Chama cha Kilaghai Tanzania...

Chama cha Kilaghai Tanzania...

Hivi kweli ZeMarcopolo kuna ulaghai unaoweza kuzidi huu wa kukusanya kodi kutoka kwa mtu masikini kwa kipindi cha miaka mitano alafu anashindwa kumpati hata dawa tu badala yake unampeleke tisheti, kanga na kofia?.

Vyama vyote vinavyovitwa walaghai vimelaghai nini kwa wa-Tanzania?. Njoo na hoja nyingine.
Watu tunaviunga mkono vyama pinzani baada ya kulaghaiwa na walio na jukumu la kututumikia, lakini wanatumikia matumbo yao na kutugeuza sisi ngazi za mafanikio yao.
 
Last edited by a moderator:
Umesomeka, umeanalyze vizuri though kuna mambo umefikiri kinyume.



Ila all in all hakuna jipya chini ya jua. Hata nchi za wenzetu waliposhinda upinzani sio kwamba walikuwa na jipya....

Jubilee haina jipya na Cord wala Kanu,
Its a matter of strategies na watu husika.
 
Akiliyako imeishia hapo katika kufikilia sitakulaumu hata kidogo ila unamatatizo makubwa hivi umejitahidi kuangalia nyumba ya jiran yako ikifuka moshi kumbe ya kwako inaungua moto, upende usipende chadema ndiyo kimbilio na tumaini la ukombozi kwa tanzania.
Hivi ufisadi unaofanywa na makada wa ccm kaika nchi hii huuoni
EPA, RICHMOND, KAGODA, MEREMETA, RADA, NA MIKATABA MIBOVU YA LASILIMALI ZETU NA WAWEKEZAJI AMBAYO HUTUONGEZEA UMASIKINI NA UTEGEMEZI hivi vyote huoni amakweli Nyani haoni kundule.
Tunapoludi ktika swala la upendeleo hv ww ulitaka apewe nani hivyo viti maalumu, huko kwenu huoni wewe nahisi ni mwehu kabisaa. Hebu jaribu kuichunguza NEC imejaa familia za watawala akiwepo raisi wa sasa na wastaafu wewe ni mwehu kwelikweli.
Wewe nazidi kusema ni mwehu kwa sababu, pamoja na kujitoa ufahamu najua kabisa ukirudi nyumbani na kutafakali hii serikali ya ccm na mr dhaifu unaona kabisa tunakoelekea siko na siku moja nchi itapigwa mnada kwa kushindwa kulipa madeni ambayo hayakuwa na tija ila kwa udhaifu wa serikali ya ccm tumeshindwa kukusanya kodi kwa wafanya biashara na kuwatafuta kodi kwa bodaboda na mama ntilie na kuacha makada wa ccm wakifa nya biashara bila kulipa kodi.
Ww ni mwehu kwa sababu hapo ulipo unasubilia 2015 ifike ndo uanzekufanyishwa kazi ya kuwarubuni wanachi kwa rushwa ili mgombea wenu apite halafu watakuacha mpaka 2020 ndio watakukumbuka tena wakati huu watoto wako na watoto wa ndugu zako wakipata elimu mbovu kwenye shule za kata. mama yako na bibi yako wakatihuo hawapati huduma za afya kule kijijini kwenu Pesa za huduma hizo uliyempigia debe kamua kuzipeleka ususi. Nazidi kukuona mwehu wa kutupwa (first class fara)
 
Mkuu onyesha basi upuuzi wa hoja kwa hoja badala ya kusema tu kwamba ni upuuzi! Basi Molemo ama Tumaini Makene atakuja na kusema kwa niamba ya Chama na kuonyesha kwamba huo ni upuuzi.

Ni upuuzi kujihusisha na hoja za kipuuzi kwa sababu wapuuzi wanatafuta wapuuzi wenzao kuchangia michango yao ya kipuuzi. Mfano tujiulize; huyu ZeMarcpolo anataka kufanikisha nini wakati yeye yuko kwenye chama chake kisicho cha kilaghai?

