Challenge ya kusave pesa UTT

Wengi hamjui ya kwamba huko UTT sio guarantee hela ya itazalishwa tu pia kuna risk tafauti na benki inakua imekaa tu
 
Ba
Nasikitika kakwambia hiyo pesa hutoifaidi inapokuwa imenona lazima mkeo akuwaishe mbele ya haki ili yeye awe huru kutumia na vijana wadogo maisha ni haya haya tunayoishi
 
Ba

Nasikitika kakwambia hiyo pesa hutoifaidi inapokuwa imenona lazima mkeo akuwaishe mbele ya haki ili yeye awe huru kutumia na vijana wadogo maisha ni haya haya tunayoishi
Usiwaze ndugu yangu hata mimi nilikuwa na mawazo kama yako ila UTT hawakulazimishi nani umuandike kama mrithi wako.

Na kwanini utangaze kuwa kuna hela umewekeza UTT kama unabusara unawaambia watu wako wa karibu tu.Ukiwa na mke kichomi haya mambo hatakiwi kabisa kujua😀😀

Mimi kwenye warithi wangu nimewaandika watoto wangu ndugu zangu na mama yangu.Kwahiyo huyo unayemuwaza kuwa atakula jasho langu hayo na hana chake hapo.

Tena unaandika na % asilimia za wao kupata.So mtu anaweza akawa mrithi ila akalamba asilimia 5 kuwa mrithi haikufanyi uwin maisha ila inategemea na aliyeandika kakupa asilimia ngapi.
 
UTT ina risk Kuna kupata na kupoteza tatizo wengi mnafata mkumbo
Kaka tumbili hebu funguka kama mwanaume mbona unarukaruka na unatoa mawazo yako kama mtu ambaye hajaelimika.

Andika vizuri na kwa kirefu unachotaka kukisema ili watu wakuelewa na ikiwezekana tukupinge kwa hoja.
 
Wekeza kwenye biashara mbalimbali, huko kwenye risk ndogo na faida ni ndogo.
Upo sahihi ila biashara siyo ya kila mtu.Sisi wengine tunaona bora kuwekeza kwenye risk ndogo,ambapo hela yangu itakuwepo na bado ntapata faida.Muda wowote nikiitaka hiyo pesa naipata.So UTT ni mgodi uliosahaulika.

Na pengine kama unauwezo wa kuwekeza kwenye biashara fanya hivyo ila usisahau kuwekeza na kwenye UTT.Biashara hazitabiriki na hazina formula.

Kwa UTT kama unapata hela ya kula basi nyingine tupia huko subiri miaka yako 10 to 15 nenda vuta mkwanja fanya mambo yako.Kutesa kwa zamu sisi zamu yetu bado,wacha tuendelee kusubiri.

📌Cha msingi na cha muhimu ni uvumilivu.
 
HIvi naweza kifungua akaunt yangu mwenyewe ya utt na kuanza kudundulizia huko bila kifika ofisi zao?
Unaweza kufungua piga *150*82#.

Utafungua account na kuruhusiwa kuwekeza ila hutaweza kuzitoa hizo hela mpaka ukakamilishe usajili.Na usajili utaukamilisha kwenye ofisi zao au kwa mawakala wao,au chukua form kwa mawakala jaza na uiscan na uwatumie kwa e-mail.

Kama utaenda ofisini kwao usisahau kubeba kitambulisho cha nida au namba ya nida na picha ya pasport.Pia na bank account namba ambayo ungependa uiunganishe na UTT.
 
Ahsante sana mkuu ...
 
Mi nataka kuona hela yangu, siiweki ukutani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…