Kitoabu
JF-Expert Member
- Jul 7, 2011
- 10,327
- 10,943
Sijaelewa unazungumzia ndoo gani? Yamaji au yarangi? Leo lazima tumfunge paka kengele.Ni kawaida ya mafukara wanapoona nyumba ya tajiri ikiungua wao kushangilia wakiamini chama chao hatimae kinapata mwanachama mpya tena wasiyemtegemea bahati mbaya hawatambui kuwa nyumba za matajiri zinakatiwa bima.
Ninachofahamu leo CR7 akishirikiana na wadau wenzie wa BBC ndani ya ardhi aliyozaliwa atakata kiu ya muda mrefu wadau wote Santiago Bernabeu kwa kutukabidhi ndoo la 10 ndani ya dkk 90.
Mtoto asili yake nepi na unapomvua asubuhi lazima ukute imeloana na imeongezeka uzito kwa mafurushi aliyoyaporomosha usiku.
cc. Kitoabu