CHADEMA waja na mpango mkakati ‘kupindua meza’

Mama Amon

JF-Expert Member
Mar 30, 2018
2,021
2,477
1674457365804.png

Freean Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa

BAADA ya zuio lisilokuwa la kikatiba wala kisheria, la mikutano ya hadhara kwa muda mrefu, sasa ni wazi kwamba, Chadema wamezindua mikutano yao ya hadhara wakiwa na lengo kubwa la kueleza wapi serikali “imekwama” kukomboa wananchi na janga la ufukara.

Mtangulizi wa Rais Samia Suluhu Hassan, John Pombe Magufuli, miaka saba iliyopita, alitoa kauli kuzuia mikutano ya hadhara, ambayo ni injini ya kuendesha na kukuza vyama vya siasa.

Rais Magufuli, bila kupima umuhimu wa kidemokrasia kuendesha nchi, alitumia ubabe wa kiutawala kueleza tu; “sasa hakuna mikutano ya hadhara ya vyama,” na ikawa sheria.

Hatua hiyo ilifuatiwa na madhila mengi kwa wanasiasa, waandishi wa habari, wafanyabiashara na watu wa kada nyingine, ikiwamo kuumizwa, kutekwa, kuteswa, kupotezwa na wengine kuminywa uhai wao.

Rais Samia kwa mabadiliko ya sasa ya kuruhusu kuwepo kwa mikutano ya hadhara na kuacha demokrasia ipumue na kuendelea kukua, unatoa mwanya wa serikali kusemwa na kukosolewa ili ijirekebishe mahali itakapokuwa imekosea.

Tayari, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kupitia kwa mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, kimepongeza hatua ya Rais Samia kuvunja zuio hilo linaloelezwa na wengi kuwa “haramu.”

Ni kwa msingi huo, Chadema wanakuja na nadharia zenye kubeba hatua kadhaa za kuinyoshea serikali kidole kwa utendaji wake.

Nadharia hizo zinaweza kuwekwa katika hatua tatu za mabadiliko ya kifikra, kisera, kisheria, na kitaasisi. Mosi, ni kutengeneza “tasnifu asilia -” (thesis) kwa kuhakikisha kwamba, hali ya mfumo uliopo kwa sasa, yaani mtazamo rasmi unaokubalika kwa sasa, unachambuliwa vizuri.

Pili, ni kutengeneza “tasnifu kinzani -” (antithesis) kwa kuhakikisha kwamba, matatizo yaliyomo katika mfumo wa sasa yanabainishwa sawasawa, ili tasnifu asilia iweze kukosolewa kwa usahihi na kwa uhakika, kwa kutumia ushahidi.

Na tatu, ni kutengeneza “tasnifu hitimisho -” (synthesis) kwa kuhakikisha kwamba, kambi zinazopingana zinafikia mwafaka, kwa kuzalisha fikra, sera au sheria inayokubalika kwa kambi zote, kwa sababu ya ushahidi uliowekwa mezani na kushuhudiwa na kambi zote, wakati wa mchakati wa majadiliano.

Katika hatua ya tatu, mrejesho kutokana na tasnifu kinzani hufanywa sehemu ya tasnifu asilia ili kuzalisha tasnifu hitimisho, inayokubalika kwa kambi zote.

Kisha, mduara wa tasnifu asilia, tasnifu kinzani na tasnifu hitimisho hujirudiarudia hadi kuunda mchakato wenye muundo wa “spairo” (spiral), kila duara la spairo likiwapeleka wahusika karibu zaidi na ukweli.

Hotuba zilizotolewa na viongozi wa Chadema, Januari 21, 2023, katika uwanja wa Furahisha, Jiji Mwanza, zinathibitisha kwamba, nadharia ya udayalektika kuhusu mabadiliko ya kijamii imeanza kutekelezwa na Chadema.

Katika kuweka uzito kwenye nadharia hizo tatu, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alilihutubia taifa jioni ya siku hiyo alisema yafuatayo;

“Serikali ya awamu ya tano ililigeuza taifa hili kuwa taifa la maumivu, mateso na misiba…

…Nikiri kwamba sisi sote tulioumizwa na mateso ya viongozi wetu, wana Chadema wameumizwa, wana CCM wameumizwa na wapo wana CCM walionufaika na mateso hayo…

… Taifa letu halipaswi kuwa taifa la kuumuza kiongozi yoyote, mwanachama yoyote, mfuasi yeyote wa chama chochote. Taifa letu linapaswa kuwa taifa la watu walioungana, wanaoshikamana, wanaosimama katika misingi ya demokrasia.

… Taifa hili limepitia mengi, taifa hili linapaswa kuwa na watu ambao wameungana, wameshikamana na kusimama katika misingi ya demokrasia, utawala wa sheria na haki kwa wote...

… Ninaposimama nikiwa mwenyekiti na kiongozi wa Chadema kudai haki, sisimami kwa ajili wa wana Chadema, bali nasimama kama kiongozi wa kudai haki za watu wote…

… Naomba nilisisitize sana, tusijenge tabia ya kuwachukia wanachama wa CCM kwa sababu ya madhila tuliyopitia. Wajibu wetu ni kuwashurutisha kwa hoja ili watambue, ndani ya Chadema kuna haki, ustawi na fursa ya kumsaidia kila mmoja na akawa raia mwema kwa nchi yetu...

… Tunahitaji kukaa kama nchi kutambua kwamba nchi hii haiwezi kuendelea kwa kuigawanya vipande vipande. Eti kuna na kipande cha Chadema, kuna kipande cha CCM, kuna kipande cha UDP…

… Chadema tuna kauli kuu inayosema ‘no hate, no fear’ (hakuna chuki, hakuna woga). Natangaza wazi kuwa chama hiki siyo chama cha chuki. Hatuwezi kujenga utaifa wa nchi hii kwa kujenga chuki…

… Dhana ya ‘no hate’ (hakuna chuki), iambatane na dhana kwamba hatumuogopi mtu…

… Nampongeza Rais Samia Suluhu kwa kukubali maridhiano. Wapo watu wanatamani maridhiano yasifanikiwe. Wao wanafaidi maisha nje ya maridhiano. Samia alikubali nia ya maridhiano kinyume na matakwa ya chama chake...

… Kwa pamoja tuna wajibu wa kujadiliana yapi ni mambo ya msingi ya kuyafanya ili kulipeleka taifa letu katika furaha, ustawi na haki kwa kila mtu…

… Katika miaka yangu 30 ya kupigania taifa hili, natamani nitakapoacha uongozi, niache taifa langu, nchi yangu, watoto wangu, wajukuu wangu wakiwa wanapendana, wanaoshikamana na kuitafuta kesho yetu pamoja.”

Na kwa maneno ya Mbowe, kuna kila dalili kwamba siasa za “kunyukana na kukingiana vifua” huenda zinaondoka Chadema na kuja na staili nyingine ya mapambano ya siasa kwa lengo la kuongoza Tanzania.

Hata hivyo, wapo baadhi ya wahafidhina ndani ya Chadema kwa hatua hii wanaona kama mwenyekiti wao, Mbowe amewasaliti na kutaja kwamba “huenda amelamba asali.”

