CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

Hivi wewe kweli unataka kusema kila mtu humu ataandika neno kwa neno la mtu alosema au unaandika ulichoelewa? Watu wote wamemuelewa hivyo, na hata viongozi wa dini wamekemea kwa hilo iweje wewe ulielewa tofauti?

Sasa kama Lowassa ameomba msamaha, kaomba msamaha kasema nini? kwamba aombewe imekuwa kosa la kuomba msamaha!? au kuna zaidi ya kuombewa! Wewe umeelewaje ile hotuba ya Lowassa pale kanisani kufikia kaomba msamaha alisema nini maana kuombewa kila mtu anasema na hakuna mahala unapozitaka dua za watu kama kanisa lako!

Zaidi ya hayo mbona humu mnaandika maneno mengi ambayo hata Dr.Slaa hakusema hivyo, lakini tumeelewa kuwa yanaendana na maana ile ile ya msemaji, iweje utake mimi niandike kila neno sawa na matamshi ya Lowassa. Kama haya sio mahaba ni nini tena dadangu!

Nashukuru sana kwa kukiri kuwa "ulichomeka maneno ya uongo kwa manufaa yako"ni hilo nililotaka kukuonyesha..
Maadam huwa sipendi kujadili mada zinazohusu udini kwa leo nitaishia hapo.


Swala la Richmond huwezi kulifuta kirahisi hivyo kwa sbaabu wewe unaona hakuna sababu. Sababu zipo na tunataka kujua yote toka kuuzwa kwa nyumba za serikali, ubinafsishaji wa mashirika, uporaji wa nyumba za serikali na mashamba, EPA, Rada, IPTL, Meremeta, Kagoda na mengineyo mengi ambayo ndio sababu kubwa ya wananchi kuichoka CCM. Mimi binafsi nitamfagilia kiongozi yeyote ambaye atakuwa tayari kurudisha maswala yote haya mezani kwa sababu hatuwezi kuzungumzia Uadilifu na uwajibikaji wakati tunaacha Kuhujumu Uchumi kuwa ni mambo yalopita, wakati sheria zipo zimekiukwa na hawa Untouchables!.

Tumefika hapa leo kwa sababu yao,na hatuwezi kuendelea kuwafuga tukitegemea mabadiliko, wana kesi kubwa ya kujibu kwa wananchi kwa sababu sisi ndio waajiri wao. What next? Tutawahukumu kwa kuujua ukweli kuliko kuendelea kuwashutumu watu pengine hawahusiki kabisa. Ukweli utawaacha huru! Leo unamsema Mwakyembe kwa dhana tu ya kuinusuru serikali wakati msimamizi wa shughuli za serikali ni Waziri mkuu. Tunachomkana Lowassa ni Ufisadi wake, hakuwa muadilifu katika kusimamia majukumu alopewa kiasi kwamba alihujumu Uchumi wetu, hii ni Kashfa kubwa kwa mgombea urais! Na kama itawezekana ukweli ukitolewa tutaandika kwa uhakika kabisa na hatutabisha..

Mpaka hapo tuko pamoja..
 
Mkandara said:
Tumefika hapa leo kwa sababu yao,na hatuwezi kuendelea kuwafuga tukitegemea mabadiliko, wana kesi kubwa ya kujibu kwa wananchi kwa sababu sisi ndio waajiri wao. What next? Tutawahukumu kwa kuujua ukweli kuliko kuendelea kuwashutumu watu pengine hawahusiki kabisa. Ukweli utawaacha huru! Leo unamsema Mwakyembe kwa dhana tu ya kuinusuru serikali wakati msimamizi wa shughuli za serikali ni Waziri mkuu. Tunachomkana Lowassa ni Ufisadi wake, hakuwa muadilifu katika kusimamia majukumu alopewa kiasi kwamba alihujumu Uchumi wetu, hii ni Kashfa kubwa kwa mgombea urais! Na kama itawezekana ukweli ukitolewa tutaandika kwa uhakika kabisa na hatutabisha..
Mkandara, utake usitake Raisi ajaye atatoka ama CCM au UKAWA kupitia Chadema; ama atakuwa Magufuli au atakuwa Lowassa. Sasa mimi Mag3 nampigia debe Lowassa wa Chadema chini ya UKAWA, je wewe mwenzangu? Tulipofikia naomba tuache unafiki na kwa kuwa mimi si mnafiki msimamo wangu sina haja ya kuuficha, je wewe mwenzangu unao huo ubavu? Ukiweza kunijibu tutaweza kuendelea na mjadala vizuri kabisa kwani tutakuwa kwenye nafasi nzuri tu ya kujadili hatma ya taifa letu mikononi mwa mojawapo katika hao wawili.

Kuendelea kuwalilia watu kama Dr. Slaa, Prof. Lipumba na wengineo hakutufikishi popote; they are out of the picture and that's fact and a memo.

Baada ya hiyo introduction inaonekana wengi wetu neno mabadiliko tunalichukulia kimzaha mzaha, niruhusuni niwape tu kaushauri, binadamu akishaamua kwamba anataka mabadiliko, kama hakuyapata kwa amani, atayadai kwa nguvu. Wakati wa mabadiliko ukifika umefika na natamani watawala wetu wangezingatia hilo wanapofanya maamuzi mbali mbali ili mwisho wa siku tuweze kudumisha amani na utulivu bila kuminya haki.
 
NasDaz Si kweli kuwa ninatetea mgombea wangu, kwa kweli nitasema uongo kama nitasema nina mahaba na Lowassa..rejea maandishi yangu ya nyuma. Lakini nashindwa kuelewa mtu anapomwanga petrol kwenye nyumba inayowaka moto unategemea nini..

Sipendi kujadili mambo ya dini, kwenye mjadala ya dini huwa ninakuwa na kigugumizi gafla lakini hapo hapo sipendi kuona mtu anamtia maneno binadamu mwenzake ili akidhi haja zake.. Alichokifanya Lowassa ni kosa na ameona hilo na kuomba msamaha...

Bado ninafahamu kuwa nina deni la kujibu hoja zako..


