Chama Kipya Kuundwa Karibuni!!

Chama Kipya Kuundwa Karibuni!!

Nilitaka nijibu
lakini nikaiogopa avatar yako.

Heri ya mwaka mpya Feedback
Sasa Zitto atapumua uenyekiti huooo anaukwaa,

ushauri atangulize masilahi ya chama mbele na si Zitto kwanza atafanikiwa.
 
Last edited by a moderator:
maskini Rungwe amebaki mwenyewe CHAUMMA,uvumilivu wote anavuna usaliti
Waberoya,
kuna thread ya 2010 uliwataja 'hawa' kuwa walihusika na mapinduzi Udsm 2002/03
 
Last edited by a moderator:
Vimeshaundwa vyama vingi sana kabla ya hichi kipya! nothing new
 
1.jpg

HAWA JAMAA HAWAWEZI KULA KWENYE ZIZ MOJA. NAFUU KILA MTUA APATE CHUMBA CHAKE
 
maskini Rungwe amebaki mwenyewe CHAUMMA,uvumilivu wote anavuna usaliti
Waberoya,
kuna thread ya 2010 uliwataja 'hawa' kuwa walihusika na mapinduzi Udsm 2002/03
Bei Mbaya umenikumbusha, ile thread Waberoya alimponda sana Zitto kuwa ni msaliti wa demokrasia akishirikiana na Ridhwani na akina Omalyas ngoja niitafute.
 
Huyo msajili hafanyi due deligence? Mtu aliyefukuzwa Chama fulani ina maana hana adabu. Sasa akianzisha chake si ndio balaa tupu. Hawa ndio huzalisha maalshabab. Think deep mr Msajili.
 
Hongera zao!
Hoep watakuwa wapinzania makini, wakiwa Vibaraka hakika tuatwapinga milele.

Mkuu umakini utatoka wapi? Ikiwa %kubwa ya hao waanzilishi ni wahanga wa vyama vilivyopo hiyo spirit wanayotoka nayo huko walikofukuzwa watahama nayo! Uctegemee jambo jipya! Kujenga chama kikakubalika c shughuli ndg! hao CDM wanazaidia ya 20yrs hadi wa2 timamu kuwakubali mi nadhani hilo wazo la ccm kutaka kugawa kura kwenye chaguzi Rejea ZAIRE kipindi cha MOBOTU,,,!
 
Sasa hivi tuko kwanza kwenye mapinduzi ya zanziba. Wakati mkifuatilia mapinduzi ya zanziba polisi wa arusha sana sana wa kituo cha usa fuatilieni jambazi lilopigwa risasi na polisi mpakani maeneo ya holili likatoroka liko arusha hospitali ya sharak linatibiwa kwa usiri mkubwa sana kwani amegawa hela kwa daktari na manerse(sisters) ili wasipeleke repot polis (hospitali iko 1km kutokea arusha mjini kabla ujafika makumira university)

Nimefuatilia, ni kweli kwamba huyu mtu amelazwa katika hospitali hiyo baada ya kupigwa risasi na Polisi. Alipigwa risasi eneo la Karangai wakati walipokuwa wamebeba mkaa wa magendo katika lori ambalo liliposimamishwa na polisi halikusimama, polisi walilifuatilia wakalipiga risasi matairi likapinduka yeye na wenzake wakashuka toka garini wakaanza kutimua mbio ndipo alipopigwa risasi, polisi waliambiwa na mtoa taarifa kuwa walikuwa ni majangili wamebeba pembe za ndovu na wana bunduki, lakini gari lilipopekuliwa halikukutwa na vitu hivyo. Hivyo utaona si kweli kuwa alipigwa risasi huko Holili, hata hivyo majeruhi huyo anayo asili ya huko Rombo/Holili jina linahifadhiwa kwani matibabu ni suala la faragha ya mgonjwa. Mtoa taarifa umefanya vizuri kutoa taarifa hizi japo zinakasoro kadhaa, zimebeba ukweli mmoja tuu, kuna mtu mwenye jeraha la risasi anatibiwa katika hospitali hiyo.
 
maskini Rungwe amebaki mwenyewe CHAUMMA,uvumilivu wote anavuna usaliti
Waberoya,
kuna thread ya 2010 uliwataja 'hawa' kuwa walihusika na mapinduzi Udsm 2002/03

Bei Mbaya umenikumbusha, ile thread Waberoya alimponda sana Zitto kuwa ni msaliti wa demokrasia akishirikiana na Ridhwani na akina Omalyas ngoja niitafute.

haa ha haaa mambo ya chuo yale

lakini niliandika kwa mtindo wa kutaka majibu, nilipata majibu yangu na niliridhika sina misimamo ya kibishi

