Changamoto nayopitia bank ya FNB

Changamoto nayopitia bank ya FNB

Yes i know...na fine ni one million kwa kila siku tangu issue imerepotiwa bila kufanyiwa kazi.so kama issue ipo pending for 30 days..basi itakua ni 30*1000,000 so total ni 30,000,000m.. therefore wwkipigwa fine ndo adabu itakuja na hiyo option yakwenda BOT ni last option baada ya hizi jitihada zake za kuhangaika na Exim bank(fnb acquirer) kugonga mwamba. Na anataikiwa a lodge official complaint kwenda bank husika na a baki na copy yake ya complain lodgement na agongewe muhuri wakuonesha complain yake ilikua received.
Mimi pia nipo financial institution najua uchungu huu na hiyo ishu yake ni ndogo sana only 30 minutes iko poa,hamna haja ya kufika huko aishie kwa Branch manager inaisha
 
Juzi kati yalinikuta NMB.
Nilikuwa sina hata 100 nikamchukua boda hadi OPEN pale biafra, kufika pale wanaweka hela. Kutokana na haraka zangu nikamwambia boda twende Morocco, kufika pale tukaambiwa ATM mbovu ina siku 2. Nikamwambia boda turudi OPEN watakuwa wameshaweka hela.

Baada ya kufika, aliyekuwa mbele yangu mteja wa bank tofauti na NMB, hela ilitoka na alipata msg, but hela haikutoka.
Roho ilisita kutoa lakini nikafanya kama nacheza kamari tu. Nikatoa, ATM ikahesabu hela kisha ikatulia na ikahesabu kwa mara ya pili, ikafungua kimlango cha kutolea hela na kufunga tena. Hapo hapo nikapata msg kuwa nimetoa hela, but no hela.

Baada ya dakika 2 nikapata msg kuwa hela imerudishwa kwenye akaunti, nikajaribu kutoa tena, ikanifanyia mchezo ule ule.
Hapo nikaamua kwenda Mwanamboka ATM ya CRDB na ndio nikafanikiwa.
Sasa hivi kadi yao nikichomeka ATM nikichagua lugha tu inatema, nikienda ATM tofauti na NMB inafanya kazi. Nilirepot tatizo wanasema kabda imekufa niombe nyingine.

Hizi ndio bank za kiz
 
Banking ni sector imeshakuwa advanced sana siku hizi.
Na ushamba wako unadhani huduma mpaka uende tawini.
Siku ukitumia stanchart ndo utajua maana ya advanced banking services.
Kwanza unaenda kwenye tawi la bank kufanya nini.?
Advanced kwa wafanyakazi na wafanyabiashara wa mjini, sio sisi wa bush hazija cater mahitaji yetu wa bushi
 
Kitambulisho tu cha taifa unafungua account
Yes tena kwa mfano Equity nilifungua na Kitambulisho cha kupigia kura tu, back 2017. Ila kwa sasa watakuwa wanataka NIDA.

Ndani ya nusu saa nilikuwa nishakamilisha kila kitu na mpaka Visa card yenye jina langu washaniprintia.

KCB ndio nilitumia NIDA na wenyewe ndani ya muda mfupi account ikawa tayari. Ila kadi nilisubiri 3 weeks maana kadi zao zinatoka Kenya.
 
Bado wapo Mkuu wanafanya kazi, huyo mtoa mada si kasema alienda bank wakampa fomu ajaze taarifa zake ?

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Bro Mimi nilikuwa na account mbili zote ziliamishiwa Exim tokea July mwaka Jana . FNB wakati wanafunga kazi wikuwa wamebaki na branch 3 tu head office ambayo ilikuwa Amani place Ohio Street, peninsula branch ambayo ilikuwa Toure drive masaki na Arusha branch. Nina fahamiana na wafanyakazi wake. wote walikipwa mafao Yao zikafungwa zote mwaka Jana . Naomba unitajie hata branch ya FNB ambayo iko wazi

 
Nimekuwa mteja wa muda mrefu wa hii bank ya Fnb kwa muda mrefu sana na sikuwahi kupitia changamoto yeyote hadi wiki iliyopita ndio nikakutana na kizaazaa!
Samahani mkuu, nje mada wewe ni Mguu wa Chemba au ni pacha wake ?
 
Kwa maneno haya unataka kusema mdau atakuwa amepigwa kwenye mshono? Nayajua maumivu yake.

Hizi bank za kuunga unga toka ile efata iondoke na million nane zangu hunikuti humo, NMB na CRDB japokuwa wana vitozo vya ajabu ajabu lakini bado wanafaa sana kwa sisi wa vipato vya kawaida.
Efata ndoo benki ipi hio mkuu.....si ungeomba refund??
 
Yes tena kwa mfano Equity nilifungua na Kitambulisho cha kupigia kura tu, back 2017. Ila kwa sasa watakuwa wanataka NIDA.

Ndani ya nusu saa nilikuwa nishakamilisha kila kitu na mpaka Visa card yenye jina langu washaniprintia.

KCB ndio nilitumia NIDA na wenyewe ndani ya muda mfupi account ikawa tayari. Ila kadi nilisubiri 3 weeks maana kadi zao zinatoka Kenya.
Naomba faida za equity bank(ikiwemo makato ukitoa benk zao n.k).......pia mahitaji ukitaka kufungua akaunti ni yapi??
 
Naomba faida za equity bank(ikiwemo makato ukitoa benk zao n.k).......pia mahitaji ukitaka kufungua akaunti ni yapi??
Beba nida nenda tawi la benk hakuna mahitaji yoyote, me nilifungua kwa voters id mwaka 2017,

By then account niliyokuwa natumia haikuwa na makato, zaidi labda wakati wa kutoa hela, ila makato ya mwezi hayakuwepo, labda wataalamu watakuja na maelezo zaidi.
 
Tanzania ni nchi iliyolala, umeweka pesa benki, unataka kuzungusha biashara. Tafuta wakili mzuri wafungulie kesi benki ukieleza jinsi ulivyoathirika na wao kuzuia pesa yako.
 
Back
Top Bottom