Chama cha Kilaghai Tanzania...

Chama cha Kilaghai Tanzania...

Njaa ni kitu kibaya sana!!! Kwa hiyo hapa malipo yako ni kiasi gani kwa leo?????!!!!! Kama huridhiki kwa nini usiende mahakamani? Povu la nini hapa???!!!

mkuu unatumia kichwaa kufugia tu nywele? mjadala umeletwa jukwaani, kama una hoja ya kupinga itoe, sio haya maneno yako yasiyo na tija kwa wasomaji.

Mods, michango ya namna hii muwe mnaifuta on spot, ili heshima ya JF kuwa mahali pa Great Thinkers irudi.
 
Natamani sana mleta mada ungetuambia baada ya uchambuzi wako nini kifanyike, wananchi waisuse chadema na kurudi ccm au tuiache ccm iendelee kuuza twiga wetu nje ya nchi na kugawana rasilimali zetu?

unapaswa kujiongeza sio kila jambo utafuniwe. Inshort, amejaribu kuonesha mapungufu hayapatikani ccm tu hata vyama vingne km cdm. Pia uone kwmba cdm ni chama chenye maslahi ya watu wachache na muelekeo wake ni wakibinafsi zaidi wanapaswa kubadilika km wanahitaji dola. Lkn mpk sshv dola kwao itabaki ndoto,hawana mkakati wa kuwafikia mwananchi wameanzisha uongozi wa kanda ambao bado ni centralizatn,ccm wamedecentralize mpk kwa balozi wht do u espect?
 
Kama umethubutu kuisemea cdm yote hayo cjui ccm itakuwa mara ngapi ya hiyo maana kila baya linalofanyika ktk nchi hii linawahusu baya zaidi hii ya kutugawa kwa nisingi ya kidini na ukabila
 
Pole sana ndugu haya mambo ungeyaleta miaka ile....siyo leo too late! kama ni ulaghai basi baba yake ni yule aliyekisajiri na ndiyetunapaswa kuanza naye. Pia fuatilia hesabu za pesa ya viwanja vya michezo, packing, vyumba vya kupangisha n.k hapa kunatatizo kubwa sana kuliko hizo sadaka za M4C.Aidha unaonekana wewe ni muungwana sana tena mtetezi mzuri wa masilahi ya wananchi hebu tuungane tudai pesa zetu za EPA, Richmond, Deepgreen, meremeta, Dowans n.k n.k n.k
 
ZeMarcopolo,hakuna chama chochote cha siasa ambacho asilimia mia moja wanasema ukweli.Kiangalie CCM chenyewe ni waongo wakutupwa mpakaa rushwa wameifanya haki.Angalia CUF leo wanongelea hiki kesho wakija wanakanusha wataongelea kingine.Hakuna chama ambacho kinaukweli kwa asilimia mia.

Kwa wanachama ulivyowapanga inategemea na utafiti wako pia,lakini sidhani kama utafiti uliofanya umefanya kwa watu gani.Kuna vijana kama Mwampapa na Shonzi walikosa kitu kidogo sana hekima ,kama wangekuwa na hekima wangekuwa supported na watanzania wengi.Tatizo lingine chama chetu tawala bado hakijapokea vyama vya upinzani kama changamoto na wamepokea kama maadui ndio maana wanatumia pesa nyingi na ngonjeara nyingi ili kuvifanya vyama hivi visisongembele na kupata wanachama au kuwapa muamko watanzania kuhusu hatima ya nchi yao na elimu ya uraia.
Ukiuliza kwa nini CCM wanapamba vyama vya upinzani kwa matamko ya udini ,ukabila ,waongo wanapenda madaraka n.k ni kwa sababu wao wenyewe ndio waanzishaji wa hayo yote.Na hakuna mwanachama wa ccm asiyependa madaraka,kwani kama wasingependa madaraka sidhani kama rushwa ingekuwa kigezo.

