Wanabodi.
Imepita mwezi na siku kadhaa toka yafanyike mauji ya Mwandisi wa Kituo cha Televisheni cha Chanel Ten, Daudi Mwangosi, baada ya kuuliwa na polisi kwa kuripuliwa na bomu.
Chama Cha Demokrasia na Maendeo Chadema wamezindua CD ya mauaji ya Davidi Mwangosi (R.I.P) na kuisambaza mitaani na kuanza kuiuza. Chadema wamepata wapi haki ya kutengeneza hiyo CD na kuiingiza sokoni kwa mauzo.
Familia ya Mwangosi (R.I.P) pamoja na Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania wanapata mgao wowote wa mauzo ya hiyo CD kama hawapati jambo ili kisheria linakuaje.
Watoto wa Marehemu ambao ni wadogo kiumri wanajua chochote kuhusu mauzo ya CD ya baba yao kipenzi.
Nanyie mmepata wapi haki ya kuua raia kila mkutano wa chadema
Mwangozi alikuwa raia au "kamanda"?
Wanabodi.
Imepita mwezi na siku kadhaa toka yafanyike mauji ya Mwandisi wa Kituo cha Televisheni cha Chanel Ten, Daudi Mwangosi, baada ya kuuliwa na polisi kwa kuripuliwa na bomu.
Chama Cha Demokrasia na Maendeo Chadema wamezindua CD ya mauaji ya Davidi Mwangosi (R.I.P) na kuisambaza mitaani na kuanza kuiuza. Chadema wamepata wapi haki ya kutengeneza hiyo CD na kuiingiza sokoni kwa mauzo.
Familia ya Mwangosi (R.I.P) pamoja na Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania wanapata mgao wowote wa mauzo ya hiyo CD kama hawapati jambo ili kisheria linakuaje.
Watoto wa Marehemu ambao ni wadogo kiumri wanajua chochote kuhusu mauzo ya CD ya baba yao kipenzi.
Mods, wakuu JF na Ritz
Kwanza samahanini kwa kuchelewa kuingia hapa na kutoa ufafanuzi na kuweka rekodi sahihi. Asubuhi tulikuwa msibani, kiongozi wetu mmoja wa kata pale Ubungo amefariki dunia. Hivyo Tulikwenda pale asubuhi na John Mnyika, kisha tukaanza safari ya kwenda Dodoma, kwenye uzinduzi wa kampeni za udiwani Kata ya Msalato.
Coming back to the point, Idara ya Habari ilipata taarifa mapema juu ya uwepo wa CD inayohusu tukio la Nyololo la kuuwawa kwa Mwandishi wa Habari, Daudi Mwangosi. Mara moja ilichukua hatua ya kumtafuta mhusika na kumwambia aache mara moja. Si sahihi na hairuhusiwi kukihusisha chama kwenye hicho alichokuwa akikifanya.
Labda hakuelewa mantiki na sababu alizoelezwa. Jana tulipopata habari kutoka Arusha kuwa CD za namna hiyo zinauzwa eneo la mkutano na zina nembo ya CHADEMA, ilibidi sasa kuchukua hatua zaidi jana hiyo hiyo.
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John Mnyika aliagiza kusimamishwa kwa uuzwaji huo mara moja, mhusika atoe taarifa ya jumla ya CD alizozalisha mpaka sasa, ameuza CD ngapi mpaka sasa na kila moja inauzwa kwa kiwango gani. Kisha akaagiza zaidi kuwa fedha zilizopatikana mpaka sasa, zote ziwasilishwe kwa familia ya marehemu Mwangosi, lakini wakati huo huo uuzwaji na uzalishaji uwe umeshasimamishwa mara moja mpaka maelekezo mengine yatakapotolewa.
Usahihi ni kwamba, CHADEMA haihusiki na uzalishaji na uuzwaji wa CD hizo, ingawa kwa makosa makubwa, aliyeamua kufanya hivyo, ameweka nembo ya chama na anauzia kwenye maeneo ya mikusanyiko ya shughuli za CHADEMA. Ndiyo maana tumechukua hatua za haraka sana kuzuia suala hilo.
Tunatumaini maagizo hayo ya John, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi yatatekelezwa mara moja tangu jana pale pale Arusha.
Asateni.
Hawa jamaa ni hatari sana, wako tayari kuuwa kwa pesa. Kifo washageuza bingo!
Wamepata haki kutoka familia ya Mwangosi. Wewe unawasemea kama nani, na inakuumia nn acha hizo mbona uulizi ni kiasi gani kinaliwa katika serikali ya ccMafisi
Mkuu unabisha au hutaki kuamini?
Mwongo mkubwa wewe mtumwa wa mafisadi usiye na haya kwa ndg zako kulala njaa kwa ingali mafisadi mandumilakuwili wachache na ndio umeamua kuwa mtumwa wao kuwasafisha humu jamvini bila hata huruma na adabu hata!
Jaribu kubadilika pamoja na kundi lako lile la kipuuzi isiyotumia kichwa kufikiri na kukubali kutumia masaburi!
Waheeeed sana wewe Ritz!
Eti CDM wamepata wapi CD ya marehemu Mwangosi! Achaga unafiki mtumwa wewe!
TAFAKARI KABLA YA KUTUA HUMU JAMVINI MTUMWA WEWE,NA LEO NI MWISHO WA WEEKEND NENDA PALE LUMUMBA STREET UKAPOKEE CHAKO!
Mwongo mkubwa wewe mtumwa wa mafisadi usiye na haya kwa ndg zako kulala njaa kwa ingali mafisadi mandumilakuwili wachache na ndio umeamua kuwa mtumwa wao kuwasafisha humu jamvini bila hata huruma na adabu hata!
Jaribu kubadilika pamoja na kundi lako lile la kipuuzi isiyotumia kichwa kufikiri na kukubali kutumia masaburi!
Waheeeed sana wewe Ritz!
Eti CDM wamepata wapi CD ya marehemu Mwangosi! Achaga unafiki mtumwa wewe!
TAFAKARI KABLA YA KUTUA HUMU JAMVINI MTUMWA WEWE,NA LEO NI MWISHO WA WEEKEND NENDA PALE LUMUMBA STREET UKAPOKEE CHAKO!
Mkuu unabisha au hutaki kuamini?
Mkuu chama,
Kama kweli Chadema hawahusiki na hizo CD kwa nini wasitoe ripoti polisi kwa kuchafuliwa jina la chama kuhusishwa na hizo CD za mauaji ya Mwangosi (R.I.P) mbaya zaidi cover za CD hizo kuna nembo ya Chadema.
Mtu wangu kama kunajambo naliunga mkono basi ni kuuza kanda hii ambayo kimsingi ni ufunguzi wa Tawi la chama Kijijini Nyororo, Chama kinapanua shughuri zake za kisiasa mpaka vijijini tukio ambalo Polisi walionesha jinsi wanavyotumika kuzorotesha au kufifisha demokrasia kwa kutumia nguvu kupita kiasi kwa watu wasio na silaha wala hatia mpaka kutoa roho ya Mwandishi Mwangosi! Unataka iwe siri kumlinda nani!!