Kubwajinga
JF-Expert Member
- Jan 23, 2008
- 2,194
- 297
- Sasa mkuu naomba uwataje wenye harufu na ubalozi ili tujiajngalie kama ni kweli, ninakuruhusu uwataje hao unaodhani wana harufu ya ubalozi.
William.
- Mkuu acha majungu huwasaidii wananchi wengi wanaotaka kwua na hii jumuiya, haya yako ni majungu hao wamekwedna ubalozini kama walivyokuja hapa kama wanavyosema, sasa haina maana hiki chama kitakwua cha JF simply huna hoja kama unayo ungetaja acha uzushi mkuu.
FMEs
Wakuu Malecela & FMEs,
Hivi mnafikiri kuna mTZ anayechukia tukipata chama cha kutujumuisha huku nyikani?
Kwanza ni kitu cha kushangaza sana na kusikitisha kuona kuwa waTZ wa jiji kama la NY na vitongoji vyake mpaka leo hii hawana jumuiya yao licha ya wingi wao katika hayo maeneo.
Lakini inaelekea tatizo sio waTZ bali ni baadhi tu ya watu wanaotaka kuanzisha vyama kwa maslahi yao binafsi halafu inaelekea hawambiliki.
Mkuu Malecela, wewe mwenyewe ambaye mke wako ndio mtumishi wa muda mrefu kuliko wote hapo ubalozini NY, sijui unategemea tukueleweje unapokuja na tangazo kuwa eti;
- Mmeshapewa rukhsa na Balozi kuanzisha chama na chama kimeshaandikishwa na wewe ambaye ni mtegemezi wa ubalozi ni mmoja wa viongozi.
- Katiba na Website ya chama tayari viko mbioni sijui nani anayevigharimia wakati wanachama hawajakutana?
- Hukutueleza ni jinsi gani mlivyokutana mkaamua kuanzisha chama kwa ajili ya waTZ wote bila kuwashirikisha hao wanaotakiwa kukimiliki chama.
- Hukutufahamisha kuwa ni nani na vipi mliteuliwa kuwa viongozi, wasifu wenu ni upi n.k, hata kama nyie ni viongozi wa muda (interim). Hapa mnaonekana kujiona kama vile mko above all other TZs ambao mnategemea kufuata mnachowaeleza tu. This is a typical behavior of waungwana serikalini, something that we are all very much familiar with.