Ndg yangu Alinda,
Ni kweli kabisa Lowassa alikosea wala hatukatai tena alikosea sana, sema tatizo watu wanamlisha maneno na kwa hakika kawa muungwana katambua makosa yake akaomba radhi, sasa tatizo linakuja kwa kwa watu ambao wao ndio wanauendeleza huo udini na kuuhubiri kana kwamba ni practice ya kila siku ya mgombea.

Iwapo mgombea angeendelea ( persistent practice) ya huo udini unaosemwa hapo ni kosa na tungempiga mawe sana, lakini yeye kakosea mara moja na hajaendelea tena, tunaopaswa kuwahoji sasa ni hawa ambao badala ya kujadili hoja na sera wao wanashupalia isu ya udini, kimsingi hao ndio wanaochochea kuni na hao ndio wadini, ilipaswa tunkukemea na kuacha kulichochea kama huyo mkosaji haendelea na hilo kosa. Ni sawa na mtoto amejisaidia kitandani na kaomba radhina hajarudia tena basi wewe kila siku unamtuhumu kwa kosa hilo hilo hilo ni ajabu, siasa za Tanzania ni ngumu sana.

Kimsingi ninachokiona kuna kitu Chama tawala hawakutarajia kukutana nacho uchaguzi wa mwaka huu na labda wali underestimates nguvu ya upinzani, sasa kama wamepigwa shock wanajitahidi kutumia kila njia kujinasua kutoka kwenye hali hii na naona inawaumiza sana na kuwachanganya, wanasema wanauhakika wa kushinda ila ukiangalia practice zao utagundua mashaka makubwa sana.

Pole kwa kuchepuka kwenye mada, niliona niongeze hii kitu baada ya kuona kuna watu wanalalamika mno.
 
Nashindwa kuandika, nashindwa kukubali, moyo wangu umejaa udhuni, simamzi na masikitiko, siamini kuwa Mohamedi Mtoi hatutamuona tena hapa JF, hatutamuona tena katika harakati zake za mabadiliko, hatutamuona tena akitimiza ndoto zake za kuwaletea wananchi wa eneo lake maendeleo, kifo chake kimekuwa cha ghafla kama kilivyokuwa cha Regia Mtema.

Hakuna cha kufanya mikono yetu imefungwa tumebaki kuangalia na tusijue cha kufanya, inabidi tukubali kuwa Kamanda Mtoi hatuko naye tena.. Pumzika kwa amani Kijana wetu hakika pengo uliloacha halitazibika.
 
Mkandara, utake usitake Raisi ajaye atatoka ama CCM au UKAWA kupitia Chadema; ama atakuwa Magufuli au atakuwa Lowassa. Sasa mimi Mag3 nampigia debe Lowassa wa Chadema chini ya UKAWA, je wewe mwenzangu? Tulipofikia naomba tuache unafiki na kwa kuwa mimi si mnafiki msimamo wangu sina haja ya kuuficha, je wewe mwenzangu unao huo ubavu? Ukiweza kunijibu tutaweza kuendelea na mjadala vizuri kabisa kwani tutakuwa kwenye nafasi nzuri tu ya kujadili hatma ya taifa letu mikononi mwa mojawapo katika hao wawili.

Kuendelea kuwalilia watu kama Dr. Slaa, Prof. Lipumba na wengineo hakutufikishi popote; they are out of the picture and that's fact and a memo.

Baada ya hiyo introduction inaonekana wengi wetu neno mabadiliko tunalichukulia kimzaha mzaha, niruhusuni niwape tu kaushauri, binadamu akishaamua kwamba anataka mabadiliko, kama hakuyapata kwa amani, atayadai kwa nguvu. Wakati wa mabadiliko ukifika umefika na natamani watawala wetu wangezingatia hilo wanapofanya maamuzi mbali mbali ili mwisho wa siku tuweze kudumisha amani na utulivu bila kuminya haki.
Mimi sina kadi ya kupiga kura wala sintopiga kura kwa sababu nje ya uwezo wangu na nadhani unalijua hilo. Aidha swali lako ni la kukejeri ama unataka tuondoke katika mjadala husika hoja iwe mimi Mkandara na sio wagombea Urais.

Jambo la muhimu hapa hatusemi wala kumwambia mtu kura yake ampe nani, isipokuwa tunazungumzia sifa na uwezo wa viongozi tunaowatarajia kutuongoza. Iwe Magufuli au Lowassa atakaye shinda atakuwa rais wetu sote hakuna rais wa UKAWA ama rais wa CCM, kwa hiyo hizi fikra za kwamba mtu kama hamkubali Lowassa (UKAWA) basi lazima ni wa Magufuli (CCM) ni kutolitazama swala hili kwa mapana zaidi maana tunazungumzia rais wa JMT na sio mwenyekiti au kiongozi wa chama.

Swala la Mabadiliko ni kauli tata siku zote maana hakuna anayeweza kuyaona ya mbele, inaweza kuwa kama Misri au Iraq waloyataka Mabadiliko ama ikawa tofauti kama Kenya, Zambia na nchi nyinginezo maana nijuavyo mimi Sijawahi kuyaona Mabadiliko ya kisiasa yenye tija kwa wananchi wake zaidi ya kisera yaani mnachagua chama chenye sera zenye kukidhi mahitaji ya wananchi lakini haya Mabadiliko ya WATU kutaka sura nyingine ziongoze wakati fikra zao ni zile zile ndio mwanzo wa machafuko maana wanagombania kitu kama madume ya faru walotoka zizi moja.

Kumbuka tu wewe na mimi ni nyasi, hawa faru wanapogombana tunaumia sisi na hawajali japo chakula chao ni nyasi! sisi ndio waajiri wao na maisha yao yanatutegemea sisi lakini leo wanaomba kura zenu kwa kuonyesha unyenyekevu lakini mwisho wa siku wakiingia IKULU hawatapafanya tena Msikitini/kanisani bali nani dume atakaye tawala!

Sintomfagilia Lowassa kwa sababu ya Chadema, kazi mhiyo nimeiacha siku nyingi baada ya kugundua pale hapakuwa na UMOJA wenye dhamira ya kweli isipokuwa kundi la watu waloona Opportunity ya kuupata utajiri na Uheshimiwa. Fikra zile zile walokuwa nazo CCM miaka yote na kama mabadiliko basi yangeanza na kuondoa fursa ya wao kujitajirisha kwa kulipwa mshahara mil.11 kwa mwezi kazi ya kujitolea wakati CEO wa Benki hapewi mishahara huo..
 