Hatua ambayo Mbowe ameikemea na kulaani wanaosambaza uongo kwamba amepokea rushwa kutoka kwa wapinzani wao ili “kumlainisha.”

Katika hotuba hii, Mbowe ameongelea mambo matatu.

Mosi, Mbowe anaongelea tasnifu asilia, isemayo kwamba, kuna wafuasi wa chama tawala ambao, tangu serikali ya awamu ya tano, wamekuwa wafuasi na watetezi wa mfumo wa kisiasa unaokuza na kuhami maslahi ya wachache na kutelekeza maslahi ya wengi.

Huu ni mfumo uliokweza dhuluma na kutweza haki, mfumo wenye kutukuza chuki dhidi ya wapinzani badala ya kufanya urafiki nao.

Ni mfumo ulioongozwa na imani hasi kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, siyo njia halali ya kusukuma gurudumu la maendeleo.

Ni mfumo uliotukuza ubaguzi wa kikanda na kiitikadi na kusahau kuimarisha umoja wa kitaifa bila kujali itikadi, ukabila na ukanda.

Pili, Mbowe anaongelea tasnifu kinzani, isemayo yafuatayo; kwamba, kwa mujibu wa ndoto ya waasisi wa nchi yetu, Tanzania ni taifa linapaswa kuongozwa na serikali inayopigania maslahi ya watu wote, badala ya kuhangaikia maslahi ya watu wachache.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kukumbatia mifumo inayokweza haki na Chadema na mpango mkakati kutweza dhuluma, inayotukuza urafiki badala ya kujenga uadui.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kukumbatia mifumo kuongozwa na kanuni kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, ndiyo njia pekee ya kusukuma gurudumu la maendeleo.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kupinga ubaguzi wa kikanda na kiitikadi na kuimarisha umoja wa kitaifa bila kujali itikadi, ukabila wala ukanda.

Na tatu, Mbowe anaongelea tasnifu hitimisho, isemayo yafuatayo; kwamba, kazi ya kujenga nchi, katika mazingira ya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, inapaswa kufanyika kwa mujibu wa kanuni kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, ndio njia pekee ya kuleta haki ya kweli, amani ya kweli, uhuru wa kweli na maendeleo ya kweli nchini Tanzania.

Tasnifu hitimisha inayoongelelwa na Mbowe, inaakisi hoja ya Profesa Euphrase Kezilahabi, kama ilivyotolewa mwaka 1978, kupitia tamthiliya yake iitwayo “Kaptura la Marx.”

Tamthiliya ilishutumu ukiritimba na matumizi mabaya ya madaraka katika mfumo wa Ujamaa uliouanzishwa enzi za Mwalimu Julius Nyerere, aliyekuwa Rais wa Tanzania.

Kwa mfano, ndani ya kitabu “Kaptula la Marx (1999),” kwenye ukurasa wa 20, maelezo ya mhusika Korchnoi Brown kwa Raisi Kapera na mawaziri wake kuhusu njia ya kufikia nchi ya usawa yanasomeka hivi;

“Mtakwenda. Halafu mtapinda, mtapinda tena, halafu tena mtapinda, mwishowe mtapindapinda hadi mtakapofika mabonde yenye matope. Mtapita katikati ya matope.

“Halafu milima, halafu misitu yenye miiba hadi mtakapofika jangwani. Kutoka jangwani mtaingia tena bondeni chini kwa chini hadi baharini. Hakuna mitumbwi wala ngalawa.

“Mtaogelea, ingawa kuna papa wengi. Mkishavuka mtafika nchi iitwayo Svoboda. Kabla ya kuondoka katika nchi hii itawabidi kupambana na majitu yanayofanana na mimi. Mkitoka hapo mtafika kwenye njia nyembamba.

“Hawa (mawaziri) hawatapita hawa. Njia hiyo itawafikisha katika nchi iitwayo Fraternite. Kutoka Fraternite mtafika Usawa. Ulizeni tu watu watawaonyesha.

“Mkifika Usawa mtawakuta Waswahili wenzenu wameketi nje ya Ikulu ndogo ya Ravensto.”


Neno “Korchnoi” ni jina la Kirusi, “Brown” jina la Kiingereza.

Majina haya yanarejea njia ya Tanzania ya Nyerere kati ya “mashariki” ya kikomunisti na “magharibi” ya kibeberu.

Neno “Fraternite” ni msamiati wa Kifaransa wenye kumaanisha “undugu.”

Ni moja ya tunu tatu zinazoyatambulisha mapinduzi ya Kifaransa, yaani “uhuru, usawa na undugu.”

Jina la nchi ya “Svoboda” linatokana na msamiati wa Kirusi wenye kumaanisha “uhuru.”

Ni jina la nchi linalorejea wito wa mapinduzi kama yaliyofanyika Ufaransa.

Hii ni sehemu ya ushahidi kwamba, tamthiliya ya “Kaptula la Marx” ilihimiza matumizi ya mbinu za kidayalektika kuhusu mabadiliko ya kijamii, kama zilivyoasisiwa na Mjerumani Georg Hegel (1770-1831), na kisha kunadiwa na Mjerumani mwenzake Karl Marx (1818- 1883).

Chadema wamechagua mbinu mwafaka, ambayo kwa sasa hutumika hata mahakamani, kulingana na mwongozo wa Profesa Stephen Toulmin (1922-2009), wa Uingereza.

Katika kitabu chake, “The Uses of Argument (1958),” Profesa Toulmin anasema kuwa hoja kamilifu, haipaswi kuwa na sehemu tatu kama alivyofundisha Aristotle, yaani hoja yenye “dokezo kuu, dokezo dogo na hitimisho.”

Bali, hoja iliyokamilika inapaswa kuwa na sehemu angalau sita, yaani, “tasnifu, ushahidi, waranti ya ushahidi, msingi wa waranti, tasnifu kinzani, majibu ya tasnifu kinzani, na majumuisho.”

Yaani, “thesis, ground, warrant, backing, objection, rebuttal, and synthesis.”

Hivyo, Chadema wamechagua barabara iliyo mwafaka. Walizindua tena rasmi mikutano ya kisiasa baada ya kuzuiwa miaka saba iliyopita kwa njia ya tamko la aliyekuwa Rais wa Tanzania John Magufuli.

Lakini, mnamo Januari 3, 2023, Rais Samia Suluhu Hassan, aliamua kuondoa zuio hilo kutokana na maridhiano ya kitaifa yaliyoasisiwa na yeye pamoja na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

Chanzo: Gazeti la Pambazuko Toleo namba 028.
 
Yani utakuta wewe unayewaita watu malofa hauna mbele wala nyuma, life limekuchapa, familia huna, kichwani hakuna kitu.

Sijui ni kwanini ustaharabu, kujadili jambo kwa staha na kufanya mijadala yenye kujenga inawashinda baadhi ya watu kama huyu
 
View attachment 2492314
Freean Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa

BAADA ya zuio lisilokuwa la kikatiba wala kisheria, la mikutano ya hadhara kwa muda mrefu, sasa ni wazi kwamba, Chadema wamezindua mikutano yao ya hadhara wakiwa na lengo kubwa la kueleza wapi serikali “imekwama” kukomboa wananchi na janga la ufukara.

