Chadema wagomea mwaliko wa Tendwa

Kwa mtazamo wangu kataa neno sio wito, ni hayo tu. N ingekua poa CDM ndio kutumia semina hii kumfundisha Tendwa.
Mkuu sidhani kama Tendwa ana mamlaka stahiki kikatiba(nazungumzia katiba ya nchi) ya kuitisha semina kama hiyo, yeye anachoweza kufanya kutoa semina juu ya taratibu za usajili wa vyama na jinsi ya kutafuta wanachama mikoa ya bara na visiwani, kifupi juu ya usajili wa vyama. Mambo ya amani na usalama wa nchi yeye anahusikaje na yupo katika kamati gani ya mambo ya amani na usalama wa nchi? Tuache mchezo huyu Mzee mwenzangu pengine anaona hana kazi ya kufanya kumbe anajiundia vijikazi vya kufanya. Ni ushauri tu, angeenda kutembelea nchi nyingine zenye vyama vyingi aone kama kuna ofisi ya aina hiyo ambayo ni ya kudumu, nadhani ni TZ tu ambako tunaweza poteza pesa kuweka ofisi kama hiyo muda wote. Naomba mwenye Job description ya Msajili wa vyama vya Siasa aweke hapa ili tuone kama kipengele cha semina za amani na usalama wa nchi kipo.
 
Dawa ya korofi ndio hiyo ni kumchanganya ki saikolojia na hatimae aondoke kwa aibu.

Na kweli Tendwa jana alikuwa mnyonge sana kwa sababu mlengwa wa mkutano wa jana ilikuwa CDM ambao walisusia.
 
Msajili Tendwa hana maadili kabisa, kama mzee wa kanisa la Roma Parokia ya Kibamba katelekeza mke huku Kibamba na kumchukua binti wa mzee mwenzie wa kanisa aitwaye Catherine ndio anaishi naye huko Kibangu. Sasa mtu kama huyu ataweze vipi kulea taasisi kama vyama vya siasa?
 
Msajili Tendwa hana maadili kabisa, kama mzee wa kanisa la Roma Parokia ya Kibamba katelekeza mke huku Kibamba na kumchukua binti wa mzee mwenzie wa kanisa aitwaye Catherine ndio anaishi naye huko Kibangu. Sasa mtu kama huyu ataweze vipi kulea taasisi kama vyama vya siasa?

Mungu mtakatifu tuhurumie....
 
Katika kile kinachoonekana kuwa ndio mwelekeo wa matukio kama Pipooz pawa itaendelea, na CDM kuendelea kumgomea Msajili wa vyama Jaji John Tendwa, yeye ameenda mbali zaidi na kutishia kukata ruzuku ya CDM.

CDM wamealikwa pamoja na vyama vingine vyote kwenye kikao cha "usuluhishi" na mashauriano kati yake na vyombo vya serikali lakini wamekataa mwaliko huo.

Kikao hiki ni kufuatia matukio mabaya sana yaliyopelekea wananchi kadhaa kupoteza maisha katika mihadara na maandamano ya CDM mikoani ambayo udhibiti wake uliofanywa na Jeshi la Polisi umeleta utata mkubwa.

Tishio la Tendwa ingawaje siyo direct, linawakaribisha CDM kuendelea kususia shughuli zinazopangwa na Msajili wa Vyama, na kwa vile ofisi ya Msajili ndiyo inayo shughulikia ruzuku ya vyama, basi matokeo yake yatakuwa dhahiri-ikiwa ni sawa na kususia ruzuku!!

Source: Majira(front page) and Mwananchi(page 4)

My Take:
CDM dont let your fame go to your head!!!
 
point blank ... cdm walisema watamsusia Tendwa personally kwani maamuzi anayofanya si ya msajili wa vyama Bali ni yake binafsi
 
Anazidi kulikoroga na anajidhihirisha ambavyo amekosa umakini.
Kwanza atafakari sababu za CHADEMA kumsusia na pili aangalie maamuzi ya kususia yalifanywa na kikao gani cha CHADEMA.
Ameshindwa kuzuia ushabiki wake na anaendelza malumbano.Ruzuku si pesa yake yeye ni msimiâmiaji tu.
Nilimsikia Tambwe Hiza jana na nikaona ni afadhali CHADEMA walisusia otherwise zingewaka ngumi humo ndani.
 
Unajua nilikuwa namfananisha mzee Tendwa na Issa Matona (RIP) aliyekuwa mwimbaji maarufu wa taarabu kwa kuona kuwa wanafanana kwa sura lakini sasa nakwenda mbali zaidi kuona hata tendwa naye anaingia kwenye mipasho. Hii ni hatari kwa ustawi na mustakabali wa democrasia nchini.
 
Msajili Tendwa hana maadili kabisa, kama mzee wa kanisa la Roma Parokia ya Kibamba katelekeza mke huku Kibamba na kumchukua binti wa mzee mwenzie wa kanisa aitwaye Catherine ndio anaishi naye huko Kibangu. Sasa mtu kama huyu ataweze vipi kulea taasisi kama vyama vya siasa?


HEEEE! Mzee wa kanisa ameweka Kidumu? Aisee!
 
Hela za ruzuku ni za watoa kodi. sio za ccm wala tendwa. yeye anatekeleza sheria zilizo wekwa na Bunge. Hata tendwa akifa ruzuku zitaendelea kutolewa sababu ni utaratibu wa kisheria tulio jiwekea. so maneno ya tendwa yanaonyesha alivyo filisika mawazo. mia
 
Back
Top Bottom