CHADEMA tunataka kuona msimamo wenu kwa vitendo kuhusu kutoshiriki uchaguzi

Desprospero

JF-Expert Member
Feb 1, 2023
887
2,201
Moja ya sifa nzuri na thabiti ya kiongozi ni kusimamia anachokiamini hata kama msimamo huo unaweza kumdhuru binafsi au na taasisi anayoongoza.

Msimamo wa CHADEMA ulioamuliwa na Kamati Kuu yake na kutangazia dunia hadharani kupitia kinywa cha Katibu Mkuu wake John Mnyika na Mwenyekiti Freeman Mbowe ni kwamba chama hicho HAKITASHIRIKI Uchaguzi WOWOTE bila kuwepo kwa Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.

Huko Mbeya Jimbo la Mbarali Jimbo liko wazi na linatakiwa kuzibwa ndani ya siku 90 kwa mujibu wa Katiba ya Sasa (isiyotakiwa na CHADEMA) kufuatia kifo cha Francis Mtega aliyefariki baada ya kugonga "pawatila" akiwa na pikipiki.

Kwa msimamo huo hatutegemei kuona CHADEMA ikisimamisha mgombea ili kuonesha msimamo.

Si hapo tu. Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni mwakani Jumapili ya mwisho wa mwezi Oktoba 2024. Hakika niliyonayo kwa muda uliosalia tutakuwa bado hatujapata Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Nitasikitika Chadema ikishiriki Uchaguzi huo.

Kwa mambo yanavyoenda ndani ya CCM na Serikali Samia hawezi kutoa Katiba Mpya ndani ya first term yake. Maana yake yake ni kwamba 2025 Katiba itakayofanya kazi ni hii hii. Kwa mantiki hiyo, sitegemei kuona CHADEMA kushiriki Uchaguzi huo Mkuu maana hakutakuwa na Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Kwa msimamo huo CHADEMA itashiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2029 na Uchaguzi Mkuu wa 2030. Simamieni uamuzi wenu ili msionekane wajinga wa maamuzi. Siku njema.
 
Tumalize la bandari zetu watanganyika kwanza, Chadema hawajawahi kutoa tamko la kushiriki uchaguzi kinyume na lile walilotoa mwanzo kutoshiriki mpaka Katiba Mpya na Tume Huru vipatikane, ukiachia mbali maneno maneno ya wanasiasa wao ambayo kimsingi sio tamko/msimamo wa chama.
 
Moja ya sifa nzuri na thabiti ya kiongozi ni kusimamia anachokiamini hata kama msimamo huo unaweza kumdhuru binafsi au na taasisi anayoongoza.

Msimamo wa CHADEMA ulioamuliwa na Kamati Kuu yake na kutangazia dunia hadharani kupitia kinywa cha Katibu Mkuu wake John Mnyika na Mwenyekiti Freeman Mbowe ni kwamba chama hicho HAKITASHIRIKI Uchaguzi WOWOTE bila kuwepo kwa Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.

Huko Mbeya Jimbo la Mbarali Jimbo liko wazi na linatakiwa kuzibwa ndani ya siku 90 kwa mujibu wa Katiba ya Sasa (isiyotakiwa na CHADEMA) kufuatia kifo cha Francis Mtega aliyefariki baada ya kugonga "pawatila" akiwa na pikipiki.

Kwa msimamo huo hatutegemei kuona CHADEMA ikisimamisha mgombea ili kuonesha msimamo.

Si hapo tu. Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni mwakani Jumapili ya mwisho wa mwezi Oktoba 2024. Hakika niliyonayo kwa muda uliosalia tutakuwa bado hatujapata Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Nitasikitika Chadema ikishiriki Uchaguzi huo.

Kwa mambo yanavyoenda ndani ya CCM na Serikali Samia hawezi kutoa Katiba Mpya ndani ya first term yake. Maana yake yake ni kwamba 2025 Katiba itakayofanya kazi ni hii hii. Kwa mantiki hiyo, sitegemei kuona CHADEMA kushiriki Uchaguzi huo Mkuu maana hakutakuwa na Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Kwa msimamo huo CHADEMA itashiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2029 na Uchaguzi Mkuu wa 2030. Simamieni uamuzi wenu ili msionekane wajinga wa maamuzi. Siku njema.
Ni lini hicho kinachoitwa msimamo uliwahi athiri shughuli za serikali? Hii nchi haiongozwi Kwa misimamo au mihemko ya kikundi Fulani Cha watu kinaongozwa Kwa mujibu wa katiba ma Sheria Sasa chadema ni kama hawana Tena hoja walilamika mama akawapa uhuru wa mikutano ya kisiasa lakini hatuoni Cha maana wanachokisema nchi ikiwa inaendelea vizuri ndio furaha yetu sisi wananchi sio migomo Wala kususa susa hovyo.
 