Mimi sina kadi ya kupiga kura wala sintopiga kura kwa sababu nje ya uwezo wangu na nadhani unalijua hilo. Aidha swali lako ni la kukejeri ama unataka tuondoke katika mjadala husika hoja iwe mimi Mkandara na sio wagombea Urais.

Jambo la muhimu hapa hatusemi wala kumwambia mtu kura yake ampe nani, isipokuwa tunazungumzia sifa na uwezo wa viongozi tunaowatarajia kutuongoza. Iwe Magufuli au Lowassa atakaye shinda atakuwa rais wetu sote hakuna rais wa UKAWA ama rais wa CCM, kwa hiyo hizi fikra za kwamba mtu kama hamkubali Lowassa (UKAWA) basi lazima ni wa Magufuli (CCM) ni kutolitazama swala hili kwa mapana zaidi maana tunazungumzia rais wa JMT na sio mwenyekiti au kiongozi wa chama.

Swala la Mabadiliko ni kauli tata siku zote maana hakuna anayeweza kuyaona ya mbele, inaweza kuwa kama Misri au Iraq waloyataka Mabadiliko ama ikawa tofauti kama Kenya, Zambia na nchi nyinginezo maana nijuavyo mimi Sijawahi kuyaona Mabadiliko ya kisiasa yenye tija kwa wananchi wake zaidi ya kisera yaani mnachagua chama chenye sera zenye kukidhi mahitaji ya wananchi lakini haya Mabadiliko ya WATU kutaka sura nyingine ziongoze wakati fikra zao ni zile zile ndio mwanzo wa machafuko maana wanagombania kitu kama madume ya faru walotoka zizi moja.

Kumbuka tu wewe na mimi ni nyasi, hawa faru wanapogombana tunaumia sisi na hawajali japo chakula chao ni nyasi! sisi ndio waajiri wao na maisha yao yanatutegemea sisi lakini leo wanaomba kura zenu kwa kuonyesha unyenyekevu lakini mwisho wa siku wakiingia IKULU hawatapafanya tena Msikitini/kanisani bali nani dume atakaye tawala!

Sintomfagilia Lowassa kwa sababu ya Chadema, kazi mhiyo nimeiacha siku nyingi baada ya kugundua pale hapakuwa na UMOJA wenye dhamira ya kweli isipokuwa kundi la watu waloona Opportunity ya kuupata utajiri na Uheshimiwa. Fikra zile zile walokuwa nazo CCM miaka yote na kama mabadiliko basi yangeanza na kuondoa fursa ya wao kujitajirisha kwa kulipwa mshahara mil.11 kwa mwezi kazi ya kujitolea wakati CEO wa Benki hapewi mishahara huo..

Come on Mkandara, usiongee kama mtu wa kijijini ambaye hakuona hata milango ya shule. Upinzani wangefanya nini zaidi ya walichofanya na wanachoendelea kuafanya katika kuwaelimisha wananchi? Unapongelea mambo kama ya mishahara, mipango ya serikali na kanuni za utumishi je unajua nani anasimamia hayo toka tupate uhuru? Juzi tu umeshuhudia harakati ya kupata katiba mpya zilivyokwama kwa sababu tu CCM haikutaka, je ulitaka upinzani ufanye nini?

Ulitaka wachukua silaha waingie msituni? CCM wameonesha kabisa hawako tayari kwa mabadiliko na hadi leo madaraka yote yako mikononi mwao hivyo unapolaumu upinzani kwa mapungufu katika mfumo, hutendi haki. Unakuwa sawa na kijana wa mtaani ambaye anamlaumu mbunge wa upinzani kwa matatizo yaliyo jimboni kwake. Hizo ni kampeni za kijinga na zinaonesha kiwango duni sana katika uelewa wa mipango ya serikali na nani anatakiwa kuitekeleza.

Kuna wakati unanihuzunisha sana Mkandara...mabadiliko yamefikia wakati wake na si lazima neema ishuke mara moja, hapana, hapa tunajenga msingi. Baada ya nyumba kukamilika ndipo ubora wake utakapoonekana kulingana na uimara wa msingi. Mabadiliko si lelemaa, mabadiliko yana machungu yake, mazuri ya mabadiliko si lazima yaonekane katika muda mfupi, hapana, ila mabadiliko wakati wake ukifika heri na salama ni kuyakumbatia, na si kuyazuia, alamsiki.
 
Naungana na Watanzania wote kuwapa pole nyingi sana familia, ndugu, jamaa na wana-Lushoto wote kwa kufikwa msiba huu mkubwa. Kifo cha kijana Mohamed kimenistua sana, na mbaya zaidi ametutoka kwa ghafla mno. Mungu ana mipango yake, na tumuombe ampumzishe mahala pema. Amina.
 
Come on Mkandara, usiongee kama mtu wa kijijini ambaye hakuona hata milango ya shule. Upinzani wangefanya nini zaidi ya walichofanya na wanachoendelea kuafanya katika kuwaelimisha wananchi? Unapongelea mambo kama ya mishahara, mipango ya serikali na kanuni za utumishi je unajua nani anasimamia hayo toka tupate uhuru? Juzi tu umeshuhudia harakati ya kupata katiba mpya zilivyokwama kwa sababu tu CCM haikutaka, je ulitaka upinzani ufanye nini?

Ulitaka wachukua silaha waingie msituni? CCM wameonesha kabisa hawako tayari kwa mabadiliko na hadi leo madaraka yote yako mikononi mwao hivyo unapolaumu upinzani kwa mapungufu katika mfumo, hutendi haki. Unakuwa sawa na kijana wa mtaani ambaye anamlaumu mbunge wa upinzani kwa matatizo yaliyo jimboni kwake. Hizo ni kampeni za kijinga na zinaonesha kiwango duni sana katika uelewa wa mipango ya serikali na nani anatakiwa kuitekeleza.