Mtangulizi wa Rais Samia Suluhu Hassan, John Pombe Magufuli, miaka saba iliyopita, alitoa kauli kuzuia mikutano ya hadhara, ambayo ni injini ya kuendesha na kukuza vyama vya siasa.

Rais Magufuli, bila kupima umuhimu wa kidemokrasia kuendesha nchi, alitumia ubabe wa kiutawala kueleza tu; “sasa hakuna mikutano ya hadhara ya vyama,” na ikawa sheria.

Hatua hiyo ilifuatiwa na madhila mengi kwa wanasiasa, waandishi wa habari, wafanyabiashara na watu wa kada nyingine, ikiwamo kuumizwa, kutekwa, kuteswa, kupotezwa na wengine kuminywa uhai wao.

Rais Samia kwa mabadiliko ya sasa ya kuruhusu kuwepo kwa mikutano ya hadhara na kuacha demokrasia ipumue na kuendelea kukua, unatoa mwanya wa serikali kusemwa na kukosolewa ili ijirekebishe mahali itakapokuwa imekosea.

Tayari, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kupitia kwa mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, kimepongeza hatua ya Rais Samia kuvunja zuio hilo linaloelezwa na wengi kuwa “haramu.”

Ni kwa msingi huo, Chadema wanakuja na nadharia zenye kubeba hatua kadhaa za kuinyoshea serikali kidole kwa utendaji wake.

Nadharia hizo zinaweza kuwekwa katika hatua tatu za mabadiliko ya kifikra, kisera, kisheria, na kitaasisi. Mosi, ni kutengeneza “tasnifu asilia -” (thesis) kwa kuhakikisha kwamba, hali ya mfumo uliopo kwa sasa, yaani mtazamo rasmi unaokubalika kwa sasa, unachambuliwa vizuri.

Pili, ni kutengeneza “tasnifu kinzani -” (antithesis) kwa kuhakikisha kwamba, matatizo yaliyomo katika mfumo wa sasa yanabainishwa sawasawa, ili tasnifu asilia iweze kukosolewa kwa usahihi na kwa uhakika, kwa kutumia ushahidi.

Na tatu, ni kutengeneza “tasnifu hitimisho -” (synthesis) kwa kuhakikisha kwamba, kambi zinazopingana zinafikia mwafaka, kwa kuzalisha fikra, sera au sheria inayokubalika kwa kambi zote, kwa sababu ya ushahidi uliowekwa mezani na kushuhudiwa na kambi zote, wakati wa mchakati wa majadiliano.

Katika hatua ya tatu, mrejesho kutokana na tasnifu kinzani hufanywa sehemu ya tasnifu asilia ili kuzalisha tasnifu hitimisho, inayokubalika kwa kambi zote.

Kisha, mduara wa tasnifu asilia, tasnifu kinzani na tasnifu hitimisho hujirudiarudia hadi kuunda mchakato wenye muundo wa “spairo” (spiral), kila duara la spairo likiwapeleka wahusika karibu zaidi na ukweli.

Hotuba zilizotolewa na viongozi wa Chadema, Januari 21, 2023, katika uwanja wa Furahisha, Jiji Mwanza, zinathibitisha kwamba, nadharia ya udayalektika kuhusu mabadiliko ya kijamii imeanza kutekelezwa na Chadema.

Katika kuweka uzito kwenye nadharia hizo tatu, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alilihutubia taifa jioni ya siku hiyo alisema yafuatayo;

“Serikali ya awamu ya tano ililigeuza taifa hili kuwa taifa la maumivu, mateso na misiba…

…Nikiri kwamba sisi sote tulioumizwa na mateso ya viongozi wetu, wana Chadema wameumizwa, wana CCM wameumizwa na wapo wana CCM walionufaika na mateso hayo…

… Taifa letu halipaswi kuwa taifa la kuumuza kiongozi yoyote, mwanachama yoyote, mfuasi yeyote wa chama chochote. Taifa letu linapaswa kuwa taifa la watu walioungana, wanaoshikamana, wanaosimama katika misingi ya demokrasia.

… Taifa hili limepitia mengi, taifa hili linapaswa kuwa na watu ambao wameungana, wameshikamana na kusimama katika misingi ya demokrasia, utawala wa sheria na haki kwa wote...

… Ninaposimama nikiwa mwenyekiti na kiongozi wa Chadema kudai haki, sisimami kwa ajili wa wana Chadema, bali nasimama kama kiongozi wa kudai haki za watu wote…

… Naomba nilisisitize sana, tusijenge tabia ya kuwachukia wanachama wa CCM kwa sababu ya madhila tuliyopitia. Wajibu wetu ni kuwashurutisha kwa hoja ili watambue, ndani ya Chadema kuna haki, ustawi na fursa ya kumsaidia kila mmoja na akawa raia mwema kwa nchi yetu...

… Tunahitaji kukaa kama nchi kutambua kwamba nchi hii haiwezi kuendelea kwa kuigawanya vipande vipande. Eti kuna na kipande cha Chadema, kuna kipande cha CCM, kuna kipande cha UDP…

… Chadema tuna kauli kuu inayosema ‘no hate, no fear’ (hakuna chuki, hakuna woga). Natangaza wazi kuwa chama hiki siyo chama cha chuki. Hatuwezi kujenga utaifa wa nchi hii kwa kujenga chuki…

… Dhana ya ‘no hate’ (hakuna chuki), iambatane na dhana kwamba hatumuogopi mtu…

… Nampongeza Rais Samia Suluhu kwa kukubali maridhiano. Wapo watu wanatamani maridhiano yasifanikiwe. Wao wanafaidi maisha nje ya maridhiano. Samia alikubali nia ya maridhiano kinyume na matakwa ya chama chake...

… Kwa pamoja tuna wajibu wa kujadiliana yapi ni mambo ya msingi ya kuyafanya ili kulipeleka taifa letu katika furaha, ustawi na haki kwa kila mtu…

… Katika miaka yangu 30 ya kupigania taifa hili, natamani nitakapoacha uongozi, niache taifa langu, nchi yangu, watoto wangu, wajukuu wangu wakiwa wanapendana, wanaoshikamana na kuitafuta kesho yetu pamoja.”

Na kwa maneno ya Mbowe, kuna kila dalili kwamba siasa za “kunyukana na kukingiana vifua” huenda zinaondoka Chadema na kuja na staili nyingine ya mapambano ya siasa kwa lengo la kuongoza Tanzania.

Hata hivyo, wapo baadhi ya wahafidhina ndani ya Chadema kwa hatua hii wanaona kama mwenyekiti wao, Mbowe amewasaliti na kutaja kwamba “huenda amelamba asali.”

Hatua ambayo Mbowe ameikemea na kulaani wanaosambaza uongo kwamba amepokea rushwa kutoka kwa wapinzani wao ili “kumlainisha.”

Katika hotuba hii, Mbowe ameongelea mambo matatu.

Mosi, Mbowe anaongelea tasnifu asilia, isemayo kwamba, kuna wafuasi wa chama tawala ambao, tangu serikali ya awamu ya tano, wamekuwa wafuasi na watetezi wa mfumo wa kisiasa unaokuza na kuhami maslahi ya wachache na kutelekeza maslahi ya wengi.

