CHADEMA yasambaratika mkoani Kigoma

CHADEMA yasambaratika mkoani Kigoma

Wana CHADEMA muwe waangalifu na nyuzi zinazoanzishwa kwa uchokozi.

Huu uzi umeanzishwa kwa uchokozi, na lengo ni kumchonganisha Zitto na wanachadema.

Suala kubwa ninalojiuliza ni kuwa kwa nini wana JF wanaompinga Dr. Slaa ndio hao hao wanamtetea Zitto kwa nguvu zote? Hivi Zitto ana tofauti gani na Slaa kiitikadi? Je wanampinga Slaa kwa itikadi gani na wanamuunga mkono Zitto kwa itikadi gani tofauti? Naomba Lilambo, Simiyu yetu, mkigoma, Lizaboni, Uncle Deo, thatha, CHAMVIGA, kati kati msaidie kunijibu maswali hayo.
 
Last edited by a moderator:
Nasikia sikia habari za ubaguzi lakini mimi sijaona mfano halisi wa ubaguzi kwenye uzi huu wala katika uhalisia wake ndani ya chama - hebu leteni mifano hai. Tusidanganyane, mimi sitoki Arusha wala Moshi, Chadema hakuna ubaguzi, hii ni propaganda iliyokwisha kushindwa tayari.
 
zito kaishiwa amebakisha mbwemwe kwenye bongofleva na ........
 
Zito sio Mungu wa chadema
akiondoka watakuaj wengine wenye uwezo zaidi yake.
watu wa kIgoma wamesoma na wana mwamko na Chadema haiwezi kusambaratika kirahisi hivo.
Nimeishi na watu wa Kigoma najua maamuzi yao yao sio ya kutetereka kirahisi kama unavodhani.
haya fasta kachukue buku saba yako,sisi tunaitetea chadema kwa moyo bia kulipwa ingawa sio mwanachama wake
 
Nasikia sikia habari za ubaguzi lakini mimi sijaona mfano halisi wa ubaguzi kwenye uzi huu wala katika uhalisia wake ndani ya chama - hebu leteni mifano hai. Tusidanganyane, mimi sitoki Arusha wala Moshi, Chadema hakuna ubaguzi, hii ni propaganda iliyokwisha kushindwa tayari.

Ila unatoka mbulu ndo wale wale chai ya rangi sles kavu!
 
bora kifia huko huko kigoma, ila kwingine ndio kwanza kinavuna wanachama!
 
Mwezi Septemba mwaka 2006, Zitto Zuberi Kabwe alitangaza nia yake ya kutogombea Ubunge mwaka 2010 na ilipofika Novemba 2009 mwaka moja kabla ya Uchaguzi Mkuu akasisitiza tena hiyo nia yake kama ifuatavyo;
Zitto said:
Mpango wangu ni kutogombea tena ubunge ili niweze kusoma na kupata Phd na niweze kuwa mhadhiri wa chuo kikuu. Ninapenda zaidi kufundisha kuliko siasa, kuna shinikizo kubwa kuwa nigombee tena, lakini nafsi yangu ni nzito sana kurudi Bungeni. Niliweka nia yangu hii toka Septemba mwaka 2006, lakini watu hawataki kabisa kuelewa hili. Nadhani sitagombea.
Aligombea na alipata Ubunge kupitia Chadema!

Septemba mwaka 2012, Zitto Zuberi Kabwe alitangaza nia yake ya kutogombea Ubunge mwaka 2015 na badala yake atagombea Uraisi kupitia Chadema;
Zitto said:
Kama Mungu ataniweka mpaka mwaka 2015, sitagombea ubunge tena kwa sababu kazi niliyofanya inatosha. Natangaza rasmi kuwa nitagombea urais kupitia chama changu cha Chadema, bila kusababisha msuguano wowote na sitaki kuingia katika historia ya kurudisha nyuma harakati za upinzani kushika dola. Kwanza nataka niwahakikishia watu wa Kigoma msiwe wanyonge…mna uwezo wa kutoa rais wa nchi hii
Mmmh! ...Juzi juzi mwaka huu wa 2013, Zitto Zuberi Kabwe kaibuka tena na kutangaza nia yake ya kutogombea Ubunge wala Uraisi mwaka 2015 na safari hii kasema hivi;
Zitto said:
Ninachokifanya ndugu zangu ninaomba mjiandae kisaikolojia katika hili, ninatamka wazi kuwa mwaka 2015 sitagombea ubunge tena katika jimbo letu hili la Kigoma Kaskazini na lengo la kufanya hivi ni kutoa fursa kwa watu wengine kutoka ndani ya CHADEMA nao waonyeshe uwezo wao wa kuwahudumia wananchi.
Safari hii mimi sitatia neno!
 