Kuna wakati unanihuzunisha sana Mkandara...mabadiliko yamefikia wakati wake na si lazima neema ishuke mara moja, hapana, hapa tunajenga msingi. Baada ya nyumba kukamilika ndipo ubora wake utakapoonekana kulingana na uimara wa msingi. Mabadiliko si lelemaa, mabadiliko yana machungu yake, mazuri ya mabadiliko si lazima yaonekane katika muda mfupi, hapana, ila mabadiliko wakati wake ukifika heri na salama ni kuyakumbatia, na si kuyazuia, alamsiki.
Mimi nadhani maana haswa ya mjadala ni uhuru wa mawazo ya kila mtu yaheshimiwe na yatazamwe kama angalizo la upande wa pili wa shilingi na sio kwamba tuko hapa kubishana nani anajua zaidi ya mwenzake.

Kosa kubwa la kubishana huishia watu kutoleana maneno makali pasipo sababu zaidi ya kwamba kila mtu akipendacho hakina chongo, na badakla ya kujadili hoja watu huanza kuzungumzia wao wenyewe ni watu wa aina gani ana akili gani. Hapa tutakuwa hatuelimishani isipokuwa kila mtu anafikri anajua zaidi ya mwingine na tutabakia sote hatujui kitu. Na ndicho kinachoendelea hapa kwani haitoshi mtu kunijibu miye kuliko kuingiza swala la kunifananisha na watu wa vijijini kana kwamba wao hawana uelewa wa serikali yao. Hii ni dharau kwanza kwa wananchi wa vijijini ambao kuihsi kwao vijijini haina maana hawana akili ama weredi wa mamlaka ya serikali.


Mag3, wala usihuzunike nami isipokuwa maamuzi yenu ndio yalotufikisha katika hatua hii ya Mjadala. Upinzani ni kina nani? ni sehemu ya serikali na ndio maana wakaitwa serikali ya Kivuli wanalipwa na kodi yetu na wanagombea Ubunge wakiahidi kutuhudumia. Serikali ina mihimili mitatu na kati ya hiyo Bunge ndilo hupitisha mambo yote haya! Sasa kama wanajua kwamba ni seeikali ya CCM inayopitipisha kila kitu iwe mishahara, posho na hata katiba ambayo wao wanaipinga kwa nini wanagombea Ubunge?

Kwa nini wabunge wenu wanawaahidi wananchi wakichaguliwa watatimiza haya na yale wakati wanajua sii kweli? Kwa nini tuna vyama 20 wakati wanajua ni nafasi 350 tu zinatakiwa! bila shaka wanajua tukiwa na vyama viwili nafasi zitakuwa mbili tu badala ya 20 kugombea kiti kimoja (ubunge) Haya nambie Kwa nini UKAWA waliamua kuacha kupigania katiba Mpya wakaamua uchaguzi kwanza wakidhani watashinda na kuiondoa CCM madarakani? Je wasipoiondoa watajiuzuru Ubunge> Hapana hawawezi kosa yote bora wakose Katiba lakini sio Ubunge!

Halafu mkuu wangu, hoja zangu hazikuanza leo juu ya Upinzani toka issue ya Katiba, viongozi kwenda kunywa soda IKULU, muulize Mnyika au Mbowe. Toka kuondolewa kwa kina Kitila muulize Mbowe, Mnyika na hata huyo Lissu na sasa nimefikia kukaribishwa Lowassa na kuondoka kwa Dr. Slaa haya ni majanga mlojitengenezea wenyewe kama tunavyoilaumu CCM kwa uongozi wake mbaya. Tunawasema viongozi wabovu, maamuzi mabaya ya JK na hata bajeti na miswada mibovu inayopitishwa na CCM.

Yes, watu wote tumeichoka CCM na haswa viongozi waliopo maana pasipo wao CCM ni taasisi tu. Hata Timu ya Mpira pasipo wachezaji huwezi kuichukia timu kwa sababu inashindwa isipokuwa unatazama walosababisha perfomance kuwa mbovu ni kina nani? sababu gani wanashindwa!. Iwe kocha na mfumo au wachezaji wenyewe. Kwa hiyo mshabiki wa timu yako akichukia maamuzi mabaya ya Uongozi kama navyowasikia Wana Arsenal leo sii kwamba wanaichukia Timu yao ama Wenger bali wanajaribu kukosoa japo sii wajuzi wa kufundisha ama kucheza. Na ndicho nilikuwa nikifanya mimi kwa miaka yote kuikosoa Chadema pale ilipofanya maamuzi mabaya. Watu wengi hawakupenda kwa sababu wao washabiki wa damu..

Sasa What if UKAWA sijui Chadema hawakushinda uchaguzi huu hao wabunge wenu watajiuzuru Ubunge? ama wataendelea na hadith ile ile ya kuilaumu CCM maana ndio siasa zenyewe mchawi hakosekani. Hakuna nchi Upinzani wamefanikiwa kubadilisha sera za chama tawala ama kupitishwa bajeti na miswada isipokuwa pale walipounda serikali ya Mseto vyama vingine vikapewa nafasi sawa na hii hutokana na kura za wananchi. Sisi hatuna mfumo huo kwa hiyo sioni sababu ya kuahidi kujenga nyumba wakati huna mchoro wa ramani..

Na pia huwezi jenga msingi wa nyumba wakati huna kibali wala hati ya kuhodhi kiwanja, UKAWA wanachokifanya ni kuomba ridhaa ya kumiliki ardhi ambayo wao wameahidi kujenga nyumba ya kusadikika lakini tatizo la wananchi wengi ni dhamira ya mchora ramani (Architect) mwenyewe! Maana Uzuri wa nyumba upo katika ramani (sera) nia na malengo ya jengo hilo kama yana tija kwa wakazi wake - Hatuzioni faida, isipokuwa tunaambiwa kwanza fukuza mpangaji kaharibu nyumba. Super wa nyumba leo ndiye anataka kuhodhi madaraka yote na asipimwe kwa nini hakuweza kusimamia wakati wake?

