Wadau, kama mnavyofahamu ni kwamba chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinafanya uchaguzi wake wa ndani ambapo kwa sasa upo ngazi ya wilaya. Tanzania ina Wilaya zaidi ya 100 ambazo ndizo zinazotumiwa na CHADEMA kama mamlaka yake ya kichaguzi.
Ijapokuwa uchaguzi huo unafanyika nchi nzima, Jana Tarehe 27 Julai ilikuwa ni uchaguzi wa kuwapata viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Arusha Mjini. Huwezi kuamini, Mzee wa Tengeru, Edwin Mtei na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe walikuwa ni miongoni mwa wageni walioshuhudia uchaguzi huo. Watu wengi walikuwa wanajiuliza, Arusha kunani mpaka ikawasukuma mtu na mkwewe kushiriki uchaguzi huo? Kama ni uwajibikaji wa mwenyekiti huyo, mbona hajaenda Kasulu au Nkasi au Kibaha au Rufiji? Arusha kunani? Wakati tunajadili haya, tukumbuke kuwa kwa sasa Jiji la Arusha linaongoza kwa miripuko ya mabomu ambayo chanzo chake bado hakijabainishwa.