Wana CHADEMA muwe waangalifu na nyuzi zinazoanzishwa kwa uchokozi.

Huu uzi umeanzishwa kwa uchokozi, na lengo ni kumchonganisha Zitto na wanachadema.

Suala kubwa ninalojiuliza ni kuwa kwa nini wana JF wanaompinga Dr. Slaa ndio hao hao wanamtetea Zitto kwa nguvu zote? Hivi Zitto ana tofauti gani na Slaa kiitikadi? Je wanampinga Slaa kwa itikadi gani na wanamuunga mkono Zitto kwa itikadi gani tofauti? Naomba Lilambo, Simiyu yetu, mkigoma, Lizaboni, Uncle Deo, thatha, CHAMVIGA, kati kati msaidie kunijibu maswali hayo.

So simple zitto ni mtanzania mwenye uchungu na watanzania. Anasimamia watanzania wala sio wanachadema. Ni mtu asiye na chuki, kinyongo, sio mbaguzi wa dini,kabila wala kanda. Anajiweka wazi ni kiongozi wa kuwatumikia wanyonge. Siasa huwa kwake zinaishia kwenye uchaguzi after anawatumikia watanzania bila kujali chama. Anapendwa na watu wa ccm,cuf, et al kwakuwa anaweka maslahi ya taifa mbele. Sinahaja kuandika sana ila zitto ni kuwa mzalendo.
 
Last edited by a moderator:
So simple zitto ni mtanzania mwenye uchungu na watanzania. Anasimamia watanzania wala sio wanachadema. Ni mtu asiye na chuki, kinyongo, sio mbaguzi wa dini,kabila wala kanda. Anajiweka wazi ni kiongozi wa kuwatumikia wanyonge. Siasa huwa kwake zinaishia kwenye uchaguzi after anawatumikia watanzania bila kujali chama. Anapendwa na watu wa ccm,cuf, et al kwakuwa anaweka maslahi ya taifa mbele. Sinahaja kuandika sana ila zitto ni kuwa mzalendo.

ccm na cuf wanampenda sababu wanajua ni pandikizi lao ndani ya cdm,na kwa sababucdm kumejaa watu wenye weledi wa kutosha mradi wake umekwama,2015 ccm watampa chuo cha kufundisha and most likely ni UDOM.Mwambie aje atuambie kwa nini alinunuliwa na barick hadi kafungwa mdomo!!!!
mtu ana utajiri wa kutisha(hummer,vogue)
 
Kutokana na mvutano unaoendelea ndani ya Chama cha demokrasia na maendeleo na Chadema imesababisha Chama hicho kusambaratika na kupoteza mvuto mkoani kigoma, sababu hasa inaonekana ni kutengwa kwa kijana wao zitto kabwe ndani ya chama hicho, na hata tetesi zinazoongelewa katika vijiwe vya siasa mkoani kigoma, aliye kuwa mgombea wa chama cha chadema Mwaka 2010 Ally mlee akakihama Chama muda wowote kuanzia sasa. Hali ni mbaya mkoani hapa, kila kijiwe kinaongelea ubaguzi ndani ya chama hicho.
Unaweza kufafanua hapo kwenye RED Zitto ametengwa katika nyanja zipi weka mifano ueleweke la sivyo tutaichukulia taarifa hii kama ya UDAKU ambazo tumezoea kuzisikia kila kukicha kwani Arusha mlisema haya kilichotokea 4 - 0
 
anae mwona zito hajafanya lolote ndani ya cdm nimwehu.siyo kigoma tu.zito kasaidia chadema songea watu kuifaham.zito alifanya kazi hiyo pale alipokuja kumnadi diwani wa kata ya majengo.kata ya majengo songea ndio ilikuwa chachu ya chadema kukubalika mjin songea.wewe unae sema zito hajafanya lolote.tukupime akili zako.je wewe umekifanyia nini chadema?.zito nikiongozi pekee tanzania mchapakazi.
 
