Mratibu wa kampeni wa cuf Julius Mtatiro ameishtumu vikali chadema kwamba kiimeenda Igunga kwa lengo la kugawa kura za Cuf.Mtatiro amesema chadema wanajua wazi hawana nguvu yoyote Igunga lakini wameamua kwenda huko ili ccm ishinde.Mtatiro amemueleza mwandishi wa habari hizi kwamba chadema wasijidanganye kuambulia hata nafasi ya pili bali watakuwa namba 3 nyuma ya ccm na cuf.Mtatiro amesema cuf wamejipanga kuwaeleza wananchi wa igunga ukweli wote kuhusu chadema ili waamue wenyewe.