Chadema wamepata wapi haki ya kutengeneza CD mauaji ya Mwangosi (R.I.P) na kuiuza

:embarassed2:
A%20S%20embarassed.gif
 
kweli pesa hizi zitatupeleka pabaya.

naona sasa unachanganyikiwa.

Kama kweli unataka majibu ungemfuata mjane wa mwangossi ili akupe majibu yake,kisha uende ofisi za chadema wakupatie majibu,halafu uje hapa ukiwa kamili.

Sasa unapokurupuka huko na kujakutuuliza maswali sisi tunashindwa kukuelewa,na pia tunapata taabu kufahamu uwezo wako wa kufikiri.
 
Chadema mmewashirikisha familia ya Mwangosi (R.I.P) kwenye kutengeza hiyo CD Chadema wametengeza Copy 30,000 na wanauza CD moja Sh 5000 hizo pesa wanazoingiza kutokana na hayo mauzo kiasi gani kinakwenda kwenye familia ya Mwangosi kumsaidia mjane wa marehemu.

Wewe kijana punguza kuchonga domo. HAKUNA IYO MAMBO!
 
Waliosema kufa ni kufaana waliona mbali!
Kifo cha Mwangosi kimebadili maisha ya watu, kwa mf. Wengine wamefahamika na wengine wamepata dili ya pesa kama hao waliokuwa kwenye kamati/tume ya kuchunguza mauaji hayo.
 
Ingekua wewe ungetaka kiasi gan ili umsahau alie kutoka?waulize polisccm maana wao walijianda kufanya tukio hilo hawakukurupuka kama wewe naamini walikua na wapigapicha wao?cdm tuknmae hawatuwez police sisiemu mmoja raia 1600 watawezaa?itafahamika tu
 
Mkuu Ritz heshima mbeeele kwanza japo ni mtani wangu wa kule Magambani,

Kwa mujibu wa swali uliloliuliza hapo juu bana hebu tufahamishe japo kidogo ya kwamba siku hizi haki kama hiyo huuzwa katika duka gani siku hizi mkuu?? Bwana Ritz, hapa katikati kidogo naona kam vile umepwaya sana kwenye aina ya maswali unayoyauliza.

Hakika, nielewavyo mimi, CHADEMA kama chama kina haki zote za kuelimisha umma juu yaa jambo lolote lenye maslahi kwao kwa kutumia msaada wa njia mbalimbali halali za kuwawezesha kufikisha vema zaidi ujumbe wowote watakaokua nao wakati wowote na mahali popote pale ilmradi taarifa wanazozitumia ni sahihi za zenye kuthibitika.

Kwa mfano, niliposoma pale ulipokua ukihoji juu ya uwezekano wa Mhe Lema kwepo katika jimbo la Simanjiro naa vile vile kuripotiwa kuongoza mkutano mwingine wa kukata na shoka pale Daraja Mbili mjini Arusha kidogo uliniacha hoi na mbavu kuniuma sana kwa kicheko huku nikijiuliza kwamba huyu rafiki yangu hapa JF na Mtani wa kisiasa kule Magambani kapatwa na nini tena au kaibiwa ufunguo wa kufungulia ukurasa wake mtandaoni?

Kimsingi, nakubali kwamba siku zote umekua ukionyesha viwango vya juu sana ya CRITICAL THINKING CAPACITIES hivyo kunifanya wakati mwingine niwe nikivutiwa na baadhi ya hoja zako japo KIMTAZAMO wewe na mimi ni kama bingu na ardhi - wewe ukivutiwa zaidi na hii CCM nyakua nyakua ya siku hizi na mimi nikitetea chama chochote chenye msimamo kama wa CCM ya enzi za Mwalimu Nyerere (ambacho kwa sasa ni CHADEMA pekee).

Hadi hapo mkuu sasa hebu nielimishe kidogo; kulikoni, kumekupata nini tena hadi kuhoji utitiri wa maswali chini ya kiwango hivi??

Mkuu, huyo yawezekana alikuwa anatungiwa hoja za kuzileta humu jamvini. Watungaji mahiri walipovua magamba, kabaki mpweke na hana hoja nzito ndiyo maana maswali na hoja zake siku hizi zinastaajabisha.
 
hiyo Dvd ni mali ya nani? kwa akili yako, hivi ukiwa unaact movie halafu akapita Senga nae akachukuliwa kwenye huo mkanda ndo atakuwa mmiliki wa hiyo DVD, kumbuka tukio lilikuwa ufunguzi wa tawi mwangosi kama mwandishi wa habari akawepo baadaye askari wasiokuwa na huruma wakafanya walio fanya je mwangosi atakuwa ndo mmilik wa hiyo dvd, japo kwa mapenzi yao Chadema waweza kufanya kitu kwa ndugu wa marehem kupitia hilo.
 
Wanabodi.

Imepita mwezi na siku kadhaa toka yafanyike mauji ya Mwandisi wa Kituo cha Televisheni cha Chanel Ten, Daudi Mwangosi, baada ya kuuliwa na polisi kwa kuripuliwa na bomu.

Chama Cha Demokrasia na Maendeo Chadema wamezindua CD ya mauaji ya Davidi Mwangosi (R.I.P) na kuisambaza mitaani na kuanza kuiuza. Chadema wamepata wapi haki ya kutengeneza hiyo CD na kuiingiza sokoni kwa mauzo.

