View attachment 141083
Hapa nitaainisha baadhi ya mambo
yanayoiondoa CHADEMA usoni na moyoni mwa
watanzania wanaotaka chama kinachopinga
ufisadi.
1. Mmiliki wa jengo lililopangishwa na
CHADEMA Kinondoni kama ofisi za makao makuu na bei ya pango kwa mwezi vimefanywa
siri. Mara kadhaa swali hili limeibuliwa lakini
hakuna jibu lililoweza kutolewa na uongozi wa
CHADEMA.
2. Wanachama walioomba fursa ya kushiriki
tenda ya kununua magari ya chama wamenyimwa fursa hiyo na hatimaye tenda
hiyo imetolewa kwa usiri mkubwa. Chris Lukosi
amekuwa akishutumiwa kuwa sababu ya kujitoa
kwake CHADEMA ni kunyimwa tenda hii, lakini
pale wadau walipohoji baada ya Lukosi
kunyimwa tenda hiyo ni nani amepewa na kwa vigezo vipi?, kinaibuka kigugumizi.
3. Swala la Katibu Mkuu wa chama kujikopesha
mamilioni ya shilingi zilizochangwa na
walalahoi kwa ajili ya shughuli za chama.
Ikumbukwe kuwa watu waliochangia M4C
walifanya hivyo kwa vile waliamini kuwa michango yao itakiwezesha chama kujiimarisha.
Taarifa kuwa pesa zimetumika kifisadi
zimewavunja watu moyo.
4. Taarifa za Josephine Mushumbusi kulipwa
mamilioni ya shilingi za chama kwa kazi
anayoiita ya kujitolea. Wadau walihoji kuwa na wao wangependa kujitolea kwenye shughuli za
chama ili walipwe hayo mamilioni. Ilidhihirika
kuwa Josephine alipata fursa hiyo kwa
upendeleo.
5. Pesa za ruzuku zimekuwa zikiishia Makao
Makuu. Watendaji wa chama mawilayani wamekuwa wakifanya kazi bila nyenzo. Hii
ilisababisha mpaka kukawa na mtafaruku huko
Mpanda kwa kukosa ofisi ya wilaya ambayo
kimsingi ni jukumu la chama makao makuu
kuhakikisha chama kina ofisi za wilaya.
Ikumbukwe pia kuwa matumizi haya mabaya ya fedha yalikuwa sababu ya mvutano wa kisiasa
kati ya marehemu Chacha Wangwe na kiongozi
Mkuu wa Chama.
6. Kumekuwa na taarifa za matumizi mabaya
ya pesa za Sabodo jambo ambalo limeelezewa
kuwa sababu ya kumfanya Sabado kuahirisha ahadi yake ya kuijengea CHADEMA ofisi za
makao makuu na chuo cha siasa.
7. Katibu Mkuu wa CHADEMA ni miongoni mwa
washutumiwa wa ufisadi wa mamilioni ya pesa
za mradi wa maji wa Karatu.
8. Viti Maalum vya ubunge vimetolewa kwa upendeleo ambapo akinamama waliojitolea
kukijenga chama wameachwa pembeni na
nafasi hizo kupewa akinamama walio karibu na
viongozi wa juu wa chama. Hapa ikumbukwe
kuwa mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la
CHADEMA (BAWACHA) wa Taifa alishinda nafasi ya uchaguzi wa viti maalum, lakini
akatolewa kwa kuambiwa kuwa hajakidhi vigezo
vya kuwa mbunge ingawa amewaongoza
wanawake wenzake kwa muda mrefu ndani ya
chadema. Wakati huohuo mwanamama
anayeishi Marekani, Leticia Nyerere amepewa Ubunge wa viti maalum kutokana na
"kufahamiana" na mwenyekiti wa chama. Hili
limewavunja moyo wengi walioanza kuiamini
chadema.
9. Vijana kama Kafulila walioonekana kuwa na
ari ya mabadiliko ndani ya chama wamekuwa wakinyimwa nafasi ya kugombea uongozi
kinyume na katiba.
10. CHADEMA kukanusha kauli ya Nape kuwa
wanapewa msaada na chama cha siasa cha
Ujerumani, baadae ikadhihirika kuwa ni kweli
wanapokea msaada huo. Hii imedhihirisha kuwa CHADEMA sio wawazi katika utendaji wao.
