CHADEMA waongeza mbunge Arusha mjini

CHADEMA waongeza mbunge Arusha mjini

Meya feki Arusha abwaga manyanga:

Nasikia meya feki wa Arusha amejiuzulu..........ni kweli?
 
Sio kama mimi,yani hadi machozi yamenitoka????Pumbavu na waongo na mafisadi na damu za marehemu ziwalilie hadi mseme ukweli kama ni kweli mlitudanganya wananchi na leo mnafanya kile kile!!!:Cry::Cry::Cry:

Kawaida ukifanya kosa ibilisi hua anakuficha for sometimes only, lakini lazima na sharti awaonyeshe watu nini ulichofanya tena kwa kupitia mhusikamwenyewe.
 
Hivi huu ujinga wa viti maalumu utaisha lini jamani?.
Huu ndio mwanzo wa fujo zote hizi, ewe katiba mpya njoo uondoe hiki kivuli tata
 
wampeleke na rose kamili ili wajihakikishie ushindi kabisa
 
chadema wakurupukaji na wanaakili za komoni(sehemu ya mbele ya kichwa)

hata kwemye suala la katiba mpya jazba zinawaongoza kuliko busara ati lipelekwe bungeni, hadi walipoambiwa kuwa likienda bungeni litakuwa limetawaliwa na chama tawala kwa kuwa wao ni wengi na kamwe cdm hawana uwezo wa kushinda bungeni ndio wameamka.

kwa hio kuuwa watu wote kwa jambo ambalo walishaambiwa kuwa taratibu zilikuwa wazi, na sasa wameanza kufanya kile kile ambacho walikipinga, hawa mavutu

Duuh mtu wa Pwani maoni ya Mnyika ndio kauli ya CHADEMA? kweli nyie CCM na hao CDM mtakuja malizana kwa vijembe , kejeli na mikogo yenu.
 
1. Mwanasheria wa Serikali ametoa ufafanuzi kwamba Mbunge wa Viti Maalumu anaweza kuingia kwenye Halmashauri kama atakavyokuwa amepangiwa na chama chake. Ndio maana Lucy Owenya na Grace Kiwelu wakaruhusiwa Hai. Kabla hao walikataliwa na madiwani wa CCM kwa kigezo sio wakazi. Wakati Hai wakizuiliwa Mary Chitanda akaruhusiwa kupiga kura Arusha. Ndipo mvurugano ukaanza.

Baada ya maandamano ya Arusha, Ijumaa tar 7. 01. 2011 ikatolewa taarifa kwamba Lucy na Grace wanaweza kupiga kura Hai.

2. Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa Arusha zinasema kwamba akidi kwa mkutano wa kwanza wa kawaida wa halmashauri ni 2/3. Mkurugenzi anadai kwamba tar 17.12.2010 kikao kiliahirishwa baada ya CDM kugomea Chitanda kupiga kura. Saa 12 jioni aliandika barua kwa madai mkutano huo utaendelea tar 18.12.2011 saa nne asubuhi. CDM hawakuingia ukumbini (sio kwamba walitoka). Mkurugenzi anadai kwamba akidi ilikamilika kwa sababu tar 18 mkutano ulikuwa ni muendelezo wa mkutano wa tar 17 siku ambayo CDM walisaini kuwepo. Hapo ndipo mvutano upo!

3. Anna Komu hajawahi kuapa sehemu nyingine yoyote. Kama Chitanda anaweza kuwa mjumbe basi hata Komu anastahili kuwa mjumbe kama Mwanasheria wa Serikali alivyotafsiri.

Kilichopo Arusha ni jitihada za kucontrol Jiji kama njia ya kuzuia upinzani kukua zaidi au kukuza upinzani zaidi. Ambaye hayuko kwenye siasa anaweza asilione au asilielewe hilo.

For CDM to grow it needs a strong influence in cities. Kuwa na Mbunge haitoshi. Maamuzi yote yanayowagusa wananchi moja kwa moja yanafanywa na Halmashauri. Meya au Mwenyekiti ni nafasi muhimu sana kwa ufanikishaji wa shughuli za maendeleo katika Wilaya au Manispaa.

Wito wangu kwa wanaJF ni vizuri tukaelekeza nguvu katika udiwani ili tuwe na Halmashauri zenye ufanisi. Nawahakikishia ni Halmashauri chache sana zina wajumbe wenye uelewa mkubwa wa mambo. Kuna Halmashauri zina wajumbe ambao uelewa wao sio mkubwa as a result kuna ufujaji wa fedha wa hali ya juu.