Zitto alijibu na nikapata uhakika kutoka kwa watu kadhaa, zitto at that time alikuwa na conflict na uongozi wa chuo wakatumia loophole ile kumsimamisha-wengine tukajua alisimamishwa kwa sababu ya yale mapinduzi. sidhani pale kama kuna issueza za usaliti
 
Huyo msajili hafanyi due deligence? Mtu aliyefukuzwa Chama fulani ina maana hana adabu. Sasa akianzisha chake si ndio balaa tupu. Hawa ndio huzalisha maalshabab. Think deep mr Msajili.
Ndugu yangu hii ndiyo Tanzania hata huko asipokuwa mwenyekiti sheria zinamruhusu kuanzisha chama kingine hadi ndoto yake itimie.
 
Mi nadhani hii sheri ya kuansishwa vyama vipya vya siasa inatakiwa iangaliwe upya! kwani mwishowe tutakuwa na vyama 300, hivi 23 ni vingi mno vipunguzwe vibaki 4 tu!

*Chadaiwa kuundwa na waliofukuzwa upinzani
WAKATI fukuto la kufukuzwa uanachama kwenye
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
likiwa bado bichi, chama kipya cha siasa kimeanzishwa
na watu wanaodaiwa kuwa ni muungano wa
wanachama waliofukuzwa kutoka vyama vya upinzani
nchini.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Ofisi
ya Msajili wa vyama vya siasa nchini, zinakitaja chama
hicho kuwa ni African Alliance for Change and
Transparence (AACT) na kwamba mipango ya usajili wa
muda wa chama hicho inadaiwa kuanza kuratibiwa kwa
takribani mwezi mmoja sasa.
MTANZANIA Jumapili limedokezwa kuwa, tayari chama
hicho kimekamilisha baadhi ya taratibu na kinatarajiwa
kupewa usajili wa muda na Ofisi ya Msajili wa Vyama
vya Siasa siku ya Jumanne, wiki ijayo.
Gazeti hili limedokezwa kuwa iwapo chama hicho
kitapata usajili huo, upo uwezekano wa wanachama
waliofukuzwa uanachama kutoka Chadema hivi karibuni
kujiunga na chama hicho.
Wanasiasa wengine wanaotajwa ama kuwa nyuma ya
kuanzishwa kwa chama hicho au wanatarajia kujiunga,
ni wale waliofukuzwa kutoka CUF, nia ikiwa ni
kuendeleza harakati zao za kisiasa.
Mmoja wa watu wanaounda chama hicho alilidokeza
gazeti hili kuwa endapo chama hicho kitapata usajili
baada ya hapo, taratibu na harakati za kuanza
kukitangaza zitafanyika katika maeneo mbalimbali
nchini.
Alisema pia wamepanga kuendesha siasa zenye
upinzani, ikiwa ni pamoja na kushiriki katika uchaguzi
wa serikali za mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2015 iwapo
kitakuwa tayari kimejiimarisha.
MTANZANIA Jumapili limedokezwa kuwa mchakato wa
kuanzisha chama kwa wanachama waliofukuzwa
upinzani, ulianza kitambo, ukilenga nia yao ya
kuhakikisha wanashiriki katika chaguzi hizo.
Hivi karibuni Kamati Kuu Chadema, iliwavua uanachama
aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha,
Samson Mwigamba na Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk.
Kitila Mkumbo, huku Mbunge wa Kigoma Kaskazini,
Zitto Kabwe, akikimbilia Mahakamani kuomba zuio la
kutojadiliwa uanachama wake na kikao hicho.
Zitto, Dk. Kitila na Mwigamba walituhumiwa na uongozi
wa juu wa Chadema kuandaa waraka wa siri wenye
lengo la kufanya mabadiliko ya uongozi ndani ya
chama, hali iliyoibua mgogoro mzito hadi kufikia uamuzi
wa kuwavua uanachama baadhi yao.
Aidha taarifa nyingine ambazo MTANZANA Jumapili
limezipata zinaeleza kuwa mbali na AACT, chama
kingine kilichopata usajili wa muda hivi karibuni ni
Chama cha Wananchi na Demokrasia (CHAWAD).
Gazeti hili lilimtafuta Msajili wa Vyama vya Siasa
nchini, Jaji Francis Mutungi, kujua iwapo kuna chama
kilichoanzishwa na wanachama waliofukuzwa upinzani,
alisema hana taarifa hizo, ingawa kuna chama
ambacho kimepata usajili wa muda na kingine kipo
kwenye mchakato huo.
MTANZANIA Jumapili lilimtafuta Mwigamba ili kujua
kama anafahamu kuhusu uanzishwaji wa chama hicho,
ambapo alisema hivi sasa bado hawajakaa pamoja na
wenzake kujadili suala la kuanzisha chama, kutokana
na kila mmoja kuwa mbali.
“Tangu maamuzi ya Kamati Kuu hatujakutana, hii ni
kwa kuwa tuko mbalimbali, mimi niko Arusha na
nashauriana kwanza na familia yangu nijue nini cha
kufanya,” alisema Mwigamba.
Alisema hivi sasa anachokifahamu ni kwamba Dk.
Mkumbo anarudi kwanza kwenye kazi yake ya awali na
Zitto anasubiri uamuzi utakaotolewa dhidi ya
uanachama wake.
Alipoulizwa Dk. Kitila kama ameshiriki na wenzake
kuanzisha chama cha siasa, alishindwa kukataa wala
kukubali, kwa kusema kuwa ukweli ama uongo wa
habari hiyo utajulikana.
Alipotajiwa chama hicho na kwamba kinatarajia kupata
usajili wa muda, alisema hafahamu hilo na hawezi
kuzungumzia.
“Sina cha kuzungumza juu ya swali lako, kuwapo kwa
chama kipya au la, nadhani ukweli utajiweka wazi nanyi
mtabaini tu, hata hilo jina la chama kipya kuitwa AACT
sijui,” alisema Dk. Kitila.
Mpaka sasa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu
nchini ni 23, ambavyo ni CCM, CUF, Chadema, UMD,
NCCR-Mageuzi, NLD, UPDP, NRA, Tadea.
Vingine ni TLP, UDP, Demokrasia Makini, Chausta, DP,
APPT-Maendeleo, Jahazi Asilia, Sau na AFP, UMD,
FORD, CCK, ADC na Chaumma.
 
