Political Conspiracy, Political sabotage, Political denial, Political clandestine, and the likes....
...Kutoka duru za usalama wa vyama vya siasa nchini ...zinaeleza kuwa kile chama cha siasa kinachunda kambi lasmi bungeni kimefanikiwa kukilaghai chama Tawala kwa kutengeneza mgogoro wa uongo wa Naibu Katibu ... wa chama hicho ("Zi..o) dhidi ya baadhi ya viongozi waandamizi wa chama hicho. Mgogoro huo wa uongo umelenga kuwanasa viongozi waandamizi wa chama cha Tawala kwa kumuamini "Zi..o kuwa anaweza kutumika kukihujumu chama chake machoni pa watanzania kama ataamua kuanzisha migogoro ndani ya chama chake ama kujitoa kwenye chama hicho na kujiunga na chama kingine cha upinzani au chama cha tawala. Viongozi hao wa tawala wako tayari kufadhili hiyo mipango "fake" ya kambi lasmi maana hawataki kujishughulisha na kuwatatulia kero raia. Kwa taarifa zilizopo wameisha anza kujifadhili ili waondolewe kwenye madaraka bila kujua.
...Kwa kujua ushawishi alionao "Zi..o kwa baadhi ya vijana na wazee kwenye siasa za nchi..."Zi..o katika kutekeleza majukumu yake aliyopewa na chama chake alifanikiwa kuunda kikundi kilichooneka cha Uasi ndani ya Chama (MASALLIA/wassalitii). Rejea threads nyingi za hapa jamvini zinazoelezea masuala haya.
...Kikundi hiki kilifanikiwa kuitia msukosuko 'fake' Chama cha kambi lasmi hasa jumuiya yake ya vijana. Msukosuko Ule ulilenga kuwawawezesha wale waliotuhumiwa kuwa wasaliti (Jully na Msherra) wafanikiwe kupokelewa vyema na tawala mara baada ya kutimuliwa. Baadaye iligundulika wasaliti hawa kabla ya kutimuliwa walishaanza kupokea 'mlungula' kutoka kwa tawala kupitia viongozi wa wake. Pia katika mlungula huo wasaliti walikatwa asilimia 80 ya kiasi walichopangiwa kupewa na Tawala. Na aliyefanikiwa kufaidi kiasi hicho cha makato hajajulikana bado... Mpango huo ulifanikwa kwani walipokelewa vyema na viongozi wa juu wa tawala.
Mgogoro huu 'fake' ulisaidia kuisahaulisha Tawala kutekeleza kazi zake kama chama tawala kinachoongoza serikali kwani kula kuku kwa mrija kuliongezeka mara dufu kwa viongozi wake waandamizi...
Hivi karibuni...chama hiki matata...kimegundua tawala wanaanza kustuka na kutambua majukumu yao....kwa raia.
Sasa ili kuwasahaulisha tena tawala majukumu yao...wameibuka na mbinu mpya ya kutumia karata yao ya turufu "Zi..o kwa kumuagiza azindue zengwe la kuhoji uhalali wa matumizi ya ....katika vyama....
Kwa kifupi kwenye kambi lasmi hakuna mgogoro...na hao waliotimuliwa hivi karibuni au hata hapo zamani (walioamia vyama vingine) bado bado wanafanya kazi za kambi lasmi.
Mytake
Watu wako kazini, ukiendelea kulala utakuta mwana si wako tena.