Kwenye mada yako ungeweka vyama vyote vya siasa kuwa ni waongo na wapenda madaraka ningekuelewa zaidi,vinginevyo ninaona hauna tu mapenzi na chadema bali unamapenzi na CCM au CUF
 
CHADEMA ni chama kinachoendeshwa kwa misingi ya ulaghai. Chama kama hiki mtu yeyote atakayetaka kukiunga mkono kwa hoja anajikuta anakwazika.
Hii imesababisha CHADEMA kuungwa mkono zaidi na makundi mawili ya watanzania:

1. wale ambao ni bendera fuata upepo.
2. wale wenye malengo ya kupanda haraka na kwa urahisi kwenye arena za kisiasa za kitaifa.

(...)

4. Taarifa za Josephine Mushumbusi kulipwa mamilioni ya shilingi za chama kwa kazi anayoiita ya kujitolea. Wadau walihoji kuwa na wao wangependa kujitolea kwenye shughuli za chama ili walipwe hayo mamilioni. Ilidhihirika kuwa Josephine alipata fursa hiyo kwa upendeleo.

6. Kumekuwa na taarifa za matumizi mabaya ya pesa ...
7. Katibu Mkuu wa CHADEMA ni miongoni mwa washutumiwa wa ufisadi wa mamilioni ya pesa za mradi wa maji wa Karatu.

8. Viti Maalum vya ubunge vimetolewa kwa upendeleo ....Ubunge wa viti maalum kutokana na "kufahamiana" na mwenyekiti wa chama. Hili limewavunja moyo wengi walioanza kuiamini chadema.

11. Hesabu za pesa ... imekuwa ni jambo la siri kubwa ndani ya CHADEMA.


Duniani kuna watu na Viatu, viatu huwa ni vingi kuliko watu maana mtu mmoja ana zaidi ya jozi moja.

Kwenye CHADEMA ungeweka CCM article yako ingeleta maana kwa Taifa.

Kwenye makundi yanayopenda CCM umesahau kundi la tatu:-

3: Ni wale wenye malengo ya kujiunga na chama ama kujipendekeza kwa "wakubwa" ili wafisadi nchi au wapate madaraka.

Kwenye mambo uliyo taja kuwa yanaiondoa CDM machoni pa watu naona ulikuwa unaisema CCM kimafumbo, mfano:-

Kwenye No. 4: Ulikuwa unamsema "First 'Red" (First Lady wa ukweli ni My wife wake wa kwanza!) anaye zunguka kukagua mikoani kwa kutumia rasilimali za nchi kama Waziri Mkuu!

No. 6: Serikali ya SSM imekuwa na Matumizi mabaya ya fedha za umma tangu mafisadi walipo shika dola!
No. 7: Hapa umemsema Kinanah na biashara yake ya ujangili wa nyara za Taifa.
No. 8: Umemsema Mkulu kwa kuteuwa wakuu wa wilaya, mikoa, wakurugenzi wa mashirika ya umma na mawaziri kwa misingi ya kujuwana kindugu, kidini, kirafiki na "kiurafiki"!
No: 11: Hapa ulikuwa unazungumzia mikataba ya madini ambayo hata wananchi kupitia wabunge wao ni marufuku kuiona, na kwa nini deni la Taifa linakuwa kwa kasi ya ajabu lakini tuna ambiwa tumepunguza utegemezi wa budget toka 44% mpaka 22%-Pesa hiyo inakopwa inakwenda wapi?