*Chadaiwa kuundwa na waliofukuzwa upinzani
WAKATI fukuto la kufukuzwa uanachama kwenye
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
likiwa bado bichi, chama kipya cha siasa kimeanzishwa
na watu wanaodaiwa kuwa ni muungano wa
wanachama waliofukuzwa kutoka vyama vya upinzani
nchini.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Ofisi
ya Msajili wa vyama vya siasa nchini, zinakitaja chama
hicho kuwa ni African Alliance for Change and
Transparence (AACT) na kwamba mipango ya usajili wa
muda wa chama hicho inadaiwa kuanza kuratibiwa kwa
takribani mwezi mmoja sasa.
MTANZANIA Jumapili limedokezwa kuwa, tayari chama
hicho kimekamilisha baadhi ya taratibu na kinatarajiwa
kupewa usajili wa muda na Ofisi ya Msajili wa Vyama
vya Siasa siku ya Jumanne, wiki ijayo.
Gazeti hili limedokezwa kuwa iwapo chama hicho
kitapata usajili huo, upo uwezekano wa wanachama
waliofukuzwa uanachama kutoka Chadema hivi karibuni
kujiunga na chama hicho.

Wanasiasa wengine wanaotajwa ama kuwa nyuma ya
kuanzishwa kwa chama hicho au wanatarajia kujiunga,
ni wale waliofukuzwa kutoka CUF, nia ikiwa ni
kuendeleza harakati zao za kisiasa.
Mmoja wa watu wanaounda chama hicho alilidokeza
gazeti hili kuwa endapo chama hicho kitapata usajili
baada ya hapo, taratibu na harakati za kuanza
kukitangaza zitafanyika katika maeneo mbalimbali
nchini.
Alisema pia wamepanga kuendesha siasa zenye
upinzani, ikiwa ni pamoja na kushiriki katika uchaguzi
wa serikali za mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2015 iwapo
kitakuwa tayari kimejiimarisha.
MTANZANIA Jumapili limedokezwa kuwa mchakato wa
kuanzisha chama kwa wanachama waliofukuzwa
upinzani, ulianza kitambo, ukilenga nia yao ya

kuhakikisha wanashiriki katika chaguzi hizo.
Hivi karibuni Kamati Kuu Chadema, iliwavua uanachama
aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha,
Samson Mwigamba na Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk.
Kitila Mkumbo, huku Mbunge wa Kigoma Kaskazini,
Zitto Kabwe, akikimbilia Mahakamani kuomba zuio la
kutojadiliwa uanachama wake na kikao hicho.
Zitto, Dk. Kitila na Mwigamba walituhumiwa na uongozi
wa juu wa Chadema kuandaa waraka wa siri wenye
lengo la kufanya mabadiliko ya uongozi ndani ya
chama, hali iliyoibua mgogoro mzito hadi kufikia uamuzi
wa kuwavua uanachama baadhi yao.
Aidha taarifa nyingine ambazo MTANZANA Jumapili
limezipata zinaeleza kuwa mbali na AACT, chama
kingine kilichopata usajili wa muda hivi karibuni ni
Chama cha Wananchi na Demokrasia (CHAWAD).