Huu ni mfumo uliokweza dhuluma na kutweza haki, mfumo wenye kutukuza chuki dhidi ya wapinzani badala ya kufanya urafiki nao.

Ni mfumo ulioongozwa na imani hasi kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, siyo njia halali ya kusukuma gurudumu la maendeleo.

Ni mfumo uliotukuza ubaguzi wa kikanda na kiitikadi na kusahau kuimarisha umoja wa kitaifa bila kujali itikadi, ukabila na ukanda.

Pili, Mbowe anaongelea tasnifu kinzani, isemayo yafuatayo; kwamba, kwa mujibu wa ndoto ya waasisi wa nchi yetu, Tanzania ni taifa linapaswa kuongozwa na serikali inayopigania maslahi ya watu wote, badala ya kuhangaikia maslahi ya watu wachache.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kukumbatia mifumo inayokweza haki na Chadema na mpango mkakati kutweza dhuluma, inayotukuza urafiki badala ya kujenga uadui.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kukumbatia mifumo kuongozwa na kanuni kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, ndiyo njia pekee ya kusukuma gurudumu la maendeleo.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kupinga ubaguzi wa kikanda na kiitikadi na kuimarisha umoja wa kitaifa bila kujali itikadi, ukabila wala ukanda.

Na tatu, Mbowe anaongelea tasnifu hitimisho, isemayo yafuatayo; kwamba, kazi ya kujenga nchi, katika mazingira ya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, inapaswa kufanyika kwa mujibu wa kanuni kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, ndio njia pekee ya kuleta haki ya kweli, amani ya kweli, uhuru wa kweli na maendeleo ya kweli nchini Tanzania.

Tasnifu hitimisha inayoongelelwa na Mbowe, inaakisi hoja ya Profesa Euphrase Kezilahabi, kama ilivyotolewa mwaka 1978, kupitia tamthiliya yake iitwayo “Kaptura la Marx.”

Tamthiliya ilishutumu ukiritimba na matumizi mabaya ya madaraka katika mfumo wa Ujamaa uliouanzishwa enzi za Mwalimu Julius Nyerere, aliyekuwa Rais wa Tanzania.

Kwa mfano, ndani ya kitabu “Kaptula la Marx (1999),” kwenye ukurasa wa 20, maelezo ya mhusika Korchnoi Brown kwa Raisi Kapera na mawaziri wake kuhusu njia ya kufikia nchi ya usawa yanasomeka hivi;

“Mtakwenda. Halafu mtapinda, mtapinda tena, halafu tena mtapinda, mwishowe mtapindapinda hadi mtakapofika mabonde yenye matope. Mtapita katikati ya matope.

“Halafu milima, halafu misitu yenye miiba hadi mtakapofika jangwani. Kutoka jangwani mtaingia tena bondeni chini kwa chini hadi baharini. Hakuna mitumbwi wala ngalawa.

“Mtaogelea, ingawa kuna papa wengi. Mkishavuka mtafika nchi iitwayo Svoboda. Kabla ya kuondoka katika nchi hii itawabidi kupambana na majitu yanayofanana na mimi. Mkitoka hapo mtafika kwenye njia nyembamba.

“Hawa (mawaziri) hawatapita hawa. Njia hiyo itawafikisha katika nchi iitwayo Fraternite. Kutoka Fraternite mtafika Usawa. Ulizeni tu watu watawaonyesha.

“Mkifika Usawa mtawakuta Waswahili wenzenu wameketi nje ya Ikulu ndogo ya Ravensto.”


Neno “Korchnoi” ni jina la Kirusi, “Brown” jina la Kiingereza.

Majina haya yanarejea njia ya Tanzania ya Nyerere kati ya “mashariki” ya kikomunisti na “magharibi” ya kibeberu.

Neno “Fraternite” ni msamiati wa Kifaransa wenye kumaanisha “undugu.”

Ni moja ya tunu tatu zinazoyatambulisha mapinduzi ya Kifaransa, yaani “uhuru, usawa na undugu.”

Jina la nchi ya “Svoboda” linatokana na msamiati wa Kirusi wenye kumaanisha “uhuru.”

Ni jina la nchi linalorejea wito wa mapinduzi kama yaliyofanyika Ufaransa.

Hii ni sehemu ya ushahidi kwamba, tamthiliya ya “Kaptula la Marx” ilihimiza matumizi ya mbinu za kidayalektika kuhusu mabadiliko ya kijamii, kama zilivyoasisiwa na Mjerumani Georg Hegel (1770-1831), na kisha kunadiwa na Mjerumani mwenzake Karl Marx (1818- 1883).

Chadema wamechagua mbinu mwafaka, ambayo kwa sasa hutumika hata mahakamani, kulingana na mwongozo wa Profesa Stephen Toulmin (1922-2009), wa Uingereza.

Katika kitabu chake, “The Uses of Argument (1958),” Profesa Toulmin anasema kuwa hoja kamilifu, haipaswi kuwa na sehemu tatu kama alivyofundisha Aristotle, yaani hoja yenye “dokezo kuu, dokezo dogo na hitimisho.”

Bali, hoja iliyokamilika inapaswa kuwa na sehemu angalau sita, yaani, “tasnifu, ushahidi, waranti ya ushahidi, msingi wa waranti, tasnifu kinzani, majibu ya tasnifu kinzani, na majumuisho.”

Yaani, “thesis, ground, warrant, backing, objection, rebuttal, and synthesis.”

Hivyo, Chadema wamechagua barabara iliyo mwafaka. Walizindua tena rasmi mikutano ya kisiasa baada ya kuzuiwa miaka saba iliyopita kwa njia ya tamko la aliyekuwa Rais wa Tanzania John Magufuli.

Lakini, mnamo Januari 3, 2023, Rais Samia Suluhu Hassan, aliamua kuondoa zuio hilo kutokana na maridhiano ya kitaifa yaliyoasisiwa na yeye pamoja na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

Chanzo: Gazeti la Pambazuko Toleo namba 028.
Vijineno vya Kiswahili vya hapa na pale.

Lakini Maudhui ni pumba na takataka kabisa.
 
View attachment 2492314
Freean Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa

BAADA ya zuio lisilokuwa la kikatiba wala kisheria, la mikutano ya hadhara kwa muda mrefu, sasa ni wazi kwamba, Chadema wamezindua mikutano yao ya hadhara wakiwa na lengo kubwa la kueleza wapi serikali “imekwama” kukomboa wananchi na janga la ufukara.

Mtangulizi wa Rais Samia Suluhu Hassan, John Pombe Magufuli, miaka saba iliyopita, alitoa kauli kuzuia mikutano ya hadhara, ambayo ni injini ya kuendesha na kukuza vyama vya siasa.

Rais Magufuli, bila kupima umuhimu wa kidemokrasia kuendesha nchi, alitumia ubabe wa kiutawala kueleza tu; “sasa hakuna mikutano ya hadhara ya vyama,” na ikawa sheria.

Hatua hiyo ilifuatiwa na madhila mengi kwa wanasiasa, waandishi wa habari, wafanyabiashara na watu wa kada nyingine, ikiwamo kuumizwa, kutekwa, kuteswa, kupotezwa na wengine kuminywa uhai wao.