Kiongozi kama Edo aloingia Chadema akitaka kuwa Mgombea Urais bila mshindani, akatoa yeye masharti zaidi ya ahadi za uongo na kwamba leo hii wapo wabunge hawana fedha za kujinadi vizuri, nguvu kubwa imewekwa kwa Edo mnategema Ushindi gani? Hili ni kanya boya ambalo hamkuliona ama kulitafakari kisawa sawa. Mimi naamini hata kama Lowassa angekuja Chadema lakini akawa tu mpiga debe akapitishwa mgombea kwa kura za maoni iwe ya wanachama au kamati maalum iwe Dr.Slaa au Lipumba basi Ukawa wangefanya vizuri Bungeni japo ushindi wa urais ni mgumu. Leo akishindwa Edo Ubunge ndio kabisaaa mtakuwa mmetumia nguvu kubwa akili kidogo kama kuli bandarini!

Leo hii picha nzima ni Lowassa against CCM, Mabadiliko ni Lowassa dhidi ya Kikwete kama vile mahitaji ya nchi hii yamekosekana kutokana na Kikwete (kocha Mbaya) hivyo tukibadilisha kocha na wachezaji wapya tutafanya vizuri wakati ukitazama sera zao wanazungumzia uchezaji ule ule - Ugali mwingi mboga kidogo..
 
Haya nambie Kwa nini UKAWA waliamua kuacha kupigania katiba Mpya wakaamua uchaguzi kwanza wakidhani watashinda na kuiondoa CCM madarakani? J
Hapa nitawaomba radhi wanajamvi, nichepuke kidogo. Mkuu kwani UKAWA walitakiwa wafanye nini kuinusuru katiba mpya?
 
Hapa nitawaomba radhi wanajamvi, nichepuke kidogo. Mkuu kwani UKAWA walitakiwa wafanye nini kuinusuru katiba mpya?
Mkuu wangu hiv unataka mimi nikujibu wewe mara ngapi.. Hili swali kama sikosei umeshaliuliza zaidi ya mara mbili huko nyuma...

Hata hivyo nitakujibu maana mwepesi kusema nimesepa swali lako. Mimi nilitaka UKAWA waendelee kuwepo bungeni kupitisha sura nyinginezo muhimu zaidi na wakubali hizo serikali 2 zibakie kiporo maana wananchi ndio watakuja fanya uamuzi. Maamuzi ya katiba Mpya kupitishwa haikuwa kazi yao, wao waliamini wakisha pitisha ndio imetoka haitakwenda kwa wananchi Lakini sheria haikusema hivyo.

Sheria ilisema wazi baada ya kuandikwa na kupitishwa na wao Katiba itakwenda kwa wananchi kupitishwa Hivyo Maamuzi ya mwisho yatafanywa na wananchi wenyewe. Kifupi niseme haikuwa kazi yao kukataa hata serikali 2 ilopitishwa na wengi na zaidi ya hapo UKAWA walijua toka mwanzo kuwa CCM ina wajumbe wengi bungeni na bado wakashiriki wakiwa wameridhika na muundo wa bunge.

Na hata walipotoka walisema CCM haiwezi kuwa na 2/3 ya wajumbe, sasa jiulize walitoka kwa nini ikiwa sura itapitishwa tu ikiwa kundi moja limepata asilimia 2/3 ya kura na wao walihakikisha CCM hawana hizo 2/3 kabla hawajatoka! Nilisema tena bora warudi Bungeni kuhakikisha maswala muhimu maana CCM imechukua sura ya sita makusudi hivyo na zaidi ya hapo hata mimi sikukubalini na serikali 3 za JUMUIYA ambazo mapato ya kodi za mambo yasokuwa ya Muungano hayaihusu serikali kuu. Biola shaka unakumbuka hilo maana tulilumbana kwa muda mrefu sana wewe na Mchambuzi..

Kifupi, kukubaliana na kupitisha sura na ibara zake iwe sababu bya kutoka, Hii haikuwa kazi ya mwisho bali wananchi ndio wangeamua na pengine swala la serikali 2 lingekwama. Ila nina hakika kama mambo mengi yangepitishwa Uchaguzi huu ungekuwa mgumu kwa CCM kuliko mnavyoutazama sasa hivi maana bado CCM ina advantage kubwa sana kutokana na Katiba ya mwaka 1977.

Na kama unakumbuka vizuri nilichomshambulia Mnyika humu baada ya wao kwenda kunywa Juice IKULU! Nilimwambia wamefanya makosa kabisa kukubali ati kwa sababu wameahidiwa kushirikishwa katika kuandika Katiba Mpya. Katiba haiandikwi na vyama isipokuwa kuandikwa na Wataalam. Vyama vitatoa tu maoni yao juu ya uhuru na haki zao ili sheria itungwe na kukabidhiwa msajili wa vyama (upande washeria) kama ambavyo taasisi na Asasi nyingine zingeweka mapendekezo ya Uhuru na haki zao zilipitishwe ili sheria iwasimamie. haikutakiwa kabisa wajumbe wa vyama, taasisi na Asasi wawe watunga katiba. Hapo ni kuzua mtafaruku na ushindani..

Nakumbuka vizuri Mnyika akasema ya kwamba kila mtu mule atakwenda kama mjumbe na mawazo Binafsi akasahau kwamba hata yeye roho yake ipo katika maamuzi ya chama. Uchama ndio uloharibu Katiba na sio CCM pekee hawa wote hawakutakiwa kuandika Katiba, tume ilochaguliwa ilitosha kukusanya maoni ya watu, vyama vya ushirika, taasisi na Asasi ili kuandika sheria. Lakini maadam walishafikia hatua ya kuandika katiba nilisema wasitoke Bungeni hadi yale mambo muhimu tuloyazungumza humu miaka nenda rudi yapitishwe....
 
Mkuu wangu hiv unataka mimi nikujibu wewe mara ngapi.. Hili swali kama sikosei umeshaliuliza zaidi ya mara mbili huko nyuma...

Hata hivyo nitakujibu maana mwepesi kusema nimesepa swali lako. Mimi nilitaka UKAWA waendelee kuwepo bungeni kupitisha sura nyinginezo muhimu zaidi na wakubali hizo serikali 2 zibakie kiporo maana wananchi ndio watakuja fanya uamuzi. Maamuzi ya katiba Mpya kupitishwa haikuwa kazi yao, wao waliamini wakisha pitisha ndio imetoka haitakwenda kwa wananchi Lakini sheria haikusema hivyo.