Gazeti hili lilimtafuta Msajili wa Vyama vya Siasa
nchini, Jaji Francis Mutungi, kujua iwapo kuna chama
kilichoanzishwa na wanachama waliofukuzwa upinzani,
alisema hana taarifa hizo, ingawa kuna chama
ambacho kimepata usajili wa muda na kingine kipo
kwenye mchakato huo.
MTANZANIA Jumapili lilimtafuta Mwigamba ili kujua
kama anafahamu kuhusu uanzishwaji wa chama hicho,
ambapo alisema hivi sasa bado hawajakaa pamoja na
wenzake kujadili suala la kuanzisha chama, kutokana
na kila mmoja kuwa mbali.
"Tangu maamuzi ya Kamati Kuu hatujakutana, hii ni
kwa kuwa tuko mbalimbali, mimi niko Arusha na
nashauriana kwanza na familia yangu nijue nini cha
kufanya," alisema Mwigamba.
Alisema hivi sasa anachokifahamu ni kwamba Dk.
Mkumbo anarudi kwanza kwenye kazi yake ya awali na
Zitto anasubiri uamuzi utakaotolewa dhidi ya
uanachama wake.
Alipoulizwa Dk. Kitila kama ameshiriki na wenzake
kuanzisha chama cha siasa, alishindwa kukataa wala
kukubali, kwa kusema kuwa ukweli ama uongo wa
habari hiyo utajulikana.
Alipotajiwa chama hicho na kwamba kinatarajia kupata
usajili wa muda, alisema hafahamu hilo na hawezi
kuzungumzia.
"Sina cha kuzungumza juu ya swali lako, kuwapo kwa
chama kipya au la, nadhani ukweli utajiweka wazi nanyi
mtabaini tu, hata hilo jina la chama kipya kuitwa AACT
sijui," alisema Dk. Kitila.
Mpaka sasa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu
nchini ni 23, ambavyo ni CCM, CUF, Chadema, UMD,
NCCR-Mageuzi, NLD, UPDP, NRA, Tadea.
Vingine ni TLP, UDP, Demokrasia Makini, Chausta, DP,
APPT-Maendeleo, Jahazi Asilia, Sau na AFP, UMD,
FORD, CCK, ADC na Chaumma
.

Interesting sababu ya kuanzisha chama ni kuwa umefukuzwa??

vyama vya siasa vilivyopo vina impact gani??

sijaona bado kama kua impact yeyote ile
 
vitaendelea kuongezeka tu, unakadiliwa mpaka mwaka 2025 tutakuwa na vyama vya siasa mia mbili, yaani itafikia jirani kwa jirani tu mnaanzisha chama, simply kwa sababu mmebishana kikaoni

demokrasia bado sana afrika

Waberoya uliona nn ukatuletea ile topic ya wasaliti chuo kikuu? Maana wapo Riz ZZK Lyas na wengine wengi.
 
haa ha haaa mambo ya chuo yale

lakini niliandika kwa mtindo wa kutaka majibu, nilipata majibu yangu na niliridhika sina misimamo ya kibishi

Zitto alijibu na nikapata uhakika kutoka kwa watu kadhaa, zitto at that time alikuwa na conflict na uongozi wa chuo wakatumia loophole ile kumsimamisha-wengine tukajua alisimamishwa kwa sababu ya yale mapinduzi. sidhani pale kama kuna issueza za usaliti
Waberoya hulka ya usaliti huwa haina tiba, Kaini alimsaliti ndugu yake matokeo yake unayajua, Yuda alimsaliti Yesu matokeo yake unayajua, ndiyo maana jeshini huwa wananyongwa kwa vile wanajua wakiwaacha kuna siku wanaweza hata kuanzisha uasi jeshini.

Ukifuatilia nyendo za Zitto nafikiri tabia ya usaliti haikuanzia Chuo kikuu inawezekana toka akiwa mdogo shule za msingi, dalili zinaonesha kabisa asipopata anachokitaka anaweza hata kuingia msituni.
 
Ndugu yangu hii ndiyo Tanzania hata huko asipokuwa mwenyekiti sheria zinamruhusu kuanzisha chama kingine hadi ndoto yake itimie.

Ndg nimecheka sana! Inaonekana kuna watu wamezaliwa kuwa wenyeviti duh,,,!
 
Mi nadhani hii sheri ya kuansishwa vyama vipya vya siasa inatakiwa iangaliwe upya! kwani mwishowe tutakuwa na vyama 300, hivi 23 ni vingi mno vipunguzwe vibaki 4 tu!

Mkuu hofu yngu ni kupatikana chama cha kigoma.
 
Back
Top Bottom