Familia ya Mwangosi (R.I.P) pamoja na Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania wanapata mgao wowote wa mauzo ya hiyo CD kama hawapati jambo ili kisheria linakuaje.

Watoto wa Marehemu ambao ni wadogo kiumri wanajua chochote kuhusu mauzo ya CD ya baba yao kipenzi.

Mods, wakuu JF na Ritz

Kwanza samahanini kwa kuchelewa kuingia hapa na kutoa ufafanuzi na kuweka rekodi sahihi. Asubuhi tulikuwa msibani, kiongozi wetu mmoja wa kata pale Ubungo amefariki dunia. Hivyo Tulikwenda pale asubuhi na John Mnyika, kisha tukaanza safari ya kwenda Dodoma, kwenye uzinduzi wa kampeni za udiwani Kata ya Msalato.

Coming back to the point, Idara ya Habari ilipata taarifa mapema juu ya uwepo wa CD inayohusu tukio la Nyololo la kuuwawa kwa Mwandishi wa Habari, Daudi Mwangosi. Mara moja ilichukua hatua ya kumtafuta mhusika na kumwambia aache mara moja. Si sahihi na hairuhusiwi kukihusisha chama kwenye hicho alichokuwa akikifanya.

Labda hakuelewa mantiki na sababu alizoelezwa. Jana tulipopata habari kutoka Arusha kuwa CD za namna hiyo zinauzwa eneo la mkutano na zina nembo ya CHADEMA, ilibidi sasa kuchukua hatua zaidi jana hiyo hiyo.

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John Mnyika aliagiza kusimamishwa kwa uuzwaji huo mara moja, mhusika atoe taarifa ya jumla ya CD alizozalisha mpaka sasa, ameuza CD ngapi mpaka sasa na kila moja inauzwa kwa kiwango gani. Kisha akaagiza zaidi kuwa fedha zilizopatikana mpaka sasa, zote ziwasilishwe kwa familia ya marehemu Mwangosi, lakini wakati huo huo uuzwaji na uzalishaji uwe umeshasimamishwa mara moja mpaka maelekezo mengine yatakapotolewa.

Usahihi ni kwamba, CHADEMA haihusiki na uzalishaji na uuzwaji wa CD hizo, ingawa kwa makosa makubwa, aliyeamua kufanya hivyo, ameweka nembo ya chama na anauzia kwenye maeneo ya mikusanyiko ya shughuli za CHADEMA. Ndiyo maana tumechukua hatua za haraka sana kuzuia suala hilo.

Tunatumaini maagizo hayo ya John, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi yatatekelezwa mara moja tangu jana pale pale Arusha.

Asateni.
 
Ritz unapokomaa kukanusha hapakuwa na ufunguzi wa tawi Nyololo,unataka kusema kilichopelekea umati wa watu na Polisi akiwemo Kamuhanda kusafiri mpaka pale Km 120 kutoka Iringa mjini ilikuwa ni nini? Kuhusu CD ambayo siamini ipo maana hujaambatanisha vielelezo sidhani kama lengo ni kuuawa kwa Mwangosi bali mwendelezo wa shughuli za ufunguzi matawi
 
Kama mwangosi aliuwawa siku ya mkutano wa cdm basi hiyo cd ni halali kuwa na matukio yote ikiwemo mauaji ya Mwangosi, kamanda wa polisi alivyo uchuna pamoja na kushuhudia mauaji! Kwa hiyo ndugu Ritz pumzika kwanza!
 
Wewe inakuhusu nini? Mbona hujawahi kuhoji Mkapa na Kikwete kusaini mikataba ya kuchimba madini bila kuwashirikisha Watanzania?

Chadema mmewashirikisha familia ya Mwangosi (R.I.P) kwenye kutengeza hiyo CD Chadema wametengeza Copy 30,000 na wanauza CD moja Sh 5000 hizo pesa wanazoingiza kutokana na hayo mauzo kiasi gani kinakwenda kwenye familia ya Mwangosi kumsaidia mjane wa marehemu.
 
Hakuna sehemu niliotetea Jeshi la Polisi kwa unyama waliofanya, mie naulizia mapato ya CD ya mauji ya Mwangosi mjane anapata kiasi gani?

anapata 100%
Haya kakojoe ukalale...
 
No evidence no right to speak!
Tuonyeshe hiyo cd kwanza ndo tuijadili. Upumbavu sometime unaiondolea jukwaa hili sifa stahiki.

Ninachokijua na ninachoamini ni kuwa kuna cd inayoonyesha matukio ya mikutano ya M4C, na mojawapo ni mauaji ya Arusha, Morogoro na Iringa ya marehemu Daudi Mwangosi.

Ritz sikuamini kama una kichwa chepesi namna hii
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Tumaini Makene,
Nimeelewa vizuri bandiko lako. Kosa lililopo hapa ni huyo muuzaji kuuza hizo CD zikiwa na nembo ya Chadema lakini kama zisingekuwa na nembo yetu sidhani kama ni kosa. Kwanza itambulike kwamba anapoouza hizo CD hana tofauti na muuza magazeti ambae anauza habari in terms of written words. Tofauti hapa ni yeye habari yake inaiuza in form of video picture.

Labda kosa lake kama atakuwa nalo ni kama biashara yake ameisajiri na ana vibali husika.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),
tumbiri@jamiiforums.com
 
Zomba nilivyokuwa nakudefine cvyo kabisa! Ni mtu mwenye busara zako! Ushahidi ni post ya kuonewa kwa nduguzako na polisi
 
Back
Top Bottom