hongeleni sana hasa wapiga kura ambao wametambua nuru na kuachana na giza.
Kwa wale mnaoendelea
kuaminishwa na propaganda za watawala kuwa CHADEMA kinachukiwa na watu,
basi fikirieni upya na jipangeni vizuri kwani moto wa chama unazidi
kuwaka na kumulika kila kona. Uchaguzi mdogo wa kiti cha mwenyekiti wa
mtaa wa Maisaka Kati Jimbo la Babati Mjini mkoa wa Manyara ni kama
ifuatavyo
CHADEMA - kura 247
CCM - kura 170
CUF - kura 2
Sasa nyie wafuasi wa Mwigulu mkisaidiwa na Job Ndungai kutaka
kuwaaminisha Watanzania kuwa CHADEMA haifai, kwa hilo mmeula wa chuya,
jipangeni upya kwani matendo yenu na maamuzi yenu mabaya ya kulinda
udharimu wenu Watanzania wa chini kabisa huku mitaani na vitongojini
wanaona na wataendelea kuona kama hamtajitambua kwa mbinu zenu chafu na
kwa mbinu zenu hizo kila uchaguzi, mtakimbia vituo kabla ya matokeo
kutangazwa