Changamoto kwenye simu za Google Pixel kwisha sasa

Changamoto kwenye simu za Google Pixel kwisha sasa

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
1,285
Reaction score
2,595
1_20260507_014952_0000.png


Hatimaye Google wameachia update mpya kwa watumiaji wa simu za Google Pixel ili kuondoa changamoto ya kukatika kwa mtandao.

Si unakumbuka wiki kadhaa zilizopita tuliposti makala kuhusu changamoto zilizowakumba watumiaji wa Simu za Google Pixel 6 series, 7 series, 8 series, 9 na 10 Series.

2_20260507_014953_0001.png
3_20260507_014953_0002.png


Update mpya imekuja kuweza kutatua changamoto mbalimbali;
🛜 tatizo la simu kupoteza network au ukipigiwa unaambiwa haupatikani.
🪫 Tatizo la betri la simu yako kuisha Haraka.

4_20260507_014953_0003.png
5_20260507_014953_0004.png


📸 Kamera kupoteza ubora kwenye kupiga picha.
📲 Kioo Cha simu kucheza cheza (display flickering) na mistari inajitokeza.
🔥 Simu kupata Sana Joto balaa nk.

6_20260507_014953_0005.png
7_20260507_014953_0006.png


Kama ulikumbana na hii Changamoto unapaswa kufanya update ili kuweza kutatua hizo shida kwenye kifaa Chako, Google wametoa update ili kuweza kujianda watumiaji wa Android kupokea toleo jipya la Android 17 wiki ijayo.

8_20260507_014953_0007.png


Pia update hii ni Muhimu ili kuongeza Usalama zaidi kwenye vifaa vya Google Pixels hakikisha unafanya update 👋.
 
Back
Top Bottom