Ni lini hicho kinachoitwa msimamo uliwahi athiri shughuli za serikali? Hii nchi haiongozwi Kwa misimamo au mihemko ya kikundi Fulani Cha watu kinaongozwa Kwa mujibu wa katiba ma Sheria Sasa chadema ni kama hawana Tena hoja walilamika mama akawapa uhuru wa mikutano ya kisiasa lakini hatuoni Cha maana wanachokisema nchi ikiwa inaendelea vizuri ndio furaha yetu sisi wananchi sio migomo Wala kususa susa hovyo.
Bila Tume HURU ya UCHAGUZI itokanayo na KATIBA mpya kupatikana,

Hapatafanyika uchaguzi mkuu, ukifanyika uchaguzi huo, mshindi hatopatikana.

Itabidi dawati na jopo la waamuzi kukaa tena Ili HAKI itendeke.

Muda wa mabadiliko umefika Nyikani, historia ilopita isiwatie Giza kuyaona yajayo.

Mungu ibariki TANZANIA.

Anen
 
Bila Tume HURU ya UCHAGUZI itokanayo na KATIBA mpya kupatikana,

Hapatafanyika uchaguzi mkuu, ukifanyika uchaguzi huo, mshindi hatopatikana.

Itabidi dawati na jopo la waamuzi kukaa tena Ili HAKI itendeke.

Muda wa mabadiliko umefika Nyikani, historia ilopita isiwatie Giza kuyaona yajayo.

Mungu ibariki TANZANIA.

Anen
Kwamba vyama 19 vikiwa tayari kwa Uchaguzi, usifanyike kisa chama kimoja kinataka Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Mnachekesha sana. Hii ni Dola huru na hii ni CCM.
 
Kwamba vyama 19 vikiwa tayari kwa Uchaguzi, usifanyike kisa chama kimoja kinataka Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Mnachekesha sana. Hii ni Dola huru na hii ni CCM.
Subiri uchaguzi wa MITAA mwaka ujao,

Tutapata taswira kamili.


Tusubiri.
 
Moja ya sifa nzuri na thabiti ya kiongozi ni kusimamia anachokiamini hata kama msimamo huo unaweza kumdhuru binafsi au na taasisi anayoongoza.

Msimamo wa CHADEMA ulioamuliwa na Kamati Kuu yake na kutangazia dunia hadharani kupitia kinywa cha Katibu Mkuu wake John Mnyika na Mwenyekiti Freeman Mbowe ni kwamba chama hicho HAKITASHIRIKI Uchaguzi WOWOTE bila kuwepo kwa Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.

Huko Mbeya Jimbo la Mbarali Jimbo liko wazi na linatakiwa kuzibwa ndani ya siku 90 kwa mujibu wa Katiba ya Sasa (isiyotakiwa na CHADEMA) kufuatia kifo cha Francis Mtega aliyefariki baada ya kugonga "pawatila" akiwa na pikipiki.

Kwa msimamo huo hatutegemei kuona CHADEMA ikisimamisha mgombea ili kuonesha msimamo.

Si hapo tu. Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni mwakani Jumapili ya mwisho wa mwezi Oktoba 2024. Hakika niliyonayo kwa muda uliosalia tutakuwa bado hatujapata Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Nitasikitika Chadema ikishiriki Uchaguzi huo.

Kwa mambo yanavyoenda ndani ya CCM na Serikali Samia hawezi kutoa Katiba Mpya ndani ya first term yake. Maana yake yake ni kwamba 2025 Katiba itakayofanya kazi ni hii hii. Kwa mantiki hiyo, sitegemei kuona CHADEMA kushiriki Uchaguzi huo Mkuu maana hakutakuwa na Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Kwa msimamo huo CHADEMA itashiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2029 na Uchaguzi Mkuu wa 2030. Simamieni uamuzi wenu ili msionekane wajinga wa maamuzi. Siku njema.
Uwe unawakumbusha mara kwa mara maana hawakawii kusahau. Halafu ajenda zao ni kama kujisikia kwenda haja maana huja anytime. Lakini vyema ukawakumbusha ni Katiba hii hii ya sasa wasiyoitaka ya mwaka 1977 ndio inawaruhusu kufanya siasa nchini Tanzania.
 
Back
Top Bottom