Mfano mwingine kuhusu hii hoja ingekuwa busara kwenda kwa wananchi hususan wanachama wa Chadema na kuwatahadhalisha kuhusu ulaghai wa hiki chama.

Mfano mwingine, hata kama ni mkakati wa CCM hapa jukwaani kutoa hoja mbadala kuiathiri CDM; hoja zilizopewa nahau ya "ulaghai" zinaishia kupingwa kwa nguvu zaidi kwa sababu lengo na mtoa hoja na hoja zake anajulikana amekengeuka kwa sababu anazozijua.


NI UPUUZI KUJIBU HOJA YA KIPUUZA lakini nifanyeje
 
CHADEMA ni chama kinachoendeshwa kwa misingi ya ulaghai. Chama kama hiki mtu yeyote atakayetaka kukiunga mkono kwa hoja anajikuta anakwazika.

Mkuu ZeMarcopolo, mie si mwanasiasa, na sitegemei asilani kujiunga na chama cha siasa. Inawezekana una point za msingi katika maoni yako, lakini sidhani kama alternative ya Chadema ni CCM, kama ninavyohisi unataka kusema. Ungewasaidia sana Watanzania kuwaeleza kama Chadema ni ya ulaghai, vyama vingine ni vya aina gani, ukianzia na CCM kilichopo madarakani.

La sivyo unanifanya nikate kauli kwamba yote usemayo ni propaganda kwa kuwa wewe ni mwanachama wa chama fulani ambacho kinaona Chadema ni tishio kwao. Ama tuambie, lengo lako hasa kwa hii osti ni nini? Kuelimisha wana JF? Kufanya propaganda? Kuichafua Chadema?
 
Ze marcopololozigo!

Soma uzezeta wako kundi Namba 1 kipengele kidogo (i)na (ii),ukidanganya kumbuka.
Mkuu Fisadidagaa msamehe huyu ZeMarcopolo yuko possessed
Hii inadhihirisha pasi na shaka kuwa hata alichokiandika hakijui kapewa alete humu.

Akili za kushikiwa, nashanga MAGAMBA hawaweki kumbukumbu vichwani mwao. "Akili ya kuambiwa changanya na zako!."
 
Last edited by a moderator:
Mkuu toa pia ushauri nini kifanyike ili CHADEMA wawe kama CCM.

hapana,jamaa hana jipya anajadili zaidi watu,CDM kama chama cha siasa kipo ktk njia sahihi hizi ni changamoto lazima tuzipitie ili tufike kule watanzania wanakokuitaji,kuwa kama ccm du!!!!juzi nasikia wameanzisha biashara ya pembe za ndovu,baada ya dowans,iptl,symbion,deep green,tangold kupungua mapato
 
Misingi ya haki haiwezi kusimamiwa na chama kinachoendeshwa kama chadema.
Je, kufuta matokeo ya uchaguzi uliompitisha mwenyekiti wa baraza la wanawake kuwa mbunge wa viti maalum na kumpa nafasi hiyo mkazi wa Marekani ndio misingi ya haki tunayotaka?
Nikukumbushe kuwa ukiona vyaelea vimeundwa,Muda mwingi wa viongozi wa CDM umeelekezwa kwenye kukemea rushwa na kutoa elimu ya uraia.CHADEMA inamaanisha Chama cha Demokrasia na Maendeleo,hivi sasa, watanzania wengi wana uelewa wa kutosha juu ya haki zao, Taifa lao linahitaji nini na ni aina gani ya chama kinaweza kuwaletea Tanzania waitakayo.
 
Hivi kweli ZeMarcopolo kuna ulaghai unaoweza kuzidi huu wa kukusanya kodi kutoka kwa mtu masikini kwa kipindi cha miaka mitano alafu anashindwa kumpati hata dawa tu badala yake unampeleke tisheti, kanga na kofia?.

