Changamoto nayopitia bank ya FNB

Changamoto nayopitia bank ya FNB

Ninavyojua tangu mwaka jana au juzi FNB ilikuwa na mpango wa kufunga shughuli zake hapa nchini na nimeshangaa kusikia kwamba bado wanaendelea na operations zao!

Nakushauri ukiweza ondoa kila kitu chako na uweke kwenye benki nyingine kwani huwezi kujua usumbufu utakaotokea endapo watafunga benki kutokana na kufilisika. Hii benki chimbuko lake ni Africa Kusini ni benki kubwa kule.
MABENKI MENGI YALITETEREKA AWAMU YA TANO, NA MENGINE KUFILISIKA KABISA, MENGI YAPO KWENYE KUJIPANGA UPYA KUTOKANA NA BIASHARA KUANZA KUFUNGUKA UPYA NA MZUNGUKO KURUDI KWENYE HALI YAKE,
Awamu ya tano ilikuwa ni janga kwa taifa letu.
ASANTE, MAMA, DR. SAMIA, KAZI IENDELEE.
 
Hio si nilisikia imefilisika.

Siku wakifungua hio akaunti chukua mpunga wako wote achana nao mazima.

Pesa zako mwenyewe ila wanakupa shida.

Ndio maana sometimes huwa Sina imani na hizi benki.
 
Kwa maneno haya unataka kusema mdau atakuwa amepigwa kwenye mshono? Nayajua maumivu yake.

Hizi bank za kuunga unga toka ile efata iondoke na million nane zangu hunikuti humo, NMB na CRDB japokuwa wana vitozo vya ajabu ajabu lakini bado wanafaa sana kwa sisi wa vipato vya kawaida.
Mkuu ilikuwaje mpaka ukaweka pesa kwenye Bank za kitapeli, huyo Efata ana mchukia Magufuli mpaka kesho.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
NMB CRDB NBC hizi ndiyo bank za TANZANIA za uhakika na salama muda wote... Tatizo lenu WaTz mnapenda sana vya bure mnataka muweke pesa bank isikatwe hata shilingi mia, sasa bank itajiendeshaje kama sio kufa na kudhulumu wateja...
Mkuu Equity nayo vipi ni Bank ya Mchongo? Mifumo yao ya kiutendaji kama ya usanii fulani, wanafungua akaunti kama unasajili lain ya simu

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
FNB ilishafunga Ofisi zote Tanzania huyu jamaa alien da FNB ipi, account zote ziliamishiwa Exim tokea mwaka Jana. FNB hakuna Tena Tanzania na hata haina mfanyakazi mmoja hapa Tanzania
Bado wapo Mkuu wanafanya kazi, huyo mtoa mada si kasema alienda bank wakampa fomu ajaze taarifa zake ?

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Watu wanaongea tu, bank kama ABSA kwangu ni bank bora kuliko bank zote za ndani ( local ), huduma za jamaa faster sana hadi unafurahi, kwa sie wafanya online transaction na internet bank ndio mwake
Hiyo Absa wanamakato makubwa yani hadi wageni wanaikimbia kutoa pesa kwenye ATM zao, Wazungu wakitaka kutoa pesa kwenye ATM wanapenda kutoa ATM za mabank ya ndani

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
unazunguka dsm, mwanza, dodoma na nje ya nchi nini? Hufiki wilayani, btw hata baadhi ya makao makuu ya mikoa hayana bank hii, kigoma mmojawapo, Mimi pia mteja wa absa since barclays days, lakini ukosefu wa mtandao wa matawi ni big weakness. Hao na kina Equity, Eco bank etc ni bank za mijini tu
Ni kweli ukipoteza kadi kama upo Songea inakubidi upande Basi kwenda Dar kufata kadi mpya.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Nimekuwa mteja wa muda mrefu wa hii bank ya Fnb kwa muda mrefu sana na sikuwahi kupitia changamoto yeyote hadi wiki iliyopita ndio nikakutana na kizaazaa!

Ipo hivi hii bank huwa natumia kusave vipesa navyopata kwa malengo ya muda mrefu kwavile huwa hawana makato ya hapa na pale!

Sasa wiki iliyopita nikawa na shida na pesa yakuzungushia kwenye biashara yangu inabidi niende kuchukua kama milioni 3 hivi mara naambiwa akaunti yangu imeblokiwa kwahiyo siwezi kufanya muamala wowote!

Sema kweli nilichanganyikiwa kutokana nilikuwa nahitaji hiyo pesa haraka sana iwezekanavyo!

Ikabidi niulize kulikoni kufunga account ya mteja bila taarifa yeyote bila sababu za msingi? Nikajibiwa kwamba inabidi nijaze taarifa zangu upya za ki bank!

