Chagonja na sinema ya mwaka!

Chagonja na sinema ya mwaka!

Hiyo habari ya Tanga itapata mashiko baada ya uchaguzi. CCM wamewekeza sana kwenye propaganda baada ya kuona watz wanajua thamani ya amani, kila tunapokuwa tunaelekea kwenye uchaguzi CCM wanakuja na propaganda mpya na baada ya uchaguzi mambo yanatulia. Nakwambia kabisa ukikuta kuna kikundi chochote kinaonekana kama tishio kwa nchi hii ujue kinalelewa na ccm, nje ya hapo hakuna kikundi kinachoweza kusumbua Polisi na JWTZ. We subiri utasikia baada ya uchaguzi.

Mh! kwamba Tz ndo mwamba kuliko Nigeria ktk Africa au Kenya kias yakwamba hakuna Kikundi chochote cha kigaidi kinaweza kufanya vurumai?

Huo ni mtazamo wako tu mkuu. Amini issue hii iko serious.
 
Hiki ni kichaka cha kuzuia maandamano yoyote yajayo.
 
Unajivamia,unajiteka,unajitorosha,unajisaka na hatimaye unatangaza kujitafuta kwa udi na uvumba.Matukio yote haya haya hayana majina ya waathirika.

Kweli siasa zimefikia mahala pake!Tutashuhudia mengi 2015.
is this true
 
Mkuu;
Naamini hii busara hapa chini itakusaidia sana,wewe pamoja na wenzako.

TuntemekeSanga;
Huyu jamaa alikuwa anawaambia maccm wenzako, ukiwemo na weye pia. Waliamka watu na vitambi vyao wakavibeza vyama vya upinzani; Hivi vyama vya msimu msijiunge nao. CCM ndo chama vingine vya msimu. Wameuona UKAWA sasa kamasi lina watoka. Kwa sababu, hawakuamini hili lingetokea. Wakadharau vyama vya upinzani kuwa vya kidini na ukanda, watz wakawagundua kuwa ni fix leo wamekaa kimyaa. Wakaingia misikitini na mabuti kutoa silaha za majambia, hata kisu cha kukatia kitunguu hamkutoa mle. Mmerushia watu mabomu mkazuia wasikamatwe kwa kuwa walikuwa wenyu, leo mbona mwasema kuwa hao si wenyu? Ukicheza na mbwa, ataingia nawe msikitini. Sasa swalaa imeharibika.
 
Naikumbuka saana 1995. Wakambuni Mrema ili aue upinzani. Mrema kuona alivyo kubalika kwa sababu ya hasira ya wananchi kwa lichama hili, akawageuka. Almanusra achukue nchi. Kama sio kubadilishiwa tangazo la kura leo mambo yangekuwa mengine.


Sasa wameamua kubuni haya magenge mara sijui Panya road, mara sijui Al-shabab. Yoote kutishia wazee wawape kura zao ati zimwi likujualo.

Mara hakuna daftari la wapiga kura. Tatizo ni kwamba, mwananchi wa leo kaamka, anajua anacho kitaka. Kuna siku, mtabuni magenge haya muwaambie wamlenge mtu kichwa nao wafanye kweli.

Siasa mbofu mbofu ziondoke kwetu jamani. Mnabadili mpaka Elim?? Miaka yoote 10 mlikuwa wapi mje kuamka leo bado siku 180?

Angalieni, mtatuletea balaa bure na hizi mbinu zenu.

Umesahau mapanga ya IGP Mahita na hayo makontena? Kumbe mapanga hayo yalichorowa rangi na bendera ya CUF pale polisi Kilwa Road. Uchaguzi unakuja, elimu bure, matokeo ya kidato cha nne WOTE wamefaulu, MUNGU wangu nchi hii.........
 
wewe kama unadhani matukio yanayoendelea ni kujiteka nadhani yafaa kupimwa akili. Wahuni wanataka kutuingiza kwenye chuki za kidini halafu unatuambia watu wanajiteka. Vipi wewe?
 
Mahala fulani huko Kakonko-Kigoma (mwaka jana) yalivumbuliwa mabomu mazito na wananchi waliokuwa wakichimba mtaro wa maji.

