 na deni la Dada yako pia shilingi 4,900. Ukijumlisha deni lililobaki la kaka yako na lile la dada yako 4,900+4,900 unapata shilingi 9,800 ukijumlisha na ile 100 uliyobakiwa nayo baada ya kuwalipa deni lao inakuwa 9,900. Jee 100 imekwenda wapi?
Kigarama nakuheshimu ujue?
Tatizo ulikimbia umande
hili toka 2008 linulizwa kwenye hii mitandao ya kijamii hadi nilishalichoka...