Umeeleza vizuri hasa kuhusu wakati kuwa bado ni mapema na pia janga la corona. Tusiharakishe.Mimi ni mdau ambaye naunga mkono sana mabadiliko ya katiba lakini mpangilio wa sasa ambao unaongozwa na Chadema sijaupenda na hautasaidia mafanikio haya kwasababu zifuatazo
1. Raisi mpya Samia hawezi kukubali kufanya katiba wakati mapema kwa kuzingatia ameingia majuzi tu na kachukuwa madaraka kwenye wakati mgumu kwa mtangulizi wake kupoteza maisha. Hii kwa nchi nyingine ambazo hazina usalama wangeweka " state of emergency" ingawa hatukufika huko Raisi anahitaji muda kwanza kupata nguvu na kuungwa mkono kabla ya kudandia swala nyeti na lenye kugawanya watu kama katiba mpya.
2. Corona ni ugojwa ni sio kitu cha kisiasa. Huu ni ugojwa na kuna Watanzania wengi wamepoteza ndugu wengi kuanzia mwaka 2019. Tuliulize ni kitu gani kimetokea kusababisha haya? jibu ni Corona. Corona imeondoa watu wengine ambao hata familia hazijui wamekufa kwa nini. Kuna watu wawili ambao nina mfano mmoja ni rafiki yangu wa Ilboru ambaye alikuwa anamiliki mgodi kule Mererani kwenye wimbi la pili alikufa ghafla wakidai alikosa pumzi na kafariki wa kisukari. Familia ikadai apimwe Corona maana alikuwa na miaka 44 tu na sukari yake haikuwa mbaya hivyo! walivyopima zaidi ya mara moja wakakuta ana Corona. Juzi pia mzazi wa rafiki yangu naye sukari imepanda akafariki Musoma baada ya familia kulazimisha apimwe wamekuta naye alikufa kwa Corona ingawa kabla ya kupima walisema sukari imepanda. Kwa ufupi huu sio wakati mzuri wa kufanya makusanyiko yeyote yasiyo ya lazima. Kwa msingi huu naunga mkono Raisi samia kwamba huu sio wakati mzuri wa kuanzisha mikutano ambayo inaweza kuongeza na sio kuzuia Corona.
3. Mkutano na Raisi: Chadema wanakosea kufanya huu mkutano mkubwa kuliko ulivyo. Chadema kukuza huu mkutano na Raisi Samia unamfanya Raisi aone kwamba anatakiwa kujiandaa sana badala ya Chadema kuuchukulia mkutano wa kawaida wa kujua. Chadema kwa faida za nchi na kisiasa wanatakiwa kuweka urafiki na Raisi na sio kufanya mkutano kama unaenda kukutana na watekaji wako. Mama anapenda sana umoja, yeye pekee ndiye alienda kumwangalia Lissu Kenya makusudi bila hata kumwambia kiongozi wake Magu. Hata safari ya Kenya inawezekana alilazimisha kwenda Kenya ili akamuone Lissu bila kuwaambia nia yake Chama. Haya yote kafanya ili Chadema wajue na yeye binafsi aweke rekodi kwamba yeye kama Samia hajahusika kwenye njama zozote za kumuumiza Lissu. Cha ajabu chadema pamoja na kuwa na mtu ambaye ataweza kufanya nao kazi wanataka wampime kijinga kwa kuweka maandamano ambayo yatawasaidia wale ndani ya CCM wanaotafuta sababu za kuwapiga upinzani kwa faida zao. Chadema ni lazima wajue kule CCM kuna wengi walikuwa wananufaika na biashara za upinzani ilikwa ni pamoja na kutumia pesa za kununua wapinzani nje ya utaratibu, kuunda vikundi vya ajabu, kuomba pesa za teknologia za kurekodi watu..... hizo zote ni biashara za mabilioni ambazo Chadema kwa kuleta mikutano ya ajabu itawapa sababu hawa walaji kwenda kwenye chama na kuanza tena kuchukua pesa baada ya kumuogopesha Raisi