Chama cha Kilaghai Tanzania...

Chama cha Kilaghai Tanzania...

Nimependa uchambuzi wako muruwa umetoa angalizo kwa Chadema ni hiyari yao kufuata au kuacha.

Vipi umemaliza mkologo ulio uleta kule facebook kuhusu ndugu yetu kibanda au ndio vamiavamia?
 
Uchambuzi huu kama unajibiwa kwa hoja, utaleta maana kubwa sana maana utawatoa watu kutoka katika mawazo mgando kua CDM ina wenyewe na wengine ni Bendera ambao hufuata upepo tu. Ni wazi hapa usitegemee majibu yanayojenga hoja kwa maana wengine kama ulivyosema wanashabikia kwa fashion hivyo hawajui hata sera gani inayo wavutia.
 
Chunguza sana kuna hawa CHADEMA kaskazini hawa ndiyo wanajiona CHADEMA kindakindaki.
 
CHADEMA kupewa msaada toka ujerumani na KINANA kujipatia msaada hapa hapa Tanzania kwa kuendesha kampeni chafu za KUUA TEMBO na kuuza meno ya tembo ipi ni afadhali?
Kinana kutumia fedha za CCM kwenda China kwa ajili ya KUREKEBISHA biashara yake ya MENO YA TEMBO na kuweka kizazi cha tembo Tanzania katika hatari ya kutoweka sio suala la kujadili? Kuendelea kuhubiri udini mliopandikiza ndio manazidi kutufanya watanzania tuendelee kuunga mkono chama cha dini YETU na kuwaachia CCM ya DINI yenu maana mnatutahadharisha kuwa huko CCM kwa USTAADHI Kikwete sisi hatutakiwi ndio maana Sekretariati yote ni waislamu
 
CHADEMA kupewa msaada toka ujerumani na KINANA kujipatia msaada hapa hapa Tanzania kwa kuendesha kampeni chafu za KUUA TEMBO na kuuza meno ya tembo ipi ni afadhali?
Kinana kutumia fedha za CCM kwenda China kwa ajili ya KUREKEBISHA biashara yake ya MENO YA TEMBO na kuweka kizazi cha tembo Tanzania katika hatari ya kutoweka sio suala la kujadili? Kuendelea kuhubiri udini mliopandikiza ndio manazidi kutufanya watanzania tuendelee kuunga mkono chama cha dini YETU na kuwaachia CCM ya DINI yenu maana mnatutahadharisha kuwa huko CCM kwa USTAADHI Kikwete sisi hatutakiwi ndio maana Sekretariati yote ni waislamu

Wewe umethibitisha uwepo wako kwenye kundi 1.(ii) kama lilivyoainishwa kwenye chapisho hili.
 
Umeshawahi kujiuliza kwanini hauko NCCR au CUF?
Please share your knowledge.
Siko CUF kwa kuwa Mahita alinionyesha VISU na MAJAMBIA yenye rangi ya CUF siku moja kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kuwa ni chama cha kigaidi na hakifai kuongoza nchi hii. Pia CCM walituambia kuwa CUF ni chama cha KIISLAM kwa hiyo sisi tusio waislam tusijiunge nacho. Nashangaa saizi CCM wanatuambia kuwa CHADEMA ni chama cha Kikiristo kwa hiyo waislam wasijiunge nacho. Which means wametugawa sisi tusiowaislam tusiipende CUF na sasa wanawagawa walio waislam waiipende CHADEMA ili mwisho wa siku watu wapende vyama kwa kufuata itikadi za Dini.