Sheria ilisema wazi baada ya kuandikwa na kupitishwa na wao Katiba itakwenda kwa wananchi kupitishwa Hivyo Maamuzi ya mwisho yatafanywa na wananchi wenyewe. Kifupi niseme haikuwa kazi yao kukataa hata serikali 2 ilopitishwa na wengi na zaidi ya hapo UKAWA walijua toka mwanzo kuwa CCM ina wajumbe wengi bungeni na bado wakashiriki wakiwa wameridhika na muundo wa bunge.

Na hata walipotoka walisema CCM haiwezi kuwa na 2/3 ya wajumbe, sasa jiulize walitoka kwa nini ikiwa sura itapitishwa tu ikiwa kundi moja limepata asilimia 2/3 ya kura na wao walihakikisha CCM hawana hizo 2/3 kabla hawajatoka! Nilisema tena bora warudi Bungeni kuhakikisha maswala muhimu maana CCM imechukua sura ya sita makusudi hivyo na zaidi ya hapo hata mimi sikukubalini na serikali 3 za JUMUIYA ambazo mapato ya kodi za mambo yasokuwa ya Muungano hayaihusu serikali kuu. Biola shaka unakumbuka hilo maana tulilumbana kwa muda mrefu sana wewe na Mchambuzi..

Kifupi, kukubaliana na kupitisha sura ama ibara haikuwa kazi ya mwisho bali wananchi ndio wangeamua. na nina hakika kama mambo mengi yangepitishwa Uchaguzi huu ungekuwa mgumu kwa CCM kuliko mnavyoutazama sasa hivi maana bado CCM ina advantage kubwa sana kutokana na Katiba ya mwaka 1977.

Na kama unakumbuka vizuri nilichomshambulia Mnyika humu baada ya wao kwenda kunywa Juice IKULU! Nilimwambia wamefanya makosa kabisa kukubali ati kwa sababu wameahidiwa kushirikishwa katika kuandika Katiba Mpya. Katiba haiandikwi na vyama isipokuwa vyama vitatoa maoni yao juu ya haki zao ili sheria itungwe na kukabidhiwa msajili wa vyama. (upande washeria) kama ambavyo taasisi na Asasi nyingine zingeweka mapendekezo ya haki zao zilipitishwe ili sheria iwasimamie sio wajumbe wa vyama taasisi na Asasi ziwe watunga katiba. Hapo ni kiuzua mtafaruku na ushindani..

Nakumbuka vizuri Mnyika akasema ya kwamba kila mtu mule atakwenda kama mjumbe na mawazo Binafsi akasahau kwamba hata yeye roho yake ipo katika maamuzi ya chama. Uchama ndio uloharibu Katiba na sio CCM pekee hawa wote hawakutakiwa kuandika Katiba, tume ilochaguliwa ilitosha kukusanya maoni ya watu, vyama vya ushirika, taasisi na Asasi ili kuandika sheria. Lakini maadam walishafikia hatua ya kuandika katiba nilisema wasitoke Bungeni hadi

Na ndicho kilichotokea.
Hapa ndipo naungana na Mag3 kushindwa kukuelewa

Mkuu ni hivi, UKAWA walitoka kwasababu taratibu zote zilizo govern na zilizokubaliwa zilikikukwa

Kwa mfano, utaratibu wa Rais kuhutubia kabla ya bunge uligeuzwa makusudi ili kufanya waliyofanya
kuondoa vifungu vilivyopendekezwa bila sababu
Kulazimisha muundo bila sababu

UKAWA si wajinga wa kuelewa kuwa katiba itapigiwa kura na wananchi, come on!

Mkandara pale kuna maprofesa na watu wenye weledi.

Huwezi kuniambia wewe una weledi wa katiba kuliko prof Palamagamba au Baregu na kwamba hao hawakuona unachokisema, please!

Huko kwa wananchi ulitegemea nini ikiwa CCM waliobaki wenyewe waliiba kura na kudanganya ili wapate 2/3

Kuamini kuwa walipata 2/3 pale ndani is anachronism, out of touch

Kuhusu kuacha mambo kiporo, katiba haindikwi kila asubuhi kama breakfast, na sijui kama unajua uzito wa katiba.

Kuhusu kuacha serikali 2, hapa napo nashangaa, maana muundo wa serikali ndiyo unaoamua mambo yaliyomo ndani ya katiba.

CCM wamejaribu na wameshindwa, kuna maeneo hawakugusa kwasababu structure haikuwepo

Mkuu wewe unashauri watu waezeke nyumba halafu wachimbe msingi!

Kuna nchi zimechukua miaka 1,2 hadi 7 kuandika katiba.

Tazama Kenya na South Africa, kuna kiporo gani kimeachwa

Kumbu kumbu zangu zinaonyesha uliwahi kusema serikali 2 zitawaumiza wazanzibar( nukuu zipo ukitaka)

Ulichotambua ni kuwa hatuandiki katiba ya kundi, tunaandika katiba ya nchi

Usidanganye watu kuwa hukubaliani na S3 kwasababu ya mapato, no! ni kwasababu ya Zanzibar, period.
Tena umebadili mwendo, ulisema gharama sasa hivi unasema mapato! mkuu wapi na wapi

Tulikuuliza gharama ni zipi, ukasema idadi ya wabunge na mabunge mawili, well, sasa hivi idadi ni kubwa kuliko ulivyosema
Umebadili uelekeo

Hivyo, tambua kuwa UKAWA walitoka si kwasababu nyingine bali uhuni na ubabe wa CCM kuchomeka katiba yao iliyoandikwa pembeni na watu kama yule mwalimu wa UDSM Fracis aliyeingi bunge la katiba kama mwakailishi wa UDSM na wana taaluma.

Juzi alikuwa katika TV akizungumzia CCM na miradi ya reli za std gauge. Huyo ndiye alikuwa anaandika na akina Cheng pembeni

Sasa wewe ulitaka rasimu ya wananchi iachwe ili tufanye ukarabati wa rasimu iliyoandikwa na watu wawili

Mkuu hapa ni kuwa process nzima ilikuwa flawed na kuendelea nayo ni kutoa uhalali wa mzoga. Mzogo hauna uhalali hata kama unasehemu isiyooza, mzoga ni mzoga tu hakuna kiporo cha mzoga

Pengine ningekubaliana nawe kuwa Mbowe na 'Juisi ya maembe' walitenda makosa kwenda kwa majadiliano bila nyarka ya kisheria.