JW waliitwa kuja kuyategua. Teh! yaani Raia walijazana hapo kama vile wako Uwanja wa Taifa kwenye maadhimisho fulani(pamoja na onyo/kalipio lililokuwa likitolewa).

Usijaribu kuonja sumu kwa kuiramba. Hata Nigeria yalianza hivihivi, "critical-thinkers" kama nyie wakawa wanayajadili easily tu kama hivi nakuhusisha matukio na propaganda za serikali tawala.

And what is going on now over there, i can not mention it as you also aware of it.
Thanks!

Tuntemeke kwa jinsi unavyojitahidi kupambana kulazimishia kwamba hili movie ni la kweli nahisi wewe ni mmoja wa watu waliotunga hili movie. Hivi nyinyi viongozi wetu mmelala kwenye kitanda cha aina gani? Toka ile michango ya jana huku ya wananchi kuonyesha wameshtukia hili movie si mngepotezea tu nani angewauliza? Zamani mlikuwa mnatunga movie za aina hii watu wanazikubali maana walikuwa bado wamelala, kumbuku majambia ya CUF, matokea yake wale waliokuwa wamelala wameamka nyinyi ndio mmeingia usingizini. Kama kazi ya ulinzi wa nchi imewashinda si muende mkacheze tu movie za kivita? Au wewe ndio ulikuwa unazunguka zamani na zile sinema za vita za Rwanda kuwaaminisha watu kwamba wakichagua upinzani kutatokea vita?

Huko kwenye jeshi la polisi kuna polisi vijana na wana elimu nzuri tu, si bora muwaachie kuliko kuendelea kuwamezesha mbinu za kizamani wakati dunia imebadilika. Maana ninachokiona baada ya kuona movie linabuma ikabidi muongeze magari kwenda huko ili mlazimishe kile watu wanachopinga, toka lini polisi wakazuia waandishi wa habari kupiga picha? Picha zinapigwa hata kwenye vita sembuse watu mnaodanganya wamejificha kwenye mapango. Halafu kwa usanii wa namna hii ndio tutegemee siku tukivamiwa kukamata adui achilia mbali kumshinda? Acheni kuchezea kodi za wananchi kwa propaganda za kizee wengine tunategemea utalii bana.
 
Ok, kwahiyo intelijensia ya geshi la Chagonja bado hawajathibitisha kama ni hawa wadudu au la?
Ila kwenye maandamano ya amani ya CUF au CDM Chagonja huwa anajuaga miezi kadhaa kabla kwamba kutakuwa na uvunjifu wa amani.
Mko vizuri

Mkuu utamfanya aache kuchangia bure.
 
  • Thanks
Reactions: 999
wewe kama unadhani matukio yanayoendelea ni kujiteka nadhani yafaa kupimwa akili. Wahuni wanataka kutuingiza kwenye chuki za kidini halafu unatuambia watu wanajiteka. Vipi wewe?

nan kakwambia kuna ugaidi tanzania wacheni mchezo bhanaa
 
mangatara.

Ninyi muishi tu kwa.. assumpitions hizohizo badala ya kustuka na kutoa ushirikiano kwa serikali,kalieni hayohayo .kwamba ni mbinu zaCCM.

Tuombe uzima. Mtakiri tu kwamba ushabiki kama huo mnaoufanya hauna mantiki hata kidogo.

Take my words with a special regards. Nakuhakikishia jambo hilo.
Mkuu lakini hii hali ya kutoaminika kwa baadhi ya mambo yakiwemo haya ya ugaidi ni CCM wenyewe ndio wamesababisha kwa ujinga wao.Mara ooh CHADEMA magaidi wakiulizwa wamefanya ugaidi gani? utawasikia wanaume wazima wanakwambia wamemwagia mtu tindikali,mara ooh Lwakatare anataka kumteka Msaky,mara ooh CHADEMA wamemteka Ulimboka huku Raisi wa nchi anacheka bila kuona athari ya ujinga huu wa akina Mwigulu.Mara ooh Chadema Wamejilipua Arusha.Wakiambiwa unda tume hawataki,mara ooh kitu chenye ncha kali kutoka wafuasi wa Chadema kilimpiga marehemu Ali Zona,mara kitu kilirushwa kutaka walipo wafuasi wa Chadema kikamlipua Mwangosi.Sasa upuuzi wote huu unawafanya raia wanaidharau serikali kwa matukio kama haya (Ugaidi) Polisi,Mwigulu,Nape na yule mkubwa wao ujinga ujinga ujinga.
 