Nimekukubali mzee wa reverse!
 
mimi nashangaa aina ya watu kama wewe, na mada dhaifu mnazozipost humu.

vyama vya upinzani na wanaharakati wanakisakama chama cha mapinduzi na serikali yake kwa kuwa ndo chama tawala, chenye dola na kinashindwa kuongoza nchi ili wakiangushe wakae wao madarakani, na wakosoaji wanajipambanua dhahiri kwa misimamo na malengo yao

ni vema basi unapoandika tuweke wazi wewe ni nani, je ni mtanzania mzalendo, ni mwanaCCM,masalia PM7, mwanaCHADEMA, au mwanaharakati???, na je katika maandiko yako, unakejeli??,unaponda?? unakebehi??,unashutumu??, unatoa ushauri, angalizo, ili tuweweze kujadili

kwa mfano rahisi ukisema mimi ni Mwanchama wa Chadema, ninakerwa na mfumu huu wa uongozi wa chama. wasomaji tutajadili kwa mtazamo huo

au ukisema mimi ni mwana CCM, napingana na itakadi na sera za CHADEMA, tutakupa jibu stahiki

sasa unataka tujadili nini??? tuseme ndiyo au hapana??? au unatoa taarifa tu??? kama ni taarifa ili iweje?? na nini kifanyike. vinginevyo unatupotezea muda kuna issues za msingi za kujadili,

  • nchi haina umeme wa uhakika,
  • huku ubungo hatuna maji,
  • wadogo zetu 95% wamefeli,
  • kuna chuo cha ugaidi ukerewe
  • kuna vikundi vya uharamia vinavyofadhiliwa na ikulu kudhuru wapinzani

Anakupotezea muda?. KWELI?
Kama angekuwa kweli kweli anakupotezea muda wako wenye gharama kubwa usingepoteza muda mwingi kuandika kwa kirefu namna hii wakati kuna issues za msingi zinahitaji sana mjadala na uchangiaji wako. Vinginevyo, kwa maandishi haya, wewe unakuwa ndiyo siyo mtunza muda mzuri.

Ni angalizo tu.
 
Sitaki kuamini si yumo humu, aje athibitishe kama ni kweli.
Nijuavyo mimi kujitoa kwake ni kwa sababu ya Mafanikio ya SERA za MACCM na ndivyo alivyotuambia hapa JF sasa haya mengine ni tuhuma za uongo sio vizuri kumfanya mwenzio aonekane ni mwenye tamaa na uroho.

Ina maaana huko kwa MACCM mmempa tenda gani?
Mkuu wewe ndiyo umeelewa vibaya sentesi inavyobainisha, jaribu kuisoma vizuri tena, utaelewa ina maana gani.
Chris Lukosi amekuwa akishutumiwa kuwa sababu ya kujitoa kwake chadema ni kunyimwa tenda hii,
 
Kwakweli tupo mahala pabaya sana tanzania. Tatizo letu naamini sio vyama bali ni watendaji ndani ya vyama hadi serikalini na tuseme ukweli kutokuwajibika,ufisadi na kujipendelea ndio kunakoleta hali ya kutugawa watanzania na mwenye kuweza kuweka sawa mambo haya sio CDM bali ni chama tawala na hadi tulipofikia kinaonesha kulegalega kuliko wazi ktk kuweka mambo sawa na ndio maana wapinzani wanapata la kusema, si mpenzi wa chama chochote cha siasa ila nimeufuatilia huu uzi nimeona kila mmoja anajaribu kuchanhia kwa kulinda maslahi ya chama chake ila iko wazi tatizo ni utawala na kwa mwendo huu tunaoenda nao tutakuja kuvuruga amani yetu tena si kwa ukabila,udini wala tofauti za vyama bali ni vita baina ya masikini[wanyonge] na matajiri ambapo kila tajiri itaaminika ni fisadi. 2015 sio mbali watanzania ili mambo yaende sawa tumchague mtu makini asiye na mzaha wala utani kwenye kusimamia taifa bila kujali atakuwa mgombea binafsi,ccm,cdm,tlp,nra au nccr. Wengi wanaopiga kelele kuhusu vyama ni watu wanaojaribu kuweka sawa maslahi yao ila mioyoni mwao wanajua tulipo ni katika wakati mbaya kwa mustakabali wa maendeleo ya taifa letu. Nawasilisha

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Hili ni Jukwaa la Siasa mkuu Hiroshima, kama hauna hoja kaa kimya.

