Changamoto za kupata wachumba wa mtandaoni

Changamoto za kupata wachumba wa mtandaoni

julius caesar

Member
Joined
Mar 20, 2015
Posts
94
Reaction score
27
Habari wakuu, natumaini mko poa.

Leo ningependa kutoa ushuhuda wangu juu ya changamoto za kupata wachumba wa mtandaoni.

Muda mrefu umepita niliwahi kutuma post ya kutafuta mchumba wa kuoa hapa Jamii Forum, nashukuru Mungu baadhi ya wasichana wali respond vizuri nikafanya nao mawasiliano then nikaamua kuchagua mmoja ambae niliona ananifaa, sema tatizo yeye alikuwa anaishi mkoa mwingine na mmi naishi mkoa mwingine, lakini mmi niliamua kumkubalia tuwe pamoja kwa sababu niliamini po siku tungeonana pengine ningeweza kwenda mkoani anapoishi au yeye kuja ninapoishi.

Tulianza kuishi kama wapenzi kwa mawasiliano lakini changamoto iliyojitokeza yule binti alianza kuniomba pesa za matumizi nimtumie lakini mmi sikumpa nilimwambia sina baada ya hivyo binti akaanza kulalamika kuwa mmi simpendi na mambo mengine mengi!, Hivi wandugu kweli inawezekana kumhudumia mpenzi ambae hujawahi kuonana nae live yani face to face? Ambae pia bado hujamsoma tabia yake vizuri zaidi?

Sio siri huyo binti moyo wangu ulimpenda sana, lakini ilikuwa ni mapema sana kumuamini, hizo pesa alizohitaji nilikuwa na uwezo wa kumhudumia sema sijawahi kumuona live nimeona picha zake tu na tumewasilana kwenye simu tu, ningependa maoni yenu wadau kwenye hili.

Hivi huyu binti anastahili kutumiwa pesa kweli?
 
Kwani mnaishi mtwara na kigoma kiasi kwamba ni shida hata wikiend moja kufika anakoishi mwenzio.??

kuna watu wanalalamikaga humu kuwa wadada wa humu wanaanzaga na kuvuna pesa badala ya kujenga trust kwanza.
hii ni changamoto ambayo dada zetu inabidi waifanyie kazi. sio kila mtu ni mpita njia kwamba maji utamuuzia. wengine ni wakaaji
 
Kama umemkubali na unazo we mpe tu, it ain't trickin if you got it, bruv. Besides, you the Caesar.
 
Bila kuonana kwanza kuhudumia mtu roho inakaaa kabisa. Fanya mipango muonane kwanza, mzungumze, alafu vingine vitafuata.
 
kwani mnaishi mtwara na kigoma kiasi kwamba ni shida hata wikiend moja kufika anakoishi mwenzio.??

kuna watu wanalalamikaga humu kuwa wadada wa humu wanaanzaga na kuvuna pesa badala ya kujenga trust kwanza.
hii ni changamoto ambayo dada zetu inabidi waifanyie kazi. sio kila mtu ni mpita njia kwamba maji utamuuzia. wengine ni wakaaji

Ni changamoto sana mkuu kwa hawa Dada zetu!
 
Tuma pesa bwana acha ubahiri huko!!! Teh teh teh
Naye si yupo humu? Subiri naye atakuja kukushauri kama umtumie au laah!
 
Usimtumie hela bali tafuta muda unakaonane naye kwanza ana kwa ana, usikute hata picha alizokutumia si zake.

Halafu kama nia yako ni uchumba kweli kweli, stuka kwa anayeomba omba hela ilhali hata hamjafahamiana vizuri, utalia baadae. Kwa taarifa yako wanawake wako wengi mno, lakini wa kuoa ni wa kumulika na tochi, si kila mwanamke ni wife material
 
Usimtumie hela bali tafuta muda unakaonane naye kwanza ana kwa ana, usikute hata picha alizokutumia si zake.

Halafu kama nia yako ni uchumba kweli kweli, stuka kwa anayeomba omba hela ilhali hata hamjafahamiana vizuri, utalia baadae. Kwa taarifa yako wanawake wako wengi mno, lakini wa kuoa ni wa kumulika na tochi, si kila mwanamke ni wife material

Wacha we mito ktk ubora wake! Acha kumbania mwenzio huko, atume hela tu mengine ni ajali kazini, teh teh teh
 
Last edited by a moderator:
Tuma pesa bwana acha ubahiri huko!!! Teh teh teh
Naye si yupo humu? Subiri naye atakuja kukushauri kama umtumie au laah!

Sista unaonaje na mimi niweke bandiko la kutafuta mke wa pili
 
Wacha we mito ktk ubora wake! Acha kumbania mwenzio huko, atume hela tu mengine ni ajali kazini, teh teh teh

Aaaaha sista bana, kumbe umeishanibamba tayari, haya nijibu hiyo quote yangu jingine basi
 
Usimtumie hela bali tafuta muda unakaonane naye kwanza ana kwa ana, usikute hata picha alizokutumia si zake.

Halafu kama nia yako ni uchumba kweli kweli, stuka kwa anayeomba omba hela ilhali hata hamjafahamiana vizuri, utalia baadae. Kwa taarifa yako wanawake wako wengi mno, lakini wa kuoa ni wa kumulika na tochi, si kila mwanamke ni wife material

Boss, sidhani kama kuna Mwanamke/Manzi yeyote humu ambaye utatangaza unatafuta mchumba/mke, ajitokeze na awe normal. Lazima ana flaws za kutosha ndio maana kashindwa kupata mtu in the real world. Vizuri havipatikani kirahisi kamwe. So wanaojitokeza kutangaza hizo nafasi, inabidi wawe wamejiandaa kisaikolojia.
 
Boss, sidhani kama kuna Mwanamke/Manzi yeyote humu ambaye utatangaza unatafuta mchumba/mke, ajitokeze na awe normal. Lazima ana flaws za kutosha ndio maana kashindwa kupata mtu in the real world. Vizuri havipatikani kirahisi kamwe. So wanaojitokeza kutangaza hizo nafasi, inabidi wawe wamejiandaa kisaikolojia.

You are right mkuu, hata mimi nina mtazamo kama wako
 
Hakikisha hufuti zile PM zote. Utakuwa unabadilisha tu kama spare za tairi hadi umpate wa ukweli.

Afu huyu atakuwa Mchaga tu(hata kama ka kwambia yupo Mbeya ni uongo; yupo Rombo huyo).
 
Back
Top Bottom