Hilo tuliwaeleza sana katika uzi wa 'juisi ya maemebe' wakakataa na ndicho kilichotokea. Aliwageuka! kwani hawamjui
 
Hapa ndipo naungana na Mag3 kushindwa kukuelewa

Mkuu ni hivi, UKAWA walitoka kwasababu taratibu zote zilizo govern na zilizokubaliwa zilikikukwa

Kwa mfano, utaratibu wa Rais kuhutubia kabla ya bunge uligeuzwa makusudi ili kufanya waliyofanya
kuondoa vifungu vilivyopendekezwa bila sababu
Kulazimisha muundo bila sababu

UKAWA si wajinga wa kuelewa kuwa katiba itapigiwa kura na wananchi, come on!

Mkandara pale kuna maprofesa na watu wenye weledi.

Huwezi kuniambia wewe una weledi wa katiba kuliko prof Palamagamba au Baregu na kwamba hao hawakuona unachokisema, please!

Huko kwa wananchi ulitegemea nini ikiwa CCM waliobaki wenyewe waliiba kura na kudanganya ili wapate 2/3

Kuamini kuwa walipata 2/3 pale ndani is anachronism, out of touch

Kuhusu kuacha mambo kiporo, katiba haindikwi kila asubuhi kama breakfast, na sijui kama unajua uzito wa katiba.

Kuhusu kuacha serikali 2, hapa napo nashangaa, maana muundo wa serikali ndiyo unaoamua mambo yaliyomo ndani ya katiba.

CCM wamejaribu na wameshindwa, kuna maeneo hawakugusa kwasababu structure haikuwepo

Mkuu wewe unashauri watu waezeke nyumba halafu wachimbe msingi!

Kuna nchi zimechukua miaka 1,2 hadi 7 kuandika katiba.

Tazama Kenya na South Africa, kuna kiporo gani kimeachwa

Kumbu kumbu zangu zinaonyesha uliwahi kusema serikali 2 zitawaumiza wazanzibar( nukuu zipo ukitaka)

Ulichotambua ni kuwa hatuandiki katiba ya kundi, tunaandika katiba ya nchi

Usidanganye watu kuwa hukubaliani na S3 kwasababu ya mapato, no! ni kwasababu ya Zanzibar, period.
Tena umebadili mwendo, ulisema gharama sasa hivi unasema mapato! mkuu wapi na wapi

Tulikuuliza gharama ni zipi, ukasema idadi ya wabunge na mabunge mawili, well, sasa hivi idadi ni kubwa kuliko ulivyosema
Umebadili uelekeo

Hivyo, tambua kuwa UKAWA walitoka si kwasababu nyingine bali uhuni na ubabe wa CCM kuchomeka katiba yao iliyoandikwa pembeni na watu kama yule mwalimu wa UDSM Fracis aliyeingi bunge la katiba kama mwakailishi wa UDSM na wana taaluma.

Juzi alikuwa katika TV akizungumzia CCM na miradi ya reli za std gauge. Huyo ndiye alikuwa anaandika na akina Cheng pembeni

Sasa wewe ulitaka rasimu ya wananchi iachwe ili tufanye ukarabati wa rasimu iliyoandikwa na watu wawili

Mkuu hapa ni kuwa process nzima ilikuwa flawed na kuendelea nayo ni kutoa uhalali wa mzoga. Mzogo hauna uhalali hata kama unasehemu isiyooza, mzoga ni mzoga tu hakuna kiporo cha mzoga

Pengine ningekubaliana nawe kuwa Mbowe na 'Juisi ya maembe' walitenda makosa kwenda kwa majadiliano bila nyarka ya kisheria.

Hilo tuliwaeleza sana katika uzi wa 'juisi ya maemebe' wakakataa na ndicho kilichotokea. Aliwageuka! kwani hawamjui
Ebu nipe kifungu kilichomkataza rais kuhutubia kabla ya Bunge... maana sikuona kifungu hicho miye na hata kama nachokumbuka UKAWA walitoka wakati wa mjadala juu ya serikali ngapi sio kuhutubia kwa JK. taratibu zilizokiukwa ni Zipi? kama CCM waliunda kundi lao na UKAWA vile vile waliunda maana UKAWA ilipatikana ndani ya Bunge.

Huwezi kupinga utaratibu kukiuka wakati wewe mwenywe unaukiuka maana makosa yalifanywa toka mwanzo walipokubali wao waandike katiba wakati hivi vyama havifungamani. Inakuw akama wanaandika SERA za pamoja (serikali ya Mseto) badala ya Katiba. UKAWA walifanya makosa wakarudia makosa na wakaendelza makosa hadi leo hii..

Hao maprefesa sii wandishi wa katiba,kama kweli wangeitumia elimu yao wangekataa vyama kutoandika katiba lakini kwa sababu ya Ulaji na posho walikubali ili kuhakikisha wao wanapata katiba waitakayo wao na sio Katiba ya wananchi.. na ndicho kilichotokea Hiyo Katiba Pendekezwa ni katiba waipendayo CCM, wangeshinda UKAWA ingekuwa katiba Pendekezwa ya UKAWA.
 
Ebu nipe kifungu kilichomkataza rais kuhutubia kabla ya Bunge... maana sikuona kifungu hicho miye na hata kama nachokumbuka UKAWA walitoka wakati wa mjadala juu ya serikali ngapi sio kuhutubia kwa JK. taratibu zilizokiukwa ni Zipi? kama CCM waliunda kundi lao na UKAWA vile vile waliunda maana UKAWA ilipatikana ndani ya Bunge.

Rasimu ya pili ya Kanuni za Bunge la katiba...