NCCR sijawahi kabisa kuwasikia,,, ingawa mwaka 1995 nilimpigia kura Mrema. kwa sasa chama hiki hakijitangazi na hata watanzania wengi hatujui kinaongozwaje. Pia tumesikia kuwa mwenyekiti wake ni BWABWA na pia kimeolewa na CCM baada ya mwenyekiti wake kupewa ubunge wa BURE,,, Labda kirudi kwa wananchi kutupa ufafanuzi
 
Chama sio timu ya mpira uishabikie.hoja,misimamo ya viongozi,dira ndio misingi.tumewaelewa chadema baada ya miaka 18.tueleze twiga,kagoda,asilimia 94 kufeli yani div 4 na 0.maji shida,umeme,foleni,wizi,huduma mbovu,wafanyakazi kujimilikisha idara,mfumo ni mbovu na hawawezi kamwe kuurekebisha kwasababu hali mbaya.hamna uwajibikaji kabisa na sisi waajiri tupo kimya au tunatetea.hata mpira hatuoni sababu msekwa ni mwenyekiti bodi ya dstv.wako kila mahali wanatafuna na watu wao,hamna uwajibikaji kabisa.system mbovuuuuuuuuuu
 
Wewe umethibitisha uwepo wako kwenye kundi 1.(ii) kama lilivyoainishwa kwenye chapisho hili.
We niweke kwenye kundi lolote unalopenda kwa upeo wako lakini ukweli ni kwamba siasa za majitaka kwa Tanzania ya sasa hazina nafasi kabisa. Huwezi wewe na wenzio Shonza na Mwampamba kuniambia Dr Slaa ni mtu mbaya, wakati huo huo mko kwenye CHAMA KIMOJA NA CHENGE NA ROSTAM. Haiingii na haitaingi kwenye akili ya Mtanzania yeyote kuwa watu kama akina Chenge au Riziwani Kikwete wamepata utajiri wa kihalali na sisi tuunge mkono chama chao cha Mapinduzi. Labda mtawapata walevi tu kuamini itikadi yenu
 
Wapo wapinzani wengi wa CHADEMA. Sijaona wala kusikia mwenye hoja dhaifu kama hii! Poor analysis! Bado unajaribu kuita CDM kuwa ni chama cha udini wakati kimesheheni wanachama wa dini zote? Fanya utafiti utaona! Bado unaita CDM chama cha ukanda wakati kimeenea nchi yote!

CDM inatawala mji wa Kigoma, (magharibi) Mji wa Mbeya, (Kusini) Jiji la Mwanza na Mji wa Musoma, (Kaskazini) Arusha na Moshi ( Kaskazini mashariki) Dar-es Salaam, (majimbo mawili) Katikati ya nchi (Singida na Iringa) Na sasa utafiti unaonesha kuwa kinaungwa mkono sana Mtwara na maeneo yote ya nchi! Bado unafikiri kuwa Chadema ni kama fasheni inayopita wakati CCM imepoteza mvuto kabisa mioyoni mwa watyanzania? Kimegeuka kuwa chama cha WALA NCHI badala ya Chama Cha Wajenga nchi. Watanzania hatukujua kuwa CCM kingetugeuka haraka kwa kiasi hiki.

Chama kilichokuwa na kinasema "RUSHWA NI ADUI WA HAKI, SITAPOKEA WALA KUTOA RUSHWA" kimekuwa mstari wa mbele kwa rushwa ndani ya chama na hata katika serikali yake. Chama kinawaonea aibu wala rushwa na mafisadi. Kimeishia kuwaita magamba tu basi. Hatukujua kuwa CCM kitawageuka wafanyakazi katika nchi hii haraka namna hii. Kilikuwa chama cha wakulima na wafanyakazi. Baada ya kufunga ndoa na mafisadi na wezi wa rasilimali za Watanzania kimewatupa wafanyakazi chini kabisa. Iko wapi morali ya madaktari leo.

Kafanye utafiti Mhimbili utaojionea mwenyewe! Waalimu wana mgomo baridi. Wanaofundisha darasani hata wale waliosahihisha mitihani ya kitaifa. Wala hapakuwa na haja ya kuunda tume kuchunguza kufeli kwa kidato cha nne. Kama wangelijibu sawali la "JINSI GANI TUBORESHE MASILAHI YA MSINGI YA WAALIMU NA KURUDISHA MORALI YAO?" wangepata jibu la kuiokoa elimu ya kizazi kijacho cha Watanzania. Lakini hata kule kwingine ambapo utendaji hauonekani dhahiri kama wa Walimu bado morali ya wafanyakazi ipo chini sana! CCM imewatupa.