Rais Samia kwa mabadiliko ya sasa ya kuruhusu kuwepo kwa mikutano ya hadhara na kuacha demokrasia ipumue na kuendelea kukua, unatoa mwanya wa serikali kusemwa na kukosolewa ili ijirekebishe mahali itakapokuwa imekosea.

Tayari, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kupitia kwa mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, kimepongeza hatua ya Rais Samia kuvunja zuio hilo linaloelezwa na wengi kuwa “haramu.”

Ni kwa msingi huo, Chadema wanakuja na nadharia zenye kubeba hatua kadhaa za kuinyoshea serikali kidole kwa utendaji wake.

Nadharia hizo zinaweza kuwekwa katika hatua tatu za mabadiliko ya kifikra, kisera, kisheria, na kitaasisi. Mosi, ni kutengeneza “tasnifu asilia -” (thesis) kwa kuhakikisha kwamba, hali ya mfumo uliopo kwa sasa, yaani mtazamo rasmi unaokubalika kwa sasa, unachambuliwa vizuri.

Pili, ni kutengeneza “tasnifu kinzani -” (antithesis) kwa kuhakikisha kwamba, matatizo yaliyomo katika mfumo wa sasa yanabainishwa sawasawa, ili tasnifu asilia iweze kukosolewa kwa usahihi na kwa uhakika, kwa kutumia ushahidi.

Na tatu, ni kutengeneza “tasnifu hitimisho -” (synthesis) kwa kuhakikisha kwamba, kambi zinazopingana zinafikia mwafaka, kwa kuzalisha fikra, sera au sheria inayokubalika kwa kambi zote, kwa sababu ya ushahidi uliowekwa mezani na kushuhudiwa na kambi zote, wakati wa mchakati wa majadiliano.

Katika hatua ya tatu, mrejesho kutokana na tasnifu kinzani hufanywa sehemu ya tasnifu asilia ili kuzalisha tasnifu hitimisho, inayokubalika kwa kambi zote.

Kisha, mduara wa tasnifu asilia, tasnifu kinzani na tasnifu hitimisho hujirudiarudia hadi kuunda mchakato wenye muundo wa “spairo” (spiral), kila duara la spairo likiwapeleka wahusika karibu zaidi na ukweli.

Hotuba zilizotolewa na viongozi wa Chadema, Januari 21, 2023, katika uwanja wa Furahisha, Jiji Mwanza, zinathibitisha kwamba, nadharia ya udayalektika kuhusu mabadiliko ya kijamii imeanza kutekelezwa na Chadema.

Katika kuweka uzito kwenye nadharia hizo tatu, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alilihutubia taifa jioni ya siku hiyo alisema yafuatayo;

“Serikali ya awamu ya tano ililigeuza taifa hili kuwa taifa la maumivu, mateso na misiba…

…Nikiri kwamba sisi sote tulioumizwa na mateso ya viongozi wetu, wana Chadema wameumizwa, wana CCM wameumizwa na wapo wana CCM walionufaika na mateso hayo…

… Taifa letu halipaswi kuwa taifa la kuumuza kiongozi yoyote, mwanachama yoyote, mfuasi yeyote wa chama chochote. Taifa letu linapaswa kuwa taifa la watu walioungana, wanaoshikamana, wanaosimama katika misingi ya demokrasia.

… Taifa hili limepitia mengi, taifa hili linapaswa kuwa na watu ambao wameungana, wameshikamana na kusimama katika misingi ya demokrasia, utawala wa sheria na haki kwa wote...

… Ninaposimama nikiwa mwenyekiti na kiongozi wa Chadema kudai haki, sisimami kwa ajili wa wana Chadema, bali nasimama kama kiongozi wa kudai haki za watu wote…

… Naomba nilisisitize sana, tusijenge tabia ya kuwachukia wanachama wa CCM kwa sababu ya madhila tuliyopitia. Wajibu wetu ni kuwashurutisha kwa hoja ili watambue, ndani ya Chadema kuna haki, ustawi na fursa ya kumsaidia kila mmoja na akawa raia mwema kwa nchi yetu...

… Tunahitaji kukaa kama nchi kutambua kwamba nchi hii haiwezi kuendelea kwa kuigawanya vipande vipande. Eti kuna na kipande cha Chadema, kuna kipande cha CCM, kuna kipande cha UDP…

… Chadema tuna kauli kuu inayosema ‘no hate, no fear’ (hakuna chuki, hakuna woga). Natangaza wazi kuwa chama hiki siyo chama cha chuki. Hatuwezi kujenga utaifa wa nchi hii kwa kujenga chuki…

… Dhana ya ‘no hate’ (hakuna chuki), iambatane na dhana kwamba hatumuogopi mtu…

… Nampongeza Rais Samia Suluhu kwa kukubali maridhiano. Wapo watu wanatamani maridhiano yasifanikiwe. Wao wanafaidi maisha nje ya maridhiano. Samia alikubali nia ya maridhiano kinyume na matakwa ya chama chake...

… Kwa pamoja tuna wajibu wa kujadiliana yapi ni mambo ya msingi ya kuyafanya ili kulipeleka taifa letu katika furaha, ustawi na haki kwa kila mtu…

… Katika miaka yangu 30 ya kupigania taifa hili, natamani nitakapoacha uongozi, niache taifa langu, nchi yangu, watoto wangu, wajukuu wangu wakiwa wanapendana, wanaoshikamana na kuitafuta kesho yetu pamoja.”

Na kwa maneno ya Mbowe, kuna kila dalili kwamba siasa za “kunyukana na kukingiana vifua” huenda zinaondoka Chadema na kuja na staili nyingine ya mapambano ya siasa kwa lengo la kuongoza Tanzania.

Hata hivyo, wapo baadhi ya wahafidhina ndani ya Chadema kwa hatua hii wanaona kama mwenyekiti wao, Mbowe amewasaliti na kutaja kwamba “huenda amelamba asali.”

Hatua ambayo Mbowe ameikemea na kulaani wanaosambaza uongo kwamba amepokea rushwa kutoka kwa wapinzani wao ili “kumlainisha.”

Katika hotuba hii, Mbowe ameongelea mambo matatu.

Mosi, Mbowe anaongelea tasnifu asilia, isemayo kwamba, kuna wafuasi wa chama tawala ambao, tangu serikali ya awamu ya tano, wamekuwa wafuasi na watetezi wa mfumo wa kisiasa unaokuza na kuhami maslahi ya wachache na kutelekeza maslahi ya wengi.

Huu ni mfumo uliokweza dhuluma na kutweza haki, mfumo wenye kutukuza chuki dhidi ya wapinzani badala ya kufanya urafiki nao.

Ni mfumo ulioongozwa na imani hasi kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, siyo njia halali ya kusukuma gurudumu la maendeleo.

Ni mfumo uliotukuza ubaguzi wa kikanda na kiitikadi na kusahau kuimarisha umoja wa kitaifa bila kujali itikadi, ukabila na ukanda.