7:
(1) Shughuli za Mkutano wa Bunge Maalum zitakuwa kama

ifuatavyo:

(a)kusomwa kwa Tangazo la Rais la kuitisha Bunge Maalum;

(b)uchaguzi wa Mwenyekiti wa muda;

(c)kuandaa na kupitisha Kanuni za Bunge Maalum;

(d)uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti;


(e)kiapo cha Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti;

(f)kiapo cha Wajumbe wa Bunge Maalum;

(g)hotuba ya mgeni rasmi

(h)uwasilishaji wa Rasimu ya Katiba;


(i)kujadili taarifa na hoja za Kamati; na

(j)
shughuli nyingine yoyote ambayo Bunge Maalum litaona


"Mgeni Rasmi "maana yake ni

Rais wa Jamhuri ya Muungano au Rais wa Zanzibar

atakayealikwa na Mwenyekiti kulihutubia
Bunge Maalum;

http://www.bungemaalum.go.tz/files/...simu_ya_Pili_ya_Kanuni_za_Bunge_Maalum_sw.pdf
 

Alinda ndugu yangu kwani unadhani hajui!! ni kutokuwa na uaminifu wa majadiliano kwa njia za ubabaishaji tu


Mfano, anasema 2/3 ilipatikana akijua suala la Zakhia Meghji, na kura za maruhani vimekukungumizwa.

CCM wanaona aibu kuzungumzia katiba yao ili kutoudhi wananchi zaidi. In fact hiyo ni moja kati ya mambo yanaowaudhi sana wananchi na kuichoka. Sasa mwenzetu anasema 2/3 ilipataikana! Kajitoa fahamu kabisa

Anasema UKAWA wangeacha kiporo suala la muundo wa muungano!
Hapa ndipo Mag3 anapompa 'blunt' utadhani hakuhudhuria shule.

Katiba haiandikwi kama breakfast kila asubuhi, wala si apple au peas, come on!

Na mwisho anasema hataki S3 kwa sababu ya gharama. Huko nyuma alisema S3 ni mzigo wa wabunge, leo ni zaidi ameabadili mwendo. Anataka S3 si kwasababu za kisiasa, anajificha ficha , tunamjua eneo alilo na ufundi nalo .
 

Alinda ndugu yangu kwani unadhani hajui!! ni kutokuwa na uaminifu wa majadiliano kwa njia za ubabaishaji tu


Mfano, anasema 2/3 ilipatikana akijua suala la Zakhia Meghji, na kura za maruhani vimekukungumizwa.

CCM wanaona aibu kuzungumzia katiba yao ili kutoudhi wananchi zaidi. In fact hiyo ni moja kati ya mambo yanaowaudhi sana wananchi na kuichoka. Sasa mwenzetu anasema 2/3 ilipataikana! Kajitoa fahamu kabisa

Anasema UKAWA wangeacha kiporo suala la muundo wa muungano!
Hapa ndipo Mag3 anapompa 'blunt' utadhani hakuhudhuria shule.

Katiba haiandikwi kama breakfast kila asubuhi, wala si apple au peas, come on!

Na mwisho anasema hataki S3 kwa sababu ya gharama. Huko nyuma alisema S3 ni mzigo wa wabunge, leo ni zaidi ameabadili mwendo. Anataka S3 si kwasababu za kisiasa, anajificha ficha , tunamjua eneo alilo na ufundi nalo .
Nguruvi3, huyo ndiye Mkandara, wakati mwingine nashindwa hata kujibizana naye maanake unajikuta uko katika level yake. Nakiri ninatofautiana na wengi tu humu ndani kuhusu ujio wa Lowassa Chadema na kuteuliwa kuwa mgombea chini ya UKAWA lakini mimi nasema na narudia, ikiwa Lowassa atatuwezesha kuliondoa hili zimwi madarakani, so be it. Kama Lowassa angeteuliwa kupeperusha bendera ya CCM, nisingemuunga mkono, nisingemtetea kwa sababu vita yangu ni dhidi ya mfumo unaotuzalishia na kuwalea ninaowaita maadui wa taifa hili, period. Wakiachana na CCM kama alivyofanya Dr. Slaa miaka mitatu baada ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, sina sababu tena ya kutowapokea.
 
Last edited by a moderator:
Rasimu ya pili ya Kanuni za Bunge la katiba...

7:
(1) Shughuli za Mkutano wa Bunge Maalum zitakuwa kama

ifuatavyo:

(a)kusomwa kwa Tangazo la Rais la kuitisha Bunge Maalum;

(b)uchaguzi wa Mwenyekiti wa muda;

(c)kuandaa na kupitisha Kanuni za Bunge Maalum;

(d)uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti;


(e)kiapo cha Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti;

(f)kiapo cha Wajumbe wa Bunge Maalum;

(g)hotuba ya mgeni rasmi

(h)uwasilishaji wa Rasimu ya Katiba;


(i)kujadili taarifa na hoja za Kamati; na

(j)
shughuli nyingine yoyote ambayo Bunge Maalum litaona


"Mgeni Rasmi "maana yake ni

Rais wa Jamhuri ya Muungano au Rais wa Zanzibar

atakayealikwa na Mwenyekiti kulihutubia
Bunge Maalum;

http://www.bungemaalum.go.tz/files/...simu_ya_Pili_ya_Kanuni_za_Bunge_Maalum_sw.pdf
Sijawaelewa labda au hatuelewani, maana nilichomsoma Nguruvi3 yeye kasema rais alivunja utaratibu wa kuhutubia mkutano kabla ya Bunge.
Kwa mfano, utaratibu wa Rais kuhutubia kabla ya bunge uligeuzwa makusudi ili kufanya waliyofanya
kuondoa vifungu vilivyopendekezwa bila sababu
Kulazimisha muundo bila sababu
. ndio maana nikaomba hiyo sheria inayomkataza kuhutubia kabla ya bunge ama kugeuza yalokusudiwa maana sidhani alipangiwa cha kusema. Hapo juu umeweka vielelezo vinavyoonyesha aliruhusiwa kufungua Bunge na kuwa mgeni rasmi na hakuna masharti wala maelezo zaidi, Sasa ni utaratibu gani Ulovunjwa na kugeuzwa anaozungumzia Nguruvi3..

Zaidi ya hapo mlitegemea kweli rais wa JMT angeacha kuzungumzia swala la serikali 3 pasipo mtazamo wake, je alipata wapi zile data zote alozitoa juu ya maoni ya wananchi kama hakupewa kuzisoma na kutafakari? Na hata mlipotoa mawazo ya kuandika katiba mpya mlimuomba akasoma maelezo yenu na kuwakubalia japo CCM walipinga na ikafanyika - He is the President mlitegemea nini..
 
Back
Top Bottom