Nicolas J Clinton Gabone
JF-Expert Member
- Mar 13, 2014
- 892
- 536
Chama Cha Democrasia na Maendeleo CHADEMA & UKAWA watakuwa kwa medani za jiji la Mwanza kesho kati ya hawa watakuwepo MBOWE, PROF SAFARI, LISU na MNYIKA medani ni kati ya FURAHISHA & MIRONGO PRIMARY. "UKAWA TUMAINI LETU"
====================
UPDATES
hawa ni baadhi ya watu waliopo mkutanoni
====================
UPDATES
Wakuu leo chama pendwa Tz CHADEMA imetikisa jiji la Mwanza kwa kufanya mkutano mkubwa wa hadhara ulifanyika katika viwanja vya shule ya msingi Mbugani.
Katika mkutano huo mkubwa uliohutubiwa na Mwenyekiti wa BAVICHA taifa kamanda Pastrobasi Pascal Katambi,Naibu katibu bara na Zanzibar John Mnyika na Salum Mwalim na wengineo .
Katika mkutano huo uliohudhuriwa na maelfu ya watu wa jiji la Mwanza ,mada kubwa zilizohutubiwa na viongozi hao wa kitaifa zilikuwa ni suala la rasimu ya katiba mpya,umuhimu wa kushiriki kwenye zoezi la uandikishaji wa daftari la kupga kura,kuwataka watu wajitokeze kwenye chaguzi za serikali za mitaa,unaotarajiwa kufanyika mwezi wa 12 mwaka huu.
Awali kabla ya mkutano huo wa wazi,ulitanguliwa na kongamano kubwa la vijana ,lililoandaliwa na BAVICHA Nyamagana na kufanyikia Tema hotel iliyopo Mkolani,ambapo katika kongamano hilo ambalo mgeni rasmi alikuwa mwenyekiti wa BAVICHA taifa,vijana walijengewa uwezo wa kushiriki kwenye chaguzi mbalimbali.
Viwanja vya mbugani vimejaa watu ni wengi sana hadi nafasi hakuna. Nnyika, Salum Mwalimu na Parobass Katambi wamefika sasa na uwanja unaendelea kujaa hakika Mungu ni taa ya UKAWA.
Gesi ya machozi inarushwa watu wanataaruki sasa maduka yanafungwa. Polisi wemejiandaa vyema watu wanapiga kelele, Viongozi wa UKAWA wanalazimishwa kuondoka bila maandamano baada ya watu kutaka kumsindikiza MNYIKA.
hawa ni baadhi ya watu waliopo mkutanoni