Pili, Mbowe anaongelea tasnifu kinzani, isemayo yafuatayo; kwamba, kwa mujibu wa ndoto ya waasisi wa nchi yetu, Tanzania ni taifa linapaswa kuongozwa na serikali inayopigania maslahi ya watu wote, badala ya kuhangaikia maslahi ya watu wachache.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kukumbatia mifumo inayokweza haki na Chadema na mpango mkakati kutweza dhuluma, inayotukuza urafiki badala ya kujenga uadui.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kukumbatia mifumo kuongozwa na kanuni kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, ndiyo njia pekee ya kusukuma gurudumu la maendeleo.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kupinga ubaguzi wa kikanda na kiitikadi na kuimarisha umoja wa kitaifa bila kujali itikadi, ukabila wala ukanda.

Na tatu, Mbowe anaongelea tasnifu hitimisho, isemayo yafuatayo; kwamba, kazi ya kujenga nchi, katika mazingira ya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, inapaswa kufanyika kwa mujibu wa kanuni kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, ndio njia pekee ya kuleta haki ya kweli, amani ya kweli, uhuru wa kweli na maendeleo ya kweli nchini Tanzania.

Tasnifu hitimisha inayoongelelwa na Mbowe, inaakisi hoja ya Profesa Euphrase Kezilahabi, kama ilivyotolewa mwaka 1978, kupitia tamthiliya yake iitwayo “Kaptura la Marx.”

Tamthiliya ilishutumu ukiritimba na matumizi mabaya ya madaraka katika mfumo wa Ujamaa uliouanzishwa enzi za Mwalimu Julius Nyerere, aliyekuwa Rais wa Tanzania.

Kwa mfano, ndani ya kitabu “Kaptula la Marx (1999),” kwenye ukurasa wa 20, maelezo ya mhusika Korchnoi Brown kwa Raisi Kapera na mawaziri wake kuhusu njia ya kufikia nchi ya usawa yanasomeka hivi;

“Mtakwenda. Halafu mtapinda, mtapinda tena, halafu tena mtapinda, mwishowe mtapindapinda hadi mtakapofika mabonde yenye matope. Mtapita katikati ya matope.

“Halafu milima, halafu misitu yenye miiba hadi mtakapofika jangwani. Kutoka jangwani mtaingia tena bondeni chini kwa chini hadi baharini. Hakuna mitumbwi wala ngalawa.

“Mtaogelea, ingawa kuna papa wengi. Mkishavuka mtafika nchi iitwayo Svoboda. Kabla ya kuondoka katika nchi hii itawabidi kupambana na majitu yanayofanana na mimi. Mkitoka hapo mtafika kwenye njia nyembamba.

“Hawa (mawaziri) hawatapita hawa. Njia hiyo itawafikisha katika nchi iitwayo Fraternite. Kutoka Fraternite mtafika Usawa. Ulizeni tu watu watawaonyesha.

“Mkifika Usawa mtawakuta Waswahili wenzenu wameketi nje ya Ikulu ndogo ya Ravensto.”


Neno “Korchnoi” ni jina la Kirusi, “Brown” jina la Kiingereza.

Majina haya yanarejea njia ya Tanzania ya Nyerere kati ya “mashariki” ya kikomunisti na “magharibi” ya kibeberu.

Neno “Fraternite” ni msamiati wa Kifaransa wenye kumaanisha “undugu.”

Ni moja ya tunu tatu zinazoyatambulisha mapinduzi ya Kifaransa, yaani “uhuru, usawa na undugu.”

Jina la nchi ya “Svoboda” linatokana na msamiati wa Kirusi wenye kumaanisha “uhuru.”

Ni jina la nchi linalorejea wito wa mapinduzi kama yaliyofanyika Ufaransa.

Hii ni sehemu ya ushahidi kwamba, tamthiliya ya “Kaptula la Marx” ilihimiza matumizi ya mbinu za kidayalektika kuhusu mabadiliko ya kijamii, kama zilivyoasisiwa na Mjerumani Georg Hegel (1770-1831), na kisha kunadiwa na Mjerumani mwenzake Karl Marx (1818- 1883).

Chadema wamechagua mbinu mwafaka, ambayo kwa sasa hutumika hata mahakamani, kulingana na mwongozo wa Profesa Stephen Toulmin (1922-2009), wa Uingereza.

Katika kitabu chake, “The Uses of Argument (1958),” Profesa Toulmin anasema kuwa hoja kamilifu, haipaswi kuwa na sehemu tatu kama alivyofundisha Aristotle, yaani hoja yenye “dokezo kuu, dokezo dogo na hitimisho.”

Bali, hoja iliyokamilika inapaswa kuwa na sehemu angalau sita, yaani, “tasnifu, ushahidi, waranti ya ushahidi, msingi wa waranti, tasnifu kinzani, majibu ya tasnifu kinzani, na majumuisho.”

Yaani, “thesis, ground, warrant, backing, objection, rebuttal, and synthesis.”

Hivyo, Chadema wamechagua barabara iliyo mwafaka. Walizindua tena rasmi mikutano ya kisiasa baada ya kuzuiwa miaka saba iliyopita kwa njia ya tamko la aliyekuwa Rais wa Tanzania John Magufuli.

Lakini, mnamo Januari 3, 2023, Rais Samia Suluhu Hassan, aliamua kuondoa zuio hilo kutokana na maridhiano ya kitaifa yaliyoasisiwa na yeye pamoja na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

Chanzo: Gazeti la Pambazuko Toleo namba 028.
Tuweke rekodi sawa,

ZUIO la Magu Lina uwezo wa kupitiliza Hadi utawala wa sa100?

Maana imepita miaka 2, Magu hayupo na ZUIO lingalipo.😳😳
 
View attachment 2492314
Freean Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa

BAADA ya zuio lisilokuwa la kikatiba wala kisheria, la mikutano ya hadhara kwa muda mrefu, sasa ni wazi kwamba, Chadema wamezindua mikutano yao ya hadhara wakiwa na lengo kubwa la kueleza wapi serikali “imekwama” kukomboa wananchi na janga la ufukara.

Mtangulizi wa Rais Samia Suluhu Hassan, John Pombe Magufuli, miaka saba iliyopita, alitoa kauli kuzuia mikutano ya hadhara, ambayo ni injini ya kuendesha na kukuza vyama vya siasa.

Rais Magufuli, bila kupima umuhimu wa kidemokrasia kuendesha nchi, alitumia ubabe wa kiutawala kueleza tu; “sasa hakuna mikutano ya hadhara ya vyama,” na ikawa sheria.

Hatua hiyo ilifuatiwa na madhila mengi kwa wanasiasa, waandishi wa habari, wafanyabiashara na watu wa kada nyingine, ikiwamo kuumizwa, kutekwa, kuteswa, kupotezwa na wengine kuminywa uhai wao.

Rais Samia kwa mabadiliko ya sasa ya kuruhusu kuwepo kwa mikutano ya hadhara na kuacha demokrasia ipumue na kuendelea kukua, unatoa mwanya wa serikali kusemwa na kukosolewa ili ijirekebishe mahali itakapokuwa imekosea.

Tayari, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kupitia kwa mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, kimepongeza hatua ya Rais Samia kuvunja zuio hilo linaloelezwa na wengi kuwa “haramu.”

Ni kwa msingi huo, Chadema wanakuja na nadharia zenye kubeba hatua kadhaa za kuinyoshea serikali kidole kwa utendaji wake.

