Under-cover
JF-Expert Member
- Nov 13, 2023
- 2,211
- 3,517
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema Viongozi wa Chama hicho akiwemo Makamu Mwenyekiti, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, na Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi wakiwa pamoja na wengine sita wamefikishwa katika Hospitali ya Mwananyamala kwa matibabu baada ya kupigwa na kutelekezwa na Polisi maeneo ya Mabwepande Jijini Dar es salaam huku Mtu mmoja kati yao akiripotiwa kufariki.
Majina ya waliotambulika hadi sasa ni Peter Alex Kilomba, Emmanuel Severin, Robert Mawege, Kanifa Musa, Emmanuel Modest Munihawa na Nasri Abdallah Saidi ambapo Chama hicho kimesema Mtu aliyefariki ameshindwa kutambuliwa kwa haraka kutokana na Polisi kutoushusha mwili wake Hospitalini hapo ambako CHADEMA walikuwa wakiusubiria.
“Hali ya Naibu Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa Fedha ni mbaya, na taratibu za kuwapeleka katika Hospitali ya juu kwa matibabu maalum zinaendelea, ukatili huu haustahili kupita kimya, tunaendelea kufuatilia kwa karibu hatua lazima zichukuliwe”
@AyoTV_ imelitafuta Jeshi la Polisi kuhusu taarifa za kifo hicho lakini juhudi hizo hazijazaa matunda, tunaendelea kufuatilia zaidi taarifa hizi. #MillardAyoU
PDATES
Majina ya waliotambulika hadi sasa ni Peter Alex Kilomba, Emmanuel Severin, Robert Mawege, Kanifa Musa, Emmanuel Modest Munihawa na Nasri Abdallah Saidi ambapo Chama hicho kimesema Mtu aliyefariki ameshindwa kutambuliwa kwa haraka kutokana na Polisi kutoushusha mwili wake Hospitalini hapo ambako CHADEMA walikuwa wakiusubiria.
“Hali ya Naibu Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa Fedha ni mbaya, na taratibu za kuwapeleka katika Hospitali ya juu kwa matibabu maalum zinaendelea, ukatili huu haustahili kupita kimya, tunaendelea kufuatilia kwa karibu hatua lazima zichukuliwe”
@AyoTV_ imelitafuta Jeshi la Polisi kuhusu taarifa za kifo hicho lakini juhudi hizo hazijazaa matunda, tunaendelea kufuatilia zaidi taarifa hizi. #MillardAyoU