CHADEMA watoana macho Bungeni

CHADEMA watoana macho Bungeni

naam, kwakweli hakuna marefu yasiyo na ncha na penye haki uongo hujiengua.methali na msemo huu umekuja baada kuuona mkanganyiko mkubwa wa kauli za chadema zinazotolewa na viongozi wao mahasimu .kauli zinazotolewa na viongozi hao zinapelekea kuyaengua mahubiri ya uongo yanaohubiriwa na viongozi hao wadhalimu.
Mikutano na maandamo haramu yanayoendeshwa na chama hicho chenye viongozi na wafuasi wenye tabia za kizulu za kupenda vita;imejikita katika kuhubiri mapambano dhidi ya rushwa,ufisadi maisha magumu na hivi karibuni kuna sakata la posho za wabunge huko dodoma.kujikanganya kwa chama hicho hasimu, kumedhihirika baada ya chama hicho kwenda tofauti na yale yanohubiriwa.
Bila shaka sote ni mashahidi kuwa chama kimekuwa kikihubiri mapambano dhidiya rushwa na ufisadi, wakati huohuo katibu mkuu wa chama hicho,padri slaa akikifanyia ufisadi chama chake kwa kukishiniza kumlipa ml.7.5 huku akipinga ml.7 zinzopokelewa na wabunge akinadi kuwa huko ni kuifilisi nchi
.evi jamani tuache kwanzwa suala ushabiki hapa,kupi kuifilisi nchi kati ya kupokea ml.7.5 na ml.7? Ambapo zote hizo ni fedha za wananchi wetu tunaojinadi kuwa tunawaonea huruma.hivyobasi, hapa ndipo chadema inapojikanganya katika kauli zake na hatimaye kutarajia anguko kubwa la chama hicho pale waloghiribiwa akili watakapouona unga wa rutuba.
Aidha mkanganyiko mwingine unajipambanua pale chama hicho kilipopanga mkakati wa kupinga posho za wabunge kikidai kuwa kupokea posho hizo ni sawa na kuwadumbukiza wananchi shimoni,huku mwenyekiti wa chama hicho,freeman mbowe, akiwa msitari wa mbele kusaini fomu za mahudhurio ambapo kwa pamoja hujumuishwa na kupewa posho wakati wa kusaini kama alivyo kaririwa spika wa bunge hilo lililoingiliwa na wana muziki wanaovesika watoapo hoja.huu ni mkanganyiko mwingine wa chama hicho ambapo viongozi wake wanajikanganya kwa yale wanayohubiri na yale wanayotenda na hii ni ishara ya kuanguka kwa chama hicho katika siku za usoni.maana wahenga walisema kuwa"jahazi linapopoteza mwelekeo kinachofuata ni kuyumba na kuzama,ndivyo ilvyo kwa chadema ya sasa.je nyie wanamagwanda hamuoni mkanganyiko huo? Unaobainisha unafiki wa viongo wenu.kwanini mmekuwa viziwi,vipofu na mabubu kiasi hicho. Tafakarini ndugu zangu.
Nimalizie kwa kusema kuwa "no one can make you better without your own efforts".
endelea kutumia tu makalio kufikiri kwani ndiyo yaliyokufikisha hapo ulipo.
Dr slaa alikataa mil 7kama mbunge(jimbo moja)
cdm inamlipa tsh 7.5kama katibu mkuu (tanzania mzima)
gari lake linatembea km * tano ya mbunge,anahudumia watz 40000000=mbunge mwenye watu wengi wa kuhudumia ni 200000=
hapo kwa akili yako ya uha.. Huoni tofauti.
Endelea kutumia hizo sehemu za haja kufikiri siku ukipata tumbo la kuharisha ndio mwisho wako.nyau we.
 
Wanaoishabikia cdm habari hii wataipotezea kwa kuwa inawataka wafunguke macho ilhali wao wamefumba na wapo usingizini. Mimi binafsi siamini mabadiliko kwa kutumia siasa ingekuwa ukiwa ccm hukai kwenye foleni barabarani basi ningeingia ccm leo na ingekuwa ukishabikia cdm hukatiwi umeme basi sasa hivi ningefanya juhudi za kuingia chamani. Ukweli utabaki uwe ccm, cdm, ltp hata jahazi asilia machungu ya mgao na foleni utayapata tu!

