Nguli wa siasa nchini na kada mashuhuri wa CCM Balozi Job Lusinde amevunja ukimya na kusema kuna kila dalili kwamba CDM inakaribia kuchaguliwa na wananchi kuongoza dola ya Tanzania.
Mkongwe huyo wa siasa amesema CDM imejipanga vyema na ina uongozi madhubuti unaopanga vyema harakati zake za kisiasa nchini.Balozi Lusinde amesema amekuwa akifurahishwa jinsi CDM inavyotangaza sera zake kwa wananchi kwa kutumia maandamano na mikutano ya hadhara.Amesema CCM inapaswa kukubali kwamba lolote linaweza kutokea katika uchaguzi mkuu wa 2015.
Kuhusu chama chake cha CCM Balozi huyo ameeleza kusikitishwa na hali ya uhasama ilivyofikia ndani ya chama hicho kufikia wanachama kutaka kuuana kwa bastola kwa uroho wa madaraka akirejea tukio lililotokea hivi karibuni huko Nzega kati ya Hamis Kigwangala na Hussein Bashe.Amesema kiuhalisia sasa CCM imekosa mwelekeo.
Source:Tanzania Daima Uk 6
Mkongwe huyo wa siasa amesema CDM imejipanga vyema na ina uongozi madhubuti unaopanga vyema harakati zake za kisiasa nchini.Balozi Lusinde amesema amekuwa akifurahishwa jinsi CDM inavyotangaza sera zake kwa wananchi kwa kutumia maandamano na mikutano ya hadhara.Amesema CCM inapaswa kukubali kwamba lolote linaweza kutokea katika uchaguzi mkuu wa 2015.
Kuhusu chama chake cha CCM Balozi huyo ameeleza kusikitishwa na hali ya uhasama ilivyofikia ndani ya chama hicho kufikia wanachama kutaka kuuana kwa bastola kwa uroho wa madaraka akirejea tukio lililotokea hivi karibuni huko Nzega kati ya Hamis Kigwangala na Hussein Bashe.Amesema kiuhalisia sasa CCM imekosa mwelekeo.
Source:Tanzania Daima Uk 6