Last edited by a moderator:
Hivi, kwa akiri ya kawaida tu mapambano ya polisi na hao wanaoitwa magaidi hakuna majeruhi wala vifo upande wa magaidi? mbona hili jeshi letu linataka kutugeuza watanzania kama matahila vile? wao waue, wajeruhi ila wao wsikamatwe hata mmoja na watumike mpka Jwtz?
.

Halafu sasa wasijue kua wanayadhalilisha sana majeshi yetu hasa jeshi mahili kama JWTZ.wananchi wanaweza kuona ni jinsi gani hawako salama ikiwa jeshi lenye vifaa vya hali ya juu na mafunzo bora kama JW linashindwa kuwamudu magaidi wachovu kama hao wanaovaa yebo tena wakiwa wamezingirwa na polisi na wanajeshi.Tunayadhalilisha sana sana majeshi yetu labda kama kuna taarifa za magaidi kuteketezwa zimefichwa.
 
Utasikia Chama fulani kinahusika.

Hahahaaa CCM bhana na Mapolisi uchwara na mipango yao ya kitoto.
 
Mkuu lakini hii hali ya kutoaminika kwa baadhi ya mambo yakiwemo haya ya ugaidi ni CCM wenyewe ndio wamesababisha kwa ujinga wao.Mara ooh CHADEMA magaidi wakiulizwa wamefanya ugaidi gani? utawasikia wanaume wazima wanakwambia wamemwagia mtu tindikali,mara ooh Lwakatare anataka kumteka Msaky,mara ooh CHADEMA wamemteka Ulimboka huku Raisi wa nchi anacheka bila kuona athari ya ujinga huu wa akina Mwigulu.Mara ooh Chadema Wamejilipua Arusha.Wakiambiwa unda tume hawataki,mara ooh kitu chenye ncha kali kutoka wafuasi wa Chadema kilimpiga marehemu Ali Zona,mara kitu kilirushwa kutaka walipo wafuasi wa Chadema kikamlipua Mwangosi.Sasa upuuzi wote huu unawafanya raia wanaidharau serikali kwa matukio kama haya (Ugaidi) Polisi,Mwigulu,Nape na yule mkubwa wao ujinga ujinga ujinga.

Na kuna methali inasema ..."Mchimba shimo kaingia mwenyewe...."sasa IMANI kwa serikali imedondoka sababu mara nyingi wanatumia uwongo ili kuwatafutia chuki wapinzani.Sasa hii imekula kwao........
 
Nyie mnaopinga ni hivi, wale kweli ni magaidi,ila kosa walilofanya polisi hadi wale magaidi wakatoroka nikwamba polisi walisahau kwenda na lile gari lao lenye maji ya KUWASHA ili wawanyunyizie tu humo shimoni au pangoni wangetoka tu wenyewe,pia wangerushiamo tubomu tuwili tu twa kutoa machozi,aah wangetoka wakiwa wanalia machozi na kujikuna na kuziacha Kalashinokov zao humohumo.Mbona akina Halima mdee huwa wanakomeshwa tu namna hii!wakijidai kuandamana?
 
Mh!
Hata wangevaa "MAGURUDUMU" kama ya masai bado wangeweza kuchafua hali ya hewa.

Hata wangevaa gun-boots na sare za kijeshi, kama unania ya kukejeri ungetunga habari nyingine tu.

Askari waliojeruhiwa au waliouawa lazima watatanabaishwa tu. Hii ni system na utaratibu wa taasisi ya kijeshi(u never know). Lakini mwisho wa siku, hakuna kitakachofichika maana kama mtu kafa, lazima atazikwa publicly.

