View attachment 141083
Hapa nitaainisha baadhi ya mambo
yanayoiondoa CHADEMA usoni na moyoni mwa
watanzania wanaotaka chama kinachopinga
ufisadi.
1. Mmiliki wa jengo lililopangishwa na
CHADEMA Kinondoni kama ofisi za makao makuu na bei ya pango kwa mwezi vimefanywa
siri. Mara kadhaa swali hili limeibuliwa lakini
hakuna jibu lililoweza kutolewa na uongozi wa
CHADEMA.
2. Wanachama walioomba fursa ya kushiriki
tenda ya kununua magari ya chama wamenyimwa fursa hiyo na hatimaye tenda
hiyo imetolewa kwa usiri mkubwa. Chris Lukosi
amekuwa akishutumiwa kuwa sababu ya kujitoa
kwake CHADEMA ni kunyimwa tenda hii, lakini
pale wadau walipohoji baada ya Lukosi
kunyimwa tenda hiyo ni nani amepewa na kwa vigezo vipi?, kinaibuka kigugumizi.
3. Swala la Katibu Mkuu wa chama kujikopesha
mamilioni ya shilingi zilizochangwa na
walalahoi kwa ajili ya shughuli za chama.
Ikumbukwe kuwa watu waliochangia M4C
walifanya hivyo kwa vile waliamini kuwa michango yao itakiwezesha chama kujiimarisha.
Taarifa kuwa pesa zimetumika kifisadi
zimewavunja watu moyo.
4. Taarifa za Josephine Mushumbusi kulipwa
mamilioni ya shilingi za chama kwa kazi
anayoiita ya kujitolea. Wadau walihoji kuwa na wao wangependa kujitolea kwenye shughuli za
chama ili walipwe hayo mamilioni. Ilidhihirika
kuwa Josephine alipata fursa hiyo kwa
upendeleo.
5. Pesa za ruzuku zimekuwa zikiishia Makao
Makuu. Watendaji wa chama mawilayani wamekuwa wakifanya kazi bila nyenzo. Hii
ilisababisha mpaka kukawa na mtafaruku huko
Mpanda kwa kukosa ofisi ya wilaya ambayo
kimsingi ni jukumu la chama makao makuu
kuhakikisha chama kina ofisi za wilaya.
Ikumbukwe pia kuwa matumizi haya mabaya ya fedha yalikuwa sababu ya mvutano wa kisiasa
kati ya marehemu Chacha Wangwe na kiongozi
Mkuu wa Chama.
6. Kumekuwa na taarifa za matumizi mabaya
ya pesa za Sabodo jambo ambalo limeelezewa
kuwa sababu ya kumfanya Sabado kuahirisha ahadi yake ya kuijengea CHADEMA ofisi za
makao makuu na chuo cha siasa.
7. Katibu Mkuu wa CHADEMA ni miongoni mwa
washutumiwa wa ufisadi wa mamilioni ya pesa
za mradi wa maji wa Karatu.
8. Viti Maalum vya ubunge vimetolewa kwa upendeleo ambapo akinamama waliojitolea
kukijenga chama wameachwa pembeni na
nafasi hizo kupewa akinamama walio karibu na
viongozi wa juu wa chama. Hapa ikumbukwe
kuwa mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la
CHADEMA (BAWACHA) wa Taifa alishinda nafasi ya uchaguzi wa viti maalum, lakini
akatolewa kwa kuambiwa kuwa hajakidhi vigezo
vya kuwa mbunge ingawa amewaongoza
wanawake wenzake kwa muda mrefu ndani ya
chadema. Wakati huohuo mwanamama
anayeishi Marekani, Leticia Nyerere amepewa Ubunge wa viti maalum kutokana na
"kufahamiana" na mwenyekiti wa chama. Hili
limewavunja moyo wengi walioanza kuiamini
chadema.
Kweli nimeamini pombe ni haramu, inaonekana Pasco kabla ya kuandika haya alipiga viroba vya kutosha!!
Kaandika kipombepombe! Siku nyingine kuwa macho makavu ndio uandike!