Kitendo cha wewe kuishabikia CHADEMA tayari umeshaonyesha upungufu wa akili kichwani mwako kwahiyo usitake kutudhihirishia upunguani wako.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Na wewe kitendo cha kushabikia ccm inaonyesha jinc gani huwa unashirikisha masaburi kwenye kupambanua kuliko akili.
 
Last edited by a moderator:
We niweke kwenye kundi lolote unalopenda kwa upeo wako lakini ukweli ni kwamba siasa za majitaka kwa Tanzania ya sasa hazina nafasi kabisa. Huwezi wewe na wenzio Shonza na Mwampamba kuniambia Dr Slaa ni mtu mbaya, wakati huo huo mko kwenye CHAMA KIMOJA NA CHENGE NA ROSTAM. Haiingii na haitaingi kwenye akili ya Mtanzania yeyote kuwa watu kama akina Chenge au Riziwani Kikwete wamepata utajiri wa kihalali na sisi tuunge mkono chama chao cha Mapinduzi. Labda mtawapata walevi tu kuamini itikadi yenu

Mkuu hemu jitambue, kama CCM inakombatia mafisadi, wahujumu uchumi na wabadhilifu wa mali za umma, hata kama CCM na serikali haitambui utawala wa sheria, haitoi uhalali kwa CHADEMA kufanya maovu yanayofanywa na CCM, hemu mlisome chapisho la mtoa mada kwa ustadi mkubwa, wenda mkisoma tena na tena mtaelewa, maana vichwa vya binadamu havifanani katika kuelewa mambo, binafsi nimemuelewa vizuri mtoa mada, yeye anataka mumpe hoja za msingi za kwanini CHADEMA itawale? wakati madudu ya CCM yameonekana onekana CHADEMA? Sio kwa lengo baya kuufanya huu mjadala, wenda ukatoa ukungu kichwani mwa watu wanaipenda CHADEMA kama hawa WAFATA UPEPO waliojaa humu JF.
 
Chadema ni chama kinachozungumzia mipango yake ya kuendesha nchi kinadharia kwa vile hakijapata fursa ya kupewa dola. Hata hivyo kinaonyesha kukerwa na ufisadi,umasikini na ukosefu wa elimu kwa wananchi wake.
CCM kimechukua dola(sio kupewa) na hakina kifanyacho,ni kama toothless bulldog, hakina uwezo wa kung'ata zaidi ya blabla na nchi inaangamia tukishuhudia. Jee kuna faida ya kuendelea kufuga "Toothless Buldog"?
Nadhani hakuna faida hiyo hata kidogo.
Kuilalamikia CDM wakati haina dola huo ni uzandiki mkubwa,kwanza mengi yaliyoibadili nchi kwa sasa hata ikaanza kuonekana kuwa ina mwelekeo ni yale yaliyopiganiwa na Chadema kwa nguvu kubwa.
Wananchi wa sasa wameshaelewa nini Chadema inafanya,propaganda zenu kwenye mitandao hazisaidii lolote kwa CCM na hazina madhara kwa Chadema. Mbona kama chama ni cha kikanda kama msemavyo wajumbe wa vikao vya CCM hapa Mwanza wajumbe wanavalia mashati yao ya kijani ukumbini? Wanaogopa nini kuyavaa mitaani siku hizi?
Zamani ilikuwa fahari kuvaa sare ya CCM hadharani mbona sasa imekuwa aibu mtaani kwa watu wa kawaida?
Ukijiuliza hayo yote ndio utapata majibu kuwa hicho chama kwa wananchi ni kama ugonjwa wa Ukoma ambao haupendwi na watu.
 