Hii habari ni vizuri ingepelekwa kwenye udaku. Haina source wala haitajihata hao wabunge watatu, kama kuna uhakika si wangetajwa majina yao?
 
CCM imetunyonya na maskini wengi wa nchi ndiyo waipendayo CCM,ila FREEDOM IS COMING.
 
source ya hii habari ni ipi vile? uhuru au mzalendo? mue mnaaandika source sio kuandika tu gazeti la kiswahili magazeti ya kiswahili yako mengi


BTW;craaaaaaap!
 
endelea kutumia tu makalio kufikiri kwani ndiyo yaliyokufikisha hapo ulipo.
Dr slaa alikataa mil 7kama mbunge(jimbo moja)
cdm inamlipa tsh 7.5kama katibu mkuu (tanzania mzima)
gari lake linatembea km * tano ya mbunge,anahudumia watz 40000000=mbunge mwenye watu wengi wa kuhudumia ni 200000=
hapo kwa akili yako ya uha.. Huoni tofauti.
Endelea kutumia hizo sehemu za haja kufikiri siku ukipata tumbo la kuharisha ndio mwisho wako.nyau we.
Haya kichana wa NAPE naona mpo bize IKULU mkiiba twiga na kusafirisha nchi ya nje,dhuruma imewajaa haya sasa endeleeni na wizi wenu dhidi ya maskini watanzania.
 
Demokrasia watu wote hawawezi kukubaliana na wabunge watatu tu kukataa hii inaonyesha kuwa majority kwa asilimia kubwa sana wanakubaliana and who cares chadema wangapi wanakubaliana na hii issue, Point ni kwamba wananchi kama mimi mlipa kodi ninaunga mkono jambo lolote ambalo litanusuru kodi yangu japo kidogo
 
Demokrasia watu wote hawawezi kukubaliana na wabunge watatu tu kukataa hii inaonyesha kuwa majority kwa asilimia kubwa sana wanakubaliana and who cares chadema wangapi wanakubaliana na hii issue, Point ni kwamba wananchi kama mimi mlipa kodi ninaunga mkono jambo lolote ambalo litanusuru kodi yangu japo kidogo
wamewezaje kumtaja Mnyika alafu wakashindwa kuwataja hao wabunge watatu. Wana maslahi gani na hao wabunge? Hii habari bado haijaniingia akilini.
 
wamewezaje kumtaja Mnyika alafu wakashindwa kuwataja hao wabunge watatu. Wana maslahi gani na hao wabunge? Hii habari bado haijaniingia akilini.
Mkuu hata kama ni kweli who cares..., tena wangewataja na hao watatu ili wananchi wao wawajue..., issue ni kwamba je Hili wazo la kukataa Posho ni wazo zuri au baya..., Jibu ni kwamba Ni Brilliant Idea..., na kati ya wabunge wote wa Chadema kama ni watatu tu wamekataa basi zipigwe kura na Kama majority watashinda basi tamko la Chadema litakuwa ni kwamba wamekataa Posho na sio kwamba baadhi wanakataa na baadhi wanakubali
 
Huili ndilo gazeti ambalo juzi lilichapa hotuba ya upinzani rasim?
 
Hiyo ndiyo demokrasia, sio lazima kila kitu wakubaliane wote, na hii siyo kwa upinzani tu bali hata kwa chama tawala hawatakiwi kila kitu kupinga kwa kuwa kimetoka upinzani au kuunga mkono kila kitu kwa kuwa kimetoka chama tawala, no, wote wanatakiwa kupinga au kukubali hoja baada ya kuichambua kama ina maslahi kwa taifa au la.
 
Kwahiyo unanishauri nini maamuma kama mie? Niingie na mie kwenye siasa kwa manufaa yangu au siyo?
Narudia kusema wanaokimbilia bungeni hawana msaada wowote na wananchi zaidi ya kujineemesha wenyewe. Hivi si tunawajua wafanyabiashara wakubwa wa upinzani? mbona wao hawathubutu kusema mishahara yao iende kusaidia wapiga kura majimboni mwao kwa kuwa wao wapo kuwatumikia wananchi na wanatosheka na wanachokipata kwenye biashara zao? si tuna mawakili maarufu wanaosimamia makesi makubwa na wanalipwa vizuri? mbona hawapo tayari ku sacrifice mishahara yao ili ilipie watoto mayatima kwenye majimbo yao ada za shule? mil 7 zinaweza kulipia watoto wangapi wa shule za kata?

Ifike wakati tutambue wanasiasa wapo kwenye siasa kwa manufaa yao na kutafuta protections na sio kwa ajili ya kukutumikia wewe! wachache wana dhamira hizo lakini kipato ni masikini na hawana biashara yoyote ndio maana wanapigania hizo posho.
 
Hawa wabunge ambao hawajali kasi ya umaskini kwa watanzania walio wengi,imejionyesha wazi kwamba wao wamekwenda bungeni kwa ajili ya mafao na posho kuliko kujali zaidi wananchi ambao wanateseka na ukata,ugumu wa maisha kiasi cha kushindwa hata kulipia gharama za hospitali.sasa hawa nadhani wananchi wa sehemu wanazotoka wawaone na wachukue hatua kutokana na utashi na uchaji wao.hawa ni wanafiki na watayumbisha upinzani,hapo walipofika ni kwa nguvu za wananchi leo hii wana wasaliti?
 

Attachments

  • gal_guinness_eyeballs[1].jpg
    gal_guinness_eyeballs[1].jpg
    40.3 KB · Views: 33
Hawa wabunge ambao hawajali kasi ya umaskini kwa watanzania walio wengi,imejionyesha wazi kwamba wao wamekwenda bungeni kwa ajili ya mafao na posho kuliko kujali zaidi wananchi ambao wanateseka na ukata,ugumu wa maisha kiasi cha kushindwa hata kulipia gharama za hospitali.sasa hawa nadhani wananchi wa sehemu wanazotoka wawaone na wachukue hatua kutokana na utashi na uchaji wao.hawa ni wanafiki na watayumbisha upinzani,hapo walipofika ni kwa nguvu za wananchi leo hii wana wasaliti?

Niko na wafanyakazi hapa wanalalamika kweli kuhusu Zitto kutaka kuziondoa posho kwa watumishi wa serikali. Ni wakali mno>

Posho zinatugawa.
 
What Chadema show is Democracy, they don't need to agree on everything; Chadema is not a rubber stamp Organization like CCM

They go with the wind even if deep inside they are not happy... so approve bogus and unwanted programs and projects to feed their bosses stomach...
 
In a democracy the poor will have more power than the rich, because there are more of them, and the will of the majority is supreme.

But CCM Democracy... while it lasts for more than 50yrs now is more bloody than either [aristocracy or monarchy]. Remember, democracy never lasts long. It soon wastes, exhausts, and murders itself like now they are rubber stamps....
 
Narudia kusema wanaokimbilia bungeni hawana msaada wowote na wananchi zaidi ya kujineemesha wenyewe. Hivi si tunawajua wafanyabiashara wakubwa wa upinzani? mbona wao hawathubutu kusema mishahara yao iende kusaidia wapiga kura majimboni mwao kwa kuwa wao wapo kuwatumikia wananchi na wanatosheka na wanachokipata kwenye biashara zao? si tuna mawakili maarufu wanaosimamia makesi makubwa na wanalipwa vizuri? mbona hawapo tayari ku sacrifice mishahara yao ili ilipie watoto mayatima kwenye majimbo yao ada za shule? mil 7 zinaweza kulipia watoto wangapi wa shule za kata?

Ifike wakati tutambue wanasiasa wapo kwenye siasa kwa manufaa yao na kutafuta protections na sio kwa ajili ya kukutumikia wewe! wachache wana dhamira hizo lakini kipato ni masikini na hawana biashara yoyote ndio maana wanapigania hizo posho.

inaonekana unachanganya.....maji na oil!!! posho si mshahara na matumizi ya mhashara ni siri ya mtu hayupo anayeweza kutoa comment kwa mshahara wa mtu!
 
Narudia kusema wanaokimbilia bungeni hawana msaada wowote na wananchi zaidi ya kujineemesha wenyewe. Hivi si tunawajua wafanyabiashara wakubwa wa upinzani? mbona wao hawathubutu kusema mishahara yao iende kusaidia wapiga kura majimboni mwao kwa kuwa wao wapo kuwatumikia wananchi na wanatosheka na wanachokipata kwenye biashara zao? si tuna mawakili maarufu wanaosimamia makesi makubwa na wanalipwa vizuri? mbona hawapo tayari ku sacrifice mishahara yao ili ilipie watoto mayatima kwenye majimbo yao ada za shule? mil 7 zinaweza kulipia watoto wangapi wa shule za kata?

Ifike wakati tutambue wanasiasa wapo kwenye siasa kwa manufaa yao na kutafuta protections na sio kwa ajili ya kukutumikia wewe! wachache wana dhamira hizo lakini kipato ni masikini na hawana biashara yoyote ndio maana wanapigania hizo posho.
rudia tena......
 
Source is not vivid, pls bring issue un biased, not all in here, we are politicians, we are just here to open up our minds wide!

Personnal interest is a personal failure!

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeingia kwenye mgogoro baada ya baadhi ya wabunge kupandwa na hasira dhidi ya wenzao wanaoendesha kampeni ya kutaka posho za vikao kwa wabunge ziondolewe.Mkwaruzano huo iliibuka ndani ya kikao cha wabunge wa Kambi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe.

Kikao hicho kiliitishwa na kambi hiyyo kwa lengo la kuweka msimamo wa kupinga posho za vikao kwa wabunge, lakini kikageuka uwanja wa vita uliozusha vurumai kubwa kiasi cha kushindwa kufikia muafaka.

Baada ya kikao hicho kufunguliwa, John Mnyika (Ubungo-Chadema) aliwasilisha hoja hiyo ya kutaka wabunge wa upinzani kuweka msimamo wa pamoja wa kupinga posho hizo ili mkakati huo ulioanzia kwenye Bunge hilo la Bajeti, uweze kufanikiwa.

Akifikiri ataungwa mkono, Mnyika aliwataka wabunge kuonyesha moyo huo wa kishujaa kwa kutosaini kitabu cha mahudhurio bungeni, lakini wawepo ndani ya vikao.

Kauli hiyo ya Mnyika ilikuwa sawa na kumwaga petroli kwenye moto unaowaka ambapo wabunge watatu wa Chadema (majina tunayahifadhi kwa sasa) walikuja juu na kupinga vikali hoja hiyo.

Upinzani huo mkali uliotolewa na wabunge hao ulidhihirisha kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyesema kuwa ingawa baadhi ya wabunge wa chama hicho wanajionyesha kimbelembele kusisitiza mpango huo, wengine wa chama hicho pia wanaumia kimoyomoyo, lakini hawasemi.

Suala la kukataa posho bungeni lilianzishwa na Zitto Kabwe (Kigoma Kaskazini-Chadema) akisema zinaenda kinyume na mpango wa Taifa wa kupambana na umasikini kwa kuondoa posho zisizo na tija.

Zitto akionekana kuwa na ushupavu mkubwa ilifikia mahali akaamua kutosaini mahudhurio Bungeni ili jina lake lisiorodheshwe miongoni mwa watakaolipwa licha ya Spika, Anne Makinda kutishia kuwa kitendo hicho kinaweza kumfukuzisha bungeni.

Mkakati wa Mnyika ulikuwa ni wabunge wote wa upinzani kuwa na mshikamano katika hilo jambo ambalo sasa limeonekena kuwa ni nyongo kiasi cha wengine kutaka kuwararua wenzao wakisema ni msimamo usio na maana.

Source:
Gazeti la habari za kiswahili la kila siku Tanzania, linaongoza

Jamaa wanaweza wakaandamana fasta kupingana wao kwa wao Teh teh
 
Back
Top Bottom