Mkurugenzi wa Halmashauri akiungana na Meya au Mwenyekiti wa Halmashauri fedha inaliwa, tenda zinatolewa kwa udanganyifu, miradi inahujumiwa nk.
 
chadema wakurupukaji na wanaakili za komoni(sehemu ya mbele ya kichwa)

hata kwemye suala la katiba mpya jazba zinawaongoza kuliko busara ati lipelekwe bungeni, hadi walipoambiwa kuwa likienda bungeni litakuwa limetawaliwa na chama tawala kwa kuwa wao ni wengi na kamwe cdm hawana uwezo wa kushinda bungeni ndio wameamka.

kwa hio kuuwa watu wote kwa jambo ambalo walishaambiwa kuwa taratibu zilikuwa wazi, na sasa wameanza kufanya kile kile ambacho walikipinga, hawa mavutu
aaah mtu wapwani umenichekesha kwelikweli,hapo mwisho ulipowaita mavutu,kweli we wapwani tena pwani yenyewe lazma uvukemaji ndio ufike,unajua umewaacha kwenye mataa hawajui vutu wala mavutu hawa,ila kwasisi tunaojua hakika msg sent.
 
thanks msandoalberto kwa maelezo sanifu. Ni kwa sababu natumia mobile phone ningekutwangia thanks
 
Baada ya maandamano ya Arusha, Ijumaa tar 7. 01. 2011 ikatolewa taarifa kwamba Lucy na Grace wanaweza kupiga kura Hai.

2. Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa Arusha zinasema kwamba akidi kwa mkutano wa kwanza wa kawaida wa halmashauri ni 2/3. Mkurugenzi anadai kwamba tar 17.12.2010 kikao kiliahirishwa baada ya CDM kugomea Chitanda kupiga kura. Saa 12 jioni aliandika barua kwa madai mkutano huo utaendelea tar 18.12.2011 saa nne asubuhi. CDM hawakuingia ukumbini (sio kwamba walitoka). Mkurugenzi anadai kwamba akidi ilikamilika kwa sababu tar 18 mkutano ulikuwa ni muendelezo wa mkutano wa tar 17 siku ambayo CDM walisaini kuwepo. Hapo ndipo mvutano upo!
Sasa nimeelewa mchezo mzima wa CCM ulipo, kumbe baada ya maandamano ndiyo wakaruhusu Lucy na Grace wa Hai kupiga kura kuhalalisha ushiriki wa Chitanda Arusha.

Na kumbe mkurugenzi hakatai kanuni ya 2/3 ila anatumia kolumu ya mkutano ulioahirishwa wa jana yake kama kolumu ya mkutano wa uchaguzi, sasa kama ni hivyo mbona wanadai Chadema walisusia wakati huohuo wanatumia majina yao. Yaani huu ni wizi wa demokrasia wa mchana kweupe.
 
1. Mwanasheria wa Serikali ametoa ufafanuzi kwamba Mbunge wa Viti Maalumu anaweza kuingia kwenye Halmashauri kama atakavyokuwa amepangiwa na chama chake. Ndio maana Lucy Owenya na Grace Kiwelu wakaruhusiwa Hai. Kabla hao walikataliwa na madiwani wa CCM kwa kigezo sio wakazi. Wakati Hai wakizuiliwa Mary Chitanda akaruhusiwa kupiga kura Arusha. Ndipo mvurugano ukaanza.

Baada ya maandamano ya Arusha, Ijumaa tar 7. 01. 2011 ikatolewa taarifa kwamba Lucy na Grace wanaweza kupiga kura Hai.

2. Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa Arusha zinasema kwamba akidi kwa mkutano wa kwanza wa kawaida wa halmashauri ni 2/3. Mkurugenzi anadai kwamba tar 17.12.2010 kikao kiliahirishwa baada ya CDM kugomea Chitanda kupiga kura. Saa 12 jioni aliandika barua kwa madai mkutano huo utaendelea tar 18.12.2011 saa nne asubuhi. CDM hawakuingia ukumbini (sio kwamba walitoka). Mkurugenzi anadai kwamba akidi ilikamilika kwa sababu tar 18 mkutano ulikuwa ni muendelezo wa mkutano wa tar 17 siku ambayo CDM walisaini kuwepo. Hapo ndipo mvutano upo!