Hivi chama chako unachokitumikia yaani CCM kimewafanyia nini watanzania kwa miaka 36?
wizi wa rasilimali,
madaraka ya kujuana
nchi maskini.
elimu duni,
ahadi hewa ambazo hazitatekelezwa kama tren za kasi kigoma dar,
meli ya kisasa ziwa tanganyika,
viwanja vya ndege vya kisasa kila mkoa,
kufuga mafisadi wa EPA, na wengineo.
kununua magari ya kifahari kama mashangingi ambayo hata Japan wanotengeneza hawayatumii,
hospitali duni..
kutuma mamluki katikia vyama vya siasa ili kuviuwa,
na madhambi negineyo mnayojua...

tukishawatoa madarakani nyie wezi wa rasilimali zetu, tukaweka chama kingine kinachofaa,
tukamweka kiongozi makini ndoto za watanzania zitatimia..
tutafaidi rasilimali zetu
tutakuwa the hub of Africa
tuna kila utajiri ambao wachache CCM ndio wanaofaidi.
HUWA NAMWONA MTU ANAESHABIKIA CCM KWA SASA LABDA SIO MSOMI AU MSOMI AMBAE HAJAELIMIKA.
HUWEZI KUWA NA AKILI TIMAMU KWA SASA UKAJIITA MWANA CCM NA UKAPITA MITAANI NA NGUO ZA KIJANI
SINA CHAMA CHA SIASA NAUNGA MKONO MAGEUZI YA KWELI
 
Katika hali isiyotarajiwa Leo katika kijiji cha Kasharara Kata Karambi Jimbo la Muleba Kusini wananchi zaidi ya 100 wamekabidhi kadi za CCM mbele ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya ndugu Mhaji pamoja na Katibu wake Wilbroad Msafiri.

Viongozi hao walikuwa wameenda kusuruhisha mgogoro wa ardhi ambao unanuka harufu ya UFISADI lakini wakakumbana na guvu ya umma na kuambulia kurudi na rundo la kadi za wanachama waliochoka kuona maisha bora kwa kila Mtanzania yakiwa yameandikwa tu nyuma ya tisheti zao huku wao wakiendelea kupigika.
Mkuu [MENTION]Ommunist[/MENTION] tujuze juu ya hiyo kitu ardhi nani amewalaghai hao watu. Maana tunaambiwa ni CDM hapa.

cc Kijakazi, ZeMarcopolo, Ng'wamapalala na Kitoabu.
 
Last edited by a moderator:
Ni upuuzi kujihusisha na hoja za kipuuzi kwa sababu wapuuzi wanatafuta wapuuzi wenzao kuchangia michango yao ya kipuuzi. Mfano tujiulize; huyu ZeMarcpolo anataka kufanikisha nini wakati yeye yuko kwenye chama chake kisicho cha kilaghai?

Mfano mwingine kuhusu hii hoja ingekuwa busara kwenda kwa wananchi hususan wanachama wa Chadema na kuwatahadhalisha kuhusu ulaghai wa hiki chama.

Mfano mwingine, hata kama ni mkakati wa CCM hapa jukwaani kutoa hoja mbadala kuiathiri CDM; hoja zilizopewa nahau ya "ulaghai" zinaishia kupingwa kwa nguvu zaidi kwa sababu lengo na mtoa hoja na hoja zake anajulikana amekengeuka kwa sababu anazozijua.


NI UPUUZI KUJIBU HOJA YA KIPUUZA lakini nifanyeje
Mkuu mbona unataka kulinyima jukwaa fursa ya kujadili mambo? Yaani ulitaka ZeMarcopolo aende kuwatafuta wanachama wa CHADEMA mitaani na kuwaambia hayo? Nadhani hapa kuna wana CHADEMA ambao wanaweza kutusaidia kujibu huu "upuuzi" wa mtoa hoja.
 
Last edited by a moderator:
ZeMarcopolo,

Wote nyie wababahishaji, kama wewe siyo mbabahishaji lete hoja zenye mashiko.