Nadharia hizo zinaweza kuwekwa katika hatua tatu za mabadiliko ya kifikra, kisera, kisheria, na kitaasisi. Mosi, ni kutengeneza “tasnifu asilia -” (thesis) kwa kuhakikisha kwamba, hali ya mfumo uliopo kwa sasa, yaani mtazamo rasmi unaokubalika kwa sasa, unachambuliwa vizuri.

Pili, ni kutengeneza “tasnifu kinzani -” (antithesis) kwa kuhakikisha kwamba, matatizo yaliyomo katika mfumo wa sasa yanabainishwa sawasawa, ili tasnifu asilia iweze kukosolewa kwa usahihi na kwa uhakika, kwa kutumia ushahidi.

Na tatu, ni kutengeneza “tasnifu hitimisho -” (synthesis) kwa kuhakikisha kwamba, kambi zinazopingana zinafikia mwafaka, kwa kuzalisha fikra, sera au sheria inayokubalika kwa kambi zote, kwa sababu ya ushahidi uliowekwa mezani na kushuhudiwa na kambi zote, wakati wa mchakati wa majadiliano.

Katika hatua ya tatu, mrejesho kutokana na tasnifu kinzani hufanywa sehemu ya tasnifu asilia ili kuzalisha tasnifu hitimisho, inayokubalika kwa kambi zote.

Kisha, mduara wa tasnifu asilia, tasnifu kinzani na tasnifu hitimisho hujirudiarudia hadi kuunda mchakato wenye muundo wa “spairo” (spiral), kila duara la spairo likiwapeleka wahusika karibu zaidi na ukweli.

Hotuba zilizotolewa na viongozi wa Chadema, Januari 21, 2023, katika uwanja wa Furahisha, Jiji Mwanza, zinathibitisha kwamba, nadharia ya udayalektika kuhusu mabadiliko ya kijamii imeanza kutekelezwa na Chadema.

Katika kuweka uzito kwenye nadharia hizo tatu, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alilihutubia taifa jioni ya siku hiyo alisema yafuatayo;

“Serikali ya awamu ya tano ililigeuza taifa hili kuwa taifa la maumivu, mateso na misiba…

…Nikiri kwamba sisi sote tulioumizwa na mateso ya viongozi wetu, wana Chadema wameumizwa, wana CCM wameumizwa na wapo wana CCM walionufaika na mateso hayo…

… Taifa letu halipaswi kuwa taifa la kuumuza kiongozi yoyote, mwanachama yoyote, mfuasi yeyote wa chama chochote. Taifa letu linapaswa kuwa taifa la watu walioungana, wanaoshikamana, wanaosimama katika misingi ya demokrasia.

… Taifa hili limepitia mengi, taifa hili linapaswa kuwa na watu ambao wameungana, wameshikamana na kusimama katika misingi ya demokrasia, utawala wa sheria na haki kwa wote...

… Ninaposimama nikiwa mwenyekiti na kiongozi wa Chadema kudai haki, sisimami kwa ajili wa wana Chadema, bali nasimama kama kiongozi wa kudai haki za watu wote…

… Naomba nilisisitize sana, tusijenge tabia ya kuwachukia wanachama wa CCM kwa sababu ya madhila tuliyopitia. Wajibu wetu ni kuwashurutisha kwa hoja ili watambue, ndani ya Chadema kuna haki, ustawi na fursa ya kumsaidia kila mmoja na akawa raia mwema kwa nchi yetu...

… Tunahitaji kukaa kama nchi kutambua kwamba nchi hii haiwezi kuendelea kwa kuigawanya vipande vipande. Eti kuna na kipande cha Chadema, kuna kipande cha CCM, kuna kipande cha UDP…

… Chadema tuna kauli kuu inayosema ‘no hate, no fear’ (hakuna chuki, hakuna woga). Natangaza wazi kuwa chama hiki siyo chama cha chuki. Hatuwezi kujenga utaifa wa nchi hii kwa kujenga chuki…

… Dhana ya ‘no hate’ (hakuna chuki), iambatane na dhana kwamba hatumuogopi mtu…

… Nampongeza Rais Samia Suluhu kwa kukubali maridhiano. Wapo watu wanatamani maridhiano yasifanikiwe. Wao wanafaidi maisha nje ya maridhiano. Samia alikubali nia ya maridhiano kinyume na matakwa ya chama chake...

… Kwa pamoja tuna wajibu wa kujadiliana yapi ni mambo ya msingi ya kuyafanya ili kulipeleka taifa letu katika furaha, ustawi na haki kwa kila mtu…

… Katika miaka yangu 30 ya kupigania taifa hili, natamani nitakapoacha uongozi, niache taifa langu, nchi yangu, watoto wangu, wajukuu wangu wakiwa wanapendana, wanaoshikamana na kuitafuta kesho yetu pamoja.”

Na kwa maneno ya Mbowe, kuna kila dalili kwamba siasa za “kunyukana na kukingiana vifua” huenda zinaondoka Chadema na kuja na staili nyingine ya mapambano ya siasa kwa lengo la kuongoza Tanzania.

Hata hivyo, wapo baadhi ya wahafidhina ndani ya Chadema kwa hatua hii wanaona kama mwenyekiti wao, Mbowe amewasaliti na kutaja kwamba “huenda amelamba asali.”

Hatua ambayo Mbowe ameikemea na kulaani wanaosambaza uongo kwamba amepokea rushwa kutoka kwa wapinzani wao ili “kumlainisha.”

Katika hotuba hii, Mbowe ameongelea mambo matatu.

Mosi, Mbowe anaongelea tasnifu asilia, isemayo kwamba, kuna wafuasi wa chama tawala ambao, tangu serikali ya awamu ya tano, wamekuwa wafuasi na watetezi wa mfumo wa kisiasa unaokuza na kuhami maslahi ya wachache na kutelekeza maslahi ya wengi.

Huu ni mfumo uliokweza dhuluma na kutweza haki, mfumo wenye kutukuza chuki dhidi ya wapinzani badala ya kufanya urafiki nao.

Ni mfumo ulioongozwa na imani hasi kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, siyo njia halali ya kusukuma gurudumu la maendeleo.

Ni mfumo uliotukuza ubaguzi wa kikanda na kiitikadi na kusahau kuimarisha umoja wa kitaifa bila kujali itikadi, ukabila na ukanda.

Pili, Mbowe anaongelea tasnifu kinzani, isemayo yafuatayo; kwamba, kwa mujibu wa ndoto ya waasisi wa nchi yetu, Tanzania ni taifa linapaswa kuongozwa na serikali inayopigania maslahi ya watu wote, badala ya kuhangaikia maslahi ya watu wachache.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kukumbatia mifumo inayokweza haki na Chadema na mpango mkakati kutweza dhuluma, inayotukuza urafiki badala ya kujenga uadui.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kukumbatia mifumo kuongozwa na kanuni kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, ndiyo njia pekee ya kusukuma gurudumu la maendeleo.

Kwamba, Tanzania ni taifa linapaswa kupinga ubaguzi wa kikanda na kiitikadi na kuimarisha umoja wa kitaifa bila kujali itikadi, ukabila wala ukanda.