CCM imewatupa wakulima. Mikoa ya Lindi na Mtwara wanalalamikia Korosho. Nyanda za juu Kusini wanalalamikia Pembejeo hasa mbolea! Lakini hata wakivuna, wanakatazwa kuuza mazao yao kama wanavyotaka. Kaskazini kule wakulima wanakatazwa kuuza mazao yao waliyolima wenyewe Kenya penye soko zuri na huku wauza mafuta wakiruhusiwa kupandisha bei kila uchao na kufanya maisha ya mkulima kuwa magumu.

Yako wapi yale maisha bora kwa kila Mtanzania tuliyoahidiwa na CCM? Huduma mbovu za katika vituo vya Afya, miundombinu mibovu, maji hakuna, pamoja nakuwa nchi yetu ina gesi lakini umeme unakatika ovyo, na bei yake iko juu, na VYOTE HIVI NA VINGINE CHANZO NI CCM NA SERIKALI YAKE. Kwa nini Mtanzania wa kawaida awe na sabababu ya kuipenda CCM? Naweza nisiipende CDM lakini sina sababu ya kuichukia kama ninavyochukia CCM kwa sababu haijawahi kupewa nchi na kufurunda kama CCM.

Watanzania wanayo sababu ya msingi ya kuichukia CCM iliyotawala miaka 50, na sasa kujizatiti kuingiza chama kingine madarakani tuone kama hapawezi kuwa na mabadiliko. Ni hoja dhaifu kuwa wafuasi wa CDM ni bendera fuata upepo. CCM imetutupa, inatunyayasa, inaiba rasilimali zetu, imetugawa kidini, inawaunga mkono mafisadi na wala rushwa, inawafumbia macho wale walioficha fedha Uswis, kwa ujumla haina habari na Mtanzania wa kawaida. Tumeiacha kwani ukijaribu kishika, kama wewe sio mnafiki utakuta inateleza. Haishikiki tena.
 
Siko CUF kwa kuwa Mahita alinionyesha VISU na MAJAMBIA yenye rangi ya CUF siku moja kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kuwa ni chama cha kigaidi na hakifai kuongoza nchi hii. Pia CCM walituambia kuwa CUF ni chama cha KIISLAM kwa hiyo sisi tusio waislam tusijiunge nacho. Nashangaa saizi CCM wanatuambia kuwa CHADEMA ni chama cha Kikiristo kwa hiyo waislam wasijiunge nacho. Which means wametugawa sisi tusiowaislam tusiipende CUF na sasa wanawagawa walio waislam waiipende CHADEMA ili mwisho wa siku watu wapende vyama kwa kufuata itikadi za Dini.

NCCR sijawahi kabisa kuwasikia,,, ingawa mwaka 1995 nilimpigia kura Mrema. kwa sasa chama hiki hakijitangazi na hata watanzania wengi hatujui kinaongozwaje. Pia tumesikia kuwa mwenyekiti wake ni BWABWA na pia kimeolewa na CCM baada ya mwenyekiti wake kupewa ubunge wa BURE,,, Labda kirudi kwa wananchi kutupa ufafanuzi

Sawasawam asante kwa maelezo yako.

Kwa maelezo yako moja kwa moja umekiri kwa maneno yako mwenyewe kuwa uko kwenye kundi 1.(ii).

Lengo la hii thread ni kuwasaidia watafiti kuthibitisha uwepo wa makundi yaliyoanishwa na asante kwa kufanikisha hilo.
 
Naona moja kwa moja umeahidiwa kasafari ktk msafara wa katibu wa magamba katakachokusaidia kaposho ili uweze kulipa ada ya mwanao yule alopo ktk shule ya upili.
 