Ngoja nikukumbushe: Watanzania hatuhangalii nani anasema upuuzi gani, tunataka kuaminishwa huduma bora za jamii, Elimu, Afya na upatikanaji wa maji na umeme wa uhakika. Hatuitaji barabara mnazozizungumza kila siku bila haibu,nani anasafiri?

Tunataka reli yetu irudi kwa uhakika.

Hata haibu hamuoni, barabara hazina viwango wala hazivutii. Nenda Kenya uliza barabara mpya ziko wapi, utapenda na kuvutiwa. Siyo ninyi propaganda kila kukicha.

Uandishi wako unafanya hoja yako iwe na utapia mlo, jifunze uandishi unaovutia ili hoja yako ionekane, kama hizo barabara za Kenya.
 
CHADEMA ni chama kinachoendeshwa kwa misingi ya ulaghai. Chama kama hiki mtu yeyote atakayetaka kukiunga mkono kwa hoja anajikuta anakwazika.
Hii imesababisha CHADEMA kuungwa mkono zaidi na makundi mawili ya watanzania:

1. wale ambao ni bendera fuata upepo.
2. wale wenye malengo ya kupanda haraka na kwa urahisi kwenye arena za kisiasa za kitaifa.

Nitayachambua makundi haya mawili kama ifuatavyo:

1. Wale ambao ni bendera fuata upepo. Katika kundi hili kuna watu wa aina tatu:

i) Wale ambao wamedanganyika na propaganda kuwa chadema ni chama cha kikabila au cha kikanda na kwa vile wao wanatoka kwenye kanda hizo basi wanajisikia ukaribu zaidi na chadema. Hapa utaona kuwa propaganda za kukichafua chama kuwa ni cha kikabila au cha kikanda kimeweza kuwaongezea chadema nguvu katika maeneo inayoshutumiwa kuyapendelea.

ii)Wale ambao wamelaghaika na propaganda za kuwa chadema ni chama cha udini. Kuna waumini wengi wameviunga mkono vyama vya chadema na CUF kwa sababu tu wamekuwa wakisikia kuwa vyama hivyo vinashabiiana na dini zao. Hawa ni bendera fuata upepo ambao hawachuji ukweli wa taarifa na hawajiulizi chama kinaweza kuwanufaishi vipi kama waumini wa dini husika.

iii)Kundi la tatu katika bendera fuata upepo ni vijana ambao wanaona kuwa chadema ni kama fashion. Ukikaa nao chini vijana hawa kuwauliza kwanini wanaiunga mkono chadema hawana lolote la kuongea. Mfano wa watu waliomo kwenye kundi hili ni members wa jamiiforums ambao hurusha matusi kwa kila mtu anayehoji jambo juu ya chadema.


10. CHADEMA kukanusha kauli ya Nape kuwa wanapewa msaada na chama cha siasa cha Ujerumani, baadae ikadhihirika kuwa ni kweli wanapokea msaada huo. Hii imedhihirisha kuwa CHADEMA sio wawazi katika utendaji wao. Wadau wanajiuliza chama hicho cha siasa kinataka nini Tanzania mpaka kikipinge chama kilichoasisiwa na wapigania Uhuru na kutaka chadema iingie madarakani? Ikumbukwe kuwa muasisi wa CHADEMA Mzee Mtei, alikataa kushiriki harakati za kupigania uhuru na pia alikataa kujitolea kuijenga nchi baada ya Uhuru.

11. Hesabu za pesa zinazochangwa na walalahoi kwa ajili ya M4C imekuwa ni jambo la siri kubwa ndani ya CHADEMA.

Ndugu umetoa maelezo mengi ambayo sio mageni sana kwetu ebu naomba nifafanulie yafuatayo

1.Kuna kundi umesema linataka kupanda haraka kisiasa na hapo hapo umesema ni chama cha Kilaghai inakuwaje mtu atake kupanda kisiasa kwenye chama cha kilaghai ambacho kwa mtazamo wako akina mvuto wala mwelekeo?

