Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,217
- 10,285
Ninavyoelewa mimi ni kuwa kama hapatakuwa na mabaliko katika mfumo na utaratibu wa chaguzi zetu basi hapatakuwa na uchaguzi. Kimsingi sio wazo baya ila panahiajika ufafanuzi. Nina mawazo yafuatayo:
1. Nani ataamua kuwa reform zilizofanyika ni za dhati na zitaleta kweli mabadiliko. K.m. zimetangazwa nafasi za wasimamizi wao uchaguzi ila ukiangalia sifa zinazotakiwa ni kuwa ni walewale watarudi ingawa mabadiliko yamefanyika.
2. Nini maana ya "No elections"?
Hii inaweza kutimizwa kama wapiha kura hawatajitokeza. Hii ni ngumu kufanikiwa bila kutumia nguvu ( kuwazuia watu kutoka au kufunga vituo vya kupigoa kura) kwa sababu wako watu wengi tu ambao wangependa kupiga kura na hamna quorum ya uchaguzi.
Namna nyingine ni vyama vyote vya upinzani kugomea uchaguzi. Hili nalo ni ngumu kutimizwa maana kuna vyama vitaona ni fursa kutokana na vyama vikubwa vya upinzani kutoshiriki. Na hamna mahali panaposema kuwa uchaguzi unapoteza uhalali kama vyama fulani havitashiriki.
Mtego mwingine ni wagombea wazuri wa Chadema kukosa nafasi ya kujinadi kwa wananchi kwa sababu sera ya chama chao inasema No Elections. Kwa sababu hiyo hata "reforms " zikifanyika uwezo wa kushinda utapungua. Lakini kwa upande mwingine wanaweza kupata kura zaidi kama shukrani kutoka kwa wananchi kwa kuleta mabadiliko.
3. Chadema itangaze kuwa itajitayarisha kushiriki lakini uamuzi wa kushiriki au kutoshiriki utafanyika baadae.
4. Wakati huo Chadema kifanye juhudi za dhati za kutibu majeraha kwa kuwasikiliza wale wanaoamini hawatendewi haki. Wanaweza kuanza na Njombe kuhakikisha kuwa hakuna anaejiona kuwa ni mtoto wa kambo na mwingine ndio mwana mpendwa.
Wakubali kuwa kuna wanachama hawakubaliani na hii sera kama ambavyo wako ambao hawakukubaliana na sera ya maridhiano. Wawaache tu waongee maana wataweza kuiboresha kutokana na majadiliano hayo. Waache vitisho visio na maana.
Soma Pia:
Amandla...
1. Nani ataamua kuwa reform zilizofanyika ni za dhati na zitaleta kweli mabadiliko. K.m. zimetangazwa nafasi za wasimamizi wao uchaguzi ila ukiangalia sifa zinazotakiwa ni kuwa ni walewale watarudi ingawa mabadiliko yamefanyika.
2. Nini maana ya "No elections"?
Hii inaweza kutimizwa kama wapiha kura hawatajitokeza. Hii ni ngumu kufanikiwa bila kutumia nguvu ( kuwazuia watu kutoka au kufunga vituo vya kupigoa kura) kwa sababu wako watu wengi tu ambao wangependa kupiga kura na hamna quorum ya uchaguzi.
Namna nyingine ni vyama vyote vya upinzani kugomea uchaguzi. Hili nalo ni ngumu kutimizwa maana kuna vyama vitaona ni fursa kutokana na vyama vikubwa vya upinzani kutoshiriki. Na hamna mahali panaposema kuwa uchaguzi unapoteza uhalali kama vyama fulani havitashiriki.
Mtego mwingine ni wagombea wazuri wa Chadema kukosa nafasi ya kujinadi kwa wananchi kwa sababu sera ya chama chao inasema No Elections. Kwa sababu hiyo hata "reforms " zikifanyika uwezo wa kushinda utapungua. Lakini kwa upande mwingine wanaweza kupata kura zaidi kama shukrani kutoka kwa wananchi kwa kuleta mabadiliko.
3. Chadema itangaze kuwa itajitayarisha kushiriki lakini uamuzi wa kushiriki au kutoshiriki utafanyika baadae.
4. Wakati huo Chadema kifanye juhudi za dhati za kutibu majeraha kwa kuwasikiliza wale wanaoamini hawatendewi haki. Wanaweza kuanza na Njombe kuhakikisha kuwa hakuna anaejiona kuwa ni mtoto wa kambo na mwingine ndio mwana mpendwa.
Wakubali kuwa kuna wanachama hawakubaliani na hii sera kama ambavyo wako ambao hawakukubaliana na sera ya maridhiano. Wawaache tu waongee maana wataweza kuiboresha kutokana na majadiliano hayo. Waache vitisho visio na maana.
Soma Pia:
- Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
- Tundu Lissu: Kauli ya No Reform No Election hatujasema tunasusia Uchaguzi. Tutaongea na Rais Samia lugha atakayoielewa
Amandla...