Mh. Dr. Slaa katibu mkuu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo akiwa Iringa amesema wamebariki madiwani 2 walioomba kujiuzulu Shinyanga, hiyo ndiyo Demokrasia ya kweli, madiwani hao moja ya sababu kubwa ya kujiuzulu ni kwamba wanamuunga mkono Mh. Zitto , Mh. Dr. Slaa amesema kuna taarifa pia kuwa chama cha ACT kiko mbioni kusajiliwa na baadhi ya wale waliovuliwa uanachama CHADEMA.
Kama ni kweli chama hicho kitasajiliwa na viongozi wake ni miongoni mwa waliovuliwa uanachama CHADEMA, basi Dr. Kitila Mkumbo atakuwa ni mtu wa kuogopwa kama UGONJWA WA KUFISHA, ataogopwa na kizazi kilichoshuhudia usaliti wake na kizazi kitakacho kuja kuzaliwa na kusimuliwa kisa hiki.
Kama watafanya kosa hilo la kusajili chama hicho , natabiri wakiweza kupata wanachama hata elfu kumi kwa nchi nzima basi ntajua watanzania wengi hatunazo akili. Dr. Kitila amekuwa akinukuliwa na magazeti baada ya usaliti wake kukwama na kuvuliwa uanachama akisema tunahitaji chama mbadala cha upizani zaidi ya CHADEMA kumbe malengo yake yalikuwa ni hayo. Huyu mtu ni msomi mzuri lakini nashawishika kusema siasa sio mahali pake alikosea njia, na kama ni mahali pake basi anauchu mbaya sana na tamaa ya madaraka.
Tunahitaji kuikomboa Tanzania kwa kuiondoa CCM madarakani