Kweli nikafanya hivyo na ukizingatia pia nilishajaza taarifa zangu upya miaka miwili tu iliyopita,lkn cha ajabu hadi leo siku ya 8 hawajafungua akaunti yangu ni danadana tu kwa kwenda mbele,nimeenda bank mara mbili mwendo ni kujaza fomu kila kukicha!

Nimejaribu kupiga simu huduma kwa wateja wanasema ombi langu wanalishughulikia hadi nimechoka wakuu!
Msaada wakuu nina ninachotakiwa kufanya maana mipango yangu imesimama huku nikiteseka na pesa zangu mwenyewe!
Mayu paso wa ya lia ku mwako [emoji23] somethings went wrong manka ku BOT fastaaaa
 
Barclay ,Stanbic and the like ni uchafu tuuu!!? Eti benk Ina tawi Samora avenue tuu!! Na masaki!! Sasa ukiwa iramba masharika inakuwaje!?acha ulimbukeni aisee
Banking ni sector imeshakuwa advanced sana siku hizi.
Na ushamba wako unadhani huduma mpaka uende tawini.
Siku ukitumia stanchart ndo utajua maana ya advanced banking services.
Kwanza unaenda kwenye tawi la bank kufanya nini.?
 
Nimekuwa mteja wa muda mrefu wa hii bank ya Fnb kwa muda mrefu sana na sikuwahi kupitia changamoto yeyote hadi wiki iliyopita ndio nikakutana na kizaazaa!

Ipo hivi hii bank huwa natumia kusave vipesa navyopata kwa malengo ya muda mrefu kwavile huwa hawana makato ya hapa na pale!

Sasa wiki iliyopita nikawa na shida na pesa yakuzungushia kwenye biashara yangu inabidi niende kuchukua kama milioni 3 hivi mara naambiwa akaunti yangu imeblokiwa kwahiyo siwezi kufanya muamala wowote!

Sema kweli nilichanganyikiwa kutokana nilikuwa nahitaji hiyo pesa haraka sana iwezekanavyo!

Ikabidi niulize kulikoni kufunga account ya mteja bila taarifa yeyote bila sababu za msingi? Nikajibiwa kwamba inabidi nijaze taarifa zangu upya za ki bank!

Kweli nikafanya hivyo na ukizingatia pia nilishajaza taarifa zangu upya miaka miwili tu iliyopita,lkn cha ajabu hadi leo siku ya 8 hawajafungua akaunti yangu ni danadana tu kwa kwenda mbele,nimeenda bank mara mbili mwendo ni kujaza fomu kila kukicha!

Nimejaribu kupiga simu huduma kwa wateja wanasema ombi langu wanalishughulikia hadi nimechoka wakuu!
Msaada wakuu nina ninachotakiwa kufanya maana mipango yangu imesimama huku nikiteseka na pesa zangu mwenyewe!
Kesho asubuhi amka ongoza BOT moja kwa moja
 
NMB CRDB NBC hizi ndiyo bank za TANZANIA za uhakika na salama muda wote... Tatizo lenu WaTz mnapenda sana vya bure mnataka muweke pesa bank isikatwe hata shilingi mia, sasa bank itajiendeshaje kama sio kufa na kudhulumu wateja...
Hayo mabilioni ya pesa wanayokaa nayo si wanakopesha huko na kulipisha riba za mabilioni ya pesa. Huoni kama inatosha kabisa kuwa sababu ya kutowachaji wateja wa account za akiba chochote kwa kuweka hela zao hapo bank?!
 
FNB ilishafunga Ofisi zote Tanzania huyu jamaa alien da FNB ipi, account zote ziliamishiwa Exim tokea mwaka Jana. FNB hakuna Tena Tanzania na hata haina mfanyakazi mmoja hapa Tanzania
Mbona kuna ATM yao moja naionaga OYSTERBAY shopping centre pale na nina hisi ina fanya kazi maana bado ipo mpaka leo.
 
MABENKI MENGI YALITETEREKA AWAMU YA TANO, NA MENGINE KUFILISIKA KABISA, MENGI YAPO KWENYE KUJIPANGA UPYA KUTOKANA NA BIASHARA KUANZA KUFUNGUKA UPYA NA MZUNGUKO KURUDI KWENYE HALI YAKE,
Awamu ya tano ilikuwa ni janga kwa taifa letu.
ASANTE, MAMA, DR. SAMIA, KAZI IENDELEE.
Bank kabla ya awamu ya tano zilikuwa vibaya na hata sasa zipo vibaya, na hili ni dunia nzimaa... ikichangiwa pia na covid kama moja wa sababu..
 
Back
Top Bottom