Mtundiko (thread hii) huu utafungwa haraka sana na aliyeutundika hapa atapigwa "ban" asionekane tena jamii forums. Mimi binafsi nimeshipigwa ban mara kadhaa humu, tena ban la kudumu, lakini bado nimo tuu humu. Kuna wimbo mmoja wa Bob Marley unaitwa "Bad Card". Katika bad card kuna mstari Bob Marley anasema "You a-go tired fe see me face, Can't get me out of the race, Oh, man you said I'm in your place, And then you draw bad cyard, A-make you draw bad cyard, And then you draw bad cyard"
Hiyo ndiyo Jamii Forums, usipokubaliana na uchadema, wanaona "you are in their place".
Kama alivyosema mtoa mada, ndani ya CHADEMA, "nepotism" ndiyo uendeshaji wa chama. Hata CCM nao pia ndiyo hivyo hivyo, ingawa wao kidogo wanachanganya nepotism na "cronyism".
Neno nepotism linatokana na neno la ki-Italiano "nipote". Neno nipote kwa kiingereza linakuwa "nephew". Sasa neno nepotism limeanza kutumika kutokana na tabia ya "papa" wa kanisa katoliki kuwapendelea watoto wao wa kuwazaa wenyewe na kuja kuwa ma-kardinali; na baadaye ma-kardinali hao huwa papa. Lakini kutokana na kwamba "papa" au "pope" hatakiwi kuwa na mtoto, basi watoto wa papa, (popes) walikuwa wakiitwa "nephews" au "nipote" badala ya "sons". Kwa mfano; Pope Callixtus III alimchagua "nephew" Rodrigo kuwa Kardinali. Baadaye Kardinali Rodrigo akaja kuwa papa Alexander VI. Mfumo huu ulishamiri sana ndani ya kanisa katoliki kwa miaka mia kadhaa mpaka alipokuja papa Innocent XII, akakataza tabia ya watu kuwachagua "nephews" kuwa kardinali kuanzia mwaka 1692.
Sasa Chadema kinachofanywa na CHADEMA siyo kitu kipya. CCM nao wanafanya hivyo hivyo. Ingawa kutokana na historia na uzee wa CCM, hakuna mkoa au kanda inayoweza kusema kwamba CCM ni mali yao.
Kuhusu CHADEMA,..... well, waingereza wanasema "the proof is in the pudding"- Godbless Lema. Godbless Lema hana hata sifa ya kuwa "class-monitor" wa darasa la nne wa shule ya msingi. Lakini yupo katika kitovu cha nguvu na utawala wa CHADEMA. Kwanini? kwa sababu - "one of the nephews".