Wadau wanajiuliza chama hicho cha siasa
kinataka nini Tanzania mpaka kikipinge chama
kilichoasisiwa na wapigania Uhuru na kutaka
chadema iingie madarakani? Ikumbukwe kuwa
muasisi wa CHADEMA Mzee Mtei, alikataa kushiriki harakati za kupigania uhuru na pia
alikataa kujitolea kuijenga nchi baada ya Uhuru.
11. Hesabu za pesa zinazochangwa na
walalahoi kwa ajili ya M4C imekuwa ni jambo la
siri kubwa ndani ya CHADEMA
Hivi nitakosea nikimuweka mleta mada kwenye kundi la book 7?
Tiba
naomba ukumbuke tarehe ya comment yakoINAWEZEKANA wala si la kushangaaa maana hata slaa akifukuzwa chadema ata rudi CCM
Hivi nitakosea nikimuweka mleta mada kwenye kundi la book 7?
Tiba
naomba ukumbuke tarehe ya comment yako
Tayari nimeandika!! maana baada ya zito anafuata yeye!! Maana katumika sana kama zito Kabwe utamu ulivyoisha hawamtaki tena!
Lini mtazinduka nyie misukule? Kila kitu kupinga tu, hata ukweli hamuutaki! Mtei lini aligombea uhuru?
Kumbe Chadema pale Ufipa wamepanga, ruzuku yote wanaochukuwa kila mwezi inakwenda wapi, wameshindwa kununua jengo lolote hapo mjini.
R.I.P
rafiki yangu Pascal Ndege shabikia CCM upate pesa lakini fahamu watanzania wanaumia kuna watanzania wanfanya kazi kwenye makampuni ya nguo wanalipwa less than 120000 wewe unashabikia CCM
rafiki sijui kama unajua unayoyatete pale CCM
unafahamu kuwa kuna watanzania hawapati chakula cha mchana ..........na kuna mikataba ya ajabu kwenye madini yetu
ushawahi ona PPA yoyote viongozi wako wa chama walio sign
je unafahamu kuwa kuna kampuni inawauzia tanesco Umeme sent 6 za kimarekani sawa na shiling 97 za kitanzania lakini wewe unauziwa shiling 305 tshs
je unajua watu wa aina ganin wanatawala uchumi wa Tanzania
unafahamu watu dar -es - salaam less than 10% wanapata maji safi
Hizi ni pumba mbona hutaji kiasi cha pesa? au unabuni? majungu tuuuu unataka waweke kila kitu hadharani kwani ni chama tawala hicho? mbona chama tawala mali zao huzijui? hata madeni ya nchi na makusanyo ya kodi huyajui? shida yako ni cdm hao ndio wanakuletea maisha bora? peleka u.j.i.n.g.a hukoView attachment 141083
Hapa nitaainisha baadhi ya mambo
yanayoiondoa CHADEMA usoni na moyoni mwa
watanzania wanaotaka chama kinachopinga
ufisadi.
1. Mmiliki wa jengo lililopangishwa na
CHADEMA Kinondoni kama ofisi za makao makuu na bei ya pango kwa mwezi vimefanywa
siri. Mara kadhaa swali hili limeibuliwa lakini
hakuna jibu lililoweza kutolewa na uongozi wa
CHADEMA.
2. Wanachama walioomba fursa ya kushiriki
tenda ya kununua magari ya chama wamenyimwa fursa hiyo na hatimaye tenda
hiyo imetolewa kwa usiri mkubwa. Chris Lukosi
amekuwa akishutumiwa kuwa sababu ya kujitoa
kwake CHADEMA ni kunyimwa tenda hii, lakini
pale wadau walipohoji baada ya Lukosi
kunyimwa tenda hiyo ni nani amepewa na kwa vigezo vipi?, kinaibuka kigugumizi.
3. Swala la Katibu Mkuu wa chama kujikopesha
mamilioni ya shilingi zilizochangwa na
walalahoi kwa ajili ya shughuli za chama.
Ikumbukwe kuwa watu waliochangia M4C
walifanya hivyo kwa vile waliamini kuwa michango yao itakiwezesha chama kujiimarisha.