Vyama vyote vinavyovitwa walaghai vimelaghai nini kwa wa-Tanzania?. Njoo na hoja nyingine.
Watu tunaviunga mkono vyama pinzani baada ya kulaghaiwa na walio na jukumu la kututumikia, lakini wanatumikia matumbo yao na kutugeuza sisi ngazi za mafanikio yao.

Swala hapa nafikiri siyo kwamba CCM ni bora au siyo bora, bali pamoja na matatizo yote yanayoendana na uongozi wa CCM, Je kuna Chama mbadala, nikiamaanisha kwamba ni Chama gani ambacho utakiangalia na kusema hawa watakuwa bora au watakuwa tofauti? Hilo ndilo swali la msingi!

Ngoja nikupe mfano mdogo sana, baadhi yetu tunaamini kwamba CHADEMA ndio mkombozi na wako tofauti na CCM, lkn ukiingalia sana CHADEMA hawana tofauti kubwa na CCM kwa mfano, Wabunge wengi wa CHADEMA wanaishi Dar kama vile Bw. Mbowe anaishi Mikocheni, Bw. Lisu anaishi Tegeta, Bw Zito Kabwe Dar, Bw. Sugu n.k sasa hawa pia kama Wabunge wa CCM wanafuja mali ya Umma kwa maana Wabunge wote wana Ofisi Majimboni kwao, na wanalipwa fedha na Serikali kuziendesha hizo Ofisi, hivyo ili kutumia pesa za Watz vizuri walipaswa kila siku wawe ofisini kwao ilikusikiliza Wananchi wao waliowachagua, sasa wewe niambie tofauti hapo iko wapi kati ya Wapinzania na CCM?

Ukiangalia siku ambazo Bw. Mbowe yuko Hai ofisini kwake kwa mwaka hata miwezi 2 haifiki, sasa wanatumia kigezo gani kusema CCM wanafuja fedha zetu?
Kama unaniambia fulani ni mbaya basi wewe lazima uonyeshe mfano kwa kuwa tofauti, lkn ukifanya yale yale, basi ni bora nibaki na yule mbaya lkn namjua kwa muda mrefu, hiyo ndio hoja hapa!
 
Msalimie Shigela na Nape hapo lumumba.
Kwa staili hii tuna safari ndefu sana.Mwenyezi Mungu shusha roho za ufahamu kwa waja wako wanaangamia kwa kukosa maarifa.Na kwa taarifa yako sina maslahi na chama chochote kile cha siasa naishi kwa jasho langu tena kwa jembe la mkono na ufugaji mdogo mdogo huku kijijini kusini mwa nchi.Ila nasikitishwa sana na baadhi ya vijana wasomi kama nyinyi ambao tunawategemea mtukomboe kutoka kwenye lindi kubwa la umaskini na ujinga tulionao kwa jinsi mnavyojiingiza kwenye siasa za majitaka na za kipuuzi.Wengi wenu mmejaaa tamaa za utajiri wa haraka na uchu wa madaraka HAMNA JIPYA.Lazima tuwapigie kelele mbadilike hatuwezi kuvumilia mkifanya ujinga wenu kupitia migongo ya vyama vya siasa.Njooni porini mjifunze maisha halisi ya Mtanzania na sio kubwabwaja tu hovyo hovyo.
 
Niamini kweli we ni Kitoabu kitu kinachopendwa sana na warabu na huliwa gizani hasa kipindi cha baridi.
Namuomba mungu aniepushe na lugha chafu ( ma2si ) kwakua wazee wangu wamenilea ktk misingi ya heshima napenda kuheshimu na kuheshimiwa. Ila sikatazi mtu akiamua kunitusi.
 
Last edited by a moderator:
Mti wenye matunda ndo unaopigwa mawe, kama kweli CHADEMA si tishio kwako na chama ongelea na vyama vingine uvianike.
 
Njaa ni kitu cha kuogopa sana,hata haki ugeuka kuwa si haki
endeleeni kutetea chama kilichotufikisha hapa tulipo kisa viposho uchwara
Naionea huruma eeh yerusalem (the bible says)
 
Back
Top Bottom