2. Unaposema wadau wanajiuliza CDM kinataka nini hadi kipinge chama kilichoasisiwa na wapigania Uhuru? ebu tupe maelezo wakati CCM ikiongozwa na Baba wa Taifa (R.I.P) mambo yaliyokuwa yakifanyika wakati huo na sasa ni sawa? je alivyo Makongoro Nyerere na Riz 1 ni sawa? na je yanayosemwa na CDM na vyama vingine kuhusu udhaifu wa Serikali unayoipenda ni uongo? pia jiulize mbona Kenya (KANU) na zambia na baadhi ya nchi vyama vilivyoleta ukombozi wa nchi hizo havipo madarakani na vilipingwa na wananchi wakachagua vyama vingine.

3. Pia naomba utuambie kwa nini unaishambulia sana CDM? hivi haujui kuna msemo unaosema **MTI WENYE MATUNDA NDO UPOPOLEWA MAWE**
 
Akiliyako imeishia hapo katika kufikilia sitakulaumu hata kidogo ila unamatatizo makubwa hivi umejitahidi kuangalia nyumba ya jiran yako ikifuka moshi kumbe ya kwako inaungua moto, upende usipende chadema ndiyo kimbilio na tumaini la ukombozi kwa tanzania.
Hivi ufisadi unaofanywa na makada wa ccm kaika nchi hii huuoni
EPA, RICHMOND, KAGODA, MEREMETA, RADA, NA MIKATABA MIBOVU YA LASILIMALI ZETU NA WAWEKEZAJI AMBAYO HUTUONGEZEA UMASIKINI NA UTEGEMEZI hivi vyote huoni amakweli Nyani haoni kundule.
Tunapoludi ktika swala la upendeleo hv ww ulitaka apewe nani hivyo viti maalumu, huko kwenu huoni wewe nahisi ni mwehu kabisaa. Hebu jaribu kuichunguza NEC imejaa familia za watawala akiwepo raisi wa sasa na wastaafu wewe ni mwehu kwelikweli.
Wewe nazidi kusema ni mwehu kwa sababu, pamoja na kujitoa ufahamu najua kabisa ukirudi nyumbani na kutafakali hii serikali ya ccm na mr dhaifu unaona kabisa tunakoelekea siko na siku moja nchi itapigwa mnada kwa kushindwa kulipa madeni ambayo hayakuwa na tija ila kwa udhaifu wa serikali ya ccm tumeshindwa kukusanya kodi kwa wafanya biashara na kuwatafuta kodi kwa bodaboda na mama ntilie na kuacha makada wa ccm wakifa nya biashara bila kulipa kodi.
Ww ni mwehu kwa sababu hapo ulipo unasubilia 2015 ifike ndo uanzekufanyishwa kazi ya kuwarubuni wanachi kwa rushwa ili mgombea wenu apite halafu watakuacha mpaka 2020 ndio watakukumbuka tena wakati huu watoto wako na watoto wa ndugu zako wakipata elimu mbovu kwenye shule za kata. mama yako na bibi yako wakatihuo hawapati huduma za afya kule kijijini kwenu Pesa za huduma hizo uliyempigia debe kamua kuzipeleka ususi. Nazidi kukuona mwehu wa kutupwa (first class fara)



Mkuu punguza hasira,una hoja nzuri ila umeharibu neno mwehu na ---- first class.....sio mazuri usiwe kama wao wamezoea matusi,tujitofautishe kwa hoja na wao
 
kuna hoja zingine hazihitaji hata kujadiliwa kwa sababu mleta hoja analeta kwa malengo yake toka huko walikomtuma.
ndo maana wachangiaji wanajibu wanavyojisikia kwa sababu mada imeegemea zaidi kimasilahi zaidi.
 
Back
Top Bottom