Usiiidanganye akili yako ukatumia macho kufikiri.[QUO
1. wale ambao ni bendera fuata upepo.
2. wale wenye malengo ya kupanda haraka na kwa urahisi kwenye arena za
kisiasa za kitaifa.
Nitayachambua makundi haya mawili kama ifuatavyo:
1. Wale ambao ni bendera fuata upepo. Katika kundi hili kuna watu wa
aina tatu:
i) Wale ambao wamedanganyika na propaganda kuwa chadema ni chama cha
kikabila au cha kikanda na kwa vile wao wanatoka kwenye kanda hizo basi
wanajisikia ukaribu zaidi na chadema. Hapa utaona kuwa propaganda za
kukichafua chama kuwa ni cha kikabila au cha kikanda kimeweza
kuwaongezea chadema nguvu katika maeneo inayoshutumiwa kuyapendelea.
ii)Wale ambao wamelaghaika na propaganda za kuwa chadema ni chama cha
udini. Kuna waumini wengi wameviunga mkono vyama vya chadema na CUF kwa
sababu tu wamekuwa wakisikia kuwa vyama hivyo vinashabiiana na dini zao.
Hawa ni bendera fuata upepo ambao hawachuji ukweli wa taarifa na
hawajiulizi chama kinaweza kuwanufaishi vipi kama waumini wa dini
husika.
iii)Kundi la tatu katika bendera fuata upepo ni vijana ambao wanaona
kuwa chadema ni kama fashion. Ukikaa nao chini vijana hawa kuwauliza
kwanini wanaiunga mkono chadema hawana lolote la kuongea. Mfano wa watu
waliomo kwenye kundi hili ni members wa jamiiforums ambao hurusha matusi
kwa kila mtu anayehoji jambo juu ya chadema.
Makundi haya matatu ya bendera fuata upepo huwa ni rahisi sana kuvunjwa
moyo na kukikimbia chama mara tu upepo utakapoelekea upande tofauti. Kwa
mfano, iwapo chadema itafanya jitihada za kuhakikisha jamii inajua
ukweli kuwa siyo chama cha ukanda wala ukabila, basi makundi haya mawili
i) na ii) yatatoweka.
Vilevile iwapo chadema itasambaza elimu ya uraia na kuwawezesha wananchi
kuchagua vyama vyama vya kuviunga mkono kwa hoja, basi makundi yote
iii),ii) na i) itayapoteza.
Hizi ni changamoto zinazohitaji political calculations kudeal nazo.
2. Wale wenye malengo ya kupanda haraka na kwa urahisi kwenye arena za
kisiasa za kitaifa:
Katika kundi hili wamo wanasiasa kama Dr. Wilbroad Slaa na Shibuda.
Misingi ya wanasiasa wa aina hii kuhama kutoka kwenye chama kimoja mpaka
kingine ni kuhakikisha tu kuwa wanaendelea kuwepo kwenye shughuli za
kisiasa katika nafasi za uongozi. Hawana ugomvi wa kiitikadi na CCM.
Kimsingi hawa ni watu ambao iwapo leo hii CCM itawahakikishia kuwa
watapata fursa ya kuwa viongozi wa juu, basi wako tayari kujiunga nayo.
Wamejitoa CCM kwa sababu tu walinyimwa fursa ya kuwa viongozi katika
ngazi walizogombea. Iwapo chadema itawanyima fursa ya kuwa viongozi,
wataikimbia pia.
Mfano mzuri umeonekana hivi karibuni Lushoto ambaye kijana mpya katika
siasa
Deogratius
Kisandu aliikimbia chadema kwa kukosa fursa za uongozi ambapo
kimsingi alijiunga chadema kwa kuamini kuwa fursa hizo atazipata kwa
urahisi zaidi ndani ya chama hicho.
CHADEMA imekosa uungwaji mkono katika misingi ya itikadi. Hii
imesababishwa na ukweli kwamba cHADEMA imechukua itikadi zilezile za
CCM, TANU na ASP na kushindwa kuwapa wananchi chaguo jipya. Zaidi ya
hayo, hata kwenye ilani za uchaguzi za chadema hakuna offer tofauti na
zile ambazo wananchi wanapewa na CCM. Kuthibitisha hili, chadema imepata
wakati mgumu sana kupokelewa katika maeneo ambayo kuna chama kingine
cha upinzani kilichojijenga kama Zanzibar. Iwapo chadema wangekuwa na
itikadi au sera mpya ambazo utekelezaji wake unaelezeka, isingekuwa
vigumu kupata wafuasi katika maeneo hayo.
Kwa vile CCM imeshapewa fursa ya kutawala, mapungufu yake yameonekana.
Jukumu la chadema kwenye hili linatakiwa ni kuja na mkakati unaoelezea
kwa undani ni vipi watafanya tofauti na CCM. Badala yake, kazi pekee
inayofanywa na chadema ni kuainisha matatizo na kuyahubiri majukwaani
bila kuelezea iwapo wana mkakati wowote mpya ili wananchi waupime. Hii
inasababisha hata wasomi wanapovifananisha hivi vyama wanakosa zile
tofauti za kuzijadili na mwishowe hujadili tabia za viongozi vya vyama
na utendaji wao badala ya kujadili sera zake na itikadi.
Ulaghai wa CHADEMA ni sababu nyingine iliyofanya chama hiki kupoteza
wafuasi makini. Mtu yeyote atakayejaribu kuichunguza chadema kidogo tu
atagundua kuna mambo mengi yasiyofaa yanayofanywa na viongozi wake.
Viongozi hawa hufanya hivi kujinufaisha wao wenyewe na familia zao. Kwa
vile umaarufu wa chadema umetokana na uhubiri wa ufisadi, uwepo wa
ufisadi ndani ya chadema umewavunja sana moyo wananchi walioamini kuwa
wamepata tumaini jipya. Wale wanaoishabikia chadema kwa kufuata upepo
wanapojua ulaghai huu, huvunjwa moyo na kuikimbia. Mfano wa hili ni
kijana
Mtela
Mwampamba ambaye aliamini kuwa chadema ni tumaini jipya mpaka
pale alipojionea mw