Taarifa kuwa pesa zimetumika kifisadi
zimewavunja watu moyo.
4. Taarifa za Josephine Mushumbusi kulipwa
mamilioni ya shilingi za chama kwa kazi
anayoiita ya kujitolea. Wadau walihoji kuwa na wao wangependa kujitolea kwenye shughuli za
chama ili walipwe hayo mamilioni. Ilidhihirika
kuwa Josephine alipata fursa hiyo kwa
upendeleo.
5. Pesa za ruzuku zimekuwa zikiishia Makao
Makuu. Watendaji wa chama mawilayani wamekuwa wakifanya kazi bila nyenzo. Hii
ilisababisha mpaka kukawa na mtafaruku huko
Mpanda kwa kukosa ofisi ya wilaya ambayo
kimsingi ni jukumu la chama makao makuu
kuhakikisha chama kina ofisi za wilaya.
Ikumbukwe pia kuwa matumizi haya mabaya ya fedha yalikuwa sababu ya mvutano wa kisiasa
kati ya marehemu Chacha Wangwe na kiongozi
Mkuu wa Chama.
6. Kumekuwa na taarifa za matumizi mabaya
ya pesa za Sabodo jambo ambalo limeelezewa
kuwa sababu ya kumfanya Sabado kuahirisha ahadi yake ya kuijengea CHADEMA ofisi za
makao makuu na chuo cha siasa.
7. Katibu Mkuu wa CHADEMA ni miongoni mwa
washutumiwa wa ufisadi wa mamilioni ya pesa
za mradi wa maji wa Karatu.
8. Viti Maalum vya ubunge vimetolewa kwa upendeleo ambapo akinamama waliojitolea
kukijenga chama wameachwa pembeni na
nafasi hizo kupewa akinamama walio karibu na
viongozi wa juu wa chama. Hapa ikumbukwe
kuwa mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la
CHADEMA (BAWACHA) wa Taifa alishinda nafasi ya uchaguzi wa viti maalum, lakini
akatolewa kwa kuambiwa kuwa hajakidhi vigezo
vya kuwa mbunge ingawa amewaongoza
wanawake wenzake kwa muda mrefu ndani ya
chadema. Wakati huohuo mwanamama
anayeishi Marekani, Leticia Nyerere amepewa Ubunge wa viti maalum kutokana na
"kufahamiana" na mwenyekiti wa chama. Hili
limewavunja moyo wengi walioanza kuiamini
chadema.
9. Vijana kama Kafulila walioonekana kuwa na
ari ya mabadiliko ndani ya chama wamekuwa wakinyimwa nafasi ya kugombea uongozi
kinyume na katiba.
10. CHADEMA kukanusha kauli ya Nape kuwa
wanapewa msaada na chama cha siasa cha
Ujerumani, baadae ikadhihirika kuwa ni kweli
wanapokea msaada huo. Hii imedhihirisha kuwa CHADEMA sio wawazi katika utendaji wao.
Wadau wanajiuliza chama hicho cha siasa
kinataka nini Tanzania mpaka kikipinge chama
kilichoasisiwa na wapigania Uhuru na kutaka
chadema iingie madarakani? Ikumbukwe kuwa
muasisi wa CHADEMA Mzee Mtei, alikataa kushiriki harakati za kupigania uhuru na pia
alikataa kujitolea kuijenga nchi baada ya Uhuru.
11. Hesabu za pesa zinazochangwa na
walalahoi kwa ajili ya M4C imekuwa ni jambo la
siri kubwa ndani ya CHADEMA
Sikuelewi jimbo la mtela na mwisho mwampamba wanahusikaje na hii mada ya leo???
Au ndio wale wale wasiyojua maana ya mgongano wa mawazo?
sijui kwanini hii dhambi ya ufisadi ipo kila kona!!! Sielewi chanzo!! Mnisaidie jamii forum
Sasa kama huna takwimu ndio Umeandika nini hapa? mtwela bana ....Muuulize mwanachama wa chadema maana anatakwimu zote anaogopa kuZitoa maana atajulikana!!
Sasa kama huna takwimu ndio Umeandika nini hapa? mtwela bana ....