Albedo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 5,559
- 1,452
Kabla ya Dodoma ilikuwa tuende Shinyanga ambapo maandalizi ya awali yalishafanyika yaani yale ya kupima GPS ili helkopta iweze kutua but unfortunately Shinyanga kulikuwa na mvua kubwa hivyo tulishindwa kwenda huko.Kama mvua itakuwa imeisha tutaelekea huko.
Nimesikitishwa sana na jimbo la Mtera.Pamoja na kwamba Malecera amewahi kushika ntadhifa mbalimbali Serikalini ambako naamini ana network kubwa ya ndani na nje ya nchi lakini chakushangaza jimbo lake bado liko nyuma sana kimaendeleo.Jana nilikuwa katika kata moja inaitwa Fufu i was suprised kukuta mapka leo bado watu wanishi kwenye nyumba za tembe.Katika Kata hiyo ina vijiji vitano kikiwemo cha Fufu ambako ndio Makao Makuu ya kata ndipo tulipofanyia mkutano.Wakazi wote kasoro Diwani na Tajiri mmoja wa mifugo ndio wanaishi kwenye nyumba za bati wengine wote kwenye tembe.Shule ya Msingi ina walimu wa 5 tu na ya sekondari ina walimu 4 tu.Mwaka jana katika shule hiyo ya sekondari walimaliza wanafunzi 19 hakuna hata mmoja aliyefanya vizuri kwani kulikuwa na div 4 na 0 tu...Inasikitisha.Kina mama wajawazito wanajifungulia kwenye chumba cha Sindano cha Zahanati.
Nasikitika sio mtaalamu wa kupiga picha vizuri picha zangu hazijatoka vizuri hivyo siwezi kuzituma humu...Nimemuomba Joseph Senga anifundishe kupiga vizuri hope kuanzia kesho nitakuwa nawatumia picha za hali halisi za vijijini sio hizi za mikutano.
Asante sana GS! Kwa Sababu wewe uko kwenye site basi tungependa utuhabarishe mambo yanayotokea huko. Na hilo suala la Picha jitahidi sana ili tuweze kuona Hali halisi ya Vijijini.
Asante