3. Anna Komu hajawahi kuapa sehemu nyingine yoyote. Kama Chitanda anaweza kuwa mjumbe basi hata Komu anastahili kuwa mjumbe kama Mwanasheria wa Serikali alivyotafsiri.

Kilichopo Arusha ni jitihada za kucontrol Jiji kama njia ya kuzuia upinzani kukua zaidi au kukuza upinzani zaidi. Ambaye hayuko kwenye siasa anaweza asilione au asilielewe hilo.

For CDM to grow it needs a strong influence in cities. Kuwa na Mbunge haitoshi. Maamuzi yote yanayowagusa wananchi moja kwa moja yanafanywa na Halmashauri. Meya au Mwenyekiti ni nafasi muhimu sana kwa ufanikishaji wa shughuli za maendeleo katika Wilaya au Manispaa.

Wito wangu kwa wanaJF ni vizuri tukaelekeza nguvu katika udiwani ili tuwe na Halmashauri zenye ufanisi. Nawahakikishia ni Halmashauri chache sana zina wajumbe wenye uelewa mkubwa wa mambo. Kuna Halmashauri zina wajumbe ambao uelewa wao sio mkubwa as a result kuna ufujaji wa fedha wa hali ya juu.

Mkurugenzi wa Halmashauri akiungana na Meya au Mwenyekiti wa Halmashauri fedha inaliwa, tenda zinatolewa kwa udanganyifu, miradi inahujumiwa nk.
Hii ungeianzishia thread yake maana iko wazi na inajieleza kabisa.
 
Hii ungeianzishia thread yake maana iko wazi na inajieleza kabisa.

Nakubaliana nawe, ila kwa sababu wengi wanachangia kwenye hii thread nikaona vyema nipost humu humu. Kilichotokea Arusha kimeelezewa sana kwa kutumia u-CCM na u-CDM kiasi kwamba kwa wale ambao hawana upande ukweli umepotoshwa.
 
thanks msandoalberto kwa maelezo sanifu. Ni kwa sababu natumia mobile phone ningekutwangia thanks

Kesho asbh katwange kamanda si unajua wanazuoni humu ndani huwa wanacheki namba ya posts na thanks......inapokuwa posts 1,250 thanks 20 watu wanatilia mashaka post content!
 
cdm imempeleka mbunge wa viti maalum anna maulida komu kwenye halmashauri ya jiji la arusha Mama huyo mkongwe na mkomavu kisiasa aliripoti ijumaa kwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo. Soc. tanzania daima My take sasa cdm wanakuwa na uhakika wa ushindi endapo uchaguzi wa meya utarudiwa
kwani maulida komu ni mbunge wa wapi? Mbona unachanganya habari? Ulishawahi kusikia mbunge anahamishwa? Chanzo chako siyo credible!
 
Naomba kuuliza, hivi CCM ilichokifanya na Chatanda, kinatofauti gani na Mbowe alichokifanya kule Hai na hili la kuongeza mbunge mmoja Arusha?.

Kama tofauti ni kura moja, jee CCM nao wakiamua kuhamishia wabunge wake watano wa viti maalum kuhudumu Arusha itakuwaje?.

Pasco!
Ndugu yangu kwenye hii dunia kama hutatumia ubongo wako vizuri utakumbana na watu ambao kupandikiza chuki ,kupindisha ukweli,kuugeuza ukweli kuwa uongo na uongo kuwa ukweli,kupandikiza fitina kwa gharama ya maisha ya wengine,hivi mpaka leo hujajiuliza kuna tuhuma nyingi ambazo chadema wamesema wanaushahidi wa kutosha lkn hakuna hata moja ambayo wameshaifikisha sehemu husika ili sheria ichukue mkondo wake.Mchungaji Mtikila kuna sehemu anapotoka na kuna sehemu amekuwa na ushahidi na tumeona mara zote pale anapokuwa na ushahidi amekuwa akiibuka kidedea.Wacha tuwaruhusu watu wachache wajenge fitina ndani ya hii nchi bila ya kujiandaa kuongoza nchi kwa usalama tutafikia mahala tutaona majuto ni mjukuu.Angalia Tunisia waliona Rais ndiyo tatizo na ukweli inawezekana ndiyo huo lkn njia zilizotumika kumuondoa na kuondoka kuaicha nchi ilivyo hivi sasa kweli zimewasaidia nini watunisia waliowengi.Hivi huyu ambaye wote walikuwa wanamuona adui ameathirika vipi na matukio yanayoendelea hivi sasa Nchini Tunisia.
 
Back
Top Bottom