Mwezi Septemba mwaka 2006, Zitto Zuberi Kabwe alitangaza nia yake ya kutogombea Ubunge mwaka 2010 na ilipofika Novemba 2009 mwaka moja kabla ya Uchaguzi Mkuu akasisitiza tena hiyo nia yake kama ifuatavyo;

Aligombea na alipata Ubunge kupitia Chadema!

Septemba mwaka 2012, Zitto Zuberi Kabwe alitangaza nia yake ya kutogombea Ubunge mwaka 2015 na badala yake atagombea Uraisi kupitia Chadema;

Mmmh! ...Juzi juzi mwaka huu wa 2013, Zitto Zuberi Kabwe kaibuka tena na kutangaza nia yake ya kutogombea Ubunge wala Uraisi mwaka 2015 na safari hii kasema hivi;

Safari hii mimi sitatia neno!
mkuu Mag3 nimekusoma between the lines,this guy is a liar,,can't be trusted.
 
So simple zitto ni mtanzania mwenye uchungu na watanzania. Anasimamia watanzania wala sio wanachadema. Ni mtu asiye na chuki, kinyongo, sio mbaguzi wa dini,kabila wala kanda. Anajiweka wazi ni kiongozi wa kuwatumikia wanyonge. Siasa huwa kwake zinaishia kwenye uchaguzi after anawatumikia watanzania bila kujali chama. Anapendwa na watu wa ccm,cuf, et al kwakuwa anaweka maslahi ya taifa mbele. Sinahaja kuandika sana ila zitto ni kuwa mzalendo.
Una ushahidi kuwa Slaa anabagua na anasimamia wanachadema tu?

Je una ushahidi wa hiyo chuki na kinyongo? Je una ushahidi wa wazi dhidi ya ubaguzi wa dini kabila na kanda?

Je Slaa alipokuwa mbunge bungeni, alimbagua nani? Una mifano gani ya kukosa uzalendo kwa Dr. Slaa na viongozi wengine wa CHADEMA?

Umeongelea siasa za chuki. Nadhani wanasiasa wanaoeneza chuki wanajulikana. Unasemaje juu ya aina ya siasa za Shonza, Mwampamba, Nape na Mwigulu? Nassari alipigwa na nani na kwa nini wakati wa uchaguzi Mdogo wa madiwani hivi karibuni? Hizo ndizo siasa za upendo? Kesi za kubambikiziwa ambazo zinazidi kushindwa mahakamani ndizo siasa za upendo?
 
Kutokana na mvutano unaoendelea ndani ya Chama cha demokrasia na maendeleo na Chadema imesababisha Chama hicho kusambaratika na kupoteza mvuto mkoani kigoma, sababu hasa inaonekana ni kutengwa kwa kijana wao zitto kabwe ndani ya chama hicho, na hata tetesi zinazoongelewa katika vijiwe vya siasa mkoani kigoma, aliye kuwa mgombea wa chama cha chadema Mwaka 2010 Ally mlee akakihama Chama muda wowote kuanzia sasa. Hali ni mbaya mkoani hapa, kila kijiwe kinaongelea ubaguzi ndani ya chama hicho.

wewe huna story nyingine tofauti na chadema? acha kujivua ufahamu we tahira
 
ccm mtaweweseka sana,na bado! cdm ipo ndani ya mioyo ya wazalendo wote wa nchi hii,CDM NI TAASISI KUBWA
 
kwa faida yako we gamba,cdm inapasua mawimbi kila kona ya tz,huku usukumani ndo balaa ule msemo wa NDUHU TABU tumeuzika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom