Speaker
JF-Expert Member
- Aug 12, 2010
- 6,324
- 2,238
VIONGOZI na wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wameomba wanancvhi kutowanyanyapaa na kuwabagua watu wenye ulemavu nchini na badala yake wajenge utamaduni wa kuwasaidia kila pale inapowezekana.
Ombi hilo limetolewa jana na mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe alipokuwa akikabidhi msaada kwa mlemavu wa miguu, Bi. Edna Katinga (20) mkazi wa Kijiji cha Kitendaguro Manispaa ya Bukoba ambaye pamoja na mwanawe, Joanes George (5) ni walemavu wa miguu na hutembea kwa kutambaa chini.
Bw. Mbowe alimkabidhi Bi. Katinga sh. 6,393,000 ambazo zilichangwa na viongozi na wanachama wa CHADEMA wa mkoani Kagera katika hafla fupi ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na uongozi wa CHADEMA mkoani humo juzi usiku.
Katika kiasi hicho, Bw. Mbowe binafsi alichanga sh. 2,000,000 taslimu ambapo mbunge wa viti maalumu kwa tiketi ya CHADEMA kutoka mkoa wa Morogoro, Bi. Regia Mtema alijitolea kumchangia mlemavu huyo shilingi 100,000 kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia hiyo juzi.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa alijitolea kumpeleka mtoto Joanes katika hospitali maalumu ya watu wenye ulemavu wa viungo ya CCRBT iliyoko Dar es Salaam ambako atafanyiwa uchunguzi wa kitalaamu ili kuangalia uwezekano wa kumwezesha kutembea kawaida.
Nenda hapa:http://majira-hall.blogspot.com/2011/03/chadema-wamchangia-mlemavu-mil-6.html
Ombi hilo limetolewa jana na mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe alipokuwa akikabidhi msaada kwa mlemavu wa miguu, Bi. Edna Katinga (20) mkazi wa Kijiji cha Kitendaguro Manispaa ya Bukoba ambaye pamoja na mwanawe, Joanes George (5) ni walemavu wa miguu na hutembea kwa kutambaa chini.
Bw. Mbowe alimkabidhi Bi. Katinga sh. 6,393,000 ambazo zilichangwa na viongozi na wanachama wa CHADEMA wa mkoani Kagera katika hafla fupi ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na uongozi wa CHADEMA mkoani humo juzi usiku.
Katika kiasi hicho, Bw. Mbowe binafsi alichanga sh. 2,000,000 taslimu ambapo mbunge wa viti maalumu kwa tiketi ya CHADEMA kutoka mkoa wa Morogoro, Bi. Regia Mtema alijitolea kumchangia mlemavu huyo shilingi 100,000 kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia hiyo juzi.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa alijitolea kumpeleka mtoto Joanes katika hospitali maalumu ya watu wenye ulemavu wa viungo ya CCRBT iliyoko Dar es Salaam ambako atafanyiwa uchunguzi wa kitalaamu ili kuangalia uwezekano wa kumwezesha kutembea kawaida.
Nenda hapa:http://majira-hall.blogspot.com/2011/03/chadema-wamchangia-mlemavu-mil-6.html