Naogopa kwamba hata majeruhi & huyo alofariki wakioneshwa wazi, mtasema ni MAZINGAOMBWE! Teh! kazi sana Bongo-land...

Hivi we TuntemekeSanga unatuona sisi ni watoto sana. Hakukuwa na sakata la richmond hapa nchini mpaka akaletwa mmiliki fake anaitwa sijui Ali Adawi na akagoma kupigwa picha? Unatutishia sijui kuna mambo ya system na upuuzi gani sijui, hiyo system si mpaka sasa hivi ipo na kuna hela zimechotwa huko stanbic na majina hakuna. Ni hivi kinachoendelea hapo Tanga ni kiini macho na hii iwafanye mjipange upya kwani wananchi wamekuwa na uelewa mpana sana kuliko nyinyi tuliowapa madaraka.

Tumefikaje hapa kwenye hii hali kama taifa? Hali hii ililetwa na J. Nyerere yeye ndio alituona watanzania hatuna akili za kufikiri na kuchagua viongozi bora, akawa na tabia ya kuchagua viongozi aliowaamini yeye. Kumbe hakujua watu walikuwa na wanatabia za kinafiki na woga. Walipopata madaraka ndio tabia zao halisi zikafahamika, viongozi hao wakawa ni sawa na chui aliyekabidhiwa mwanambuzi ili amchunge. Na kwa kuwa watanzania wengi walikuwa na tabia ya kuamini bila kupima wakawa hawajali hata kupiga kura kuchagua viongozi bora, matokeo yake wakaingia viongozi wengi wabovu na wezi kwenye taasisi za maamuzi, ndio maana hivi leo unaona tume ya uchaguzi inafanya kazi kwa kuacha sheria na kufuata matwakwa ya watawala nyuma ya pazia. Wapinzani wanashinda baada ya mapambano makubwa, kwa kuwa watawala hawakuwa kwa niaba ya wananchi bali maslahi yao. Huko kwenye taasisi za ulinzi watu wanafanya kazi kwa mazoea na kujipendekeza kwa watawala kwani sasa wamekuwa kitu kimoja katika kuliibia taifa. kwa hiyo hicho unachokioona hapa Tanga ni seheme ya huo uhuni unaofanywa na wanasiasa wa ccm wakishirikiana na viongozi wa jeshi kuuhadaa umma kwa faida za kisiasa. Kama utakumbuka vizuri mwanzoni juzi jumamosi taarifa ilitoka ni magaidi, baada ya kupima upepo na kuona watu wamestuka ndio kauli inabadilika eti ni majambazi tu, hivi majambazi ndio wakumaliza kodi za wananchi kwa kupeleka vikosi vyote vile na magari ya polisi kucheza movie isiyo na kichwa wala miguu? Kama ni majambazi tu kwanini wasiende polisi gari 2 zinatosha mpaka kamashna eti naye anakwenda. Hizo nguvu kama zingetumika namna hiyo mbona leo hii tungekuwa na majina yote ya walioiba hela stanbic. Katafuteni watoto muwaambie hayo mambo yenu, hizo mbinu za kizee hazina nafasi kwa nyinyi kuchezea kodi zetu ndugu.
 
TuntemekeSanga kama huna mtoto mdogo wa mwaka mmoja aliyeanza kuota meno mawili basi tafuta hata kwa jirani ukikabeba uwe unakadanganya haya mambo kwa kumuimbia kama wimbo ili alale
 
Last edited by a moderator:
Yetu macho...

Eti magaidi... inakuwaje watu waingize silaha nzito nzito za kivita mpaka waweke kambi!! Mapango ya mamwe nisehemu ambayo watu kila kukicha wanashinda huko kuvuma amwe ya kuuza...ati leeo ni pango la magaidi...

Wazee wa kushika hatamu wamefilisika, wananjuua hakuna wimbo watakaoleta tuwasikilize, wamegundua vitisho.

Najiuliza, kwani kikiingia magogoni chama chochote si watambapana tu na magaidi au lazima wawe wao... waiti a minute, wakishinda..."magaidi" watapotea...
 
Back
Top Bottom