CHADEMA yaigaragaza CCM

CHADEMA yaigaragaza CCM

CDM Kilianza Kwa Nguvu Kilimanjaro polepole kikatoboa Arusha kwa kupitia Karatu....Muda si muda kikatoboa Mbulu....Kidogo kidogo kinatoboa Babati na Hanang....kwa mtu anayejua ramani ya Tanzania Hiyo ni Njia ya kuelekea Singida...Kwa hiyo wana Singida mkae mkao wa kukipokea....Uzuri wake chadema ishatanguliza Ngome moja Singida mashariki kwa Tundu Lisu.....Kwa upande Wa kanda ya Ziwa Chadema Ilianza Tarime....hiyooo ghafla ikatoboa Musoma Mjini ikatokezea Mwanza ( Ilemela,na nyamagana na Ukerewe), Ikaruka kwa wakati huo huo kwenda Shinyanga Kishapu, Maswa Na pande za Ngara huko. kanda ya Magharibu ilianza Kigoma....Pole pole ikarukia Mpanda na hivyo inaelekea tabora..... Kanda ya Nyanda za Juu kusini Ilianzia Mbeya..ikashamiri weee.... ikatoboa Iringa....Sasa inazidi kusambaa mpaka ifike Songea.....Kanda ya pwani Hasa dar imeingia ila bado kidogo nguvu kidogo zinahitajika ili iweze kusonga mbele mpaka pwani ya kusini...VIVA CDM.
hahahaaa! Maumivu ya kichwa huanza pooole pole, dawa ni kuchagua Chadema tu
 
Huu uchaguzi wa nini tena? Ina maana nchi hii chaguzi haziishi?

Nawasiwasi wanasiasa baada ya uchaguzi wanasema uchaguzi umeisha yatupasa kujenga taifa sasa chaguzi hazimaliziki sielewe taifa linajengeka au la?
 
cc vijana na wazelendo wa nchi hii lazima turudishe heshima ya taifa mikononi mwa wazawa sio wauza unga wanaongozwa na RIZ1, HONGERENI HOME BOYS TUKO PAMOJA SANA, CCM NI LAANA KWA VIZAZI VYETU
 
Pamoja na huo ushindi ambao CHADEMA kimeupata lakini mimi nadhani ushindi mkubwa uliopo sasa hivi hi ule ambapo vyama vyote vyeme uwakilishi makini bungeni ukiondoa vyama viwili vimeungana na kuwa na sauti moja. Hilo ni tishio, vyama hivi vya kimapinduzi vitatu viachane na siasa za itikadi na kushikamana kama kweli vinataka mabadiliko katika nchi hii mwaka 2015. Lazima viige mfano uliotumika Kenya katika kumpa ushindi Uhuru Kenyatta. Hakuna njia ya mkato katika hilo. Vuguvugu lianzie pale Jangwani katika mkutano wa leo na lisonge mbele na kukamata nchi nzima kabla ya uchaguzi.Kuna mikoa ambayo muungano huu uivalie njuga: Dodoma, Tabora, Tanga, Pwani, Morogoro, Njombe na Ruvuma.
 
Nawe nae, umeona maiska kwenye watu wasiozidi mia nne ndiko kwa kupima umaarufu wa chama? kuna watu milioni 44 sasa hao watu 400 ni peanut kuweza kupima umaarufu, na wala sio pa kujigamba ati umeigalagaza CCM. angalia uwiano uone, pole mdanganyika...
Kwa wale mnaoendelea kuaminishwa na propaganda za watawala kuwa CHADEMA kinachukiwa na watu, basi fikirieni upya na jipangeni vizuri kwani moto wa chama unazidi kuwaka na kumulika kila kona. Uchaguzi mdogo wa kiti cha mwenyekiti wa mtaa wa Maisaka Kati Jimbo la Babati Mjini mkoa wa Manyara ni kama ifuatavyo

CHADEMA - kura 247
CCM - kura 170
CUF - kura 2

Sasa nyie wafuasi wa Mwigulu mkisaidiwa na Job Ndungai kutaka kuwaaminisha Watanzania kuwa CHADEMA haifai, kwa hilo mmeula wa chuya, jipangeni upya kwani matendo yenu na maamuzi yenu mabaya ya kulinda udharimu wenu Watanzania wa chini kabisa huku mitaani na vitongojini wanaona na wataendelea kuona kama hamtajitambua kwa mbinu zenu chafu na kwa mbinu zenu hizo kila uchaguzi, mtakimbia vituo kabla ya matokeo kutangazwa
 
Haya wee ngoja tuone hiyo toboa toboa yako unayojigamba nayo. ila nafurahi umekiri kimeanzia kilimanjaro kwa hiyo ni cha wakilimanjaro. Mwaka 2014 kuna chaguzi za serikali za mitaa na 2015 kuna msema kweli....acha kimuhemuhe subiri ....utavuka daraja ukilifikia, ndipo tutaamini maneno yako... lakini nikuhakikishie tu kuwa hayo ni majigambo yasiyo na mashiko... angalia CDM kitakavyogaragazwa 2015
hahahaaa! Maumivu ya kichwa huanza pooole pole, dawa ni kuchagua Chadema tu
 
Mabadiliko yataletwa na sisi sote(mimi wewe na yule)je nawe umeshaiandaa familia yako kuleta mabadiliko?????VITENGE,KOFIA,UBWABWA na SKAFU chukueni ila kura kwa M4C
 
Chadema upande wa wing ya wanawake ni very weak ; kuna haja ya kuwakalisha chini hawa wabunge wanawake na kuwapangia kazi ya kufanya za mobilization ya wanawake nchini. Yule binti Wassira anaweza kufanya kazi hii vizuri akiwezeshwa!!! kumbukeni kuwa a significant proportion of the electorate ni wanawake na wenzenu magamba wanatarget hii kwa sana tu!!
 
pole na majukumu ndugu mpendwa.Ninajambo linanichanganya sana kiongozi na mtu mwenye umli mkubwa anaposem maneno kama haya,nanukuu[uwenyekiti wa SINGIDA kuanzia leo tarehe 03/11/2013 nakuaidi kuwa nitapamba mpaka mwisho wa tone la damu ya uhai wangu kuhakikisha demokrasia ya ndani ya chama hiki inahishimiwa na kwamba watanzania hawadanganywi tena mwisho wa kunukuu] swali akiwa mwenyekiti alishindwa je akiwa mwanacha wakawaida ataweza?huku sio kutapatapa kwa mfa maji.
 
Haya wee ngoja tuone hiyo toboa toboa yako unayojigamba nayo. ila nafurahi umekiri kimeanzia kilimanjaro kwa hiyo ni cha wakilimanjaro. Mwaka 2014 kuna chaguzi za serikali za mitaa na 2015 kuna msema kweli....acha kimuhemuhe subiri ....utavuka daraja ukilifikia, ndipo tutaamini maneno yako... lakini nikuhakikishie tu kuwa hayo ni majigambo yasiyo na mashiko... angalia CDM kitakavyogaragazwa 2015

Waswahili wanasema dalili ya mvua ni mawingi '' sasa wewe kalabagaho na ukabila wako!!! Mimi nimeeleza jinsi chama kilivyo anza mpaka leo Mwanzilishi wake ni Mtei mwejeji wa kilimanjaro ndio lakini huwezi kusema kwa kuwa muanzilishi wake ni mwenyeji wa kilimanjaro basi ni cha kilimanjaro!!! kama ni hivyo basi Hata CCM ni ya Musoma-Butiama. Kwa hiyo kama wewe si wa musoma basi ujue si chama chako.
 
Back
Top Bottom