Na tatu, Mbowe anaongelea tasnifu hitimisho, isemayo yafuatayo; kwamba, kazi ya kujenga nchi, katika mazingira ya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, inapaswa kufanyika kwa mujibu wa kanuni kwamba, ukosoaji wa mifumo iliyopo kwa lengo la kuibua ukweli mpya, na hivyo kujenga mifumo bora zaidi, ndio njia pekee ya kuleta haki ya kweli, amani ya kweli, uhuru wa kweli na maendeleo ya kweli nchini Tanzania.

Tasnifu hitimisha inayoongelelwa na Mbowe, inaakisi hoja ya Profesa Euphrase Kezilahabi, kama ilivyotolewa mwaka 1978, kupitia tamthiliya yake iitwayo “Kaptura la Marx.”

Tamthiliya ilishutumu ukiritimba na matumizi mabaya ya madaraka katika mfumo wa Ujamaa uliouanzishwa enzi za Mwalimu Julius Nyerere, aliyekuwa Rais wa Tanzania.

Kwa mfano, ndani ya kitabu “Kaptula la Marx (1999),” kwenye ukurasa wa 20, maelezo ya mhusika Korchnoi Brown kwa Raisi Kapera na mawaziri wake kuhusu njia ya kufikia nchi ya usawa yanasomeka hivi;

“Mtakwenda. Halafu mtapinda, mtapinda tena, halafu tena mtapinda, mwishowe mtapindapinda hadi mtakapofika mabonde yenye matope. Mtapita katikati ya matope.

“Halafu milima, halafu misitu yenye miiba hadi mtakapofika jangwani. Kutoka jangwani mtaingia tena bondeni chini kwa chini hadi baharini. Hakuna mitumbwi wala ngalawa.

“Mtaogelea, ingawa kuna papa wengi. Mkishavuka mtafika nchi iitwayo Svoboda. Kabla ya kuondoka katika nchi hii itawabidi kupambana na majitu yanayofanana na mimi. Mkitoka hapo mtafika kwenye njia nyembamba.

“Hawa (mawaziri) hawatapita hawa. Njia hiyo itawafikisha katika nchi iitwayo Fraternite. Kutoka Fraternite mtafika Usawa. Ulizeni tu watu watawaonyesha.

“Mkifika Usawa mtawakuta Waswahili wenzenu wameketi nje ya Ikulu ndogo ya Ravensto.”


Neno “Korchnoi” ni jina la Kirusi, “Brown” jina la Kiingereza.

Majina haya yanarejea njia ya Tanzania ya Nyerere kati ya “mashariki” ya kikomunisti na “magharibi” ya kibeberu.

Neno “Fraternite” ni msamiati wa Kifaransa wenye kumaanisha “undugu.”

Ni moja ya tunu tatu zinazoyatambulisha mapinduzi ya Kifaransa, yaani “uhuru, usawa na undugu.”

Jina la nchi ya “Svoboda” linatokana na msamiati wa Kirusi wenye kumaanisha “uhuru.”

Ni jina la nchi linalorejea wito wa mapinduzi kama yaliyofanyika Ufaransa.

Hii ni sehemu ya ushahidi kwamba, tamthiliya ya “Kaptula la Marx” ilihimiza matumizi ya mbinu za kidayalektika kuhusu mabadiliko ya kijamii, kama zilivyoasisiwa na Mjerumani Georg Hegel (1770-1831), na kisha kunadiwa na Mjerumani mwenzake Karl Marx (1818- 1883).

Chadema wamechagua mbinu mwafaka, ambayo kwa sasa hutumika hata mahakamani, kulingana na mwongozo wa Profesa Stephen Toulmin (1922-2009), wa Uingereza.

Katika kitabu chake, “The Uses of Argument (1958),” Profesa Toulmin anasema kuwa hoja kamilifu, haipaswi kuwa na sehemu tatu kama alivyofundisha Aristotle, yaani hoja yenye “dokezo kuu, dokezo dogo na hitimisho.”

Bali, hoja iliyokamilika inapaswa kuwa na sehemu angalau sita, yaani, “tasnifu, ushahidi, waranti ya ushahidi, msingi wa waranti, tasnifu kinzani, majibu ya tasnifu kinzani, na majumuisho.”

Yaani, “thesis, ground, warrant, backing, objection, rebuttal, and synthesis.”

Hivyo, Chadema wamechagua barabara iliyo mwafaka. Walizindua tena rasmi mikutano ya kisiasa baada ya kuzuiwa miaka saba iliyopita kwa njia ya tamko la aliyekuwa Rais wa Tanzania John Magufuli.

Lakini, mnamo Januari 3, 2023, Rais Samia Suluhu Hassan, aliamua kuondoa zuio hilo kutokana na maridhiano ya kitaifa yaliyoasisiwa na yeye pamoja na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

Chanzo: Gazeti la Pambazuko Toleo namba 028.
Mbowe apongezwe.
 
Hotuba ya Mbowe ni rafiki KWA mwenye madaraka kumuachia asie na madaraka!

Naiona serikali ya umoja wa kitaifa huko mbeleni!

PM au makamu wa Rais akatokea UPINZANI!

TUSUBIRI!
 
BAADA ya zuio lisilokuwa la kikatiba wala kisheria, la mikutano ya hadhara kwa muda mrefu, sasa ni wazi kwamba, Chadema wamezindua mikutano yao ya hadhara wakiwa na lengo kubwa la kueleza wapi serikali “imekwama” kukomboa wananchi na janga la ufukara.
Mkuu Mama Amon , thanks for this
P
 
Tuweke rekodi sawa,

ZUIO la Magu Lina uwezo wa kupitiliza Hadi utawala wa sa100?

Maana imepita miaka 2, Magu hayupo na ZUIO lingalipo.😳😳

Bila presha ya CHADEMA hata Samiah angeendekeza zuio mpaka 2025. Kujishusha kwa CHADEMA ndio matunda yake hayo.
 
Shida kubwa waliofanya muafaka hawajui maana ya malidhiano! Kama mmekubaliana kuanza upya kunasababu gani kuleta mambo ya zamani na kujaza lawama Kwa Mtu ambaye hayupo?
Kwamfano NCHI kama Rwanda,Afrika Kusini nk walifungua ukurasa mpya baada ya Yale yaliyotokea na kuanza upya.

Kwetu Tanzania lazima tupate watu wapya wenye fikra sahihi badala ya watu wa zamani ambao wanataka huruma Kwa Wananchi kwa mambo yamepita na ambayo kwasasa hayapo.

Matusi ya rejareja yanapunguza Sana wateja kwasababu watu wengi hawapendi uzalilisha na katika jumuiya ni vema ukakubali kuto kukubaliana unaweza kumtukana mtu mmoja unasahau kwamba anawafuasi wake ambao ukiwaelewesha wanaweza kukuunga Mkono lakini Kwa kuwatukania mtu wao unaongeza chuki na uhasama Jambo linalokinzana na muafaka uliofikiwa.
 
Bila presha ya CHADEMA hata Samiah angeendekeza zuio mpaka 2025. Kujishusha kwa CHADEMA ndio matunda yake hayo.
Kumbe ilibidi wajishushe? Sasa mbona Lissu kule Aljazeera anasema kuwa ni pressure kubwa ya CDM waliyompatia Rais ndiyo imepelekea kuruhusiwa mikutano ya hadhara?
 
Back
Top Bottom