Kama wewe si mgonjwa wa akili basi ni lazima utakuwa unajipendekeza kwa magaidi na wauwaji wa taifa hili aidha kwa malipo au umeolewa na.....!
Ni aibu sana kwa mtu anaejua jinsi nchi hii ilivyomalizwa na watawala kwa kupitia katika chama cha mapinduzi, mateso na mauaji wanayoyapata watanzania kisha akaandika ujinga kama uliouandika hapa. Unashughulika sana na masuala ya watu binafsi ambao hawana athari yeyote kwa usalama na uchumi wa nchi hii. SHAME ON YOU!.
 
Sawasawam asante kwa maelezo yako.

Kwa maelezo yako moja kwa moja umekiri kwa maneno yako mwenyewe kuwa uko kwenye kundi 1.(ii).

Lengo la hii thread ni kuwasaidia watafiti kuthibitisha uwepo wa makundi yaliyoanishwa na asante kwa kufanikisha hilo.
Kwa hiyo unanishauri nini?

Niwasaliti wale watoto waliofeli mwaka huu baada ya kupewa elimu mbovu kwa kujiunga na CCM??

View attachment 86583

Niwasaliti hawa watoto ambao wanapata ADHABU ya kusoma kwa kuiunga mkono CCM iendelee kuwaharibia future yao?

Naomba ushauri ZeMarcopolo kama nimepotea kwa kuunga mkono ukombozi wa pili wa Mtanzania ambao ni mgumu zaidi kwa kuwa mkoloni ni mweusi mwenzetu.
 
Kwa hiyo unanishauri nini?

Niwasaliti wale watoto waliofeli mwaka huu baada ya kupewa elimu mbovu kwa kujiunga na CCM??

View attachment 86583

Niwasaliti hawa watoto ambao wanapata ADHABU ya kusoma kwa kuiunga mkono CCM iendelee kuwaharibia future yao?

Naomba ushauri ZeMarcopolo kama nimepotea kwa kuunga mkono ukombozi wa pili wa Mtanzania ambao ni mgumu zaidi kwa kuwa mkoloni ni mweusi mwenzetu.

Solution pekee iliyopendekezwa na chadema kwenye hili ni kufanya maandamano!!!
 
Kunawatu hawapendi/hawataki kuheshim fikra za wenzao, wanapenda waamiwe kila wanacho amini wao, naukitaka kuwajua watu wa dezine hiyo, jaribu kuhoji mapungufu ya CDM. Hapo utadhihakiwa na kuonekana kiroja, hii sio democratsia inayo itajika katika kutukomboa waTanzania
 
Solution pekee iliyopendekezwa na chadema kwenye hili ni kufanya maandamano!!!

Naunga mkono maandamano kwa kuwa yata create public awareness to the problem. Kama CCM hawashauriki bungeni ambako Mh Nassari alikuwa na hoja binafsi nzuri yenye lengo la kuboresha utendaji wa baraza la mitihani ikatupwa kapuni kisiasa, unadhani kuna uwezekano wa CHADEMA kuishauri CCM kwa lolote lile kwa njia ya majadiliano?

Ushauri wa njia za kibunge unaletewa propaganda, CDM waliwahi kufanya majadiliano na Mwenyekiti wa CCM mkawakejeli kuwa wameenda kugonga chai na juice. Leo hii CDM wamegoma kujadiliana na mkoloni mweusi na kuamua kufikisha ujumbe kwetu wananchi moja kwa moja. Sio watanzania wote wana access na JF au TV na magazeti and in fact vyombo vingi vya habari CCM imehodhi na inatesa na kuua waandishi wa habari waogope kuikosoa serikali, kwa maana hiyo njia pekee ya CHADEMA kufikisha ujumbe kwa wananchi ni kufanya maandamano. Sisi wananchi wa kawaida tunafarijika sana tunapoungana na viongozi wa chama tunachokipenda cha CHADEMA kufanya maandamano. Pia tunapata fursa ya kuchangia kile kidogo tulichonacho kuendeleza chama kupitia M4C
 
Back
Top Bottom